< Luka 4 >

1 Yesu, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akarudi kutoka Yordani. Akaongozwa na Roho Mtakatifu hadi nyikani,
And Jesus, full of the Holy Ghost, returned from the Jordan and was led by the Spirit into the wilderness, tempted by the devil forty days.
2 mahali ambako kwa siku arobaini alikuwa akijaribiwa na ibilisi. Kwa siku zote hizo hakula chochote, hivyo baada ya muda huo akaona njaa.
And He ate nothing during those days; and they having been completed, He afterward hungered.
3 Ibilisi akamwambia, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”
And the devil said to Him, If thou art the Son of God, speak to this stone, in order that it may become bread.
4 Yesu akajibu akamwambia, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu.’”
And Jesus responded to him, saying; It has been written, That man shall not live upon bread alone, but upon every word of God.
5 Ibilisi akampeleka hadi juu ya mlima mrefu akamwonyesha milki zote za dunia kwa mara moja.
And the devil leading Him up, he showed Him all the kingdoms of the world in a moment of time.
6 Akamwambia, “Nitakupa mamlaka juu ya milki hizi na fahari zake zote, kwa maana zimekabidhiwa mkononi mwangu nami ninaweza kumpa yeyote ninayetaka.
And the devil said to Him, I will give all the authority and glories of these to thee: because it has been given unto me: and I give it to whom I may wish;
7 Hivyo ikiwa utanisujudia na kuniabudu, vyote vitakuwa vyako.”
then if thou mayest worship before me all shall belong to thee.
8 Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Mwabudu Bwana Mungu wako na umtumikie yeye peke yake.’”
And Jesus responding said to him; It has been written, Thou shalt worship the Lord thy God and Him only shalt thou serve.
9 Kisha ibilisi akampeleka mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa,
And he led Him into Jerusalem, and placed Him on a pinnacle of the temple, and said to Him, If thou art the Son of God cast thyself down from thence;
10 kwa maana imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake ili wakulinde;
for it has been written, That He will give His angels charge concerning thee, in order to guard thee,
11 nao watakuchukua mikononi mwao, usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
and they will bear thee upon their hands, lest at any time thou mayest dash thy foot against a stone.
12 Yesu akamjibu, “Imesemwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
And Jesus responding said to him; That it has been said, Thou shalt not tempt the Lord thy God.
13 Ibilisi alipomaliza kila jaribu, akamwacha Yesu mpaka wakati mwingine ufaao.
And the devil having perfected every temptation, departed from Him for a season.
14 Kisha Yesu akarudi mpaka Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, nazo habari zake zikaenea katika sehemu zote za nchi za kandokando.
And Jesus returned in the power of the spirit into Galilee. And the fame concerning Him went throughout the whole country.
15 Akaanza kufundisha kwenye masinagogi yao, na kila mmoja akamsifu.
And He was teaching in their synagogues, being glorified by all.
16 Yesu akaenda Nazareti, alipolelewa, na siku ya Sabato alikwenda katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome,
And He came into Nazareth, where He was brought up: and according to the custom to Him, He came into the synagogue on the Sabbath-day, and stood up to read.
17 naye akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na kukuta mahali palipoandikwa:
And the Book of Isaiah the prophet was given to Him; and having opened the book, He found the place where it was written,
18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa sababu amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, na vipofu kupata kuona tena, kuwaweka huru wanaoonewa,
The Spirit of the Lord is upon me, because He anointed me to preach the gospel to the poor: hath sent me to heal the brokenhearted, to proclaim deliverance to the captives, and sight to the blind, and to set at liberty them that are bruised,
19 na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubalika.”
to proclaim the acceptable year of the Lord.
20 Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
And having closed the book, and giving it back to the officer, He sat down: and the eyes of all in the synagogue were fastened on Him.
21 Ndipo akaanza kwa kuwaambia, “Leo Andiko hili limetimia mkiwa mnasikia.”
And He began to say to them; This day has this Scripture been fulfilled in your ears.
22 Wote waliokuwako wakamsifu na kuyastaajabia maneno yake yaliyojaa neema, wakaulizana, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”
And they all continued to witness to Him, and wonder at the words of grace proceeding out from His mouth: and say, Is not this the son of Joseph?
23 Yesu akawaambia, “Bila shaka mtatumia mithali hii: ‘Tabibu, jiponye mwenyewe! Mambo yale tuliyosikia kwamba uliyafanya huko Kapernaumu, yafanye na hapa kwenye mji wako.’”
And He said to them, You truly speak to me this parable, Physician, heal thyself: so many things as we heard having been done in Capernaum, do also here in thy own country.
24 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna nabii anayekubalika katika mji wake mwenyewe.
And He said, Truly I say unto you, that no prophet is acceptable in his own country.
25 Lakini ukweli ni kwamba palikuwa na wajane wengi katika Israeli wakati wa Eliya, mbingu zilipofungwa kwa miaka mitatu na miezi sita pakawa na njaa kuu katika nchi nzima.
