< Luka 6 >
1 Ikawa siku moja ya Sabato Yesu alikuwa akipita katika mashamba ya nafaka, nao wanafunzi wake wakaanza kuvunja masuke ya nafaka, wakayafikicha kwa mikono yao na kula punje zake.
IT was on the shabath, while Jeshu was walking among the corn, and his disciples gathered the ears, and rubbed in their hands and ate (them).
2 Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya mambo yasiyo halali kufanywa siku ya Sabato?”
But some of the Pharishee said to them, Why do you a thing which it is not lawful on the shabuth to do?
3 Yesu akawajibu, “Je, ninyi hamjasoma kamwe alivyofanya Daudi wakati yeye na wenzake walikuwa na njaa?
Jeshu answered and said to them, And this have you not read, what David did when he hungered, and they who were with him?
4 Aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akaichukua na kuila ile mikate iliyowekwa wakfu, ambayo ni halali kuliwa na makuhani peke yao. Naye pia akawapa wenzake.”
that he went into the house of Aloha, and the bread of the table of the Lord he took, ate, and gave to them who were with him, that (bread) which was not lawful to eat, except by the priests only?
5 Yesu akawaambia, “Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
And he said to them, That the Lord of the shabath is the Son of man.
6 Ikawa siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia ndani ya sinagogi na akawa anafundisha. Huko palikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
And it was on another shabath (that) he entered into the synagogue, and taught. And there was a man whose right hand was dried:
7 Mafarisayo na walimu wa sheria walikuwa wakitafuta sababu ya kumshtaki Yesu. Kwa hivyo wakawa wanamwangalia sana ili waone kama ataponya katika siku ya Sabato.
and the Sophree and Pharishee watched him, if he would heal on the shabath, that they might accuse him.
8 Lakini Yesu alijua mawazo yao, hivyo akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka usimame mbele ya watu wote.” Hivyo yule mtu akainuka, akasimama mbele yao wote.
But he knew their thoughts, and said to the man whose hand was dried, Rise (and) come into the midst of the assembly.
9 Ndipo Yesu akawaambia wale walimu wa sheria na Mafarisayo, “Nawauliza ninyi, ni lipi lililo halali siku ya Sabato? Ni kutenda mema au kutenda mabaya? Ni kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
And when he had come and stood, Jeshu said to them, I ask you which is lawful to do on the shabath, good or evil, life to save or to destroy?
10 Akawatazama watu wote waliokuwepo, kisha akamwambia yule aliyepooza mkono, “Nyoosha mkono wako!” Akaunyoosha na mkono wake ukaponywa kabisa.
And he beheld them all, and said to him, Stretch forth thine hand: and he stretched it forth, and his hand was restored as its fellow.
11 Wale wakuu wakakasirika sana, wakashauriana wao kwa wao ni nini watakachomtendea Yesu.
But they were filled with envy, and spake one with another what they should do with Jeshu.
12 Ikawa katika siku hizo Yesu alikwenda mlimani kuomba, akakesha usiku kucha akimwomba Mungu.
BUT it was in those days that Jeshu went forth into a mountain to pray; and there remained he all night in the prayer of Aloha.
13 Kulipopambazuka, akawaita wanafunzi wake, naye akachagua kumi na wawili, ambao pia aliwaita mitume:
And when the day brake, he called his disciples, and chose from them twelve, those whom he named Apostles,
14 Simoni aliyemwita Petro, Andrea nduguye, Yakobo, Yohana, Filipo, Bartholomayo,
Shemun, he whose name was Kipha, and Andreas his brother, and Jacub, and Juchanon, and Philipos, and Bar Tholmai,
15 Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni aliyeitwa Zelote,
and Mathai, and Thoma, and Jakub bar Chalphai, and Shemun who was called the Zealous,
16 Yuda mwana wa Yakobo, na Yuda Iskariote ambaye alikuwa msaliti.
and Jihuda bar Jakub, and Jihuda Scaruta, he who was the traitor.
17 Akashuka pamoja nao, akasimama mahali penye uwanja tambarare. Hapo palikuwa na idadi kubwa ya wanafunzi wake na umati mkubwa wa watu kutoka sehemu zote za Uyahudi, kutoka Yerusalemu, na kutoka pwani ya Tiro na Sidoni.
