< Luka 7 >
1 Baada ya Yesu kumaliza kusema haya yote watu wakiwa wanamsikiliza, akaingia Kapernaumu.
Now when He had finished his discourse in the audience of the people, He entered into Capernaum: and a certain centurion's servant,
2 Mtumishi wa jemadari mmoja wa Kirumi, ambaye bwana wake alimthamini sana, alikuwa mgonjwa sana karibu kufa.
whom he had a great value for, was ill and ready to die;
3 Jemadari huyo aliposikia habari za Yesu, aliwatuma wazee wa Kiyahudi kwake, wakamwomba aje kumponya mtumishi wa huyo jemadari.
and having heard of Jesus, he sent unto Him the elders of the Jews, beseeching him that He would come and heal his servant.
4 Wale wazee walipofika kwa Yesu, wakamsihi sana amsaidie yule jemadari wakisema, “Mtu huyu anastahili wewe umfanyie jambo hili,
And when they came to Jesus, they intreated Him earnestly, saying, he is worthy of this favor:
5 kwa sababu analipenda taifa letu tena ametujengea sinagogi.”
for he loveth our nation, and hath built us a synagogue.
6 Hivyo Yesu akaongozana nao, lakini alipokuwa hayuko mbali na nyumbani, yule jemadari akatuma rafiki zake kumwambia Yesu, “Bwana, usijisumbue, kwani mimi sistahili wewe kuingia chini ya dari yangu.
So Jesus went with them. And when He was now not far from the house, the centurion sent some of his friends to Him, saying Lord, trouble not thyself, for I am not worthy that thou shouldst enter under my roof:
7 Ndiyo maana sikujiona hata ninastahili kuja kwako wewe. Lakini sema neno tu, naye mtumishi wangu atapona.
neither did I think myself worthy to come unto thee. But speak the word, and my servant will be recovered.
8 Kwa kuwa mimi mwenyewe ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, nikiwa na askari chini yangu. Nikimwambia huyu, ‘Nenda,’ yeye huenda; na mwingine nikimwambia, ‘Njoo,’ yeye huja. Nikimwambia mtumishi wangu, ‘Fanya hivi,’ yeye hufanya.”
For I also am a man placed under the authority of others, and have soldiers under me; and I say to one, Go, and he goeth; and to another, Come, and he cometh; and to my servant, Do this, and he doth it.
9 Yesu aliposikia maneno haya, alishangazwa naye sana. Akaugeukia ule umati wa watu uliokuwa unamfuata, akawaambia, “Sijaona imani kubwa namna hii hata katika Israeli.”
And when Jesus heard these things, He marvelled, and turning about, said to the multitude that followed Him, I declare unto you, I have not found so great faith, no not in Israel.
10 Nao wale watu waliokuwa wametumwa kwa Yesu waliporudi nyumbani walimkuta yule mtumishi amepona.
And when they that were sent, returned to the house, they found the servant well, that had been sick.
11 Baadaye kidogo, Yesu alikwenda katika mji mmoja ulioitwa Naini. Nao wanafunzi wake na umati mkubwa wa watu walikwenda pamoja naye.
And the day after He went to a city called Nain; and many of his disciples went with Him, and a great multitude besides:
12 Alipokaribia lango la mji, alikutana na watu waliokuwa wamebeba maiti wakitoka nje ya mji. Huyu aliyekufa alikuwa mwana pekee wa mwanamke mjane. Umati mkubwa wa watu wa mji ule ulikuwa pamoja na huyo mwanamke.
and as He came near to the gate of the city, behold, there was a dead man carrying out to be buried, his mother's only son, and she was a widow: and many of the people of the city were with her.
13 Bwana Yesu alipomwona yule mjane, moyo wake ulimhurumia, akamwambia, “Usilie.”
And when the Lord saw her, He was moved with compassion for her, and said to her, Do not weep.
14 Kisha akasogea mbele akaligusa lile jeneza na wale waliokuwa wamelibeba wakasimama kimya. Akasema, “Kijana, nakuambia inuka.”
And He came up and touched the bier, (and the bearers stopped, ) and He said, Young man, I say unto thee, arise.
15 Yule aliyekuwa amekufa akaketi akaanza kuongea, naye Yesu akamkabidhi kwa mama yake.
And the dead person sat up, and began to speak: and He delivered him to his mother.
16 Watu wote wakajawa na hofu ya Mungu, nao wakamtukuza Mungu wakisema, “Nabii mkuu ametokea miongoni mwetu, Mungu amekuja kuwakomboa watu wake.”
And an awe seized them all, and they glorified God, saying, a great prophet is risen up among us, and God hath visited his people.
