< Luka 5 >

1 Siku moja Yesu alipokuwa amesimama karibu na Ziwa la Genesareti, watu wengi wakiwa wanasongana kumzunguka ili wapate kusikia neno la Mungu,
In pripetilo se je, medtem ko je množica pritiskala nanj, da sliši Božjo besedo, [da] je stal ob Genezareškem jezeru
2 akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa, zikiwa zimeachwa hapo na wavuvi waliokuwa wanaosha nyavu zao.
in zagledal dve ladji, pripravljeni pri jezeru, toda ribiči so odšli iz njiju ter izpirali svoje mreže.
3 Akaingia katika mojawapo ya hizo mashua ambayo ilikuwa ya Simoni, akamwomba aisogeze ndani ya maji kidogo kutoka ufuoni. Kisha akaketi na kufundisha watu akiwa mle ndani ya mashua.
In vstopil je v eno izmed ladij, ki je bila Simonova in ga prosil, da bi odrinil malce proč od kopnega. In usedel se je ter iz ladje učil množico.
4 Alipomaliza kunena, akamwambia Simoni, “Sasa peleka mashua hadi kilindini kisha mshushe nyavu zenu mkavue samaki.”
Torej, ko je prenehal govoriti, je rekel Simonu: »Kreni na globoko in spusti dol svoje mreže za vleko.«
5 Simoni akamjibu, “Bwana, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha na hatukuvua chochote. Lakini, kwa neno lako nitazishusha nyavu.”
Simon pa mu odgovori in reče: »Učitelj, celó noč smo garali, pa nismo nič ujeli. Vendar bom na tvojo besedo to mrežo spustil dol.«
6 Nao walipozishusha nyavu zao, wakavua samaki wengi sana, nyavu zao zikajaa zikaanza kukatika.
In ko so to storili, so zajeli veliko množino rib in njihova mreža se je pretrgala.
7 Wakawaashiria wavuvi wenzao kwenye ile mashua nyingine ili waje kuwasaidia. Wakaja, wakajaza mashua zote mbili samaki hata zikaanza kuzama.
In dali so znamenje svojim družabnikom, ki so bili na drugi ladji, da naj pridejo ter jim pomagajo. In prišli so ter napolnili obe ladji, tako da sta se začeli potapljati.
8 Simoni Petro alipoona haya yaliyotukia, alianguka miguuni mwa Yesu na kumwambia, “Bwana, ondoka kwangu. Mimi ni mtu mwenye dhambi!”
Ko je Simon Peter to videl, je pri Jezusovih kolenih padel dol, rekoč: »Odidi od mene, oh Gospod, kajti grešen človek sem.«
9 Kwa kuwa yeye na wavuvi wenzake walikuwa wameshangazwa sana na wingi wa samaki waliokuwa wamepata.
Kajti nad ulovom rib, ki so jih zajeli, je bil osupel on in vsi ti, ki so bili z njim;
10 Vivyo hivyo wenzake Simoni, yaani Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, walishangazwa pia. Ndipo Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, tangu sasa utakuwa mvuvi wa watu.”
in tako sta bila tudi Jakob in Janez, Zebedejeva sinova, ki sta bila Simonova družabnika. In Jezus je Simonu rekel: »Ne boj se, odslej boš lovil ljudi.«
11 Hivyo wakasogeza mashua zao mpaka ufuoni mwa bahari, wakaacha kila kitu na kumfuata.
In ko so svoji ladji pripeljali do kopnega, so vse zapustili in mu sledili.
12 Ikawa siku moja Yesu alipokuwa katika mji fulani, mtu mmoja mwenye ukoma mwili mzima akamjia. Alipomwona Yesu, alianguka chini mpaka uso wake ukagusa ardhi, akamsihi akisema, “Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa.”
In pripetilo se je, ko je bil v nekem mestu, [da] zagleda človeka polnega gobavosti. Ko je [le-ta] zagledal Jezusa, je padel na svoj obraz ter ga rotil, rekoč: »Gospod, če hočeš, me lahko očistiš.«
13 Yesu akanyoosha mkono wake, akamgusa yule mtu, akamwambia, “Nataka. Takasika!” Na mara ukoma wake ukatakasika.
In iztegnil je svojo roko ter se ga dotaknil, rekoč: »Hočem, bodi čist.« In gobavost je takoj odšla od njega.
