< Luka 3 >
1 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato akiwa mtawala wa Uyahudi, Herode akiwa mfalme wa Galilaya, Filipo ndugu yake akiwa mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania akiwa mfalme wa Abilene,
In the fiftenthe yeare of the raygne of Tiberius the Emperoure Pontius Pylate beinge leftenaut of Iurie and Herode beinge Tetrach of Galile and his brother Philip Tetrach in Iturea and in the region of Traconites and Lysanias the Tetrach of Abyline
2 nao Anasi na Kayafa wakiwa makuhani wakuu, neno la Mungu likamjia Yohana, mwana wa Zekaria huko jangwani.
when Anna and Cayphas were the hye prestes: the worde of God came vnto Iohn ye sonne of zacharias in the wildernes.
3 Akaenda katika nchi yote kandokando ya Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
And he came in to all the coostes aboute Iordan preachynge the baptyme of repentaunce for the remission of synnes
4 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.
at it is written in the boke of the sayinges of Esaias ye Prophet which sayeth: The voyce of a cryar in wyldernes prepare the waye of the Lorde make hys pathes strayght.
5 Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitashushwa. Njia zilizopinda zitanyooshwa, na zilizoparuza zitasawazishwa.
Every valley shalbe fylled and every moutayne and hyll shalbe brought lowe. And crocked thinges shalbe made streight: and the rough wayes shalbe made smoth:
6 Nao watu wote watauona wokovu wa Mungu.’”
and all flesshe shall se the saveour sent of God.
7 Yohana akauambia ule umati wa watu uliokuwa unakuja ili kubatizwa naye, “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
Then sayde he to the people that were come to be baptysed of him: O generacion of vipers who hath taught you to flye from the wrath to come?
8 Basi zaeni matunda yastahiliyo toba. Wala msianze kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Kwa maana nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka mawe haya.
Bringe forth due frutes of repentaunce and begynne not to saye in youre selves we have Abraham to oure father. For I saye vnto you: God is able of these stones to reyse vp chyldren vnto Abraham.
9 Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti. Basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.”
Now also ys the axe leyd vnto the rote of the trees: so yt every tree which bringeth not forth good frute shalbe hewe doune and caste in to ye fyre.
10 Ule umati wa watu ukamuuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?”
And the people axed him sayinge: What shall we do then?
11 Yohana akawaambia, “Aliye na kanzu mbili amgawie asiye nayo, naye aliye na chakula na afanye vivyo hivyo.”
He answered and sayde vnto them: He that hath two coottes let him parte with him that hath none: and he that hath meate let him do lyke wyse.
12 Watoza ushuru nao wakaja ili wabatizwe, wakamuuliza, “Bwana na sisi inatupasa tufanyeje?”
Then came ther Publicans to be baptised and sayde vnto him: Master what shall we do?
13 Akawaambia, “Msichukue zaidi ya kiwango mlichopangiwa.”
And he sayde vnto the: requyre no more then that which ys appoynted vnto you.
14 Askari nao wakamuuliza, “Je, nasi inatupasa tufanye nini?” Akawaambia, “Msimdhulumu mtu wala msimshtaki mtu kwa uongo, bali mridhike na mishahara yenu.”
The soudyoures lyke wyse demaunded of hym sayinge: and what shall we do? And he sayde to them: Do violence to noo ma: nether trouble eny man wrongfully: but be content with youre wages.
15 Watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wanajiuliza mioyoni mwao iwapo Yohana angeweza kuwa ndiye Kristo.
As the people were in a doute and all men disputed in their hertes of Iohn whether he were very Christ:
16 Yohana akawajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji. Lakini atakuja aliye na nguvu kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
Ihon answered and sayde to them all: I baptyse you wt water but a stronger then I cometh after me whose shue latchet I am not worthy to vnlouse: he will baptise you with the holy goost and with fyre:
17 Pepeto lake liko mkononi, tayari kusafisha sakafu yake ya kupuria na kuikusanya ngano ghalani, lakini makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.”
which hath his fanne in his hond and will pourge his floore and will gader the corne into his barne: but the chaffe wyll he bourne with fyre that never shalbe quenched.
18 Basi, kwa maonyo mengine mengi Yohana aliwasihi na kuwahubiria watu Habari Njema.
And many other thinges in his exhortacion preached he vnto the people.
19 Lakini Yohana alipomkemea Mfalme Herode kuhusu uhusiano wake na Herodia, mke wa ndugu yake, na maovu mengine aliyokuwa amefanya,
Then Herode the Tetrach (when he was rebuked of him for Herodias his brother Philippes wyfe and for all the evyls which Herod had done)
20 Herode aliongezea jambo hili kwa hayo mengine yote: alimfunga Yohana gerezani.
added this above all and leyd Iohn in preson.
21 Baada ya watu wote kubatizwa, Yesu naye akabatizwa. Naye alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka.
And yt fortuned as all the people receaved baptyme (and when Iesus was baptised and dyd praye) that heave was opened
22 Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa umbo kama la hua, nayo sauti kutoka mbinguni ikasema: “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
and the holy goost came doune in a bodely shape lyke a dove vpo him and a voyce came fro heve sayinge: Thou arte my dere sonne in the do I delyte.
