< Luka 24 >

1 Mnamo siku ya kwanza ya juma, alfajiri na mapema, wale wanawake walichukua yale manukato waliyokuwa wameyaandaa, wakaenda kaburini.
Now upon the first [day] of the week, very early in the morning, they came to the sepulcher, bringing the spices which they had prepared, and certain [others] with them.
2 Wakakuta lile jiwe limevingirishwa kutoka kwenye kaburi,
And they found the stone rolled away from the sepulcher.
3 lakini walipoingia ndani, hawakuuona mwili wa Bwana Yesu.
And they entered in, and found not the body of the Lord Jesus.
4 Walipokuwa wanashangaa juu ya jambo hili, ghafula watu wawili waliokuwa wamevaa mavazi yanayongʼaa kama umeme wakasimama karibu nao.
And it came to pass, as they were much perplexed at this, behold, two men stood by them in shining garments.
5 Wale wanawake, wakiwa na hofu, wakainamisha nyuso zao mpaka chini. Lakini wale watu wakawaambia, “Kwa nini mnamtafuta aliye hai miongoni mwa wafu?
And as they were afraid, and bowed down [their] faces to the earth, they said to them, Why seek ye the living among the dead?
6 Hayuko hapa; amefufuka! Kumbukeni alivyowaambia alipokuwa bado yuko pamoja nanyi huko Galilaya kwamba:
He is not here, but is risen. Remember how he spoke to you when he was yet in Galilee,
7 ‘Ilikuwa lazima Mwana wa Adamu atiwe mikononi mwa watu wenye dhambi na waovu ili asulubiwe, na siku ya tatu afufuke.’”
Saying, The Son of man must be delivered into the hands of sinful men, and be crucified, and the third day rise again.
8 Ndipo wakayakumbuka maneno ya Yesu.
And they remembered his words,
9 Waliporudi kutoka huko kaburini, wakawaeleza wale wanafunzi kumi na mmoja pamoja na wengine wote mambo haya yote.
And returned from the sepulcher, and told all these things to the eleven, and to all the rest.
10 Basi Maria Magdalene, Yoana, na Maria mama yake Yakobo, pamoja na wanawake wengine waliofuatana nao ndio waliwaelezea mitume habari hizi.
It was Mary Magdalene, and Joanna, and Mary [the mother] of James, and other [women that were] with them, who told these things to the apostles.
11 Lakini hawakuwasadiki hao wanawake, kwa sababu maneno yao yalionekana kama upuzi.
And their words seemed to them as idle tales, and they believed them not.
12 Hata hivyo, Petro akainuka na kukimbia kwenda kule kaburini. Alipoinama kuchungulia, akaona vile vitambaa vya kitani, ila hakuona kitu kingine. Naye akaenda zake akijiuliza nini kilichotokea.
Then Peter arose, and ran to the sepulcher, and stooping down, he beheld the linen clothes laid by themselves, and departed, wondering in himself at that which had come to pass.
13 Ikawa siku iyo hiyo, wanafunzi wawili wa Yesu walikuwa njiani wakienda kijiji kilichoitwa Emau, yapata maili saba kutoka Yerusalemu.
And behold, two of them went that same day to a village called Emmaus, which was from Jerusalem [about] sixty furlongs.
14 Walikuwa wakizungumza wao kwa wao kuhusu mambo yote yaliyotukia.
And they talked together of all these things which had happened.
15 Walipokuwa wakizungumza na kujadiliana, Yesu mwenyewe akaja akatembea pamoja nao,
And it came to pass, that, while they communed [together], and reasoned, Jesus himself drew near, and went with them.
16 lakini macho yao yakazuiliwa ili wasimtambue.
But their eyes were held, that they should not know him.
17 Akawauliza, “Ni mambo gani haya mnayozungumza wakati mnatembea?” Wakasimama, nyuso zao zikionyesha huzuni.
And he said to them, What manner of communications [are] these that ye have one to another, as ye walk, and are sad?
