< Luka 3 >
1 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato akiwa mtawala wa Uyahudi, Herode akiwa mfalme wa Galilaya, Filipo ndugu yake akiwa mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania akiwa mfalme wa Abilene,
NOW in the fifteenth year of the reign of Tiberios Cesar, in the government of Pontios Pilatos in Jehud, Herodes being chief of the Fourth in Galila, and Philipos his brother chief of the Fourth in Ituria and in the region of Trakona, and Lusania chief of the Fourth of Abilini;
2 nao Anasi na Kayafa wakiwa makuhani wakuu, neno la Mungu likamjia Yohana, mwana wa Zekaria huko jangwani.
in the high priesthood of Chanan and of Kaiopha, was the word of Aloha unto Juchanon bar Zakaria in the desert.
3 Akaenda katika nchi yote kandokando ya Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
And he came into the whole country about the Jurdan, preaching the baptism of repentance for the remission of sins.
4 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.
As it is written in the book of the words of Eshaia the prophet, who said, The voice which crieth in the desert, Prepare the way of the Lord, And make straight in the plain the highways for our Aloha.
5 Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitashushwa. Njia zilizopinda zitanyooshwa, na zilizoparuza zitasawazishwa.
All valleys shall be filled, And all mountains and heights be brought low, And the mound shall be a level (place), And the rough place a plain,
6 Nao watu wote watauona wokovu wa Mungu.’”
And all flesh shall see the salvation of Aloha.
7 Yohana akauambia ule umati wa watu uliokuwa unakuja ili kubatizwa naye, “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
And he said to those multitudes who came to him to be baptized, O brood of vipers, who hath showed you to flee from the wrath that cometh?
8 Basi zaeni matunda yastahiliyo toba. Wala msianze kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Kwa maana nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka mawe haya.
Work therefore fruits which are worthy of repentance. And begin not to say within yourselves that Abraham is father to us; for I tell you, that from these stones Aloha is able to raise up sons unto Abraham.
9 Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti. Basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.”
But, behold, the axe is laid at the root of the trees. Every tree therefore which good fruit maketh not, is cut down and into the fire falleth.
10 Ule umati wa watu ukamuuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?”
And the assemblies inquired of him, saying, What then shall we do?
11 Yohana akawaambia, “Aliye na kanzu mbili amgawie asiye nayo, naye aliye na chakula na afanye vivyo hivyo.”
He answered and said to them, Whoever hath two tunics, let him give to him who hath none; and whoever hath food, so let him do (likewise).
12 Watoza ushuru nao wakaja ili wabatizwe, wakamuuliza, “Bwana na sisi inatupasa tufanyeje?”
The publicans also came to be baptized, and they said to him, Malphona, what shall we do?
13 Akawaambia, “Msichukue zaidi ya kiwango mlichopangiwa.”
But he said to them, Demand not any thing more upon what is prescribed to you to require.
14 Askari nao wakamuuliza, “Je, nasi inatupasa tufanye nini?” Akawaambia, “Msimdhulumu mtu wala msimshtaki mtu kwa uongo, bali mridhike na mishahara yenu.”
And the military servants asked of him and said, What shall we also do? And he said to them, Molest no man, oppress no man, and let your wages satisfy you.
15 Watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wanajiuliza mioyoni mwao iwapo Yohana angeweza kuwa ndiye Kristo.
But while the people thought concerning Juchanon, and all of them reasoned in their hearts whether he were the Meshicha,
16 Yohana akawajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji. Lakini atakuja aliye na nguvu kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
Juchanon answered and said to them, Behold, I baptize you with waters, but there cometh after me He who is mightier than I; He, the latchet of whose sandals I am not worthy to unloose; He shall baptize you with the Spirit of Holiness and with fire:
17 Pepeto lake liko mkononi, tayari kusafisha sakafu yake ya kupuria na kuikusanya ngano ghalani, lakini makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.”
He who, holding the fan in his hand, and cleansing his floors, gathereth the wheat into his garners, and the chaff he will burn in the fire which is not quenched.
18 Basi, kwa maonyo mengine mengi Yohana aliwasihi na kuwahubiria watu Habari Njema.
But many other things he also taught and preached to the people.
19 Lakini Yohana alipomkemea Mfalme Herode kuhusu uhusiano wake na Herodia, mke wa ndugu yake, na maovu mengine aliyokuwa amefanya,
But Herodes Tetrarka, because he was reproved by Juchanon concerning Herodia the wife of Philipos his brother, and concerning all the evil things which he had done,
20 Herode aliongezea jambo hili kwa hayo mengine yote: alimfunga Yohana gerezani.
added this also upon all, and shut up Juchanon in the house of the chained.
21 Baada ya watu wote kubatizwa, Yesu naye akabatizwa. Naye alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka.
But it was when he had baptized all the people, and also Jeshu he baptized. And while he prayed,
22 Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa umbo kama la hua, nayo sauti kutoka mbinguni ikasema: “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
the heavens were opened, and the Spirit of Holiness descended upon him in the bodily likeness of a dove: and the voice was from the heavens, which said, Thou art my Son the Beloved One, in thee I have delighted.
