< Luka 4 >

1 Yesu, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akarudi kutoka Yordani. Akaongozwa na Roho Mtakatifu hadi nyikani,
Jezus pa, svetega Duha poln, vrne se od Jordana; in odpelje ga Duh v puščavo.
2 mahali ambako kwa siku arobaini alikuwa akijaribiwa na ibilisi. Kwa siku zote hizo hakula chochote, hivyo baada ya muda huo akaona njaa.
In štirideset dnî ga je izkušal hudič. In ničesar ni jedel v teh dnéh; in ko minejo, potem postane lačen.
3 Ibilisi akamwambia, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”
In reče mu hudič: Če si sin Božji, reci temu kamenu, naj postane kruh.
4 Yesu akajibu akamwambia, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu.’”
In odgovorí mu Jezus, govoreč: Pisano je: "Ne bo živel človek o samem kruhu, nego o vsakej besedi Božjej."
5 Ibilisi akampeleka hadi juu ya mlima mrefu akamwonyesha milki zote za dunia kwa mara moja.
In popeljavši ga hudič na visoko goro, pokaže mu vsa kraljestva sveta v pičici časa.
6 Akamwambia, “Nitakupa mamlaka juu ya milki hizi na fahari zake zote, kwa maana zimekabidhiwa mkononi mwangu nami ninaweza kumpa yeyote ninayetaka.
In reče mu hudič: Tebi bom dal vso to oblast in njih slavo; kajti meni je izročena, in dám jo, komurkoli jo hočem.
7 Hivyo ikiwa utanisujudia na kuniabudu, vyote vitakuwa vyako.”
Ti torej če se pokloniš pred menoj, tvoje bo vse.
8 Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Mwabudu Bwana Mungu wako na umtumikie yeye peke yake.’”
In odgovarjajoč, reče mu Jezus: Poberi se od mene, satan! Kajti pisano je: "Poklanjaj se Gospodu Bogu svojemu, in njemu edinemu služi."
9 Kisha ibilisi akampeleka mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa,
In pelje ga v Jeruzalem, in postavi ga na vrh tempeljna, in reče mu: Če si sin Božji, vrzi se odtod dol:
10 kwa maana imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake ili wakulinde;
Kajti pisano je: "Angeljem svojim bo zapovedal za te, naj te varujejo:
11 nao watakuchukua mikononi mwao, usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
In vzeli te bodo na roko, da se kje z nogo svoje ne udariš o kamen."
12 Yesu akamjibu, “Imesemwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
In odgovarjajoč, reče mu Jezus: Povedano je: "Ne izkušaj Gospoda Boga svojega."
13 Ibilisi alipomaliza kila jaribu, akamwacha Yesu mpaka wakati mwingine ufaao.
In končavši hudič vso izkušnjavo, odide od njega do časa.
14 Kisha Yesu akarudi mpaka Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, nazo habari zake zikaenea katika sehemu zote za nchi za kandokando.
In vrne se Jezus z močjó duhovno v Galilejo; in glas o njem izide po vsem okolnem kraji.
15 Akaanza kufundisha kwenye masinagogi yao, na kila mmoja akamsifu.
In on je učil po njih shajališčih, in vsi so ga slavili.
16 Yesu akaenda Nazareti, alipolelewa, na siku ya Sabato alikwenda katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome,
In pride v Nazaret, kjer je odrastel; in vnide po navadi svojej, v sobotni dan, v shajališče, in vstane, da bere.
17 naye akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na kukuta mahali palipoandikwa:
In dadó mu bukve Izaija preroka; in ko razgane bukve, najde mesto, kjer je bilo pisano:
18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa sababu amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, na vipofu kupata kuona tena, kuwaweka huru wanaoonewa,
"Duh Gospodov je na meni: za to, ker me je pomazilil; da oznanim evangelj ubogim, poslal me je, da uzdravim potrte v srcu, da oznanim jetnikom, da se bodo izpustili, in slepcem, da bodo spregledali, da izpustim sužnje v svobodo,
19 na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubalika.”
Da oznanim prijetno leto Gospodovo."
20 Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
In zgane bukve, in dá strežaju, in sede; in vsi v shajališči so gledali na-nj.
21 Ndipo akaanza kwa kuwaambia, “Leo Andiko hili limetimia mkiwa mnasikia.”
In začne jim govoriti: Danes se je izpolnilo to pismo v ušesih vaših.
22 Wote waliokuwako wakamsifu na kuyastaajabia maneno yake yaliyojaa neema, wakaulizana, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”
In vsi so mu pričali, in čudili so se besedam milosti, ktere so izhajale iz ust njegovih, in govorili so: Ali ni ta Jožefov?
23 Yesu akawaambia, “Bila shaka mtatumia mithali hii: ‘Tabibu, jiponye mwenyewe! Mambo yale tuliyosikia kwamba uliyafanya huko Kapernaumu, yafanye na hapa kwenye mji wako.’”
In reče jim: Gotovo mi boste povedali to priliko: Zdravnik, uzdravi se sam! Karkoli smo slišali, da se je zgodilo v Kapernaumu, stóri tudi tu v domovini svojej.
24 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna nabii anayekubalika katika mji wake mwenyewe.
Reče pa: Resnično vam pravim, da ni noben prerok prijeten v domovini svojej.
25 Lakini ukweli ni kwamba palikuwa na wajane wengi katika Israeli wakati wa Eliya, mbingu zilipofungwa kwa miaka mitatu na miezi sita pakawa na njaa kuu katika nchi nzima.
