< Luka 3 >
1 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato akiwa mtawala wa Uyahudi, Herode akiwa mfalme wa Galilaya, Filipo ndugu yake akiwa mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania akiwa mfalme wa Abilene,
Afost činčsprjače d aj kum caru alu Rimuluj Tiberije ančiput s vladjaskă. Poncije Pilat afost upravitelju ăn regije Judeje. Herod avladit ăn regije Galileje, a fratusov Filip avladit ăn regije Itureje š Trahonitide, a Lizanije avladit ăn regije Abilene.
2 nao Anasi na Kayafa wakiwa makuhani wakuu, neno la Mungu likamjia Yohana, mwana wa Zekaria huko jangwani.
Š Ana š Kaifa afost marj popurj ăn Jeruzalem. Ăn vrijamjaja Dimizov rubja alu Ivan, bijatu alu Zaharija, ăn pustinje.
3 Akaenda katika nchi yote kandokando ya Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
Jel apljikat ăn tuatje lokurj pănglă apă Jordan s rubjaskă alu lumjej k trjebje s s bătjază s pokazaskă kum sa okrinit dăla grešală š Dimizov lja oprostit grešala.
4 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.
Kum askris proroku Izaija, Ivan afost “glasu karje strigă ăn pustinje: ‘Pripremic drumu d Domnu š očistic d jel stazilje!
5 Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitashushwa. Njia zilizopinda zitanyooshwa, na zilizoparuza zitasawazishwa.
Ispunic tuată dolina š poravnic tot djalu š brjegu! Ispravic drumu karje strămb š poravnic aja čije nuje ravno!
6 Nao watu wote watauona wokovu wa Mungu.’”
Tuată lumja osă vjadje spasjala alu Dimizovuluj!”
7 Yohana akauambia ule umati wa watu uliokuwa unakuja ili kubatizwa naye, “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
Ivan rubja alu mulc lumje karje vinja s s bătjază: “Voj, šarpilor! Činje va zăs k aša d ljaznje putjec s fuđic dăla kaznă karje Dimizov trimjatje?
8 Basi zaeni matunda yastahiliyo toba. Wala msianze kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Kwa maana nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka mawe haya.
Fičec binje karje arată k vas okrinit dăla grešala avuastră. Š vu ănšălăc akă găndic k ištjec sigurni samo daja če ištjec sămănca alu Abraham. Ali jo vu zăk, Dimizov puatje d bulovanjištja s stvurjaskă kupi alu Abraham!
9 Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti. Basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.”
Dimizov uskoro osă luvjaskă ku sukurja ăn tot ljemnu karje nu dă bun plod. Tot ljemnu karje nu dă bun plod osă fije tijat š arunkat ăn fok.”
10 Ule umati wa watu ukamuuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?”
Antribat mulc lumje p Ivan: “Atunča če trjebje s fičem?”
11 Yohana akawaambia, “Aliye na kanzu mbili amgawie asiye nayo, naye aliye na chakula na afanye vivyo hivyo.”
Ivan lja zăs: “Činje arje duavă kămăšj, trjebje s dja alu ălja karje narje ničuna. A činje arje mănkarje, trjebje s podiljaskă ku ălja karje narje.”
12 Watoza ushuru nao wakaja ili wabatizwe, wakamuuliza, “Bwana na sisi inatupasa tufanyeje?”
Avinjit s s bătjază čak š carinikurlje š la tribat: “Učiteljulje, če trjebje s fičem?”
13 Akawaambia, “Msichukue zaidi ya kiwango mlichopangiwa.”
Ivan lja zăs: “Nu lăc maj marje porezu njego če je lumja datorj.”
14 Askari nao wakamuuliza, “Je, nasi inatupasa tufanye nini?” Akawaambia, “Msimdhulumu mtu wala msimshtaki mtu kwa uongo, bali mridhike na mishahara yenu.”
Š la tribat vuastja: “A če trjebje noj s fičem?” Ivan lja zăs: “Nu lăc banji dăla nimilja ku săla š p nimilja nu punjec minčunj s dobidic banji. Njego fic zadovoljni ku plata avuastră.”
15 Watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wanajiuliza mioyoni mwao iwapo Yohana angeweza kuwa ndiye Kristo.
Kum lumja očekuja k Kristu ăndată vinje, toc ăn inimă s ăntriba dal je Ivan Kristu.