17 Habari hizi za mambo aliyoyafanya Yesu zikaenea Uyahudi wote na sehemu zote za jirani.
And this report of Him was spread through all Judea, and in all the country round about.
18 Wanafunzi wa Yohana Mbatizaji wakamweleza Yohana mambo haya yote. Hivyo Yohana akawaita wanafunzi wake wawili
And the disciples of John told him of all these things: so John called two of his disciples to him,
19 na kuwatuma kwa Bwana ili kumuuliza, “Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?”
and sent them to Jesus, saying, Art thou He that was to come, or are we to expect another?
20 Wale watu walipofika kwa Yesu wakamwambia, “Yohana Mbatizaji ametutuma tukuulize, ‘Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?’”
And the men came to Him, and said, John the baptist hath sent us unto thee, saying, Art thou He that was to come, or are we to expect another?
21 Wakati huo huo, Yesu aliwaponya wengi waliokuwa na magonjwa, maradhi na pepo wachafu, na pia akawafungua vipofu wengi macho wakapata kuona.
(Now at that very time He cured many of their diseases and plagues, and of evil spirits, and gave sight to many that were blind.)
22 Hivyo akawajibu wale wajumbe, “Rudini mkamwambie Yohana yote mnayoyaona na kuyasikia: Vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa na maskini wanahubiriwa habari njema.
And Jesus answering said unto them, Go and tell John what ye have seen and heard: that the blind recover sight, the lame walk, lepers are cleansed, the deaf hear, the dead are raised, the poor have the gospel preached to them,
23 Amebarikiwa mtu yule asiyechukizwa na mimi.”
and happy is he who shall not be offended at any thing in me.
24 Wajumbe wa Yohana walipoondoka, Yesu akaanza kusema na makutano kuhusu Yohana Mbatizaji. Akawauliza, “Mlipokwenda kule nyikani, mlikwenda kuona nini? Je, ni unyasi ukipeperushwa na upepo?
When the messengers of John were departed, He began to speak unto the people concerning John, what went ye out into the wilderness to see?
25 Kama sivyo, mlikwenda kuona nini basi? Mtu aliyevaa mavazi ya kifahari? La hasha, watu wanaovaa mavazi ya kifahari na kuishi maisha ya anasa wako katika majumba ya kifalme.
a reed shaken by the wind? but what did ye go out to see? a man clothed in soft raiment? behold, they that are dressed in fine clothes and live delicately, are in palaces, not in deserts: but what went ye out to see?
26 Lakini mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, nawaambia, yeye ni zaidi ya nabii.
a prophet? yea, I say unto you, and much more than a prophet.
27 Huyu ndiye ambaye habari zake zimeandikwa: “‘Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako.’
This is he of whom it is written, "Behold I send my messenger before thy face, who shall prepare thy way before thee:"
28 Nawaambia, miongoni mwa wale waliozaliwa na wanawake, hakuna aliye mkuu kuliko Yohana. Lakini yeye aliye mdogo kabisa katika Ufalme wa Mungu ni mkuu kuliko Yohana.”
for I tell you that among the sons of men there is not a greater prophet than John the baptist: (though the least in the kingdom of God is greater than he: )
29 (Watu wote hata watoza ushuru waliposikia maneno ya Yesu, walikubali kwamba mpango wa Mungu ni haki, maana walikuwa wamebatizwa na Yohana.
---and all the people that heard him, even the publicans, justified God, being baptized with the baptism of John;
30 Lakini Mafarisayo na wataalamu wa sheria walikataa mpango wa Mungu kwao kwa kutokubali kubatizwa na Yohana.)
but the pharisees indeed and the lawyers rejected the counsel of God within themselves, and were not baptized by him.---
31 Yesu akawauliza, “Niwafananishe na nini watu wa kizazi hiki? Wanafanana na nini?
Whereunto therefore shall I compare the men of this generation?
32 Wao ni kama watoto waliokaa sokoni wakiitana wao kwa wao, wakisema: “‘Tuliwapigia filimbi, lakini hamkucheza; tuliwaimbia nyimbo za maombolezo, lakini hamkulia.’
and to what are they like? they are like children sitting in the market-place, and calling to one another, and saying, "We have played pleasant tunes to you, and ye have not danced; we have sung mournful ones and ye have not wept:"
33 Kwa maana Yohana Mbatizaji alikuja, alikuwa hali mkate wala hanywi divai, nanyi mkasema, ‘Yeye ana pepo mchafu.’
for John the baptist came neither eating bread, nor drinking wine, and ye say, he hath a demon:
34 Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa, nanyi mnasema: ‘Tazameni huyu mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na “wenye dhambi.”’
the Son of man is come eating and drinking like other men, and ye call Him a gluttonous man and a wine bibber, and a friend of publicans and sinners.