18 Mmoja wao, aliyeitwa Kleopa, akamuuliza, “Je, wewe ndiye peke yako mgeni huku Yerusalemu ambaye hufahamu mambo yaliyotukia humo siku hizi?”
And one of them, whose name was Cleopas, answering, said to him, Art thou only a stranger in Jerusalem, and hast not known the things which have come to pass there in these days?
19 Akawauliza, “Mambo gani?” Wakamjibu, “Mambo ya Yesu wa Nazareti. Yeye alikuwa nabii, mwenye uwezo mkuu katika maneno yake na matendo yake, mbele za Mungu na mbele ya wanadamu wote.
And he said to them, What things? And they said to him, Concerning Jesus of Nazareth, who was a prophet mighty in deed and word before God, and all the people:
20 Viongozi wa makuhani na viongozi wetu walimtoa ahukumiwe kufa, nao wakamsulubisha.
And how the chief priests and our rulers delivered him to be condemned to death, and crucified him.
21 Lakini tulikuwa tumetegemea kwamba yeye ndiye angelikomboa Israeli. Zaidi ya hayo, leo ni siku ya tatu tangu mambo haya yatokee.
But we trusted that it had been he who would have redeemed Israel: and besides all this, to-day is the third day since these things were done.
22 Isitoshe, baadhi ya wanawake katika kundi letu wametushtusha. Walikwenda kaburini leo alfajiri,
Yes, and certain women also of our company made us astonished, who were early at the sepulcher.
23 lakini hawakuukuta mwili wake. Walirudi wakasema wameona maono ya malaika ambao waliwaambia kwamba Yesu yu hai.
And when they found not his body, they came, saying, that they had also seen a vision of angels, who said that he was alive.
24 Kisha baadhi ya wenzetu walikwenda kaburini wakalikuta kama vile wale wanawake walivyokuwa wamesema, lakini yeye hawakumwona.”
And certain of them who were with us, went to the sepulcher, and found [it] even so as the women had said: but him they saw not.
25 Yesu akawaambia, “Ninyi ni wajinga kiasi gani, nanyi ni wazito mioyoni mwenu kuamini mambo yote yaliyonenwa na manabii!
Then he said to them, O fools, and slow of heart to believe all that the prophets have spoken!
26 Je, haikumpasa Kristokuteswa kwa njia hiyo na kisha aingie katika utukufu wake?”
Ought not Christ to suffer these things, and to enter into his glory?
27 Naye akianzia na Sheria ya Mose na Manabii wote, akawafafanulia jinsi Maandiko yalivyosema kumhusu yeye.
And beginning at Moses, and all the prophets, he expounded to them in all the scriptures the things concerning himself.
28 Nao walipokaribia kile kijiji walichokuwa wakienda, Yesu akawa kama anaendelea mbele.
And they drew nigh to the village whither they were going: and he made as though he would go further.
29 Lakini wao wakamsihi sana akae nao, wakisema, “Kaa hapa nasi, kwa maana sasa ni jioni na usiku unaingia.” Basi akaingia ndani kukaa nao.
But they constrained him, saying, Abide with us: for it is towards evening, and the day is far spent. And he went in to tarry with them.
30 Alipokuwa mezani pamoja nao, akachukua mkate, akashukuru, akaumega, akaanza kuwagawia.
And it came to pass, as he sat at table with them, he took bread, and blessed [it], and broke, and gave to them.
31 Ndipo macho yao yakafumbuliwa, nao wakamtambua, naye akatoweka machoni pao. Hawakumwona tena.
And their eyes were opened, and they knew him: and he vanished out of their sight.
32 Wakaulizana wao kwa wao, “Je, mioyo yetu haikuwakawaka kwa furaha ndani yetu alipokuwa anazungumza nasi njiani na kutufafanulia Maandiko?”
And they said one to another, Did not our heart burn within us while he talked with us by the way, and while he opened to us the scriptures?
33 Wakaondoka mara, wakarudi Yerusalemu. Wakawakuta wale wanafunzi kumi na mmoja na wale waliokuwa pamoja nao, wamekusanyika
And they rose the same hour, and returned to Jerusalem, and found the eleven assembled, and them that were with them,
34 wakisema, “Ni kweli! Bwana amefufuka, naye amemtokea Simoni.”