Ali v resnici vam pravim, da je bilo veliko vdov v dnéh Elija v Izraelu, ko se je nebo zaprlo tri leta in šest mesecev, tako, da je nastala velika lakota po vsej zemlji;
26 Hata hivyo Eliya hakutumwa hata kwa mmoja wao, bali kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni.
In k nobenej od njih ni bil poslan Elija, razen v Sarepto Sidonsko k ženi vdovi.
27 Pia palikuwa na wengi wenye ukoma katika Israeli katika siku za nabii Elisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyetakaswa, isipokuwa Naamani mtu wa Shamu.”
In veliko gobavcev je bilo za Eliseja preroka v Izraelu; in nobeden od njih se ni očistil, razen Naaman Sirijan.
28 Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, wakakasirika sana.
In vsi v shajališči se napolnijo jeze, ko to slišijo.
29 Wakasimama, wakamtoa nje ya mji, wakamchukua hadi kwenye kilele cha mlima mahali ambapo mji huo ulikuwa umejengwa, ili wamtupe chini kutoka kwenye mteremko mkali.
In vstavši, izženó ga ven iz mesta, in odpeljejo ga na vrh gore, na kterej je bilo njih mesto sezidano, da bi ga dol pahnili.
30 Lakini yeye akapita papo hapo katikati ya huo umati wa watu akaenda zake.
Ali on prejde posredi njih, in odide.
31 Kisha Yesu akashuka kwenda Kapernaumu, mji wa Galilaya, na katika siku ya Sabato akawa anafundisha.
In snide v Kapernaum mesto Galilejsko; in učil jih je ob sobotah.
32 Wakashangazwa sana na mafundisho yake, maana maneno yake yalikuwa na mamlaka.
In čudili so se nauku njegovemu, ker je bila beseda njegova silna.
33 Ndani ya sinagogi palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu. Naye akapiga kelele kwa nguvu akisema,
In v shajališči je bil človek, kteri je imel nečistega duha hudičevega, in zakričí z močnim glasom,
34 “Tuache! Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
Govoreč: Pojenjaj, kaj imaš z nami, Jezus Nazarečan? Prišel si, da bi nas pogubil? Poznam te, kdo si – svetnik Božji.
35 Basi Yesu akamkemea yule pepo mchafu, akisema, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!” Yule pepo mchafu akamwangusha yule mtu chini mbele yao wote, akatoka pasipo kumdhuru.
In zapretí mu Jezus, govoreč: Umolkni, in izidi iž njega! In trešči ga hudič na sredo, in izide iž njega, in nič ga ni oškodoval.
36 Watu wote wakashangaa, wakaambiana, “Mafundisho haya ni ya namna gani? Anawaamuru pepo wachafu kwa mamlaka na nguvu, nao wanatoka!”
In obide jih groza vse, in pomenkovali so se med seboj, govoreč: Kakošna je ta beseda, da z oblastjo in močjó ukazuje nečistim duhovom, ter izhajajo?
37 Habari zake zikaanza kuenea kila mahali katika sehemu ile.
In razglasí se glas o njem po vsem okolnem kraji.
38 Yesu akatoka katika sinagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Basi huko alimkuta mama mkwe wa Simoni akiwa ameshikwa na homa kali, nao wakamwomba Yesu amsaidie.
Vstavši pa iz shajališča, vnide v hišo Simonovo. Tašča pa Simonova imela je hudo mrzlico; in zaprosijo ga za njo.
39 Hivyo Yesu akamwinamia na kukemea ile homa, nayo ikamwacha. Akaamka saa ile ile, naye akaanza kuwahudumia.
In stoječ nad njo, zapretí mrzlici, in pustí jo; in precej je vstala, ter jim je stregla.
40 Jua lilipokuwa linatua, watu wakamletea Yesu watu wote waliokuwa na maradhi mbalimbali, naye akaweka mikono yake juu ya kila mgonjwa, naye akawaponya.
Ko je pa solnce zahajalo, vsi, kteri so imeli bolnike z različnimi boleznimi, dovažali so jih k njemu; a on je na vsakega od njih pokladal roke, ter jih je uzdravljal.
41 Pepo wachafu pia wakawatoka watu wengi, nao walipokuwa wakitoka wakapiga kelele, wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea na kuwazuia wasiseme, kwa maana walimjua kuwa yeye ndiye Kristo.
Izhajali pa so tudi hudiči iz mnogih, kričeč in govoreč: Ti si Kristus sin Božji. In grozeč se, ni jim dal govoriti, ker so vedeli, da je on Kristus.
42 Kesho yake, kulipopambazuka, Yesu alikwenda mahali pa faragha. Watu wengi wakawa wanamtafuta kila mahali, nao walipomwona wakajaribu kumzuia asiondoke.
Ko se pa zdaní, izide, in odide na samoten kraj; in ljudstvo ga je iskalo, in pridejo k njemu, in pridržavali so ga, da ne bi šel od njih.
43 Lakini yeye akawaambia, “Imenipasa kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, kwa maana kwa kusudi hili nilitumwa.”
On jim pa reče: Tudi drugim mestom moram oznanjevati evangelj o kraljestvu Božjem! kajti za to sem poslan.
44 Naye aliendelea kuhubiri katika masinagogi ya Uyahudi.
In oznanjeval je po shajališčih Galilejskih.

< Luka 4 >