< Luka 4 >
1 Yesu, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akarudi kutoka Yordani. Akaongozwa na Roho Mtakatifu hadi nyikani,
And Jesus being full of the Holy Ghost, returned from the Jordan, and was led by the Spirit into the desert,
2 mahali ambako kwa siku arobaini alikuwa akijaribiwa na ibilisi. Kwa siku zote hizo hakula chochote, hivyo baada ya muda huo akaona njaa.
For the space of forty days; and was tempted by the devil. And he ate nothing in those days; and when they were ended, he was hungry.
3 Ibilisi akamwambia, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”
And the devil said to him: If thou be the Son of God, say to this stone that it be made bread.
4 Yesu akajibu akamwambia, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu.’”
And Jesus answered him: It is written, that Man liveth not by bread alone, but by every word of God.
5 Ibilisi akampeleka hadi juu ya mlima mrefu akamwonyesha milki zote za dunia kwa mara moja.
And the devil led him into a high mountain, and shewed him all the kingdoms of the world in a moment of time;
6 Akamwambia, “Nitakupa mamlaka juu ya milki hizi na fahari zake zote, kwa maana zimekabidhiwa mkononi mwangu nami ninaweza kumpa yeyote ninayetaka.
And he said to him: To thee will I give all this power, and the glory of them; for to me they are delivered, and to whom I will, I give them.
7 Hivyo ikiwa utanisujudia na kuniabudu, vyote vitakuwa vyako.”
If thou therefore wilt adore before me, all shall be thine.
8 Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Mwabudu Bwana Mungu wako na umtumikie yeye peke yake.’”
And Jesus answering said to him: It is written: Thou shalt adore the Lord thy God, and him only shalt thou serve.
9 Kisha ibilisi akampeleka mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa,
And he brought him to Jerusalem, and set him on a pinnacle of the temple, and he said to him: If thou be the Son of God, cast thyself from hence.
10 kwa maana imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake ili wakulinde;
For it is written, that He hath given his angels charge over thee, that they keep thee.
11 nao watakuchukua mikononi mwao, usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
And that in their hands they shall bear thee up, lest perhaps thou dash thy foot against a stone.
12 Yesu akamjibu, “Imesemwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
And Jesus answering, said to him: It is said: Thou shalt not tempt the Lord thy God.
13 Ibilisi alipomaliza kila jaribu, akamwacha Yesu mpaka wakati mwingine ufaao.
And all the temptation being ended, the devil departed from him for a time.
14 Kisha Yesu akarudi mpaka Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, nazo habari zake zikaenea katika sehemu zote za nchi za kandokando.
And Jesus returned in the power of the spirit, into Galilee, and the fame of him went out through the whole country.
15 Akaanza kufundisha kwenye masinagogi yao, na kila mmoja akamsifu.
And he taught in their synagogues, and was magnified by all.
16 Yesu akaenda Nazareti, alipolelewa, na siku ya Sabato alikwenda katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome,
And he came to Nazareth, where he was brought up: and he went into the synagogue, according to his custom, on the sabbath day; and he rose up to read.
17 naye akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na kukuta mahali palipoandikwa:
And the book of Isaias the prophet was delivered unto him. And as he unfolded the book, he found the place where it was written:
18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa sababu amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, na vipofu kupata kuona tena, kuwaweka huru wanaoonewa,
The Spirit of the Lord is upon me. Wherefore he hath anointed me to preach the gospel to the poor, he hath sent me to heal the contrite of heart,
19 na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubalika.”
To preach deliverance to the captives, and sight to the blind, to set at liberty them that are bruised, to preach the acceptable year of the Lord, and the day of reward.
20 Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
And when he had folded the book, he restored it to the minister, and sat down. And the eyes of all in the synagogue were fixed on him.
21 Ndipo akaanza kwa kuwaambia, “Leo Andiko hili limetimia mkiwa mnasikia.”
And he began to say to them: This day is fulfilled this scripture in your ears.
22 Wote waliokuwako wakamsifu na kuyastaajabia maneno yake yaliyojaa neema, wakaulizana, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”
And all gave testimony to him: and they wondered at the words of grace that proceeded from his mouth, and they said: Is not this the son of Joseph?
23 Yesu akawaambia, “Bila shaka mtatumia mithali hii: ‘Tabibu, jiponye mwenyewe! Mambo yale tuliyosikia kwamba uliyafanya huko Kapernaumu, yafanye na hapa kwenye mji wako.’”
And he said to them: Doubtless you will say to me this similitude: Physician, heal thyself: as great things as we have heard done in Capharnaum, do also here in thy own country.
24 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna nabii anayekubalika katika mji wake mwenyewe.
And he said: Amen I say to you, that no prophet is accepted in his own country.