Saying, The Lord is risen indeed, and hath appeared to Simon.
35 Kisha wale wanafunzi wawili wakaeleza yaliyotukia njiani na jinsi walivyomtambua Yesu alipoumega mkate.
And they told what things [were done] in the way, and how he was known to them in breaking of bread.
36 Walipokuwa bado wanazungumza hayo, Yesu mwenyewe akasimama katikati yao, akasema, “Amani iwe nanyi!”
And as they were thus speaking, Jesus himself stood in the midst of them, and saith to them, Peace [be] to you.
37 Wakashtuka na kuogopa wakidhani kwamba wameona mzuka.
But they were terrified and affrighted, and supposed that they had seen a spirit.
38 Lakini Yesu akawauliza, “Kwa nini mnaogopa? Kwa nini mna shaka mioyoni mwenu?
And he said to them, Why are ye troubled? and why do thoughts arise in your hearts?
39 Tazameni mikono yangu na miguu yangu, mwone kuwa ni mimi hasa. Niguseni mwone; kwa maana mzuka hauna nyama na mifupa, kama mnionavyo kuwa navyo.”
Behold my hands and my feet, that it is I myself: handle me, and see; for a spirit hath not flesh and bones, as ye see me have.
40 Aliposema haya, akawaonyesha mikono na miguu yake.
And when he had thus spoken, he showed them [his] hands and [his] feet.
41 Wakashindwa kuamini kwa ajili ya furaha na mshangao waliokuwa nao. Akawauliza, “Mna chakula chochote hapa?”
And while they yet believed not for joy, and wondered, he said to them, Have ye here any thing for food?
42 Wakampa kipande cha samaki aliyeokwa,
And they gave him a piece of a broiled fish, and a honey-comb.
43 naye akakichukua na kukila mbele yao.
And he took [it], and ate before them.
44 Akawaambia, “Haya ndiyo yale niliyowaambia nilipokuwa bado niko pamoja nanyi, kwamba yote yaliyoandikwa kunihusu mimi katika Sheria ya Mose, Manabii na Zaburi hayana budi kutimizwa.”
And he said to them, These [are] the words which I spoke to you, while I was yet with you, that all things must be fulfilled, which were written in the law of Moses, and [in] the prophets, and [in] the psalms, concerning me.
45 Ndipo akafungua fahamu zao ili waweze kuyaelewa Maandiko.
Then he opened their understanding, that they might understand the scriptures,
46 Akawaambia, “Haya ndiyo yaliyoandikwa: Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka kwa wafu.
And said to them, Thus it is written, and thus it behooved Christ to suffer, and to rise from the dead the third day:
47 Toba na msamaha wa dhambi zitatangaziwa mataifa yote kupitia jina lake kuanzia Yerusalemu.
And that repentance and remission of sins should be preached in his name among all nations, beginning at Jerusalem.
48 Ninyi ni mashahidi wa mambo haya.
And ye are witnesses of these things.
49 “Tazama nitawatumia ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini hadi mtakapovikwa uwezo utokao juu.”
And behold, I send the promise of my Father upon you: but tarry ye in the city of Jerusalem, until ye are endued with power from on high.
50 Akiisha kuwaongoza mpaka kwenye viunga vya Bethania, akainua mikono yake juu na kuwabariki.
And he led them out as far as to Bethany: and he lifted up his hands, and blessed them.
51 Alipokuwa anawabariki, akawaacha, akachukuliwa mbinguni.
And it came to pass, while he was blessing them, he was parted from them, and carried up into heaven.
52 Kisha wakamwabudu na kurudi Yerusalemu wakiwa wamejawa na furaha kuu.
And they worshiped him, and returned to Jerusalem with great joy:
53 Nao wakadumu ndani ya Hekalu wakimtukuza Mungu. Amen.
And were continually in the temple, praising and blessing God. Amen.

< Luka 24 >