And in truth I say unto you, There were many widows in Israel in the days of Elijah. When the heaven was shut up three years and six months, how the famine was great over all the land;
26 Hata hivyo Eliya hakutumwa hata kwa mmoja wao, bali kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni.
and Elijah was sent to none of them, except to a widow woman in Sarepta of Sidon.
27 Pia palikuwa na wengi wenye ukoma katika Israeli katika siku za nabii Elisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyetakaswa, isipokuwa Naamani mtu wa Shamu.”
And there were many lepers in Israel in the time of the prophet Elisha; and none of them were cleansed except Naaman the Syrian.
28 Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, wakakasirika sana.
And all in the synagogue, hearing these things, were filled with wrath.
29 Wakasimama, wakamtoa nje ya mji, wakamchukua hadi kwenye kilele cha mlima mahali ambapo mji huo ulikuwa umejengwa, ili wamtupe chini kutoka kwenye mteremko mkali.
And rising up, they cast Him out of the city, and were leading Him to the brink of the mountain on which their city was built, to hurl Him down;
30 Lakini yeye akapita papo hapo katikati ya huo umati wa watu akaenda zake.
and He having passed through the midst of them went away.
31 Kisha Yesu akashuka kwenda Kapernaumu, mji wa Galilaya, na katika siku ya Sabato akawa anafundisha.
And He came down into Capernaum, a city of Galilee, And He was teaching them on the Sabbath.
32 Wakashangazwa sana na mafundisho yake, maana maneno yake yalikuwa na mamlaka.
And they were astonished at His teaching; because His word was with authority.
33 Ndani ya sinagogi palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu. Naye akapiga kelele kwa nguvu akisema,
And in the synagogue there was a man having a spirit of an unclean demon, and he cried with a great voice,
34 “Tuache! Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
saying, Let me alone; what is there to us and to thee, O Jesus the Nazarene? Hast thou come to destroy us? I know thee who thou art, the Holy One of God.
35 Basi Yesu akamkemea yule pepo mchafu, akisema, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!” Yule pepo mchafu akamwangusha yule mtu chini mbele yao wote, akatoka pasipo kumdhuru.
Jesus rebuked him, saying, Be silent and come out from him; and the demon having thrown him down in the midst came out from him, not having injured him.
36 Watu wote wakashangaa, wakaambiana, “Mafundisho haya ni ya namna gani? Anawaamuru pepo wachafu kwa mamlaka na nguvu, nao wanatoka!”
And fear came upon them all, and they were talking together to one another, saying, What word is this? because with authority and power He commands the unclean spirits, and they come out.
37 Habari zake zikaanza kuenea kila mahali katika sehemu ile.
And the report concerning Him was going out into every place in the surrounding country,
38 Yesu akatoka katika sinagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Basi huko alimkuta mama mkwe wa Simoni akiwa ameshikwa na homa kali, nao wakamwomba Yesu amsaidie.
Having arisen up from the synagogue, He came into the house of Simon. And the mother-in-law of Simon was afflicted with a great fever; and they asked Him concerning her.
39 Hivyo Yesu akamwinamia na kukemea ile homa, nayo ikamwacha. Akaamka saa ile ile, naye akaanza kuwahudumia.
And He, standing over her, rebuked the fever; and dismissed it; and immediately, having stood up, she continued to minister unto them.
40 Jua lilipokuwa linatua, watu wakamletea Yesu watu wote waliokuwa na maradhi mbalimbali, naye akaweka mikono yake juu ya kila mgonjwa, naye akawaponya.
And the sun having gone down, all so many as had people afflicted with various diseases continued to lead them to Him; and He having put His hands on each one of them, healed them.
41 Pepo wachafu pia wakawatoka watu wengi, nao walipokuwa wakitoka wakapiga kelele, wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea na kuwazuia wasiseme, kwa maana walimjua kuwa yeye ndiye Kristo.
And the demons continued to go out from many, crying, and saying, Thou art the Christ, the Son of God. And rebuking them, He did not suffer them to speak, because they knew that He was the Christ.
42 Kesho yake, kulipopambazuka, Yesu alikwenda mahali pa faragha. Watu wengi wakawa wanamtafuta kila mahali, nao walipomwona wakajaribu kumzuia asiondoke.
And it being day, having come out, He departed into a desert place: and the multitudes continued to seek Him; and they came unto Him, and they constrained Him not to depart from them.
43 Lakini yeye akawaambia, “Imenipasa kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, kwa maana kwa kusudi hili nilitumwa.”
And He said to them, That, it behooveth me to preach the gospel of the kingdom of God to many other cities: because unto this I have been sent.
44 Naye aliendelea kuhubiri katika masinagogi ya Uyahudi.
And He was preaching in the synagogues of Galilee.

< Luka 4 >