< Luka 4 >
1 Yesu, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akarudi kutoka Yordani. Akaongozwa na Roho Mtakatifu hadi nyikani,
And Jesus, full of the Holy Spirit, returned from the Jordan, and was led by the Spirit in the wilderness
2 mahali ambako kwa siku arobaini alikuwa akijaribiwa na ibilisi. Kwa siku zote hizo hakula chochote, hivyo baada ya muda huo akaona njaa.
during forty days, being tempted of the devil. And he did eat nothing in those days: and when they were completed, he hungered.
3 Ibilisi akamwambia, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”
And the devil said unto him, If thou art the Son of God, command this stone that it become bread.
4 Yesu akajibu akamwambia, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu.’”
And Jesus answered unto him, It is written, Man shall not live by bread alone.
5 Ibilisi akampeleka hadi juu ya mlima mrefu akamwonyesha milki zote za dunia kwa mara moja.
And he led him up, and shewed him all the kingdoms of the world in a moment of time.
6 Akamwambia, “Nitakupa mamlaka juu ya milki hizi na fahari zake zote, kwa maana zimekabidhiwa mkononi mwangu nami ninaweza kumpa yeyote ninayetaka.
And the devil said unto him, To thee will I give all this authority, and the glory of them: for it hath been delivered unto me; and to whomsoever I will I give it.
7 Hivyo ikiwa utanisujudia na kuniabudu, vyote vitakuwa vyako.”
If thou therefore wilt worship before me, it shall all be thine.
8 Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Mwabudu Bwana Mungu wako na umtumikie yeye peke yake.’”
And Jesus answered and said unto him, It is written, Thou shalt worship the Lord thy God, and him only shalt thou serve.
9 Kisha ibilisi akampeleka mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa,
And he led him to Jerusalem, and set him on the pinnacle of the temple, and said unto him, If thou art the Son of God, cast thyself down from hence:
10 kwa maana imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake ili wakulinde;
for it is written, He shall give his angels charge concerning thee, to guard thee:
11 nao watakuchukua mikononi mwao, usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
and, On their hands they shall bear thee up, Lest haply thou dash thy foot against a stone.
12 Yesu akamjibu, “Imesemwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
And Jesus answering said unto him, It is said, Thou shalt not tempt the Lord thy God.
13 Ibilisi alipomaliza kila jaribu, akamwacha Yesu mpaka wakati mwingine ufaao.
And when the devil had completed every temptation, he departed from him for a season.
14 Kisha Yesu akarudi mpaka Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, nazo habari zake zikaenea katika sehemu zote za nchi za kandokando.
And Jesus returned in the power of the Spirit into Galilee: and a fame went out concerning him through all the region round about.
15 Akaanza kufundisha kwenye masinagogi yao, na kila mmoja akamsifu.
And he taught in their synagogues, being glorified of all.
16 Yesu akaenda Nazareti, alipolelewa, na siku ya Sabato alikwenda katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome,
And he came to Nazareth, where he had been brought up: and he entered, as his custom was, into the synagogue on the sabbath day, and stood up to read.
17 naye akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na kukuta mahali palipoandikwa:
And there was delivered unto him the book of the prophet Isaiah. And he opened the book, and found the place where it was written,
18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa sababu amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, na vipofu kupata kuona tena, kuwaweka huru wanaoonewa,
The Spirit of the Lord is upon me, Because he anointed me to preach good tidings to the poor: He hath sent me to proclaim release to the captives, And recovering of sight to the blind, To set at liberty them that are bruised,
19 na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubalika.”
To proclaim the acceptable year of the Lord.
20 Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
And he closed the book, and gave it back to the attendant, and sat down: and the eyes of all in the synagogue were fastened on him.
21 Ndipo akaanza kwa kuwaambia, “Leo Andiko hili limetimia mkiwa mnasikia.”
And he began to say unto them, Today hath this scripture been fulfilled in your ears.
22 Wote waliokuwako wakamsifu na kuyastaajabia maneno yake yaliyojaa neema, wakaulizana, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”
And all bare him witness, and wondered at the words of grace which proceeded out of his mouth: and they said, Is not this Joseph’s son?
23 Yesu akawaambia, “Bila shaka mtatumia mithali hii: ‘Tabibu, jiponye mwenyewe! Mambo yale tuliyosikia kwamba uliyafanya huko Kapernaumu, yafanye na hapa kwenye mji wako.’”
And he said unto them, Doubtless ye will say unto me this parable, Physician, heal thyself: whatsoever we have heard done at Capernaum, do also here in thine own country.
24 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna nabii anayekubalika katika mji wake mwenyewe.
And he said, Verily I say unto you, No prophet is acceptable in his own country.
25 Lakini ukweli ni kwamba palikuwa na wajane wengi katika Israeli wakati wa Eliya, mbingu zilipofungwa kwa miaka mitatu na miezi sita pakawa na njaa kuu katika nchi nzima.
