< Luka 6 >
1 Ikawa siku moja ya Sabato Yesu alikuwa akipita katika mashamba ya nafaka, nao wanafunzi wake wakaanza kuvunja masuke ya nafaka, wakayafikicha kwa mikono yao na kula punje zake.
And it came to pass on the second sabbath after the first, that he went through corn-fields; and his disciples plucked the ears of corn, and ate, rubbing [them] in [their] hands.
2 Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya mambo yasiyo halali kufanywa siku ya Sabato?”
And certain of the Pharisees said to them, Why do ye that which it is not lawful to do on the sabbath-days?
3 Yesu akawajibu, “Je, ninyi hamjasoma kamwe alivyofanya Daudi wakati yeye na wenzake walikuwa na njaa?
And Jesus answering them, said, Have ye not read so much as this, what David did, when himself was hungry, and they who were with him;
4 Aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akaichukua na kuila ile mikate iliyowekwa wakfu, ambayo ni halali kuliwa na makuhani peke yao. Naye pia akawapa wenzake.”
How he went into the house of God, and took and ate the show-bread, and gave also to them that were with him, which it is not lawful to eat but for the priests alone?
5 Yesu akawaambia, “Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
And he said to them, That the Son of man is Lord also of the sabbath.
6 Ikawa siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia ndani ya sinagogi na akawa anafundisha. Huko palikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
And it came to pass also on another sabbath, that he entered into the synagogue, and taught: and there was a man whose right hand was withered:
7 Mafarisayo na walimu wa sheria walikuwa wakitafuta sababu ya kumshtaki Yesu. Kwa hivyo wakawa wanamwangalia sana ili waone kama ataponya katika siku ya Sabato.
And the scribes and Pharisees watched him, [to see] whether he would heal on the sabbath; that they might find an accusation against him.
8 Lakini Yesu alijua mawazo yao, hivyo akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka usimame mbele ya watu wote.” Hivyo yule mtu akainuka, akasimama mbele yao wote.
But he knew their thoughts, and said to the man who had the withered hand, Rise, and stand forth in the midst. And he arose, and stood forth.
9 Ndipo Yesu akawaambia wale walimu wa sheria na Mafarisayo, “Nawauliza ninyi, ni lipi lililo halali siku ya Sabato? Ni kutenda mema au kutenda mabaya? Ni kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
Then said Jesus to them, I will ask you one thing; Is it lawful on the sabbath-days to do good, or to do evil? to save life, or to destroy [it]?
10 Akawatazama watu wote waliokuwepo, kisha akamwambia yule aliyepooza mkono, “Nyoosha mkono wako!” Akaunyoosha na mkono wake ukaponywa kabisa.
And looking around upon them all, he said to the man, Stretch forth thy hand. And he did so: and his hand was restored whole as the other.
11 Wale wakuu wakakasirika sana, wakashauriana wao kwa wao ni nini watakachomtendea Yesu.
And they were filled with madness; and communed one with another what they might do to Jesus.
12 Ikawa katika siku hizo Yesu alikwenda mlimani kuomba, akakesha usiku kucha akimwomba Mungu.
And it came to pass in those days, that he went out to a mountain to pray, and continued all night in prayer to God.
13 Kulipopambazuka, akawaita wanafunzi wake, naye akachagua kumi na wawili, ambao pia aliwaita mitume:
And when it was day, he called [to him] his disciples: and of them he chose twelve, whom also he named Apostles;
14 Simoni aliyemwita Petro, Andrea nduguye, Yakobo, Yohana, Filipo, Bartholomayo,
Simon (whom he also named Peter) and Andrew his brother, James and John, and Philip and Bartholomew,
15 Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni aliyeitwa Zelote,
Matthew and Thomas, James the [son] of Alpheus, and Simon called Zelotes,
16 Yuda mwana wa Yakobo, na Yuda Iskariote ambaye alikuwa msaliti.
And Judas [the brother] of James, and Judas Iscariot, who also was the traitor.
17 Akashuka pamoja nao, akasimama mahali penye uwanja tambarare. Hapo palikuwa na idadi kubwa ya wanafunzi wake na umati mkubwa wa watu kutoka sehemu zote za Uyahudi, kutoka Yerusalemu, na kutoka pwani ya Tiro na Sidoni.