23 Yesu alikuwa na umri wa miaka thelathini alipoanza huduma yake. Alikuwa akidhaniwa kuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Eli,
NOW Jeshu himself was as a son of thirty years, and was considered the son of Jauseph bar Heli,
24 Eli alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi, Lawi alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Yanai, Yanai alikuwa mwana wa Yosefu,
bar Mattath, bar Levi, bar Malki, bar Jani, bar Jauseph,
25 Yosefu alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Amosi, Amosi alikuwa mwana wa Nahumu, Nahumu alikuwa mwana wa Esli, Esli alikuwa mwana wa Nagai,
bar Mattha, bar Amuts, bar Nachum, bar Chesli, bar Nagi,
26 Nagai alikuwa mwana wa Maathi, Maathi alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Semeini, Semeini alikuwa mwana wa Yoseki, Yoseki alikuwa mwana wa Yoda,
bar Math, bar Matath, bar Shemri, bar Jauseph, bar Jihuda,
27 Yoda alikuwa mwana wa Yoanani, Yoanani alikuwa mwana wa Resa, Resa alikuwa mwana wa Zerubabeli, Zerubabeli alikuwa mwana wa Shealtieli, Shealtieli alikuwa mwana wa Neri,
bar Juchanon, bar Rosa, bar Zurbobel, bar Shelathiel, bar Niri,
28 Neri alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Adi, Adi alikuwa mwana wa Kosamu, Kosamu alikuwa mwana wa Elmadamu, Elmadamu alikuwa mwana wa Eri,
bar Malki, bar Adi, bar Kusam, bar Elmudod, bar Ir,
29 Eri alikuwa mwana wa Yoshua, Yoshua alikuwa mwana wa Eliezeri, Eliezeri alikuwa mwana wa Yorimu, Yorimu alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi,
bar Jose, bar Eleazar, bar Juram, bar Mathitha, bar Levi,
30 Lawi alikuwa mwana wa Simeoni, Simeoni alikuwa mwana wa Yuda, Yuda alikuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Yonamu, Yonamu alikuwa mwana wa Eliakimu, Eliakimu alikuwa mwana wa Melea,
bar Shemun, bar Jihuda, bar Jauseph, bar Jonam, bar Eliakim,
31 Melea alikuwa mwana wa Mena, Mena alikuwa mwana wa Matatha, Matatha alikuwa mwana wa Nathani, Nathani alikuwa mwana wa Daudi,
bar Malia, bar Mani, bar Mattha, bar Nathan, bar David,
32 Daudi alikuwa mwana wa Yese, Yese alikuwa mwana wa Obedi, Obedi alikuwa mwana wa Boazi, Boazi alikuwa mwana wa Salmoni, Salmoni alikuwa mwana wa Nashoni,
bar Jeshi, bar Ubid, bar Boos, bar Salmon, bar Nachshun,
33 Nashoni alikuwa mwana wa Aminadabu, Aminadabu alikuwa mwana wa Aramu, Aramu alikuwa mwana wa Hesroni, Hesroni alikuwa mwana wa Peresi, Peresi alikuwa mwana wa Yuda,
bar Aminodob, bar Aram, bar Chetsrun, bar Pharets, bar Jihuda,
34 Yuda alikuwa mwana wa Yakobo, Yakobo alikuwa mwana wa Isaki, Isaki alikuwa mwana wa Abrahamu, Abrahamu alikuwa mwana wa Tera, Tera alikuwa mwana wa Nahori,
bar Jakub, bar Ishok, bar Abraham, bar Tarach, bar Nachur,
35 Nahori alikuwa mwana wa Serugi, Serugi alikuwa mwana wa Reu, Reu alikuwa mwana wa Pelegi, Pelegi alikuwa mwana wa Eberi, Eberi alikuwa mwana wa Sala,
bar Soruk, bar Aru, bar Pholeg, bar Ebor, bar Shaloch,
36 Sala alikuwa mwana wa Kenani, Kenani alikuwa mwana wa Arfaksadi, Arfaksadi alikuwa mwana wa Shemu, Shemu alikuwa mwana wa Noa, Noa alikuwa mwana wa Lameki,
bar Kainan, bar Arphakshad, bar Shim, bar Nuch, bar Lamek,
37 Lameki alikuwa mwana wa Methusela, Methusela alikuwa mwana wa Enoki, Enoki alikuwa mwana wa Yaredi, Yaredi alikuwa mwana wa Mahalaleli, Mahalaleli alikuwa mwana wa Kenani,
bar Mathushalach, bar Chanuk, bar Jared, bar Mahloleel, bar Kainan,
38 Kenani alikuwa mwana wa Enoshi, Enoshi alikuwa mwana wa Sethi, Sethi alikuwa mwana wa Adamu, Adamu alikuwa mwana wa Mungu.
bar Anush, bar Sheth, bar Adom, who was from Aloha.