14 Yesu akamwagiza akisema, “Usimwambie mtu yeyote, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
In naročil mu je, da ne pove nobenemu človeku: »Temveč pojdi in se pokaži duhovniku ter daruj za svoje očiščenje glede na Mojzesovo zapoved, njim v pričevanje.«
15 Lakini habari zake Yesu zikazidi sana kuenea kotekote kuliko wakati mwingine wowote. Makutano makubwa ya watu yalikuwa yakikusanyika ili kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao.
Toda beseda o njem je toliko bolj na veliko šla naokoli in velike množice so prišle skupaj, da poslušajo in da bi bile po njem ozdravljene svojih slabotnosti.
16 Lakini mara kwa mara Yesu alijitenga nao ili kwenda mahali pa faragha kuomba.
On pa se je umaknil v divjino in molil.
17 Siku moja Yesu alipokuwa akifundisha, Mafarisayo na walimu wa sheria, waliokuwa wametoka kila kijiji cha Galilaya na kutoka Uyahudi na Yerusalemu, walikuwa wameketi huko. Nao uweza wa Bwana ulikuwa juu yake kuponya wagonjwa.
In pripetilo se je na določeni dan, medtem ko je učil, da so bili tam, sedeči poleg, farizeji in učeni možje postave, ki so prišli iz vsakega mesta Galileje, Judeje in Jeruzalema. In Gospodova moč je bila prisotna, da jih ozdravi.
18 Wakaja watu wamembeba mgonjwa aliyepooza kwenye mkeka. Wakajaribu kumwingiza ndani ili wamweke mbele ya Yesu.
In glej, možje so prinesli na postelji človeka, ki je bil prevzet s paralizo in iskali so načine, da ga prinesejo noter in da ga položijo predenj.
19 Walipokuwa hawawezi kufanya hivyo kwa sababu ya umati wa watu, wakapanda juu ya paa, wakaondoa baadhi ya matofali, wakamteremsha yule mgonjwa kwa mkeka wake hadi katikati ya ule umati pale mbele ya Yesu.
Ko pa zaradi množice niso mogli najti, po kateri poti bi ga lahko prinesli noter, so odšli na hišno streho in ga z njegovim ležiščem vred spustili navzdol skozi strešno kritino v sredo pred Jezusa.
20 Yesu alipoiona imani yao, akamwambia yule mgonjwa, “Rafiki, dhambi zako zimesamehewa.”
In ko je videl njihovo vero, mu je rekel: »Človek, tvoji grehi so ti odpuščeni.«
21 Mafarisayo na wale walimu wa sheria wakaanza kuuliza, “Ni nani mtu huyu anayesema maneno ya kukufuru? Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”
In pisarji in farizeji so začeli premišljevati, rekoč: »Kdo je ta, ki govori bogokletja? Kdo lahko odpušča grehe razen samo Bog?«
22 Yesu akijua mawazo yao akawauliza, “Kwa nini mnawaza hivyo mioyoni mwenu?
Toda ko je Jezus zaznal njihove misli, jim je odgovoril in rekel: »Kaj razmišljate v svojih srcih?
23 Je, ni lipi lililo rahisi zaidi, kumwambia, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Inuka, uende’?
Ali je lažje reči: ›Tvoji grehi naj ti bodo odpuščeni‹ ali reči: ›Dvigni se in hôdi?‹
24 Lakini ili mpate kujua kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani kusamehe dhambi…” Akamwambia yule aliyepooza, “Nakuambia, inuka, chukua mkeka wako, uende nyumbani kwako.”
Toda da boste lahko vedeli, da ima Sin človekov na zemlji oblast odpuščati grehe, « (je rekel bolnemu zaradi paralize) »jaz ti pravim: ›Vstani in vzemi svoje ležišče in pojdi v svojo hišo.‹«
25 Mara yule mtu aliyekuwa amepooza akasimama mbele yao wote, akachukua mkeka wake, akaenda zake nyumbani, huku akimtukuza Mungu.