And Jeshu descended with them, and stood in the plain, and a great assembly of his disciples and a multitude of people from all Jehud, and from Urishlem, and from the sea-coast of Tsur and Tsaidon,
18 Walikuwa wamekuja kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao. Wale waliokuwa wakiteswa na pepo wachafu akawaponya.
who had come to hear his words, and to be healed of their diseases; and they who were vexed by unclean spirits, and they were healed.
19 Watu wote walikuwa wanajitahidi kumgusa kwa sababu nguvu zilikuwa zikimtoka na kuwaponya wote.
And all the multitudes sought to approach to him, for the power went forth from him, and all of them he healed.
20 Akawatazama wanafunzi wake, akasema: “Mmebarikiwa ninyi mlio maskini, kwa sababu Ufalme wa Mungu ni wenu.
AND he lifted up his eyes upon his disciples, and said, Blessed are you poor, for yours is the kingdom of Aloha.
21 Mmebarikiwa ninyi mlio na njaa sasa, kwa sababu mtashibishwa. Mmebarikiwa ninyi mnaolia sasa, kwa sababu mtacheka.
Blessed are you who hunger now, for you shall be satisfied. Blessed are you who weep now, for you shall laugh.
22 Mmebarikiwa ninyi, watu watakapowachukia, watakapowatenga na kuwatukana na kulikataa jina lenu kama neno ovu, kwa ajili ya Mwana wa Adamu.
Blessed are you when the sons of man hate you, and separate you, and revile you, and cast out your name as evil, for the sake of the Son of man.
23 “Furahini na kurukaruka kwa shangwe, kwa sababu thawabu yenu ni kubwa mbinguni, kwa kuwa hivyo ndivyo baba zao walivyowatenda manabii.
Rejoice in that day, and exult, for your reward is great in heaven; for thus did they to your fathers the prophets.
24 “Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, kwa sababu mmekwisha kupokea faraja yenu.
But woe to you (who are) rich, because you have received your consolation.
25 Ole wenu ninyi mlioshiba sasa, maana mtaona njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka sasa, maana mtaomboleza na kulia.
Woe to you (who are) full, for you shall hunger. Woe to you who laugh now, for you shall weep and lament.
26 Ole wenu watu watakapowasifu, kwani ndivyo baba zao walivyowasifu manabii wa uongo.
Woe to you when the sons of men shall speak well of you, for so did to the prophets of falsity their fathers.
27 “Lakini nawaambia ninyi mnaonisikia: Wapendeni adui zenu. Watendeeni mema wanaowachukia.
But I say to you who hear, Love your adversaries, and do good to those who hate you,
28 Wabarikini wale wanaowalaani, waombeeni wale wanaowatendea mabaya.
and bless those who execrate you, and pray for those who lead you by violence.
29 Kama mtu akikupiga shavu moja, mgeuzie na la pili pia. Mtu akikunyangʼanya koti lako, usimzuie kuchukua joho pia.
And to one who striketh you on your cheek, offer to him the other: and whosoever taketh your cloak, forbid him not your coat also.
30 Mpe kila akuombaye, na kama mtu akichukua mali yako usitake akurudishie.
To every one who asketh of you give; and from him who taketh of yours demand not (again).
31 Watendeeni wengine kama ambavyo mngetaka wawatendee ninyi.
And as you will that the sons of man should do to you, so do you also to them.
32 “Kama mkiwapenda tu wale wanaowapenda, mwapata sifa gani? Hata ‘wenye dhambi’ huwapenda wale wawapendao.
For if you love them who love you, what is your grace? for sinners also love those who love them.
33 Tena mkiwatendea mema wale tu wanaowatendea ninyi mema, mwapata sifa gani? Hata ‘wenye dhambi’ hufanya vivyo hivyo.
And if you do good to those who benefit you, what is your grace? for the sinners also thus do.
34 Tena mnapowakopesha wale tu mnaotegemea wawalipe, mwapata sifa gani? Hata ‘wenye dhambi’ huwakopesha ‘wenye dhambi’ wenzao wakitarajia kulipwa mali yao yote.
And if you lend to them from whom you expect to be recompensed, what is your grace? for sinners also lend to sinners, that they might be profited.
