< Luka 4 >
1 Yesu, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akarudi kutoka Yordani. Akaongozwa na Roho Mtakatifu hadi nyikani,
And Jesus, full of the Holy Spirit, turned back from the Jordan, and was brought in the Spirit into the wilderness,
2 mahali ambako kwa siku arobaini alikuwa akijaribiwa na ibilisi. Kwa siku zote hizo hakula chochote, hivyo baada ya muda huo akaona njaa.
being tempted by the Devil forty days, and He did not eat anything in those days, and they having been ended, He afterward hungered,
3 Ibilisi akamwambia, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”
and the Devil said to Him, “If You are [the] Son of God, speak to this stone that it may become bread.”
4 Yesu akajibu akamwambia, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu.’”
And Jesus answered him, saying, “It has been written, that, Not on bread only will man live, but on every saying of God.”
5 Ibilisi akampeleka hadi juu ya mlima mrefu akamwonyesha milki zote za dunia kwa mara moja.
And the Devil having brought Him up to a high mountain, showed to Him all the kingdoms of the world in a moment of time,
6 Akamwambia, “Nitakupa mamlaka juu ya milki hizi na fahari zake zote, kwa maana zimekabidhiwa mkononi mwangu nami ninaweza kumpa yeyote ninayetaka.
and the Devil said to Him, “To You I will give all this authority, and their glory, because to me it has been delivered, and to whomsoever I will, I give it;
7 Hivyo ikiwa utanisujudia na kuniabudu, vyote vitakuwa vyako.”
You, then, if You may worship me—all will be Yours.”
8 Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Mwabudu Bwana Mungu wako na umtumikie yeye peke yake.’”
And Jesus answering him said, “[[Get behind Me, Satan, for]] it has been written: You will worship the LORD your God, and Him only you will serve.”
9 Kisha ibilisi akampeleka mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa,
And he brought Him to Jerusalem, and set Him on the pinnacle of the temple, and said to Him, “If You are the Son of God, cast Yourself down from here,
10 kwa maana imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake ili wakulinde;
for it has been written: To His messengers He will give charge concerning you, to guard over you;
11 nao watakuchukua mikononi mwao, usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
and: On hands they will bear you up, lest at any time you may dash your foot against a stone.”
12 Yesu akamjibu, “Imesemwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
And Jesus answering said to him, “It has been said, You will not tempt the LORD your God.”
13 Ibilisi alipomaliza kila jaribu, akamwacha Yesu mpaka wakati mwingine ufaao.
And having ended all temptation, the Devil departed from Him until a convenient season.
14 Kisha Yesu akarudi mpaka Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, nazo habari zake zikaenea katika sehemu zote za nchi za kandokando.
And Jesus turned back in the power of the Spirit to Galilee, and a fame went forth through all the surrounding region concerning Him,
15 Akaanza kufundisha kwenye masinagogi yao, na kila mmoja akamsifu.
and He was teaching in their synagogues, being glorified by all.
16 Yesu akaenda Nazareti, alipolelewa, na siku ya Sabato alikwenda katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome,
And He came to Nazareth, where He has been brought up, and He went in, according to His custom, on the day of the Sabbaths, into the synagogue, and stood up to read;
17 naye akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na kukuta mahali palipoandikwa:
and there was given over to Him a scroll of Isaiah the prophet, and having unfolded the scroll, He found the place where it has been written:
18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa sababu amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, na vipofu kupata kuona tena, kuwaweka huru wanaoonewa,
“The Spirit of the LORD [is] on Me, Because He anointed Me To proclaim good news to the poor, Sent Me to heal the broken of heart, To proclaim to captives deliverance, And to blind receiving of sight, To send the bruised away with deliverance,
19 na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubalika.”
To proclaim the acceptable year of the LORD.”
20 Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
And having folded the scroll, having given [it] back to the officer, He sat down, and the eyes of all in the synagogue were gazing on Him.
21 Ndipo akaanza kwa kuwaambia, “Leo Andiko hili limetimia mkiwa mnasikia.”
And He began to say to them, “Today this writing has been fulfilled in your ears”;
22 Wote waliokuwako wakamsifu na kuyastaajabia maneno yake yaliyojaa neema, wakaulizana, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”
and all were bearing testimony to Him, and were wondering at the gracious words that are coming forth out of His mouth, and they said, “Is this not the Son of Joseph?”
23 Yesu akawaambia, “Bila shaka mtatumia mithali hii: ‘Tabibu, jiponye mwenyewe! Mambo yale tuliyosikia kwamba uliyafanya huko Kapernaumu, yafanye na hapa kwenye mji wako.’”