In ta je pred njimi takoj vstal ter pobral to, na čemer je ležal in odšel k svoji lastni hiši, proslavljajoč Boga.
26 Kila mmoja akashangaa na kumtukuza Mungu. Wakajawa na hofu ya Mungu, wakasema, “Leo tumeona mambo ya ajabu.”
In vsi so bili osupli in slavili Boga in izpolnjeni so bili s strahom, rekoč: »Danes smo videli čudne stvari.«
27 Baada ya haya, Yesu alitoka na kumwona mtoza ushuru mmoja jina lake Lawi akiwa amekaa forodhani, mahali pake pa kutoza ushuru. Akamwambia, “Nifuate.”
Po teh stvareh pa je odšel dalje in zagledal davkarja, imenovanega Levi, ki je sedel pri kraju plačevanja davkov in mu rekel: »Sledi mi.«
28 Naye Lawi akaacha kila kitu, akaondoka, akamfuata.
In ta je pustil vse, vstal ter mu sledil.
29 Kisha Lawi akamfanyia Yesu karamu kubwa nyumbani kwake, nao umati mkubwa wa watoza ushuru na watu wengine walikuwa wakila pamoja nao.
In Levi mu je v svoji lastni hiši pripravil veliko praznovanje; in bila je velika skupina davkarjev in drugih, ki so se z njimi usedli.
30 Lakini Mafarisayo na walimu wa sheria waliokuwa wa dhehebu lao wakawalalamikia wanafunzi wa Yesu, wakisema, “Mbona mnakula na kunywa pamoja na watoza ushuru na ‘wenye dhambi’?”
Toda njihovi pisarji in farizeji so godrnjali zoper njegove učence, rekoč: »Zakaj jeste in pijete z davkarji in grešniki?«
31 Yesu akawajibu, “Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio wagonjwa.
In Jezus jim odgovori ter reče: »Tisti, ki so zdravi, ne potrebujejo zdravnika, temveč tisti, ki so bolni.
32 Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi wapate kutubu.”
Nisem prišel klicat pravičnih, temveč grešnike h kesanju.«
33 Wakamwambia Yesu, “Wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo mara kwa mara hufunga na kuomba, lakini wanafunzi wako wanaendelea kula na kunywa.”
In rekli so mu: »Zakaj se Janezovi učenci pogosto postijo in opravljajo molitve in enako učenci farizejev, tvoji pa jedo in pijejo?«
34 Yesu akawajibu, “Je, mnaweza kuwafanya wageni wa bwana arusi kufunga wakati yuko pamoja nao?
Rekel jim je: »Ali lahko primorate otroke svatovske sobe, da se postijo, medtem ko je z njimi ženin?
35 Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kwao. Hapo ndipo watakapofunga.”
Toda prišli bodo dnevi, ko bo ženin odvzet od njih in tedaj, v tistih dneh, se bodo postili.«
36 Yesu akawapa mfano huu, akawaambia: “Hakuna mtu achanaye kiraka kutoka kwenye nguo mpya na kukishonea kwenye nguo iliyochakaa. Akifanya hivyo, atakuwa amechana nguo mpya, na kile kiraka hakitalingana na ile nguo iliyochakaa.
In povedal jim je tudi prispodobo: »Nihče ne polaga koščka iz nove obleke na staro; če drugače, potem nov dela raztrganino in tudi košček, ki je bil odvzet iz nove, se ne ujema s staro.
37 Hakuna mtu awekaye divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, hiyo divai mpya itavipasua hivyo viriba, nayo yote itamwagika.
In novega vina nihče ne vliva v stare mehove, sicer bo novo vino mehove razgnalo in bo izlito in mehovi bodo propadli.
38 Divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya.
Toda novo vino mora biti vlito v nove mehove in oboje je ohranjeno.
39 Wala hakuna mtu anayependelea divai mpya baada ya kunywa divai ya zamani, bali husema, ‘Ile ya zamani ni nzuri zaidi.’”
Prav tako nihče, ki je pil staro vino, noče nemudoma novega, kajti pravi: ›Staro je boljše.‹«

< Luka 5 >