< Luka 3 >

1 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato akiwa mtawala wa Uyahudi, Herode akiwa mfalme wa Galilaya, Filipo ndugu yake akiwa mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania akiwa mfalme wa Abilene,
Umwaha, ugwa kumi na tano owalongozye hwakwe Kaisari Tiberia, Pantio Pilato nali liwali owayahudi, na Herode omwene owa Galilaya, no Filipo oholo wakwe omwene uwa Iturea nensi eya Trakoniti, na Lisania no mwene owa Abilene,
2 nao Anasi na Kayafa wakiwa makuhani wakuu, neno la Mungu likamjia Yohana, mwana wa Zekaria huko jangwani.
Wakati owa kohani ogosi owa anasi no Kayafa, izu elya NGOLOBHE lya fishiye oYohana omwana owa Zakaria, mwipoli.
3 Akaenda katika nchi yote kandokando ya Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
Afishele mnsi yonti yelikaribu ne Yordani, alombeleye owoziwa owa lete usajilwa olwa hwefwe embibhi.
4 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.
Neshe shahwasimbilwe chuo eshe mazu aga kuwe Isaya, “Izu ya mntu wali mwipoli, “Lilenganyi idala elya GOSI, gagalosyaji omwashile hwakwe.
5 Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitashushwa. Njia zilizopinda zitanyooshwa, na zilizoparuza zitasawazishwa.
Entebha yonti yayimema nigamba nagamba hayisiwa, papatejile payibha pagoloshe papakwanyushe paile nganiha.
6 Nao watu wote watauona wokovu wa Mungu.’”
Bhonti abhebele bhayihulo owaule owa NGOLOBHE.”
7 Yohana akauambia ule umati wa watu uliokuwa unakuja ili kubatizwa naye, “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
Basi, abhabholele amabongano bhala bhabhaliye ili abhoziwe amwe mpapwo wenzoha wenu yabhasundile amwe ayinjile enkuni yehayenza?
8 Basi zaeni matunda yastahiliyo toba. Wala msianze kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Kwa maana nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka mawe haya.
Basi fumyaje amadondo gagahwanziwa ulusajilo, wala mgajeahwanza ayanje mmoyo genyu, “Tilinawo udada uIbrahimu eshi embabhola yaje amawe ega, ONGOLOBHE abhajiye ahwubhosrzye uIbrahimu abhana.
9 Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti. Basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.”
Neshi etwanga tayari ebhehwelwe pamashinshi age makwi. Basi, kila likwi lya sagalipapa amadondo aminza, lidumlwa nalitaje mmwoto.
10 Ule umati wa watu ukamuuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?”
Amabungano gabhozya, “Tikhozye wole eshi?”
11 Yohana akawaambia, “Aliye na kanzu mbili amgawie asiye nayo, naye aliye na chakula na afanye vivyo hivyo.”
Wabhajibu wabhabhozya, “Yali na magolola gabhele na apele yasaga aunigolola yali nevyalye wape abhombe eshoshesho.”
12 Watoza ushuru nao wakaja ili wabatizwe, wakamuuliza, “Bwana na sisi inatupasa tufanyeje?”
Bhabhasonjezya bhape bhenza ahwoziwe, bhabhozya,”Manyiziji, tubhombe yenu ate?
13 Akawaambia, “Msichukue zaidi ya kiwango mlichopangiwa.”
Wabhabhola, “Mgaje sonjezye ahantu zaidi ya hata hahapangwilwe.
14 Askari nao wakamuuliza, “Je, nasi inatupasa tufanye nini?” Akawaambia, “Msimdhulumu mtu wala msimshtaki mtu kwa uongo, bali mridhike na mishahara yenu.”
Asikali bhape bhabhozya bhayanga, “ate nate tibhombe wele? Wabhabhole msafwele omntu wala msashitake ilenka antele myanje no mshahara gwenyu.”
15 Watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wanajiuliza mioyoni mwao iwapo Yohana angeweza kuwa ndiye Kristo.
Basi, abhantu nabhali bhabhagola gaganzafumile, wonti bhasega sebhaga mmoyo gabho enongwa ezya Yohana nkashe umwene Kristi.
16 Yohana akawajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji. Lakini atakuja aliye na nguvu kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
UYohana wagalula wabhabhozya bhonti lyoli ane embozya namenze lelo ahwenza ohwemaha ashile ane sembwezizye ayengezye olwabho olye vilato vyakwe. omwahale ayibhoziwa hupepo ozelu no mwoto.
17 Pepeto lake liko mkononi, tayari kusafisha sakafu yake ya kupuria na kuikusanya ngano ghalani, lakini makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.”
Afwanaje ubheto lwakwa lulimakho no wape ayozya tee mhati yakwe na bhonganye engano yakwe. Mshanga, antele amapetelo aigapemba mmwoto gwa sagaguzima.
18 Basi, kwa maonyo mengine mengi Yohana aliwasihi na kuwahubiria watu Habari Njema.
Basi hurusundo hugamwabho aminji, abhalombeleye abhantu.
19 Lakini Yohana alipomkemea Mfalme Herode kuhusu uhusiano wake na Herodia, mke wa ndugu yake, na maovu mengine aliyokuwa amefanya,
Lelo omwene oHerode akhalipiwe nomwe kwajili ya Herode, ushe wa holo wakwe, namabhibhi gonti gabhombile o Herode.
20 Herode aliongezea jambo hili kwa hayo mengine yote: alimfunga Yohana gerezani.
Ahonjezye eli neli afunjile oyohani mwijela.