And he came down with them, and stood in the plain; and the company of his disciples, and a great multitude of people out of all Judea and Jerusalem, and from the sea-coast of Tyre and Sidon, who came to hear him, and to be healed of their diseases;
18 Walikuwa wamekuja kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao. Wale waliokuwa wakiteswa na pepo wachafu akawaponya.
And they that were afflicted with unclean spirits: and they were healed.
19 Watu wote walikuwa wanajitahidi kumgusa kwa sababu nguvu zilikuwa zikimtoka na kuwaponya wote.
And the whole multitude sought to touch him; for there went virtue out of him, and healed [them] all.
20 Akawatazama wanafunzi wake, akasema: “Mmebarikiwa ninyi mlio maskini, kwa sababu Ufalme wa Mungu ni wenu.
And he lifted up his eyes on his disciples, and said, Blessed [are ye] poor: for yours is the kingdom of God.
21 Mmebarikiwa ninyi mlio na njaa sasa, kwa sababu mtashibishwa. Mmebarikiwa ninyi mnaolia sasa, kwa sababu mtacheka.
Blessed [are] ye that hunger now: for ye shall be filled. Blessed [are ye] that weep now: for ye shall laugh.
22 Mmebarikiwa ninyi, watu watakapowachukia, watakapowatenga na kuwatukana na kulikataa jina lenu kama neno ovu, kwa ajili ya Mwana wa Adamu.
Blessed are ye when men shall hate you, and when they shall separate you [from their company], and shall reproach [you], and cast out your name as evil, on account of the son of man.
23 “Furahini na kurukaruka kwa shangwe, kwa sababu thawabu yenu ni kubwa mbinguni, kwa kuwa hivyo ndivyo baba zao walivyowatenda manabii.
Rejoice ye in that day, and leap for joy: for behold, your reward [is] great in heaven: for in the like manner did their fathers to the prophets.
24 “Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, kwa sababu mmekwisha kupokea faraja yenu.
But woe to you that are rich! for ye have received your consolation.
25 Ole wenu ninyi mlioshiba sasa, maana mtaona njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka sasa, maana mtaomboleza na kulia.
Woe to you that are full! for ye shall hunger. Woe to you that laugh now! for ye shall mourn and weep.
26 Ole wenu watu watakapowasifu, kwani ndivyo baba zao walivyowasifu manabii wa uongo.
Woe to you, when all men shall speak well of you! for so did their fathers to the false prophets.
27 “Lakini nawaambia ninyi mnaonisikia: Wapendeni adui zenu. Watendeeni mema wanaowachukia.
But I say to you who hear, Love your enemies, do good to them who hate you,
28 Wabarikini wale wanaowalaani, waombeeni wale wanaowatendea mabaya.
Bless them that curse you, and pray for them who despitefully use you.
29 Kama mtu akikupiga shavu moja, mgeuzie na la pili pia. Mtu akikunyangʼanya koti lako, usimzuie kuchukua joho pia.
And to him that smiteth thee on the [one] cheek, offer also the other; and him that taketh away thy cloke, forbid not [to take thy] coat also.
30 Mpe kila akuombaye, na kama mtu akichukua mali yako usitake akurudishie.
Give to every man that asketh of thee; and of him that taketh away thy goods, ask [them] not again.
31 Watendeeni wengine kama ambavyo mngetaka wawatendee ninyi.
And as ye would that men should do to you, do ye also to them likewise.
32 “Kama mkiwapenda tu wale wanaowapenda, mwapata sifa gani? Hata ‘wenye dhambi’ huwapenda wale wawapendao.
For if ye love them who love you, what thanks have ye? for sinners also love those that love them.
33 Tena mkiwatendea mema wale tu wanaowatendea ninyi mema, mwapata sifa gani? Hata ‘wenye dhambi’ hufanya vivyo hivyo.
And if ye do good to them who do good to you, what thanks have ye? for sinners also do even the same.
34 Tena mnapowakopesha wale tu mnaotegemea wawalipe, mwapata sifa gani? Hata ‘wenye dhambi’ huwakopesha ‘wenye dhambi’ wenzao wakitarajia kulipwa mali yao yote.
And if ye lend [to them] from whom ye hope to receive, what thanks have ye? for sinners also lend to sinners, to receive as much in return.
35 Lakini wapendeni adui zenu, watendeeni mema, wakopesheni bila kutegemea kurudishiwa mlichokopesha. Ndipo thawabu yenu itakapokuwa kubwa, nanyi mtakuwa wana wa Aliye Juu Sana, kwa sababu yeye ni mwema kwa watu wasio na shukrani na kwa wale waovu.
