< Luka 7 >

1 Baada ya Yesu kumaliza kusema haya yote watu wakiwa wanamsikiliza, akaingia Kapernaumu.
Jesuh naw ngthu pyen law päng lü Kapenawma citki.
2 Mtumishi wa jemadari mmoja wa Kirumi, ambaye bwana wake alimthamini sana, alikuwa mgonjwa sana karibu kufa.
Acunüng Romah ngvai naw a jawngnaka m'ya mat thi law hlü khaia a mhnat awmki.
3 Jemadari huyo aliposikia habari za Yesu, aliwatuma wazee wa Kiyahudi kwake, wakamwomba aje kumponya mtumishi wa huyo jemadari.
Jesuha mawng a ngjak üng, a m'ya mdaw law be khaia, Jesuh va nghui na u lü, khü khai hea, Judah ngvai he a jah tüih.
4 Wale wazee walipofika kwa Yesu, wakamsihi sana amsaidie yule jemadari wakisema, “Mtu huyu anastahili wewe umfanyie jambo hili,
Jesuha veia law u lü aktäa nghui naki he naw, “Hina khyang ta na kpüi vaia ngkawi ve,
5 kwa sababu analipenda taifa letu tena ametujengea sinagogi.”
ani cun mi khyang he jah jawng na lü, Sinakok pi jah sak peki ni,” ami ti.
6 Hivyo Yesu akaongozana nao, lakini alipokuwa hayuko mbali na nyumbani, yule jemadari akatuma rafiki zake kumwambia Yesu, “Bwana, usijisumbue, kwani mimi sistahili wewe kuingia chini ya dari yangu.
Acuna Jesuh ami veia citki. Acunüng a pha law tawm tawm la Romah ngvai naw a püi he jah tüi lü, “Bawipa aw, ka im na luhnak ngkawi vaia am kya ve, ä kha heia,
7 Ndiyo maana sikujiona hata ninastahili kuja kwako wewe. Lakini sema neno tu, naye mtumishi wangu atapona.
acunakyase, na veia ka law vaia pi ka ngkawikia am ngai kyu veng, ngthu däng pyen lü, ka m'ya daw be khai ni.
8 Kwa kuwa mimi mwenyewe ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, nikiwa na askari chini yangu. Nikimwambia huyu, ‘Nenda,’ yeye huenda; na mwingine nikimwambia, ‘Njoo,’ yeye huja. Nikimwambia mtumishi wangu, ‘Fanya hivi,’ yeye hufanya.”
“Isetiakyaküng, kei haw anaa takia keha ka awmki. Ka keha yekap he awmki he, mat am ‘cita’ ka ti üng citki, akce mat am ‘lawa’ ka ti üng lawki, ka m'ya am hin pawha ka ti üng pawhki,” a ti.
9 Yesu aliposikia maneno haya, alishangazwa naye sana. Akaugeukia ule umati wa watu uliokuwa unamfuata, akawaambia, “Sijaona imani kubwa namna hii hata katika Israeli.”
Jesuh naw acun a ngjak üng, cäieiki naw, mang hü lü, amät läkia khyang he üng, “Isarel he üng pi ahikba sena jumeiki am hmu khawi nawng,” a ti.
10 Nao wale watu waliokuwa wametumwa kwa Yesu waliporudi nyumbani walimkuta yule mtumishi amepona.
A khyang tüihe ima ami ceh be üng, m'ya cun daw be se ami hmuh.
11 Baadaye kidogo, Yesu alikwenda katika mji mmoja ulioitwa Naini. Nao wanafunzi wake na umati mkubwa wa watu walikwenda pamoja naye.
Acun käna Jesuh Nai ami tia mlüha cit se, axüisaw he la khyang khawjah a veia cit hngaki he.
12 Alipokaribia lango la mji, alikutana na watu waliokuwa wamebeba maiti wakitoka nje ya mji. Huyu aliyekufa alikuwa mwana pekee wa mwanamke mjane. Umati mkubwa wa watu wa mji ule ulikuwa pamoja na huyo mwanamke.
Mlüh mkawt pei a pha law üng, hmeinu naw mat däng a canak, khyang kthi ami yawknak kawt law u se, mlüh üngka he khawjah law hngaki he.
13 Bwana Yesu alipomwona yule mjane, moyo wake ulimhurumia, akamwambia, “Usilie.”
Acunüng, Bawipa naw acuna hmeinu a hmuh üng, m'yenei leng leng lü, “Ä kyapa” a ti.