25 Lakini ukweli ni kwamba palikuwa na wajane wengi katika Israeli wakati wa Eliya, mbingu zilipofungwa kwa miaka mitatu na miezi sita pakawa na njaa kuu katika nchi nzima.
In truth I say to you, there were many widows in the days of Elias in Israel, when heaven was shut up three years and six months, when there was a great famine throughout all the earth.
26 Hata hivyo Eliya hakutumwa hata kwa mmoja wao, bali kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni.
And to none of them was Elias sent, but to Sarepta of Sidon, to a widow woman.
27 Pia palikuwa na wengi wenye ukoma katika Israeli katika siku za nabii Elisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyetakaswa, isipokuwa Naamani mtu wa Shamu.”
And there were many lepers in Israel in the time of Eliseus the prophet: and none of them was cleansed but Naaman the Syrian.
28 Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, wakakasirika sana.
And all they in the synagogue, hearing these things, were filled with anger.
29 Wakasimama, wakamtoa nje ya mji, wakamchukua hadi kwenye kilele cha mlima mahali ambapo mji huo ulikuwa umejengwa, ili wamtupe chini kutoka kwenye mteremko mkali.
And they rose up and thrust him out of the city; and they brought him to the brow of the hill, whereon their city was built, that they might cast him down headlong.
30 Lakini yeye akapita papo hapo katikati ya huo umati wa watu akaenda zake.
But he passing through the midst of them, went his way.
31 Kisha Yesu akashuka kwenda Kapernaumu, mji wa Galilaya, na katika siku ya Sabato akawa anafundisha.
And he went down into Capharnaum, a city of Galilee, and there he taught them on the sabbath days.
32 Wakashangazwa sana na mafundisho yake, maana maneno yake yalikuwa na mamlaka.
And they were astonished at his doctrine: for his speech was with power.
33 Ndani ya sinagogi palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu. Naye akapiga kelele kwa nguvu akisema,
And in the synagogue there was a man who had an unclean devil, and he cried out with a loud voice,
34 “Tuache! Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
Saying: Let us alone, what have we to do with thee, Jesus of Nazareth? art thou come to destroy us? I know thee who thou art, the holy one of God.
35 Basi Yesu akamkemea yule pepo mchafu, akisema, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!” Yule pepo mchafu akamwangusha yule mtu chini mbele yao wote, akatoka pasipo kumdhuru.
And Jesus rebuked him, saying: Hold thy peace, and go out of him. And when the devil had thrown him into the midst, he went out of him, and hurt him not at all.
36 Watu wote wakashangaa, wakaambiana, “Mafundisho haya ni ya namna gani? Anawaamuru pepo wachafu kwa mamlaka na nguvu, nao wanatoka!”
And there came fear upon all, and they talked among themselves, saying: What word is this, for with authority and power he commandeth the unclean spirits, and they go out?
37 Habari zake zikaanza kuenea kila mahali katika sehemu ile.
And the fame of him was published into every place of the country.
38 Yesu akatoka katika sinagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Basi huko alimkuta mama mkwe wa Simoni akiwa ameshikwa na homa kali, nao wakamwomba Yesu amsaidie.
And Jesus rising up out of the synagogue, went into Simon’s house. And Simon’s wife’s mother was taken with a great fever, and they besought him for her.
39 Hivyo Yesu akamwinamia na kukemea ile homa, nayo ikamwacha. Akaamka saa ile ile, naye akaanza kuwahudumia.
And standing over her, he commanded the fever, and it left her. And immediately rising, she ministered to them.
40 Jua lilipokuwa linatua, watu wakamletea Yesu watu wote waliokuwa na maradhi mbalimbali, naye akaweka mikono yake juu ya kila mgonjwa, naye akawaponya.
And when the sun was down, all they that had any sick with divers diseases, brought them to him. But he laying his hands on every one of them, healed them.
41 Pepo wachafu pia wakawatoka watu wengi, nao walipokuwa wakitoka wakapiga kelele, wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea na kuwazuia wasiseme, kwa maana walimjua kuwa yeye ndiye Kristo.
And devils went out from many, crying out and saying: Thou art the Son of God. And rebuking them he suffered them not to speak, for they knew that he was Christ.
42 Kesho yake, kulipopambazuka, Yesu alikwenda mahali pa faragha. Watu wengi wakawa wanamtafuta kila mahali, nao walipomwona wakajaribu kumzuia asiondoke.
And when it was day, going out he went into a desert place, and the multitudes sought him, and came unto him: and they stayed him that he should not depart from them.
43 Lakini yeye akawaambia, “Imenipasa kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, kwa maana kwa kusudi hili nilitumwa.”
To whom he said: To other cities also I must preach the kingdom of God: for therefore am I sent.
44 Naye aliendelea kuhubiri katika masinagogi ya Uyahudi.
And he was preaching in the synagogues of Galilee.