21 Baada ya watu wote kubatizwa, Yesu naye akabatizwa. Naye alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka.
Bhabhantu wonti bhabhamaushe ahinziwe no Yesu wape ahoziwe wape alabhile emwanya zya higushe.
22 Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa umbo kama la hua, nayo sauti kutoka mbinguni ikasema: “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
Upepo uzelu ahishile pamwanya yakwe hufwano ongwebelebele, neshe enjebha izu lya fumile amwanya, “Awe wemwana wane wegene. Ensogwezewe nawe.”
23 Yesu alikuwa na umri wa miaka thelathini alipoanza huduma yake. Alikuwa akidhaniwa kuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Eli,
No Yesu yoyo nahandile amanyizye, ali apate umri wakwe neshe amaha salathini. ategemelwa ajemwana wa Yusufu, wa Eli,
24 Eli alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi, Lawi alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Yanai, Yanai alikuwa mwana wa Yosefu,
Wo Mathati, walawi, wa MeIki, wayana wa Yusufu,
25 Yosefu alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Amosi, Amosi alikuwa mwana wa Nahumu, Nahumu alikuwa mwana wa Esli, Esli alikuwa mwana wa Nagai,
Wa Matathia, wa Amosi, wa Nahumu, wa Esli, wa Nagai,
26 Nagai alikuwa mwana wa Maathi, Maathi alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Semeini, Semeini alikuwa mwana wa Yoseki, Yoseki alikuwa mwana wa Yoda,
Wa Maati, wa Matathia, wa Semeini, wa Yusufu, wa Yuda,
27 Yoda alikuwa mwana wa Yoanani, Yoanani alikuwa mwana wa Resa, Resa alikuwa mwana wa Zerubabeli, Zerubabeli alikuwa mwana wa Shealtieli, Shealtieli alikuwa mwana wa Neri,
Wa Yohana, wa Rese, wa Zerubabeli, wa SheaItieli, wa Neri,
28 Neri alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Adi, Adi alikuwa mwana wa Kosamu, Kosamu alikuwa mwana wa Elmadamu, Elmadamu alikuwa mwana wa Eri,
MeIki, wa Adi, wa Kosamu, wa Elmadamu, wa Eri,
29 Eri alikuwa mwana wa Yoshua, Yoshua alikuwa mwana wa Eliezeri, Eliezeri alikuwa mwana wa Yorimu, Yorimu alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi,
Wa Yoshua, wa Eliezeri, wa Yorimu, wa Matathi, wa Lawi,
30 Lawi alikuwa mwana wa Simeoni, Simeoni alikuwa mwana wa Yuda, Yuda alikuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Yonamu, Yonamu alikuwa mwana wa Eliakimu, Eliakimu alikuwa mwana wa Melea,
Wa Simioni, wa Yuda, wa Yusufu, wa Yonamu, wa Eliyakimu,
31 Melea alikuwa mwana wa Mena, Mena alikuwa mwana wa Matatha, Matatha alikuwa mwana wa Nathani, Nathani alikuwa mwana wa Daudi,
Wa Melea, wa Mena, wa Matatha, wa nathani, wa Daudi,
32 Daudi alikuwa mwana wa Yese, Yese alikuwa mwana wa Obedi, Obedi alikuwa mwana wa Boazi, Boazi alikuwa mwana wa Salmoni, Salmoni alikuwa mwana wa Nashoni,
Wa Yese, wa Obedi, wa Boazi wa Salmoni, wa Nashoni,
33 Nashoni alikuwa mwana wa Aminadabu, Aminadabu alikuwa mwana wa Aramu, Aramu alikuwa mwana wa Hesroni, Hesroni alikuwa mwana wa Peresi, Peresi alikuwa mwana wa Yuda,
Wa Abinadabu, wa Aramu, wa Hesroni, wa Peresi, wa Yuda,
34 Yuda alikuwa mwana wa Yakobo, Yakobo alikuwa mwana wa Isaki, Isaki alikuwa mwana wa Abrahamu, Abrahamu alikuwa mwana wa Tera, Tera alikuwa mwana wa Nahori,
Wa Yakobo, wa Isaka, wa Ibrahimu, wa Tera, wa Nahori,
35 Nahori alikuwa mwana wa Serugi, Serugi alikuwa mwana wa Reu, Reu alikuwa mwana wa Pelegi, Pelegi alikuwa mwana wa Eberi, Eberi alikuwa mwana wa Sala,
Wa Seruig, wa Ragau, wa Pelegi, wa Eberi, wa Sala,
36 Sala alikuwa mwana wa Kenani, Kenani alikuwa mwana wa Arfaksadi, Arfaksadi alikuwa mwana wa Shemu, Shemu alikuwa mwana wa Noa, Noa alikuwa mwana wa Lameki,
Wa Kenani, wa Arfaksadi, wa Shemu, wa Nuhu, wa Lameki,
37 Lameki alikuwa mwana wa Methusela, Methusela alikuwa mwana wa Enoki, Enoki alikuwa mwana wa Yaredi, Yaredi alikuwa mwana wa Mahalaleli, Mahalaleli alikuwa mwana wa Kenani,
Wa Methusela, wa Henoko, wa Yaredi, wa Mahalalei, wa Kenani,
38 Kenani alikuwa mwana wa Enoshi, Enoshi alikuwa mwana wa Sethi, Sethi alikuwa mwana wa Adamu, Adamu alikuwa mwana wa Mungu.
Wa Enoshi, wa Sethi, wa Adamu, wa NGOLOBHE.

< Luka 3 >