< Luka 6 >

1 Ikawa siku moja ya Sabato Yesu alikuwa akipita katika mashamba ya nafaka, nao wanafunzi wake wakaanza kuvunja masuke ya nafaka, wakayafikicha kwa mikono yao na kula punje zake.
Or, le deuxième sabbat après le premier, il parcourait les champs de blé. Ses disciples arrachaient les épis et mangeaient en les frottant dans leurs mains.
2 Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya mambo yasiyo halali kufanywa siku ya Sabato?”
Mais quelques-uns des pharisiens leur dirent: « Pourquoi faites-vous ce qu'il n'est pas permis de faire le jour du sabbat? »
3 Yesu akawajibu, “Je, ninyi hamjasoma kamwe alivyofanya Daudi wakati yeye na wenzake walikuwa na njaa?
Jésus, prenant la parole, leur dit: « N'avez-vous pas lu ce que fit David quand il eut faim, lui et ceux qui étaient avec lui,
4 Aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akaichukua na kuila ile mikate iliyowekwa wakfu, ambayo ni halali kuliwa na makuhani peke yao. Naye pia akawapa wenzake.”
comment il entra dans la maison de Dieu, prit et mangea le pain de proposition, et en donna aussi à ceux qui étaient avec lui, ce qu'il n'est pas permis de manger, si ce n'est pour les prêtres seuls? »
5 Yesu akawaambia, “Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
Il leur répondit: « Le Fils de l'homme est maître du sabbat. »
6 Ikawa siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia ndani ya sinagogi na akawa anafundisha. Huko palikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
Un autre sabbat, il entra dans la synagogue et enseigna. Il y avait là un homme, dont la main droite était desséchée.
7 Mafarisayo na walimu wa sheria walikuwa wakitafuta sababu ya kumshtaki Yesu. Kwa hivyo wakawa wanamwangalia sana ili waone kama ataponya katika siku ya Sabato.
Les scribes et les pharisiens l'observaient, pour voir s'il ferait une guérison le jour du sabbat, afin de trouver une accusation contre lui.
8 Lakini Yesu alijua mawazo yao, hivyo akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka usimame mbele ya watu wote.” Hivyo yule mtu akainuka, akasimama mbele yao wote.
Mais Jésus connaissait leurs pensées, et il dit à l'homme qui avait la main desséchée: « Lève-toi et tiens-toi au milieu. » Il se leva et se tint debout.
9 Ndipo Yesu akawaambia wale walimu wa sheria na Mafarisayo, “Nawauliza ninyi, ni lipi lililo halali siku ya Sabato? Ni kutenda mema au kutenda mabaya? Ni kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
Alors Jésus leur dit: « Je vais vous poser une question: est-il permis, le jour du sabbat, de faire du bien ou de faire du mal? De sauver une vie, ou de tuer? »
10 Akawatazama watu wote waliokuwepo, kisha akamwambia yule aliyepooza mkono, “Nyoosha mkono wako!” Akaunyoosha na mkono wake ukaponywa kabisa.
Il les regarda tous, et dit à l'homme: « Étends ta main. » Il le fit, et sa main fut rendue aussi saine que l'autre.
11 Wale wakuu wakakasirika sana, wakashauriana wao kwa wao ni nini watakachomtendea Yesu.
Mais ils étaient remplis de rage, et ils parlaient entre eux de ce qu'ils pourraient faire à Jésus.
12 Ikawa katika siku hizo Yesu alikwenda mlimani kuomba, akakesha usiku kucha akimwomba Mungu.
En ces jours-là, il se rendit sur la montagne pour prier, et il passa toute la nuit à prier Dieu.
13 Kulipopambazuka, akawaita wanafunzi wake, naye akachagua kumi na wawili, ambao pia aliwaita mitume:
Le jour venu, il appela ses disciples, et il en choisit douze, qu'il appela aussi apôtres:
14 Simoni aliyemwita Petro, Andrea nduguye, Yakobo, Yohana, Filipo, Bartholomayo,
Simon, qu'il appela aussi Pierre; André, son frère; Jacques; Jean; Philippe; Barthélemy;
15 Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni aliyeitwa Zelote,
Matthieu; Thomas; Jacques, fils d'Alphée; Simon, appelé le Zélote;
16 Yuda mwana wa Yakobo, na Yuda Iskariote ambaye alikuwa msaliti.
Judas, fils de Jacques; et Judas Iscariote, qui devint aussi un traître.
17 Akashuka pamoja nao, akasimama mahali penye uwanja tambarare. Hapo palikuwa na idadi kubwa ya wanafunzi wake na umati mkubwa wa watu kutoka sehemu zote za Uyahudi, kutoka Yerusalemu, na kutoka pwani ya Tiro na Sidoni.
