< Luka 24 >
1 Mnamo siku ya kwanza ya juma, alfajiri na mapema, wale wanawake walichukua yale manukato waliyokuwa wameyaandaa, wakaenda kaburini.
Nädala esimese päeva varahommikul võtsid naised kaasa lõhnarohud, mis nad olid valmis pannud, ja läksid hauale.
2 Wakakuta lile jiwe limevingirishwa kutoka kwenye kaburi,
Nad leidsid kivi haua eest ära lükatuna,
3 lakini walipoingia ndani, hawakuuona mwili wa Bwana Yesu.
aga kui nad hauda sisse läksid, ei leidnud nad sealt Issanda Jeesuse ihu.
4 Walipokuwa wanashangaa juu ya jambo hili, ghafula watu wawili waliokuwa wamevaa mavazi yanayongʼaa kama umeme wakasimama karibu nao.
Ja kui nad selle üle pead murdsid, seisid järsku nende kõrval kaks meest välguna helkivates riietes.
5 Wale wanawake, wakiwa na hofu, wakainamisha nyuso zao mpaka chini. Lakini wale watu wakawaambia, “Kwa nini mnamtafuta aliye hai miongoni mwa wafu?
Aga kui naised hirmunult näoga vastu maad kummardasid, ütlesid mehed neile: „Miks te otsite elavat surnute juurest?“
6 Hayuko hapa; amefufuka! Kumbukeni alivyowaambia alipokuwa bado yuko pamoja nanyi huko Galilaya kwamba:
Teda ei ole siin! Ta on üles tõusnud! Tuletage meelde, mida ta teile ütles veel Galileas olles:
7 ‘Ilikuwa lazima Mwana wa Adamu atiwe mikononi mwa watu wenye dhambi na waovu ili asulubiwe, na siku ya tatu afufuke.’”
„Inimese Poeg tuleb anda patuste kätte ja risti lüüa ja kolmandal päeval ta tõuseb jälle üles.“
8 Ndipo wakayakumbuka maneno ya Yesu.
Siis neile meenusid Jeesuse sõnad.
9 Waliporudi kutoka huko kaburini, wakawaeleza wale wanafunzi kumi na mmoja pamoja na wengine wote mambo haya yote.
Kui nad pöördusid haua juurest tagasi, kuulutasid nad kõike seda neile üheteistkümnele ja kõigile teistele.
10 Basi Maria Magdalene, Yoana, na Maria mama yake Yakobo, pamoja na wanawake wengine waliofuatana nao ndio waliwaelezea mitume habari hizi.
Need olid Maarja Magdaleena ja Johanna ja Maarja, Jaakobuse ema, ja teised naised koos nendega, kes rääkisid sellest apostlitele.
11 Lakini hawakuwasadiki hao wanawake, kwa sababu maneno yao yalionekana kama upuzi.
Aga nad ei uskunud nende juttu, see tundus neile kui mõttetus.
12 Hata hivyo, Petro akainuka na kukimbia kwenda kule kaburini. Alipoinama kuchungulia, akaona vile vitambaa vya kitani, ila hakuona kitu kingine. Naye akaenda zake akijiuliza nini kilichotokea.
Peetrus aga tõusis püsti ja jooksis haua juurde. Ja kummargil sisse vaadates nägi ta surilinu ning ta läks ära pead murdes selle üle, mis oli sündinud.
13 Ikawa siku iyo hiyo, wanafunzi wawili wa Yesu walikuwa njiani wakienda kijiji kilichoitwa Emau, yapata maili saba kutoka Yerusalemu.
Selsamal päeval läksid kaks nendest külla nimega Emmaus, see on Jeruusalemmast umbes üheteistkümne kilomeetri kaugusel.
14 Walikuwa wakizungumza wao kwa wao kuhusu mambo yote yaliyotukia.
Nad vestlesid omavahel kõigest, mis oli juhtunud.
15 Walipokuwa wakizungumza na kujadiliana, Yesu mwenyewe akaja akatembea pamoja nao,
Ja kui nad vestlesid ning neid asju arutasid, tuli nende juurde Jeesus ise ja kõndis nendega kaasa,
16 lakini macho yao yakazuiliwa ili wasimtambue.
aga nad ei tundnud teda ära.
17 Akawauliza, “Ni mambo gani haya mnayozungumza wakati mnatembea?” Wakasimama, nyuso zao zikionyesha huzuni.
Jeesus küsis nende käest: „Mida te siin omavahel kõndides arutate?“Nad seisid vaikselt ja vaatasid kurvalt maha.
18 Mmoja wao, aliyeitwa Kleopa, akamuuliza, “Je, wewe ndiye peke yako mgeni huku Yerusalemu ambaye hufahamu mambo yaliyotukia humo siku hizi?”