And He said to them, “Certainly you will say to Me this allegory, Physician, heal yourself; as great things as we heard done in Capernaum, do also here in Your country”;
24 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna nabii anayekubalika katika mji wake mwenyewe.
and He said, “Truly I say to you, no prophet is accepted in his own country;
25 Lakini ukweli ni kwamba palikuwa na wajane wengi katika Israeli wakati wa Eliya, mbingu zilipofungwa kwa miaka mitatu na miezi sita pakawa na njaa kuu katika nchi nzima.
and of a truth I say to you, many widows were in the days of Elijah, in Israel, when the sky was shut for three years and six months, when great famine came on all the land,
26 Hata hivyo Eliya hakutumwa hata kwa mmoja wao, bali kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni.
and to none of them was Elijah sent, but—to Sarepta of Sidon, to a woman, a widow;
27 Pia palikuwa na wengi wenye ukoma katika Israeli katika siku za nabii Elisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyetakaswa, isipokuwa Naamani mtu wa Shamu.”
and many lepers were in the time of Elisha the prophet, in Israel, and none of them was cleansed, but—Naaman the Syrian.”
28 Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, wakakasirika sana.
And all in the synagogue were filled with wrath, hearing these things,
29 Wakasimama, wakamtoa nje ya mji, wakamchukua hadi kwenye kilele cha mlima mahali ambapo mji huo ulikuwa umejengwa, ili wamtupe chini kutoka kwenye mteremko mkali.
and having risen, they put Him forth outside the city, and brought Him to the brow of the hill on which their city had been built—to cast Him down headlong,
30 Lakini yeye akapita papo hapo katikati ya huo umati wa watu akaenda zake.
and He, having gone through the midst of them, went away.
31 Kisha Yesu akashuka kwenda Kapernaumu, mji wa Galilaya, na katika siku ya Sabato akawa anafundisha.
And He came down to Capernaum, a city of Galilee, and was teaching them on the Sabbaths,
32 Wakashangazwa sana na mafundisho yake, maana maneno yake yalikuwa na mamlaka.
and they were astonished at His teaching, because His word was with authority.
33 Ndani ya sinagogi palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu. Naye akapiga kelele kwa nguvu akisema,
And in the synagogue was a man having a spirit of an unclean demon, and he cried out with a great voice,
34 “Tuache! Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
“Aah! What [regards] us and You, Jesus, O Nazarene? You came to destroy us; I have known who You are—the Holy One of God!”
35 Basi Yesu akamkemea yule pepo mchafu, akisema, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!” Yule pepo mchafu akamwangusha yule mtu chini mbele yao wote, akatoka pasipo kumdhuru.
And Jesus rebuked him, saying, “Be silenced, and come forth out of him”; and the demon having cast him into the midst, came forth from him, having hurt him nothing;
36 Watu wote wakashangaa, wakaambiana, “Mafundisho haya ni ya namna gani? Anawaamuru pepo wachafu kwa mamlaka na nguvu, nao wanatoka!”
and amazement came on all, and they were speaking together with one another, saying, “What [is] this word, that with authority and power He commands the unclean spirits, and they come forth?”
37 Habari zake zikaanza kuenea kila mahali katika sehemu ile.
And there was going forth a fame concerning Him to every place of the surrounding region.
38 Yesu akatoka katika sinagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Basi huko alimkuta mama mkwe wa Simoni akiwa ameshikwa na homa kali, nao wakamwomba Yesu amsaidie.
And having risen out of the synagogue, He entered into the house of Simon, and the mother-in-law of Simon was pressed with a great fever, and they asked Him about her,
39 Hivyo Yesu akamwinamia na kukemea ile homa, nayo ikamwacha. Akaamka saa ile ile, naye akaanza kuwahudumia.
and having stood over her, He rebuked the fever, and it left her, and immediately, having risen, she was ministering to them.
40 Jua lilipokuwa linatua, watu wakamletea Yesu watu wote waliokuwa na maradhi mbalimbali, naye akaweka mikono yake juu ya kila mgonjwa, naye akawaponya.
And at the setting of the sun, all, as many as had any ailing with manifold diseases, brought them to Him, and He, having put hands on each one of them, healed them.
41 Pepo wachafu pia wakawatoka watu wengi, nao walipokuwa wakitoka wakapiga kelele, wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea na kuwazuia wasiseme, kwa maana walimjua kuwa yeye ndiye Kristo.
And demons were also coming forth from many, crying out and saying, “You are the Christ, the Son of God”; and rebuking, He did not permit them to speak, because they knew Him to be the Christ.
42 Kesho yake, kulipopambazuka, Yesu alikwenda mahali pa faragha. Watu wengi wakawa wanamtafuta kila mahali, nao walipomwona wakajaribu kumzuia asiondoke.
And day having come, having gone forth, He went on to a desolate place, and the multitudes were seeking Him, and they came to Him, and were restraining Him—not to go on from them,
43 Lakini yeye akawaambia, “Imenipasa kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, kwa maana kwa kusudi hili nilitumwa.”
and He said to them, “Also to the other cities it is necessary for Me to proclaim good news of the Kingdom of God, because for this I have been sent”;
44 Naye aliendelea kuhubiri katika masinagogi ya Uyahudi.
and He was preaching in the synagogues of Galilee.