< Luka 7 >
1 Baada ya Yesu kumaliza kusema haya yote watu wakiwa wanamsikiliza, akaingia Kapernaumu.
When he had finished his discourse in the audience of the people, he entered Capernaum.
2 Mtumishi wa jemadari mmoja wa Kirumi, ambaye bwana wake alimthamini sana, alikuwa mgonjwa sana karibu kufa.
And a centurion's servant, who was dear to his master, was sick, and in danger of dying.
3 Jemadari huyo aliposikia habari za Yesu, aliwatuma wazee wa Kiyahudi kwake, wakamwomba aje kumponya mtumishi wa huyo jemadari.
And the centurion, having heard concerning Jesus, sent to him Jewish elders, to entreat him to come and save his servant.
4 Wale wazee walipofika kwa Yesu, wakamsihi sana amsaidie yule jemadari wakisema, “Mtu huyu anastahili wewe umfanyie jambo hili,
When they came to Jesus, they earnestly besought him, saying, He is worthy of this favor;
5 kwa sababu analipenda taifa letu tena ametujengea sinagogi.”
for he loves our nations; and it was he who built our synagogue.
6 Hivyo Yesu akaongozana nao, lakini alipokuwa hayuko mbali na nyumbani, yule jemadari akatuma rafiki zake kumwambia Yesu, “Bwana, usijisumbue, kwani mimi sistahili wewe kuingia chini ya dari yangu.
Then Jesus went with them; and when he was not far from the house, the centurion sent friends to him, to say, Master, trouble not yourself; for I have not deserved that you should come under my roof;
7 Ndiyo maana sikujiona hata ninastahili kuja kwako wewe. Lakini sema neno tu, naye mtumishi wangu atapona.
wherefore neither thought I myself fit to come into your presence; say but the word, and my servant will be healed.
8 Kwa kuwa mimi mwenyewe ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, nikiwa na askari chini yangu. Nikimwambia huyu, ‘Nenda,’ yeye huenda; na mwingine nikimwambia, ‘Njoo,’ yeye huja. Nikimwambia mtumishi wangu, ‘Fanya hivi,’ yeye hufanya.”
For even I, who am under the authority of others, having soldiers under me, say to one, Go, and he goes; to another, Come, and he comes; and to my servant, Do this, and he does it.
9 Yesu aliposikia maneno haya, alishangazwa naye sana. Akaugeukia ule umati wa watu uliokuwa unamfuata, akawaambia, “Sijaona imani kubwa namna hii hata katika Israeli.”
Jesus hearing these things, admired him, and turning, said to the multitude which followed, I assure you, I have not found so great faith even in Israel.
10 Nao wale watu waliokuwa wametumwa kwa Yesu waliporudi nyumbani walimkuta yule mtumishi amepona.
And they who had been sent, having returned to the house, found the servant well, who had been sick.
11 Baadaye kidogo, Yesu alikwenda katika mji mmoja ulioitwa Naini. Nao wanafunzi wake na umati mkubwa wa watu walikwenda pamoja naye.
The day following, he went into a city called Nain, accompanied by his disciples, and a great crowd.
12 Alipokaribia lango la mji, alikutana na watu waliokuwa wamebeba maiti wakitoka nje ya mji. Huyu aliyekufa alikuwa mwana pekee wa mwanamke mjane. Umati mkubwa wa watu wa mji ule ulikuwa pamoja na huyo mwanamke.
As he approached the gate of the city, the people were carrying out a dead man, the only son of his mother, who was a widow; and many of the citizens were with her.
13 Bwana Yesu alipomwona yule mjane, moyo wake ulimhurumia, akamwambia, “Usilie.”
When the Lord saw her, he had pity upon her, and said to her, Weep not.
14 Kisha akasogea mbele akaligusa lile jeneza na wale waliokuwa wamelibeba wakasimama kimya. Akasema, “Kijana, nakuambia inuka.”
Then he advanced and touched the bier, (the bearers stopping, ) and said, Young man, arise, I command you.
15 Yule aliyekuwa amekufa akaketi akaanza kuongea, naye Yesu akamkabidhi kwa mama yake.
Then he who had been dead, sat up, and began to speak, and he delivered him to his mother.
16 Watu wote wakajawa na hofu ya Mungu, nao wakamtukuza Mungu wakisema, “Nabii mkuu ametokea miongoni mwetu, Mungu amekuja kuwakomboa watu wake.”
And all present were struck with awe, and glorified God, saying, A great prophet has arisen among us; and God has visited his people.