16 Yohana akawajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji. Lakini atakuja aliye na nguvu kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
Daja Ivan alu toc azăs: “Jo p voj bătjez ku apa, ali vinje njeko maj marje d minje, atăta d marje k jo nu sănt dostojan čak s ji fiuv argat. Jel p voj osă bătjază ku Sufljetu alu Svăntuluj š ku foku.
17 Pepeto lake liko mkononi, tayari kusafisha sakafu yake ya kupuria na kuikusanya ngano ghalani, lakini makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.”
Jel osă fije kašă omu karje odvojaštje gruvu dăla jarbă. Gruvu osă sprimjaskă ăn ostavă, a jarba osă apringă ku foku karje nikad nu prestanjaštje s argă.”
18 Basi, kwa maonyo mengine mengi Yohana aliwasihi na kuwahubiria watu Habari Njema.
Ivan rubja alu lumjej Bună vorbă d Dimizov ku multje altje opomenje.
19 Lakini Yohana alipomkemea Mfalme Herode kuhusu uhusiano wake na Herodia, mke wa ndugu yake, na maovu mengine aliyokuwa amefanya,
Ivan la intja alu toc la ukorit p Herod, karje irja vladaru dăn regije Galileje, daja če sa ănsurat ku Herodijada, karje afost mujarja alu fratisov, š d multje altje rovj ča fukut Herod.
20 Herode aliongezea jambo hili kwa hayo mengine yote: alimfunga Yohana gerezani.
Ali kănd la ukorit Ivan, Herod p tot aja adodajit još unu rov: jel adat alu vuastja aluj s puje p Ivan ăn kisuarje.
21 Baada ya watu wote kubatizwa, Yesu naye akabatizwa. Naye alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka.
Majdată njego če p Ivan la pus ăn kisuarje, kănd Ivan bătizat p toc karje avinjit la jel, jel bătizat š p Isusu. Atunča kănd Isusu sa rugat, čerju sa diškis,
22 Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa umbo kama la hua, nayo sauti kutoka mbinguni ikasema: “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
š Sufljetu alu Svăntuluj sa slubuzăt p jel ăn oblik kašă golubu. Dăn čerj sa uzăt glasu: “Tu ješt Bijatu alu mjov p karje jo vrjauv! Tu ješt radostu alu mjov!”
23 Yesu alikuwa na umri wa miaka thelathini alipoanza huduma yake. Alikuwa akidhaniwa kuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Eli,
Kănd Isusu ančiput s rubjaskă d Dimizov la intja alu toc, avut njeđe trjezăč d aj. P Isusu l kuništja k je bijatu alu Josip. Josip afost bijatu alu Eli,
24 Eli alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi, Lawi alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Yanai, Yanai alikuwa mwana wa Yosefu,
Eli afost bijatu alu Matat, Matat afost bijatu alu Levi, Levi afost bijatu alu Malki, Malki afost bijatu alu Janaj, Janaj afost bijatu alu Josip,
25 Yosefu alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Amosi, Amosi alikuwa mwana wa Nahumu, Nahumu alikuwa mwana wa Esli, Esli alikuwa mwana wa Nagai,
Josip afost bijatu alu Matatija, Matatija afost bijatu alu Amos, Amos afost bijatu alu Naum, Naum afost bijatu alu Hesli, Hesli afost bijatu alu Nagaj,
26 Nagai alikuwa mwana wa Maathi, Maathi alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Semeini, Semeini alikuwa mwana wa Yoseki, Yoseki alikuwa mwana wa Yoda,
Nagaj afost bijatu alu Mahat, Mahat afost bijatu alu Matatija, Matatija afost bijatu alu Šimij, Šimij afost bijatu alu Joseh, Joseh afost bijatu alu Joda,
27 Yoda alikuwa mwana wa Yoanani, Yoanani alikuwa mwana wa Resa, Resa alikuwa mwana wa Zerubabeli, Zerubabeli alikuwa mwana wa Shealtieli, Shealtieli alikuwa mwana wa Neri,
Joda afost bijatu alu Johanan, Johanan afost bijatu alu Resa, Resa afost bijatu alu Zerubabel, Zerubabel afost bijatu alu Šealtiel, Šealtiel afost bijatu alu Neri,