But love ye your enemies, and do good, and lend, hoping for nothing again; and your reward shall be great, and ye shall be the children of the Highest: for he is kind to the unthankful and [to] the evil.
36 Kuweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.
Be ye therefore merciful, as your Father also is merciful.
37 “Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa. Msilaumu, nanyi hamtalaumiwa. Sameheni, nanyi mtasamehewa.
Judge not, and ye shall not be judged: condemn not, and ye shall not be condemned: forgive, and ye shall be forgiven:
38 Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa. Kipimo cha kujaa na kushindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile mpimacho, ndicho mtakachopimiwa.”
Give, and it shall be given to you; good measure, pressed down, and shaken together, and running over, shall men give into your bosom. For with the same measure that ye give [to others], it shall be measured to you again.
39 Pia akawapa mfano akasema, “Je, kipofu aweza kumwongoza kipofu? Je, wote wawili hawatatumbukia shimoni?
And he spoke a parable to them; Can the blind lead the blind? will they not both fall into the ditch?
40 Mwanafunzi hawezi kumzidi mwalimu wake, ila yule aliyehitimu aweza kuwa kama mwalimu wake.
The disciple is not above his master: but every one that is perfect, shall be as his master.
41 “Mbona unatazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, wala huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe?
And why beholdest thou the mote that is in thy brother's eye, but perceivest not the beam that is in thy own eye?
42 Utawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Ndugu yangu, acha nitoe kibanzi kilicho ndani ya jicho lako,’ wakati wewe mwenyewe huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako? Ewe mnafiki, ondoa boriti ndani ya jicho lako kwanza, ndipo utaweza kuona dhahiri jinsi ya kuondoa kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako.
Either how canst thou say to thy brother, Brother, let me pull out the mote that is in thy eye, when thou thyself beholdest not the beam that is in thy own eye? Thou hypocrite, cast out first the beam out of thy own eye, and then shalt thou see clearly to pull out the mote that is in thy brother's eye.
43 “Hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala hakuna mti mbaya uzaao matunda mazuri.
For a good tree bringeth not forth corrupt fruit; neither doth a corrupt tree bring forth good fruit.
44 Kila mti hujulikana kwa matunda yake. Kwa maana watu hawachumi tini kwenye miiba, wala zabibu kwenye michongoma.
For every tree is known by its own fruit: for from thorns men do not gather figs, nor from a bramble bush do they gather grapes.
45 Vivyo hivyo mtu mwema hutoa mambo mema kutoka kwenye hazina ya moyo wake, naye mtu mwovu hutoa mambo maovu kutoka kwenye hazina ya moyo wake. Kwa kuwa mtu hunena kwa kinywa chake yale yaliyoujaza moyo wake.
A good man out of the good treasure of his heart, bringeth forth that which is good; and an evil man out of the evil treasure of his heart, bringeth forth that which is evil: for from the abundance of the heart his mouth speaketh.
46 “Kwa nini mnaniita, ‘Bwana, Bwana,’ nanyi hamfanyi ninayowaambia?
And why call ye me Lord, Lord, and do not the things which I say?
47 Nitawaonyesha jinsi alivyo mtu yule anayekuja kwangu na kusikia maneno yangu na kuyatenda.
Whoever cometh to me, and heareth my sayings, and doeth them, I will show you to whom he is like.
48 Yeye ni kama mtu aliyejenga nyumba, akachimba chini sana, na kuweka msingi kwenye mwamba. Mafuriko yalipokuja, maji ya ghafula yaliipiga ile nyumba, lakini haikutikisika, kwa sababu ilikuwa imejengwa vizuri.
He is like a man who built a house, and digged deep, and laid the foundation on a rock: and when the flood arose, the stream beat vehemently upon that house, and could not shake it: for it was founded upon a rock.
49 Lakini yeye anayesikia maneno yangu wala asiyatende, ni kama mtu aliyejenga nyumba juu ya ardhi bila kuweka msingi. Mafuriko yalipoikumba nyumba ile, ikaanguka mara na kubomoka kabisa.”
But he that heareth, and doeth not, is like a man that, without a foundation, built a house on the earth, against which the stream beat vehemently, and immediately it fell, and the ruin of that house was great.