Üks neist, Kleopas, küsis tema käest: „Sa oled vist ainus külaline Jeruusalemmas, kes veel ei tea, mis neil päevil seal on juhtunud?“
19 Akawauliza, “Mambo gani?” Wakamjibu, “Mambo ya Yesu wa Nazareti. Yeye alikuwa nabii, mwenye uwezo mkuu katika maneno yake na matendo yake, mbele za Mungu na mbele ya wanadamu wote.
„Mis siis?“küsis ta. „See, mis juhtus Naatsareti Jeesusega, “vastasid nemad. „Ta oli prohvet, vägev sõnalt ja tegudelt Jumala ja kõigi inimeste ees.
20 Viongozi wa makuhani na viongozi wetu walimtoa ahukumiwe kufa, nao wakamsulubisha.
Ülempreestrid ja meie valitsejad andsid ta ära surmamõistmiseks ja lõid ta risti,
21 Lakini tulikuwa tumetegemea kwamba yeye ndiye angelikomboa Israeli. Zaidi ya hayo, leo ni siku ya tatu tangu mambo haya yatokee.
aga meie lootsime, et tema ongi see, kes Iisraeli lunastab. Ja veel enam, täna on kolmas päev, kui see kõik juhtus.
22 Isitoshe, baadhi ya wanawake katika kundi letu wametushtusha. Walikwenda kaburini leo alfajiri,
Lisaks panid mõned naised meid hämmastuma. Nad käisid täna hommikul haua juures,
23 lakini hawakuukuta mwili wake. Walirudi wakasema wameona maono ya malaika ambao waliwaambia kwamba Yesu yu hai.
kuid ei leidnud tema ihu. Naised tulid ja rääkisid meile, et olid näinud nägemust inglitest, kes ütlesid, et Jeesus on elus.
24 Kisha baadhi ya wenzetu walikwenda kaburini wakalikuta kama vile wale wanawake walivyokuwa wamesema, lakini yeye hawakumwona.”
Siis mõned meie kaaslastest läksid haua juurde ja leidsid selle täpselt, nagu naised olid öelnud; teda ennast nad aga ei näinud.“
25 Yesu akawaambia, “Ninyi ni wajinga kiasi gani, nanyi ni wazito mioyoni mwenu kuamini mambo yote yaliyonenwa na manabii!
Ja tema ütles neile: „Kui taipamatud te olete ja kui aeglased oma südames uskuma kõike, mida prohvetid on rääkinud!
26 Je, haikumpasa Kristokuteswa kwa njia hiyo na kisha aingie katika utukufu wake?”
Kas Messias ei pidanud seda kõike kannatama ja oma kirkusesse astuma?“
27 Naye akianzia na Sheria ya Mose na Manabii wote, akawafafanulia jinsi Maandiko yalivyosema kumhusu yeye.
Ning alustades Moosesest ja kõikidest prohvetitest, seletas Jeesus neile, mida Pühakiri tema kohta ütles.
28 Nao walipokaribia kile kijiji walichokuwa wakienda, Yesu akawa kama anaendelea mbele.
Ja kui nad lähenesid külale, kuhu nad olid minemas, tegi Jeesus, nagu ta läheks edasi.
29 Lakini wao wakamsihi sana akae nao, wakisema, “Kaa hapa nasi, kwa maana sasa ni jioni na usiku unaingia.” Basi akaingia ndani kukaa nao.
Aga nad käisid talle peale: „Jää meie juurde, sest peagi on õhtu. Päev on kohe lõppemas!“Ja tema läks sisse ja jäi nendega.
30 Alipokuwa mezani pamoja nao, akachukua mkate, akashukuru, akaumega, akaanza kuwagawia.
Kui ta nendega lauas istus, võttis ta leiva, õnnistas ja murdis ning andis neile.
31 Ndipo macho yao yakafumbuliwa, nao wakamtambua, naye akatoweka machoni pao. Hawakumwona tena.
Siis avati nende silmad ja nad tundsid ta ära! Ja ta kadus nende silmist.
32 Wakaulizana wao kwa wao, “Je, mioyo yetu haikuwakawaka kwa furaha ndani yetu alipokuwa anazungumza nasi njiani na kutufafanulia Maandiko?”