17 Habari hizi za mambo aliyoyafanya Yesu zikaenea Uyahudi wote na sehemu zote za jirani.
And this report, concerning him, spread throughout Judea, and all the neighboring country.
18 Wanafunzi wa Yohana Mbatizaji wakamweleza Yohana mambo haya yote. Hivyo Yohana akawaita wanafunzi wake wawili
Now John's disciples had informed him of all these things,
19 na kuwatuma kwa Bwana ili kumuuliza, “Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?”
and he called two of them, whom he sent to Jesus, to ask him, Are you He who comes, or must we expect another?
20 Wale watu walipofika kwa Yesu wakamwambia, “Yohana Mbatizaji ametutuma tukuulize, ‘Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?’”
Being come to him, they said, John the Immerser has sent us to ask you, Are you He who comes, or must we expect another?
21 Wakati huo huo, Yesu aliwaponya wengi waliokuwa na magonjwa, maradhi na pepo wachafu, na pia akawafungua vipofu wengi macho wakapata kuona.
At that very time Jesus was delivering man from diseases and maladies, and evil spirits, and giving sight to many, who were blind.
22 Hivyo akawajibu wale wajumbe, “Rudini mkamwambie Yohana yote mnayoyaona na kuyasikia: Vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa na maskini wanahubiriwa habari njema.
And he returned this answer, Go, and report to John what you have seen and heard: the blind are made to see, the lame to walk, the deaf to hear; the leprous are cleansed, the dead are raised, glad tidings are brought to the poor.
23 Amebarikiwa mtu yule asiyechukizwa na mimi.”
And happy is he to whom I shall not prove a stumbling block.
24 Wajumbe wa Yohana walipoondoka, Yesu akaanza kusema na makutano kuhusu Yohana Mbatizaji. Akawauliza, “Mlipokwenda kule nyikani, mlikwenda kuona nini? Je, ni unyasi ukipeperushwa na upepo?
When John's messengers were departed, Jesus said to the multitude, concerning John, What did you go out into the wilderness to behold? A reed shaken by the wind?
25 Kama sivyo, mlikwenda kuona nini basi? Mtu aliyevaa mavazi ya kifahari? La hasha, watu wanaovaa mavazi ya kifahari na kuishi maisha ya anasa wako katika majumba ya kifalme.
But what did you go out to see? A man effeminately dressed? It is in royal palaces that they who wear splendid apparel, and live in luxury, are found.
26 Lakini mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, nawaambia, yeye ni zaidi ya nabii.
What then did you go to see? a prophet? Yes, I tell you, and something superior to a prophet.
27 Huyu ndiye ambaye habari zake zimeandikwa: “‘Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako.’
For this is he, concerning whom it is written, "Behold, I send my messenger before you, who shall prepare your way."
28 Nawaambia, miongoni mwa wale waliozaliwa na wanawake, hakuna aliye mkuu kuliko Yohana. Lakini yeye aliye mdogo kabisa katika Ufalme wa Mungu ni mkuu kuliko Yohana.”
For I declare to you, among those who are born of women, there is not a greater prophet than John the Immerser; yet, the least in the Reign of God is greater than he.
29 (Watu wote hata watoza ushuru waliposikia maneno ya Yesu, walikubali kwamba mpango wa Mungu ni haki, maana walikuwa wamebatizwa na Yohana.
All the people, even the publicans, who heard John, have, by receiving immersion from him, honored God;
30 Lakini Mafarisayo na wataalamu wa sheria walikataa mpango wa Mungu kwao kwa kutokubali kubatizwa na Yohana.)
whereas, the Pharisees and the lawyers, in not being immersed by him, have rejected the counsel of God with regard to themselves.
31 Yesu akawauliza, “Niwafananishe na nini watu wa kizazi hiki? Wanafanana na nini?
To what shall I compare the men of this generation? Whom are they like?
32 Wao ni kama watoto waliokaa sokoni wakiitana wao kwa wao, wakisema: “‘Tuliwapigia filimbi, lakini hamkucheza; tuliwaimbia nyimbo za maombolezo, lakini hamkulia.’
They are like children in the market place, of whom their companions complain, and say, We have played to you upon the pipe, but you have not danced; we have sung mournful songs to you, but you have not wept.
33 Kwa maana Yohana Mbatizaji alikuja, alikuwa hali mkate wala hanywi divai, nanyi mkasema, ‘Yeye ana pepo mchafu.’
For John the Immerser is come, abstaining from bread and wine, an associate of publicans and sinners; and you say, He has a demon.
34 Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa, nanyi mnasema: ‘Tazameni huyu mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na “wenye dhambi.”’