28 Neri alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Adi, Adi alikuwa mwana wa Kosamu, Kosamu alikuwa mwana wa Elmadamu, Elmadamu alikuwa mwana wa Eri,
Neri afost bijatu alu Malki, Malki afost bijatu alu Adi, Adi afost bijatu alu Kosam, Kosam afost bijatu alu Elmadam, Elmadam afost bijatu alu Er,
29 Eri alikuwa mwana wa Yoshua, Yoshua alikuwa mwana wa Eliezeri, Eliezeri alikuwa mwana wa Yorimu, Yorimu alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi,
Er afost bijatu alu Jošua, Jošua afost bijatu alu Eliezer, Eliezer afost bijatu alu Jorim, Jorim afost bijatu alu Matat, Matat afost bijatu alu Levi,
30 Lawi alikuwa mwana wa Simeoni, Simeoni alikuwa mwana wa Yuda, Yuda alikuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Yonamu, Yonamu alikuwa mwana wa Eliakimu, Eliakimu alikuwa mwana wa Melea,
Levi afost bijatu alu Šimun, Šimun afost bijatu alu Juda, Juda afost bijatu alu Josip, Josip afost bijatu alu Jonam, Jonam afost bijatu alu Elijakim,
31 Melea alikuwa mwana wa Mena, Mena alikuwa mwana wa Matatha, Matatha alikuwa mwana wa Nathani, Nathani alikuwa mwana wa Daudi,
Elijakim afost bijatu alu Meleja, Meleja afost bijatu alu Mena, Mena afost bijatu alu Matata, Matata afost bijatu alu Natan, Natan afost bijatu alu David,
32 Daudi alikuwa mwana wa Yese, Yese alikuwa mwana wa Obedi, Obedi alikuwa mwana wa Boazi, Boazi alikuwa mwana wa Salmoni, Salmoni alikuwa mwana wa Nashoni,
David afost bijatu alu Jišaj, Jišaj afost bijatu alu Obed, Obed afost bijatu alu Boaz, Boaz afost bijatu alu Sala, Sala afost bijatu alu Nahšon,
33 Nashoni alikuwa mwana wa Aminadabu, Aminadabu alikuwa mwana wa Aramu, Aramu alikuwa mwana wa Hesroni, Hesroni alikuwa mwana wa Peresi, Peresi alikuwa mwana wa Yuda,
Nahšon afost bijatu alu Aminadab, Aminadab afost bijatu alu Admin, Admin afost bijatu alu Arni, Arni afost bijatu alu Hesron, Hesron afost bijatu alu Peres, Peres afost bijatu alu Juda,
34 Yuda alikuwa mwana wa Yakobo, Yakobo alikuwa mwana wa Isaki, Isaki alikuwa mwana wa Abrahamu, Abrahamu alikuwa mwana wa Tera, Tera alikuwa mwana wa Nahori,
Juda afost bijatu alu Jakov, Jakov afost bijatu alu Izak, Izak afost bijatu alu Abraham, Abraham afost bijatu alu Terah, Terah afost bijatu alu Nahor,
35 Nahori alikuwa mwana wa Serugi, Serugi alikuwa mwana wa Reu, Reu alikuwa mwana wa Pelegi, Pelegi alikuwa mwana wa Eberi, Eberi alikuwa mwana wa Sala,
Nahor afost bijatu alu Serug, Serug afost bijatu alu Reu, Reu afost bijatu alu Peleg, Peleg afost bijatu alu Eber, Eber afost bijatu alu Sala,
36 Sala alikuwa mwana wa Kenani, Kenani alikuwa mwana wa Arfaksadi, Arfaksadi alikuwa mwana wa Shemu, Shemu alikuwa mwana wa Noa, Noa alikuwa mwana wa Lameki,
Sala afost bijatu alu Kenan, Kenan afost bijatu alu Arpakšad, Arpakšad afost bijatu alu Šem, Šem afost bijatu alu Noa, Noa afost bijatu alu Lamek,
37 Lameki alikuwa mwana wa Methusela, Methusela alikuwa mwana wa Enoki, Enoki alikuwa mwana wa Yaredi, Yaredi alikuwa mwana wa Mahalaleli, Mahalaleli alikuwa mwana wa Kenani,
Lamek afost bijatu alu Metušalah, Metušalah afost bijatu alu Henok, Henok afost bijatu alu Jered, Jered afost bijatu alu Mahalalel, Mahalalel afost bijatu alu Kenan,
38 Kenani alikuwa mwana wa Enoshi, Enoshi alikuwa mwana wa Sethi, Sethi alikuwa mwana wa Adamu, Adamu alikuwa mwana wa Mungu.
Kenan afost bijatu alu Enoš, Enoš afost bijatu alu Šet, Šet afost bijatu alu Adam, Adam afost bijatu alu Dimizov.