23 Yesu alikuwa na umri wa miaka thelathini alipoanza huduma yake. Alikuwa akidhaniwa kuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Eli,
And Iesus him silfe was about thirty yere of age when he begane beinge as men supposed the sonne of Ioseph. which Ioseph was the sonne of Heli
24 Eli alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi, Lawi alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Yanai, Yanai alikuwa mwana wa Yosefu,
which was the sonne of Mathat which was the sonne of Levi: which was the sonne of Melchi: which was the sonne of Ianna: which was the sonne of Ioseph:
25 Yosefu alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Amosi, Amosi alikuwa mwana wa Nahumu, Nahumu alikuwa mwana wa Esli, Esli alikuwa mwana wa Nagai,
which was the sonne of Matatthias: which was the sonne of Amos: which was the sonne of Nahum: which was the sonne of Esli: which was the sonne of Nagge:
26 Nagai alikuwa mwana wa Maathi, Maathi alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Semeini, Semeini alikuwa mwana wa Yoseki, Yoseki alikuwa mwana wa Yoda,
which was the sonne of Maath: which was the sonne of Matathias: which was the sonne of Semei: which was the sonne of Ioseph: which was the sonne of Iuda:
27 Yoda alikuwa mwana wa Yoanani, Yoanani alikuwa mwana wa Resa, Resa alikuwa mwana wa Zerubabeli, Zerubabeli alikuwa mwana wa Shealtieli, Shealtieli alikuwa mwana wa Neri,
which was the sonne of Iohanna: which was the sonne of Rhesya: which was the sonne of zorobabel: which was the sonne of Salathiel: which was the sonne of Neri:
28 Neri alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Adi, Adi alikuwa mwana wa Kosamu, Kosamu alikuwa mwana wa Elmadamu, Elmadamu alikuwa mwana wa Eri,
which was the sonne of Melchi: which was the sonne of Addi: which was the sonne of Cosam: which was the sonne of Helmadam: which was the sonne of Her:
29 Eri alikuwa mwana wa Yoshua, Yoshua alikuwa mwana wa Eliezeri, Eliezeri alikuwa mwana wa Yorimu, Yorimu alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi,
which was the sonne of Ieso: which was the sonne of Helieser: which was the sonne of Ioram: which was the sonne of Mattha: which was the sonne of Levi:
30 Lawi alikuwa mwana wa Simeoni, Simeoni alikuwa mwana wa Yuda, Yuda alikuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Yonamu, Yonamu alikuwa mwana wa Eliakimu, Eliakimu alikuwa mwana wa Melea,
which was the sonne of Simeon: which was the sonne of Iuda: which was the sonne of Ioseph: which was the sonne of Ionam: which was the sonne of Heliachim:
31 Melea alikuwa mwana wa Mena, Mena alikuwa mwana wa Matatha, Matatha alikuwa mwana wa Nathani, Nathani alikuwa mwana wa Daudi,
which was the sonne of Melea: which was the sonne of Menam: which was the sonne of Mathathan: which was the sonne of Nathan: which was the sonne of David:
32 Daudi alikuwa mwana wa Yese, Yese alikuwa mwana wa Obedi, Obedi alikuwa mwana wa Boazi, Boazi alikuwa mwana wa Salmoni, Salmoni alikuwa mwana wa Nashoni,
which was the sonne of Iesse: which was the sonne of Obed: which was the sonne of Boos: which was the sonne of Salmon: which was the sonne of Naason:
33 Nashoni alikuwa mwana wa Aminadabu, Aminadabu alikuwa mwana wa Aramu, Aramu alikuwa mwana wa Hesroni, Hesroni alikuwa mwana wa Peresi, Peresi alikuwa mwana wa Yuda,
which was the sonne of Aminadab: which was the sonne of Aram: which was the sonne of Esrom: which was the sonne of Phares: which was the sonne of Iuda:
34 Yuda alikuwa mwana wa Yakobo, Yakobo alikuwa mwana wa Isaki, Isaki alikuwa mwana wa Abrahamu, Abrahamu alikuwa mwana wa Tera, Tera alikuwa mwana wa Nahori,
which was the sonne of Iacob: which was the sonne of Ysaac: which was the sonne of Abraham: which was the sonne of Tharra: which was the sonne of Nachor:
35 Nahori alikuwa mwana wa Serugi, Serugi alikuwa mwana wa Reu, Reu alikuwa mwana wa Pelegi, Pelegi alikuwa mwana wa Eberi, Eberi alikuwa mwana wa Sala,
which was the sonne of Saruch: which was the sonne of Ragau: which was the sonne of Phalec: which was the sonne of Heber: which was the sonne of Sala:
36 Sala alikuwa mwana wa Kenani, Kenani alikuwa mwana wa Arfaksadi, Arfaksadi alikuwa mwana wa Shemu, Shemu alikuwa mwana wa Noa, Noa alikuwa mwana wa Lameki,
which was the sonne of Cainan: which was the sonne of Arphaxat: which was the sonne of Sem: which was the sonne of Noe: which was the sonne of Lameth:
37 Lameki alikuwa mwana wa Methusela, Methusela alikuwa mwana wa Enoki, Enoki alikuwa mwana wa Yaredi, Yaredi alikuwa mwana wa Mahalaleli, Mahalaleli alikuwa mwana wa Kenani,
which was the sonne of Mathusala: which was the sonne of Enoch: which was the sonne of Iareth: which was the sonne of Malalehel. which was the sonne of Cainan:
38 Kenani alikuwa mwana wa Enoshi, Enoshi alikuwa mwana wa Sethi, Sethi alikuwa mwana wa Adamu, Adamu alikuwa mwana wa Mungu.
which was the sonne of Enos: which was the sonne of Seth: which was the sonne of Adam: which was the sonne of God.