Il descendit avec eux et se tint sur un terrain plat, en compagnie d'une foule de ses disciples et d'un grand nombre de gens de toute la Judée, de Jérusalem et de la côte maritime de Tyr et de Sidon, qui venaient l'entendre et se faire guérir de leurs maladies,
18 Walikuwa wamekuja kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao. Wale waliokuwa wakiteswa na pepo wachafu akawaponya.
ainsi que de ceux qui étaient tourmentés par des esprits impurs; et ils étaient guéris.
19 Watu wote walikuwa wanajitahidi kumgusa kwa sababu nguvu zilikuwa zikimtoka na kuwaponya wote.
Toute la foule cherchait à le toucher, car une force sortait de lui et les guérissait tous.
20 Akawatazama wanafunzi wake, akasema: “Mmebarikiwa ninyi mlio maskini, kwa sababu Ufalme wa Mungu ni wenu.
Il leva les yeux vers ses disciples, et dit: « Heureux vous qui êtes pauvres, car le Royaume de Dieu est à vous.
21 Mmebarikiwa ninyi mlio na njaa sasa, kwa sababu mtashibishwa. Mmebarikiwa ninyi mnaolia sasa, kwa sababu mtacheka.
Heureux ceux qui ont faim maintenant, car vous serez comblé. Heureux êtes-vous ceux qui pleurent maintenant, car vous allez rire.
22 Mmebarikiwa ninyi, watu watakapowachukia, watakapowatenga na kuwatukana na kulikataa jina lenu kama neno ovu, kwa ajili ya Mwana wa Adamu.
Heureux es-tu quand les hommes te haïssent, quand ils t'excluent et se moquent de toi, et qu'ils jettent ton nom en pâture, à cause du Fils de l'homme.
23 “Furahini na kurukaruka kwa shangwe, kwa sababu thawabu yenu ni kubwa mbinguni, kwa kuwa hivyo ndivyo baba zao walivyowatenda manabii.
Réjouissez-vous en ce jour-là et tressaillez de joie, car voici que votre récompense est grande dans les cieux, car leurs pères ont agi de même envers les prophètes.
24 “Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, kwa sababu mmekwisha kupokea faraja yenu.
« Mais malheur à vous qui êtes riches! Car vous avez reçu votre consolation.
25 Ole wenu ninyi mlioshiba sasa, maana mtaona njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka sasa, maana mtaomboleza na kulia.
Malheur à vous, vous qui êtes rassasiés maintenant, car vous aurez faim. Malheur à vous qui riez maintenant, car vous serez en deuil et pleurerez.
26 Ole wenu watu watakapowasifu, kwani ndivyo baba zao walivyowasifu manabii wa uongo.
Malheur, quand les hommes disent du bien de toi, car leurs pères ont fait la même chose aux faux prophètes.
27 “Lakini nawaambia ninyi mnaonisikia: Wapendeni adui zenu. Watendeeni mema wanaowachukia.
« Mais moi, je vous dis, à vous qui m'écoutez: aimez vos ennemis, faites du bien à ceux qui vous haïssent,
28 Wabarikini wale wanaowalaani, waombeeni wale wanaowatendea mabaya.
bénissez ceux qui vous maudissent, et priez pour ceux qui vous maltraitent.
29 Kama mtu akikupiga shavu moja, mgeuzie na la pili pia. Mtu akikunyangʼanya koti lako, usimzuie kuchukua joho pia.
A celui qui te frappe sur la joue, présente aussi l'autre; et à celui qui te prend ton manteau, ne refuse pas aussi ta tunique.
30 Mpe kila akuombaye, na kama mtu akichukua mali yako usitake akurudishie.
Donne à quiconque te demande, et ne demande pas à celui qui te prive de tes biens de te les rendre.
31 Watendeeni wengine kama ambavyo mngetaka wawatendee ninyi.
« Comme vous voulez que les gens vous fassent, faites-leur exactement la même chose.
32 “Kama mkiwapenda tu wale wanaowapenda, mwapata sifa gani? Hata ‘wenye dhambi’ huwapenda wale wawapendao.
« Si vous aimez ceux qui vous aiment, en quoi cela vous honore-t-il? Car même les pécheurs aiment ceux qui les aiment.
33 Tena mkiwatendea mema wale tu wanaowatendea ninyi mema, mwapata sifa gani? Hata ‘wenye dhambi’ hufanya vivyo hivyo.
Si vous faites du bien à ceux qui vous font du bien, quel honneur cela vous fait-il? Car même les pécheurs font de même.
34 Tena mnapowakopesha wale tu mnaotegemea wawalipe, mwapata sifa gani? Hata ‘wenye dhambi’ huwakopesha ‘wenye dhambi’ wenzao wakitarajia kulipwa mali yao yote.
Si vous prêtez à ceux dont vous espérez recevoir, quel mérite avez-vous? Les pécheurs eux-mêmes prêtent aux pécheurs, pour en recevoir autant en retour.
35 Lakini wapendeni adui zenu, watendeeni mema, wakopesheni bila kutegemea kurudishiwa mlichokopesha. Ndipo thawabu yenu itakapokuwa kubwa, nanyi mtakuwa wana wa Aliye Juu Sana, kwa sababu yeye ni mwema kwa watu wasio na shukrani na kwa wale waovu.