14 Kisha akasogea mbele akaligusa lile jeneza na wale waliokuwa wamelibeba wakasimama kimya. Akasema, “Kijana, nakuambia inuka.”
Jesuh naw law lü, yawkkawng hnet se, kawtki he ngdüiki he. Acunüng Jesuh naw, “Cawngpyang, tho law, ti veng,” ti se,
15 Yule aliyekuwa amekufa akaketi akaanza kuongea, naye Yesu akamkabidhi kwa mama yake.
akthi cun tho law lü ngthuhei law se, Jesuh naw a nu üng a pet.
16 Watu wote wakajawa na hofu ya Mungu, nao wakamtukuza Mungu wakisema, “Nabii mkuu ametokea miongoni mwetu, Mungu amekuja kuwakomboa watu wake.”
Acunüng, ami van kyü lawki he naw, Pamhnam mküimto u lü, “Mi ksunga sahma akyäp awm law ve; Pamhnam a khyang he jah küikyan khaia law ve,” ami ti.
17 Habari hizi za mambo aliyoyafanya Yesu zikaenea Uyahudi wote na sehemu zote za jirani.
Acuna Jesuha mawng cun khaw avan la a pipeia hne avan üng ngthang hüki.
18 Wanafunzi wa Yohana Mbatizaji wakamweleza Yohana mambo haya yote. Hivyo Yohana akawaita wanafunzi wake wawili
Johana axüisaw he naw acuna mawng avan cun Johan üng ami mtheh.
19 na kuwatuma kwa Bwana ili kumuuliza, “Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?”
Acunüng, Johan naw axüisaw nghngih jah khüki naw, Bawipa veia jah tüi lü, “Johan naw law khai a tia khyanga na kyaki aw? Akce kami na äpei khai aw?” tia a jah va kthähsak.
20 Wale watu walipofika kwa Yesu wakamwambia, “Yohana Mbatizaji ametutuma tukuulize, ‘Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?’”
Acunüng, Jesuh veia law u lü, “Law khai mata na kyaki aw? Akce kami na äpei khai aw? tia ni kthäh vaia baptican Johan naw na veia a jah tüih law ni,” ami ti.
21 Wakati huo huo, Yesu aliwaponya wengi waliokuwa na magonjwa, maradhi na pepo wachafu, na pia akawafungua vipofu wengi macho wakapata kuona.
Acunapät üng Jesuh naw, a jah huieie, natnak khihlau akce kcea jah awmnak he, ngmüimkhya ksea awmnak he khawjah jah mdaw be lü, amikmü khawjah a jah mdeisak be.
22 Hivyo akawajibu wale wajumbe, “Rudini mkamwambie Yohana yote mnayoyaona na kuyasikia: Vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa na maskini wanahubiriwa habari njema.
Jesuh naw, “Citbe u lü, nami hmuh la nami sim he Johan üng jah va mtheh ua; amikmüe mdei law be ve u, akhawkxo he ami khaw am cit ve u, mnehkse mnehkie ngcim be ve u, ami nghnga kpangki he pi ami nghnga ngjang be ve u, akthi he xüng law be ve u, khuikha m’yetsekiea veia thangkdaw sanga kya ve.
23 Amebarikiwa mtu yule asiyechukizwa na mimi.”
“Upi, keia phäha, a mlung am hlawtlatki ta a jo sen ve,” a ti.
24 Wajumbe wa Yohana walipoondoka, Yesu akaanza kusema na makutano kuhusu Yohana Mbatizaji. Akawauliza, “Mlipokwenda kule nyikani, mlikwenda kuona nini? Je, ni unyasi ukipeperushwa na upepo?
Johana xüisaw he ami ktawih be käna, Jesuh naw Johana mawng khyang he üng jah mtheh lü, “Johana veia, khawkhyawng khawa nami ceh üng, i teng khaia ni nami ceh? Khawkhia aksün khuhlip teng khaia aw nami ceh?
25 Kama sivyo, mlikwenda kuona nini basi? Mtu aliyevaa mavazi ya kifahari? La hasha, watu wanaovaa mavazi ya kifahari na kuishi maisha ya anasa wako katika majumba ya kifalme.