35 Nayo hekima huthibitishwa kuwa kweli na watoto wake wote.”
But wisdom is justified by all her children.
36 Basi Farisayo mmoja alimwalika Yesu nyumbani kwake kwa chakula. Hivyo Yesu akaenda nyumbani mwa yule Farisayo na kukaa katika nafasi yake mezani.
And one of the pharisees asked Him to eat with him: and He went into the pharisee's house, and sat down.
37 Naye mwanamke mmoja kwenye ule mji, ambaye alikuwa mwenye dhambi, alipojua kwamba Yesu alikuwa akila chakula nyumbani kwa yule Farisayo, akaleta chupa ya marhamu yenye manukato.
And behold a woman in the city, that was a sinner, when she knew that He was at table in the pharisee's house,
38 Yule mwanamke akasimama nyuma ya miguu ya Yesu akilia. Akailowanisha miguu yake kwa machozi yake, kisha akaifuta kwa nywele zake, akaibusu na kuimiminia manukato.
brought an alabaster-box of ointment, and stood at his feet behind Him, weeping, and washed his feet with tears, and wiped them with the hairs of her head, and kissed his feet, and anointed them with the ointment.
39 Yule Farisayo aliyemwalika Yesu alipoona yanayotendeka, akawaza moyoni mwake, “Kama huyu mtu angekuwa nabii, angejua kwamba ni nani anayemgusa, na kwamba yeye ni mwanamke wa namna gani, na ya kuwa huyu mwanamke ni mwenye dhambi.”
But when the pharisee that invited Him saw it, he said within himself, This man, if he were a prophet, would have known who and what sort of a woman this is that toucheth Him; for she is a notorious sinner.
40 Yesu akanena akamwambia, “Simoni, nina jambo la kukuambia.” Simoni akajibu, “Mwalimu, sema.”
And Jesus said unto him, Simon, I have something to say to thee: (and he replied, Master, say on.)
41 “Palikuwa na mtu mmoja aliyewakopesha watu wawili fedha: Mmoja alidaiwa dinari 500na mwingine dinari hamsini.
A certain creditor had two debtors, the one owed him five hundred denaries, and the other fifty:
42 Wote wawili walipokuwa hawawezi kulipa, aliyafuta madeni yao wote wawili. Sasa ni yupi kati yao atakayempenda yule aliyewasamehe zaidi?”
and they not being able to pay him, he freely forgave them both: tell me therefore, which of them will love him most?
43 Simoni akajibu, “Nadhani ni yule aliyesamehewa deni kubwa zaidi.” Naye Yesu akamwambia, “Umehukumu kwa usahihi.”
And Simon answered, I suppose he to whom he forgave most. And Jesus said unto him, Thou hast rightly judged:
44 Kisha akamgeukia yule mwanamke, akamwambia Simoni, “Je, unamwona mwanamke huyu? Nilipoingia nyumbani mwako, hukunipa maji ya kunawa miguu yangu, lakini huyu ameninawisha miguu kwa machozi yake, na kunifuta kwa nywele zake.
and turning to the woman, He said to Simon, Dost thou see this woman? I came into thine house, and thou gavest me no water for my feet; but she has bathed my feet with her tears, and wiped them with the hairs of her head.
45 Hukunisalimu kwa busu, lakini huyu mwanamke hajaacha kuibusu miguu yangu tangu nilipoingia.
Thou gavest me not the respect of a kiss; but this woman, ever since she came in, hath not ceased to kiss my feet.
46 Hukunipaka mafuta kichwani mwangu, lakini yeye ameipaka miguu yangu manukato.
Thou didst not anoint my head with common oil, but she hath anointed even my feet with sweet ointment.
47 Kwa hiyo, nakuambia, dhambi zake zilizokuwa nyingi zimesamehewa, kwani ameonyesha upendo mwingi. Lakini yule aliyesamehewa kidogo, hupenda kidogo.”
Wherefore, I tell thee, her sins though many are forgiven, for she loved much: but he to whom little is forgiven, loveth but little.
48 Kisha akamwambia yule mwanamke, “Dhambi zako zimesamehewa.”
And He said unto her, Thy sins are forgiven.
49 Lakini wale waliokuwa wameketi pamoja naye chakulani wakaanza kusemezana wao kwa wao, “Huyu ni nani ambaye hata anasamehe dhambi?”
And they that sat at table with Him, said within themselves, Who is this that forgiveth sins also?
50 Yesu akamwambia yule mwanamke, “Imani yako imekuokoa; nenda kwa amani.”
But He said to the woman, Thy faith hath saved thee, go in peace.