35 Lakini wapendeni adui zenu, watendeeni mema, wakopesheni bila kutegemea kurudishiwa mlichokopesha. Ndipo thawabu yenu itakapokuwa kubwa, nanyi mtakuwa wana wa Aliye Juu Sana, kwa sababu yeye ni mwema kwa watu wasio na shukrani na kwa wale waovu.
But love your adversaries, and do good to them, and lend, and cut not off the hope of any one; and great shall be your reward, and you shall be the children of the Most High; for he is benign to the evil and to the ungrateful.
36 Kuweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.
Be you therefore merciful, as also your Father is merciful.
37 “Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa. Msilaumu, nanyi hamtalaumiwa. Sameheni, nanyi mtasamehewa.
JUDGE not, and you shall not be judged; condemn not, and you shall not be condemned; release, and you shall be released;
38 Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa. Kipimo cha kujaa na kushindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile mpimacho, ndicho mtakachopimiwa.”
give, and it shall be given to you; in good measure, compressed, redundant, shall they pour into your bosoms. For in that measure you mete, it shall be measured to you.
39 Pia akawapa mfano akasema, “Je, kipofu aweza kumwongoza kipofu? Je, wote wawili hawatatumbukia shimoni?
And he spake to them a parable: How can the blind lead the blind, and not fall into the ditch?
40 Mwanafunzi hawezi kumzidi mwalimu wake, ila yule aliyehitimu aweza kuwa kama mwalimu wake.
The disciple than his master is not greater; but every man who is perfect shall be as his master.
41 “Mbona unatazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, wala huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe?
For why behold you the rod that is in the eye of your brother, but the rafter in your (own) eye is not seen by you?
42 Utawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Ndugu yangu, acha nitoe kibanzi kilicho ndani ya jicho lako,’ wakati wewe mwenyewe huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako? Ewe mnafiki, ondoa boriti ndani ya jicho lako kwanza, ndipo utaweza kuona dhahiri jinsi ya kuondoa kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako.
Or how can you say to your brother, My brother, permit (that) I pull out the rod that is in your eye, and behold the rafter in your own eye is not seen by you? Hypocrite! first take out the rafter from your own eye, and then shall you see to take out the rod that is in the eye of your brother.
43 “Hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala hakuna mti mbaya uzaao matunda mazuri.
A good tree maketh not evil fruits; also an evil tree maketh not good fruits:
44 Kila mti hujulikana kwa matunda yake. Kwa maana watu hawachumi tini kwenye miiba, wala zabibu kwenye michongoma.
for every tree by its fruits is known. For how gather they from thorns figs? neither also from the bramble do they gather in grapes.
45 Vivyo hivyo mtu mwema hutoa mambo mema kutoka kwenye hazina ya moyo wake, naye mtu mwovu hutoa mambo maovu kutoka kwenye hazina ya moyo wake. Kwa kuwa mtu hunena kwa kinywa chake yale yaliyoujaza moyo wake.
The good man, from the good treasures which are in his heart, bringeth forth good things; and the evil man, from the evil treasures which are in his heart, bringeth forth evil things; for from the adundancies of the heart the lips speak.
46 “Kwa nini mnaniita, ‘Bwana, Bwana,’ nanyi hamfanyi ninayowaambia?
Why call you me, My Lord, my Lord, and the things which I say do not?
47 Nitawaonyesha jinsi alivyo mtu yule anayekuja kwangu na kusikia maneno yangu na kuyatenda.
Every man who cometh to me and heareth my words, and doeth them, I will show you to whom he is like.
48 Yeye ni kama mtu aliyejenga nyumba, akachimba chini sana, na kuweka msingi kwenye mwamba. Mafuriko yalipokuja, maji ya ghafula yaliipiga ile nyumba, lakini haikutikisika, kwa sababu ilikuwa imejengwa vizuri.
He is like a man who built a house, and digged deep, and laid the foundations upon the rock: but when there was an inundation, the inundation beat against that house, and it could not shake it, for its foundations were set upon a rock.
49 Lakini yeye anayesikia maneno yangu wala asiyatende, ni kama mtu aliyejenga nyumba juu ya ardhi bila kuweka msingi. Mafuriko yalipoikumba nyumba ile, ikaanguka mara na kubomoka kabisa.”
And he who heareth and doeth not, is like a man who built his house upon the dust, without a foundation: and when the river beat against it, it immediately fell, and the ruin was great of that house.