The Son of Man is come, using both; and you say, He is a lover of banquets, and wine, an associate of publicans and sinners.
35 Nayo hekima huthibitishwa kuwa kweli na watoto wake wote.”
But wisdom is justified by all her children.
36 Basi Farisayo mmoja alimwalika Yesu nyumbani kwake kwa chakula. Hivyo Yesu akaenda nyumbani mwa yule Farisayo na kukaa katika nafasi yake mezani.
Now one of the Pharisees asked Jesus to eat with him: and he went into the Pharisee's house, and placed himself at table.
37 Naye mwanamke mmoja kwenye ule mji, ambaye alikuwa mwenye dhambi, alipojua kwamba Yesu alikuwa akila chakula nyumbani kwa yule Farisayo, akaleta chupa ya marhamu yenye manukato.
And behold, a woman of the city who was a sinner, knowing that he eat at the house of the Pharisee, brought an alabaster box of balsam,
38 Yule mwanamke akasimama nyuma ya miguu ya Yesu akilia. Akailowanisha miguu yake kwa machozi yake, kisha akaifuta kwa nywele zake, akaibusu na kuimiminia manukato.
and standing behind at his feet weeping, bathed them with tears, and wiped them with the hairs of her head, and kissed his feet, and anointed them with the balsam.
39 Yule Farisayo aliyemwalika Yesu alipoona yanayotendeka, akawaza moyoni mwake, “Kama huyu mtu angekuwa nabii, angejua kwamba ni nani anayemgusa, na kwamba yeye ni mwanamke wa namna gani, na ya kuwa huyu mwanamke ni mwenye dhambi.”
The Pharisee, who had invited him, observing this, said within himself, If this man were a prophet, he would have known who this woman is that touches him, and of what character, for she is a sinner.
40 Yesu akanena akamwambia, “Simoni, nina jambo la kukuambia.” Simoni akajibu, “Mwalimu, sema.”
Then Jesus said to him, Simon, I have something to say to you. He answered, Say it, Rabbi.
41 “Palikuwa na mtu mmoja aliyewakopesha watu wawili fedha: Mmoja alidaiwa dinari 500na mwingine dinari hamsini.
A certain creditor had two debtors; one owed five hundred denarii, the other fifty.
42 Wote wawili walipokuwa hawawezi kulipa, aliyafuta madeni yao wote wawili. Sasa ni yupi kati yao atakayempenda yule aliyewasamehe zaidi?”
But not having the means to pay, he freely forgave them both. Say, then, which of them will love him most?
43 Simoni akajibu, “Nadhani ni yule aliyesamehewa deni kubwa zaidi.” Naye Yesu akamwambia, “Umehukumu kwa usahihi.”
Simon answered, I suppose he whom he forgave most? Jesus replied, You have judged right.
44 Kisha akamgeukia yule mwanamke, akamwambia Simoni, “Je, unamwona mwanamke huyu? Nilipoingia nyumbani mwako, hukunipa maji ya kunawa miguu yangu, lakini huyu ameninawisha miguu kwa machozi yake, na kunifuta kwa nywele zake.
Then turning to the woman, he said, Simon, Do you see this woman? When I came to your house, you gave me no water for my feet; but she has washed my feet with tears, and wiped them with her hair.
45 Hukunisalimu kwa busu, lakini huyu mwanamke hajaacha kuibusu miguu yangu tangu nilipoingia.
You gave me no kiss; but she, since she entered, has not ceased kissing my feet.
46 Hukunipaka mafuta kichwani mwangu, lakini yeye ameipaka miguu yangu manukato.
You did not anoint my head with oil; but she has anointed my feet with balsam.
47 Kwa hiyo, nakuambia, dhambi zake zilizokuwa nyingi zimesamehewa, kwani ameonyesha upendo mwingi. Lakini yule aliyesamehewa kidogo, hupenda kidogo.”
Wherefore, I tell you, her sins, which are many, are forgiven; therefore, her love is great. But he to whom little is forgiven, has little love.
48 Kisha akamwambia yule mwanamke, “Dhambi zako zimesamehewa.”
Then he said to her, Your sins are forgiven.
49 Lakini wale waliokuwa wameketi pamoja naye chakulani wakaanza kusemezana wao kwa wao, “Huyu ni nani ambaye hata anasamehe dhambi?”
Those, who were at table with him, said within themselves, Who is this, that even forgives sins?
50 Yesu akamwambia yule mwanamke, “Imani yako imekuokoa; nenda kwa amani.”
But he said to the woman, Your faith has saved you, go in peace.