Mais aimez vos ennemis, faites le bien, prêtez sans rien attendre en retour, et votre récompense sera grande, et vous serez les enfants du Très-Haut, car il est bon envers les ingrats et les méchants.
36 Kuweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.
« Soyez donc miséricordieux, comme votre Père est aussi miséricordieux.
37 “Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa. Msilaumu, nanyi hamtalaumiwa. Sameheni, nanyi mtasamehewa.
Ne jugez pas, et vous ne serez pas jugés. Ne condamnez pas, et tu ne seras pas condamné. Libérez-vous, et tu seras libéré.
38 Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa. Kipimo cha kujaa na kushindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile mpimacho, ndicho mtakachopimiwa.”
« Donnez, et l'on vous donnera: on vous donnera une bonne mesure, tassée, secouée et débordante. Car c'est avec la même mesure que vous mesurez qu'on vous mesurera. »
39 Pia akawapa mfano akasema, “Je, kipofu aweza kumwongoza kipofu? Je, wote wawili hawatatumbukia shimoni?
Il leur adressa une parabole. « Un aveugle peut-il guider un aveugle? Ne tomberont-ils pas tous deux dans une fosse?
40 Mwanafunzi hawezi kumzidi mwalimu wake, ila yule aliyehitimu aweza kuwa kama mwalimu wake.
Un disciple n'est pas au-dessus de son maître, mais chacun, lorsqu'il sera bien formé, sera comme son maître.
41 “Mbona unatazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, wala huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe?
Pourquoi vois-tu la paille qui est dans l'œil de ton frère, mais ne considères-tu pas la poutre qui est dans ton propre œil?
42 Utawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Ndugu yangu, acha nitoe kibanzi kilicho ndani ya jicho lako,’ wakati wewe mwenyewe huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako? Ewe mnafiki, ondoa boriti ndani ya jicho lako kwanza, ndipo utaweza kuona dhahiri jinsi ya kuondoa kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako.
Ou comment peux-tu dire à ton frère: « Mon frère, laisse-moi enlever la paille qui est dans ton œil », alors que tu ne vois pas toi-même la poutre qui est dans ton œil? Hypocrite! Enlève d'abord la poutre de ton œil, et alors tu pourras voir clairement pour enlever la paille qui est dans l'œil de ton frère.
43 “Hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala hakuna mti mbaya uzaao matunda mazuri.
« Car il n'y a pas de bon arbre qui produise des fruits pourris, ni d'arbre pourri qui produise de bons fruits.
44 Kila mti hujulikana kwa matunda yake. Kwa maana watu hawachumi tini kwenye miiba, wala zabibu kwenye michongoma.
Car on reconnaît chaque arbre à son fruit. Car on ne cueille pas des figues sur des épines, ni des raisins sur un buisson de ronces.
45 Vivyo hivyo mtu mwema hutoa mambo mema kutoka kwenye hazina ya moyo wake, naye mtu mwovu hutoa mambo maovu kutoka kwenye hazina ya moyo wake. Kwa kuwa mtu hunena kwa kinywa chake yale yaliyoujaza moyo wake.
L'homme bon tire du bon trésor de son cœur ce qui est bon, et l'homme mauvais tire du mauvais trésor de son cœur ce qui est mauvais, car c'est de l'abondance du cœur que parle la bouche.
46 “Kwa nini mnaniita, ‘Bwana, Bwana,’ nanyi hamfanyi ninayowaambia?
Pourquoi m'appelez-vous: « Seigneur, Seigneur », et ne faites-vous pas ce que je dis?
47 Nitawaonyesha jinsi alivyo mtu yule anayekuja kwangu na kusikia maneno yangu na kuyatenda.
Quiconque vient à moi, entend mes paroles et les met en pratique, je vous montrerai à qui il est semblable.
48 Yeye ni kama mtu aliyejenga nyumba, akachimba chini sana, na kuweka msingi kwenye mwamba. Mafuriko yalipokuja, maji ya ghafula yaliipiga ile nyumba, lakini haikutikisika, kwa sababu ilikuwa imejengwa vizuri.
Il est semblable à un homme qui construit une maison, qui a creusé et approfondi, et qui a posé le fondement sur le roc. Quand il y a eu une inondation, le torrent s'est jeté contre cette maison et n'a pu l'ébranler, parce qu'elle était fondée sur le roc.
49 Lakini yeye anayesikia maneno yangu wala asiyatende, ni kama mtu aliyejenga nyumba juu ya ardhi bila kuweka msingi. Mafuriko yalipoikumba nyumba ile, ikaanguka mara na kubomoka kabisa.”
Mais celui qui entend et ne fait pas, est semblable à un homme qui a bâti sur la terre une maison sans fondement, contre laquelle le torrent s'est brisé, et aussitôt elle est tombée; et la ruine de cette maison a été grande. »

< Luka 6 >