“Am acunüng i teng khaia ni nami ceh? Suisak akdaw suisaki teng khaia aw nami ceh? Suisak akdaw suisaki he cun sangpuxang hea ima ni ami awm khawi.
26 Lakini mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, nawaambia, yeye ni zaidi ya nabii.
“Am acunüng sahma teng khaia aw nami ceh? Ä, ka ning jah mtheki, sahmaa kthaka pi kyäp bawki hia awm ve,
27 Huyu ndiye ambaye habari zake zimeandikwa: “‘Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako.’
cangcim naw ‘Ngaia ka khyang na ma ka tüih, ani naw na maa lam pyang khai’ tia a mawng ami yuk cen ahina Johan ni.
28 Nawaambia, miongoni mwa wale waliozaliwa na wanawake, hakuna aliye mkuu kuliko Yohana. Lakini yeye aliye mdogo kabisa katika Ufalme wa Mungu ni mkuu kuliko Yohana.”
“Ka ning jah mthehki, nghnumi hea ca avan üng Johana kyäp bawki sahma am awm naw; cunsepi, Pamhnama khawa akjaw säih pi Johana kthaka kyäp bawki ni,” a ti.
29 (Watu wote hata watoza ushuru waliposikia maneno ya Yesu, walikubali kwamba mpango wa Mungu ni haki, maana walikuwa wamebatizwa na Yohana.
Acunüng, khyang avan naw ami ngjak; aktunga ngcawnklawk he cun Pamhnama ngsungpyunak vaia Johana baptican khanki he.
30 Lakini Mafarisayo na wataalamu wa sheria walikataa mpango wa Mungu kwao kwa kutokubali kubatizwa na Yohana.)
Cunsepi, Pharise he la, thum mksingki he naw, ami hama Pamhnama pyan ma u lü, Johana baptican ä khanki he.
31 Yesu akawauliza, “Niwafananishe na nini watu wa kizazi hiki? Wanafanana na nini?
Jesuh naw pyen be tü lü, “Tuhkbäiha ngsawn he hin i am ni ka jah msuimcäp kawm? Ia mäih ni ami law?
32 Wao ni kama watoto waliokaa sokoni wakiitana wao kwa wao, wakisema: “‘Tuliwapigia filimbi, lakini hamkucheza; tuliwaimbia nyimbo za maombolezo, lakini hamkulia.’
“Ahin he cun Anghmawe jawihtuknaka ngawki he, ngkhü kyu u lü, ‘Cambumak pülün ning jah tum pe ung se am nami nglamki, yawk la sa ung se pi am nami kyapki’ ti am tängki he.
33 Kwa maana Yohana Mbatizaji alikuja, alikuwa hali mkate wala hanywi divai, nanyi mkasema, ‘Yeye ana pepo mchafu.’
“Baptican Johan a law üng ei nghmü lü capyitui am aw se, ‘khawyaia awmnak’ nami tiki.
34 Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa, nanyi mnasema: ‘Tazameni huyu mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na “wenye dhambi.”’
“Khyanga Capa law lü ei aw se, ‘Teng u, eiaw aih ve, ngcawnklawk he la khyang kse hea püi cen’ nami tiki.
35 Nayo hekima huthibitishwa kuwa kweli na watoto wake wote.”
“Mhnama ksingkhyapnak cun dokhameiki he naw a cangnak mdangki he ni,” a ti.
36 Basi Farisayo mmoja alimwalika Yesu nyumbani kwake kwa chakula. Hivyo Yesu akaenda nyumbani mwa yule Farisayo na kukaa katika nafasi yake mezani.
Pharise mat naw a veia buh ei khaia khü se, Jesuh Pharisea ima lut lü buh ei khaia ngawki.
37 Naye mwanamke mmoja kwenye ule mji, ambaye alikuwa mwenye dhambi, alipojua kwamba Yesu alikuwa akila chakula nyumbani kwa yule Farisayo, akaleta chupa ya marhamu yenye manukato.
Acuna mlüh üng nghnumi kse mat awmki naw Pharisea ima Jesuh buh ei lü awmki ti, a ksing üng, alabasta um üng situi ngui lawpüiki naw,
38 Yule mwanamke akasimama nyuma ya miguu ya Yesu akilia. Akailowanisha miguu yake kwa machozi yake, kisha akaifuta kwa nywele zake, akaibusu na kuimiminia manukato.