Nad küsisid üksteiselt: „Eks meie südamed põlenud meie sees, kui ta tee peal meiega rääkis ja meile Pühakirja avas?“
33 Wakaondoka mara, wakarudi Yerusalemu. Wakawakuta wale wanafunzi kumi na mmoja na wale waliokuwa pamoja nao, wamekusanyika
Nad tõusid ja läksid tagasi Jeruusalemma. Seal nad leidsid üksteist jüngrit ja teised koos nendega,
34 wakisema, “Ni kweli! Bwana amefufuka, naye amemtokea Simoni.”
kes ütlesid: „See on tõsi! Issand on tõesti üles tõusnud ja Siimonile ilmunud!“
35 Kisha wale wanafunzi wawili wakaeleza yaliyotukia njiani na jinsi walivyomtambua Yesu alipoumega mkate.
Siis need kaks rääkisid, mis oli tee peal sündinud ja kuidas nad Jeesuse leiva murdmisest ära tundsid.
36 Walipokuwa bado wanazungumza hayo, Yesu mwenyewe akasimama katikati yao, akasema, “Amani iwe nanyi!”
Kui nad sellest alles rääkisid, seisis Jeesus ise nende keskel ja ütles: „Rahu olgu teiega!“
37 Wakashtuka na kuogopa wakidhani kwamba wameona mzuka.
Nad olid jahmunud ja hirmul, arvates, et nad näevad vaimu.
38 Lakini Yesu akawauliza, “Kwa nini mnaogopa? Kwa nini mna shaka mioyoni mwenu?
Ta ütles neile: „Miks te olete ärevuses ja miks on kahtlus tõusnud teie meeltesse?
39 Tazameni mikono yangu na miguu yangu, mwone kuwa ni mimi hasa. Niguseni mwone; kwa maana mzuka hauna nyama na mifupa, kama mnionavyo kuwa navyo.”
Vaadake mu käsi ja mu jalgu. See olen mina! Puudutage mind ja vaadake, sest vaimul ei ole liha ja luid, aga te näete, et minul on!“
40 Aliposema haya, akawaonyesha mikono na miguu yake.
Ja seda öeldes näitas Jeesus neile oma käsi ja jalgu.
41 Wakashindwa kuamini kwa ajili ya furaha na mshangao waliokuwa nao. Akawauliza, “Mna chakula chochote hapa?”
Aga kui nad rõõmu pärast ikka veel ei uskunud ja imestasid, küsis ta nende käest: „Kas teil on siin midagi süüa?“
42 Wakampa kipande cha samaki aliyeokwa,
Nad andsid talle tüki küpsetatud kala ja meekärge,
43 naye akakichukua na kukila mbele yao.
ja Jeesus võttis ja sõi nende ees.
44 Akawaambia, “Haya ndiyo yale niliyowaambia nilipokuwa bado niko pamoja nanyi, kwamba yote yaliyoandikwa kunihusu mimi katika Sheria ya Mose, Manabii na Zaburi hayana budi kutimizwa.”
Ta ütles neile: „Need on mu sõnad, mis ma teile ütlesin, kui ma olin veel teiega: kõik peab täide minema, mis Moosese Seaduses, prohvetites ja lauludes on minu kohta kirjutatud.“
45 Ndipo akafungua fahamu zao ili waweze kuyaelewa Maandiko.
Siis ta avas nende mõistuse, et nad saaksid Pühakirjast aru.
46 Akawaambia, “Haya ndiyo yaliyoandikwa: Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka kwa wafu.
Ja ütles neile: „Nõnda on kirjutatud, et Messias pidi kannatama ja kolmandal päeval üles tõusma surnuist,
47 Toba na msamaha wa dhambi zitatangaziwa mataifa yote kupitia jina lake kuanzia Yerusalemu.
ja tema nimel peab kuulutatama meeleparandust pattude andeksandmiseks kõigi rahvaste seas, alates Jeruusalemmast.
48 Ninyi ni mashahidi wa mambo haya.
Teie olete nende asjade tunnistajad.
49 “Tazama nitawatumia ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini hadi mtakapovikwa uwezo utokao juu.”
Mina läkitan teie peale oma Isa tõotuse! Teie aga jääge sellesse linna seni, kuni teid on riietatud taevase väega!“
50 Akiisha kuwaongoza mpaka kwenye viunga vya Bethania, akainua mikono yake juu na kuwabariki.
Jeesus viis nad välja Betaania lähedale, tõstis oma käed ja õnnistas neid.
51 Alipokuwa anawabariki, akawaacha, akachukuliwa mbinguni.
Ja neid õnnistades lahkus Jeesus nende juurest ja võeti üles taevasse.
52 Kisha wakamwabudu na kurudi Yerusalemu wakiwa wamejawa na furaha kuu.
Nemad aga kummardasid teda ja pöördusid suure rõõmuga tagasi Jeruusalemma.
53 Nao wakadumu ndani ya Hekalu wakimtukuza Mungu. Amen.
Ja viibisid püsivalt templis Jumalat kiites.