But of a truth I say unto you, There were many widows in Israel in the days of Elijah, when the heaven was shut up three years and six months, when there came a great famine over all the land;
26 Hata hivyo Eliya hakutumwa hata kwa mmoja wao, bali kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni.
and unto none of them was Elijah sent, but only to Zarephath, in the land of Sidon, unto a woman that was a widow.
27 Pia palikuwa na wengi wenye ukoma katika Israeli katika siku za nabii Elisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyetakaswa, isipokuwa Naamani mtu wa Shamu.”
And there were many lepers in Israel in the time of Elisha the prophet; and none of them was cleansed, but only Naaman the Syrian.
28 Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, wakakasirika sana.
And they were all filled with wrath in the synagogue, as they heard these things;
29 Wakasimama, wakamtoa nje ya mji, wakamchukua hadi kwenye kilele cha mlima mahali ambapo mji huo ulikuwa umejengwa, ili wamtupe chini kutoka kwenye mteremko mkali.
and they rose up, and cast him forth out of the city, and led him unto the brow of the hill whereon their city was built, that they might throw him down headlong.
30 Lakini yeye akapita papo hapo katikati ya huo umati wa watu akaenda zake.
But he passing through the midst of them went his way.
31 Kisha Yesu akashuka kwenda Kapernaumu, mji wa Galilaya, na katika siku ya Sabato akawa anafundisha.
And he came down to Capernaum, a city of Galilee. And he was teaching them on the sabbath day:
32 Wakashangazwa sana na mafundisho yake, maana maneno yake yalikuwa na mamlaka.
and they were astonished at his teaching; for his word was with authority.
33 Ndani ya sinagogi palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu. Naye akapiga kelele kwa nguvu akisema,
And in the synagogue there was a man, which had a spirit of an unclean devil; and he cried out with a loud voice,
34 “Tuache! Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
Ah! what have we to do with thee, thou Jesus of Nazareth? art thou come to destroy us? I know thee who thou art, the Holy One of God.
35 Basi Yesu akamkemea yule pepo mchafu, akisema, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!” Yule pepo mchafu akamwangusha yule mtu chini mbele yao wote, akatoka pasipo kumdhuru.
And Jesus rebuked him, saying, Hold thy peace, and come out of him. And when the devil had thrown him down in the midst, he came out of him, having done him no hurt.
36 Watu wote wakashangaa, wakaambiana, “Mafundisho haya ni ya namna gani? Anawaamuru pepo wachafu kwa mamlaka na nguvu, nao wanatoka!”
And amazement came upon all, and they spake together, one with another, saying, What is this word? for with authority and power he commandeth the unclean spirits, and they come out.
37 Habari zake zikaanza kuenea kila mahali katika sehemu ile.
And there went forth a rumour concerning him into every place of the region round about.
38 Yesu akatoka katika sinagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Basi huko alimkuta mama mkwe wa Simoni akiwa ameshikwa na homa kali, nao wakamwomba Yesu amsaidie.
And he rose up from the synagogue, and entered into the house of Simon. And Simon’s wife’s mother was holden with a great fever; and they besought him for her.
39 Hivyo Yesu akamwinamia na kukemea ile homa, nayo ikamwacha. Akaamka saa ile ile, naye akaanza kuwahudumia.
And he stood over her, and rebuked the fever; and it left her: and immediately she rose up and ministered unto them.
40 Jua lilipokuwa linatua, watu wakamletea Yesu watu wote waliokuwa na maradhi mbalimbali, naye akaweka mikono yake juu ya kila mgonjwa, naye akawaponya.
And when the sun was setting, all they that had any sick with divers diseases brought them unto him; and he laid his hands on every one of them, and healed them.
41 Pepo wachafu pia wakawatoka watu wengi, nao walipokuwa wakitoka wakapiga kelele, wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea na kuwazuia wasiseme, kwa maana walimjua kuwa yeye ndiye Kristo.
And devils also came out from many, crying out, and saying, Thou art the Son of God. And rebuking them, he suffered them not to speak, because they knew that he was the Christ.
42 Kesho yake, kulipopambazuka, Yesu alikwenda mahali pa faragha. Watu wengi wakawa wanamtafuta kila mahali, nao walipomwona wakajaribu kumzuia asiondoke.
And when it was day, he came out and went into a desert place: and the multitudes sought after him, and came unto him, and would have stayed him, that he should not go from them.
43 Lakini yeye akawaambia, “Imenipasa kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, kwa maana kwa kusudi hili nilitumwa.”
But he said unto them, I must preach the good tidings of the kingdom of God to the other cities also: for therefore was I sent.
44 Naye aliendelea kuhubiri katika masinagogi ya Uyahudi.
And he was preaching in the synagogues of Galilee.