Jesuha hnu, a khaw kunga kyap lü ngdüiki. A miktui naw a khawpha msüi se, a lusam am xüt lü, a khawpha mhnamki naw, situi ng'ui am a hluk.
39 Yule Farisayo aliyemwalika Yesu alipoona yanayotendeka, akawaza moyoni mwake, “Kama huyu mtu angekuwa nabii, angejua kwamba ni nani anayemgusa, na kwamba yeye ni mwanamke wa namna gani, na ya kuwa huyu mwanamke ni mwenye dhambi.”
Pharise naw hmu lü, a mlung k'uma, “Hin hin sahma kcanga a kya vai sü, hnetkia nghnuminu hin u ni, ia mäih ni ti ksing khai sü. Khyangka kyalang se,” a ti.
40 Yesu akanena akamwambia, “Simoni, nina jambo la kukuambia.” Simoni akajibu, “Mwalimu, sema.”
Jesuh naw, “Sihmon, na veia ngthu mat ka pyen vai awm ve,” ti lü a msang. Acunüng Sihmon naw, “Saja aw pyena,” a ti.
41 “Palikuwa na mtu mmoja aliyewakopesha watu wawili fedha: Mmoja alidaiwa dinari 500na mwingine dinari hamsini.
Jesuh naw, “Ngui jah kpuki, mat naw, khyang nghngih üng ngui a jah kpu; mat üng phya mhma a kpu, mat am mhmakip a kpu.
42 Wote wawili walipokuwa hawawezi kulipa, aliyafuta madeni yao wote wawili. Sasa ni yupi kati yao atakayempenda yule aliyewasamehe zaidi?”
“Ani thungnak be vai am ta ni se, ani nghngih a jah mhlät. Acunüng, acun xawi üng u naw jawng na bawk khai ni?” a ti.
43 Simoni akajibu, “Nadhani ni yule aliyesamehewa deni kubwa zaidi.” Naye Yesu akamwambia, “Umehukumu kwa usahihi.”
Sihmon naw, “A mhlät däm naw jawng na bawk khaia ngai veng,” ti lü, msang se, Jesuh naw, “Cang veki,” a ti.
44 Kisha akamgeukia yule mwanamke, akamwambia Simoni, “Je, unamwona mwanamke huyu? Nilipoingia nyumbani mwako, hukunipa maji ya kunawa miguu yangu, lakini huyu ameninawisha miguu kwa machozi yake, na kunifuta kwa nywele zake.
Acunüng, nghnumi nghlat si lü, Sihmona veia, “Hina nghnuminu na hmuki aw? Na ima lut law ni se, ka khaw ka mthinak vaia tui am na na peki, hina nghnuminu naw a miktui am ka khaw mthi lü, a lusam am xütki.
45 Hukunisalimu kwa busu, lakini huyu mwanamke hajaacha kuibusu miguu yangu tangu nilipoingia.
“Nang naw am na na mhnamki, hina nghnumi naw ka luh law üng tün lü ka khawpha am pyai lü mhnamki.
46 Hukunipaka mafuta kichwani mwangu, lakini yeye ameipaka miguu yangu manukato.
“Nang naw ka lü situi am na hluki, hina nghnumi naw ka khawpha situi am hluki.
47 Kwa hiyo, nakuambia, dhambi zake zilizokuwa nyingi zimesamehewa, kwani ameonyesha upendo mwingi. Lakini yule aliyesamehewa kidogo, hupenda kidogo.”
“Acunakyase, ning mtheh veng, aktäa jawng nakia kyase, a katnak he khawjah cun mhlät pänga kya ve. A katnak ajaw däng mhlät naw ajawha jawng naki,” a ti.
48 Kisha akamwambia yule mwanamke, “Dhambi zako zimesamehewa.”
Acunüng, Jesuh naw nghnumi üng, “Na katnak he jah mhlät pänga kya ve,” a ti.
49 Lakini wale waliokuwa wameketi pamoja naye chakulani wakaanza kusemezana wao kwa wao, “Huyu ni nani ambaye hata anasamehe dhambi?”
Buh a eipüi he naw, “Katnak pi jah mhlätki hin u ni,” ami ti.
50 Yesu akamwambia yule mwanamke, “Imani yako imekuokoa; nenda kwa amani.”
Acunüng, Jesuh naw nghnumi üng, “Na jumnak naw ning küikyan ve, dim’yenak am cita,” a ti.

< Luka 7 >