< Luka 23 >

1 Kisha umati wote wa watu ukainuka na kumpeleka Yesu kwa Pilato.
tataH sabhAsthAH sarvvalOkA utthAya taM pIlAtasammukhaM nItvAprOdya vaktumArEbhirE,
2 Nao wakaanza kumshtaki wakisema: “Tumemwona huyu mtu akipotosha taifa letu, akiwazuia watu wasilipe kodi kwa Kaisari na kujiita kuwa yeye ni Kristo, mfalme.”
svamabhiSiktaM rAjAnaM vadantaM kaimararAjAya karadAnaM niSEdhantaM rAjyaviparyyayaM kurttuM pravarttamAnam Ena prAptA vayaM|
3 Basi Pilato akamuuliza Yesu, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe wasema.”
tadA pIlAtastaM pRSTavAn tvaM kiM yihUdIyAnAM rAjA? sa pratyuvAca tvaM satyamuktavAn|
4 Pilato akawaambia viongozi wa makuhani na watu wote waliokuwepo, “Sioni sababu ya kutosha kumshtaki mtu huyu!”
tadA pIlAtaH pradhAnayAjakAdilOkAn jagAd, ahamEtasya kamapyaparAdhaM nAptavAn|
5 Lakini wao wakakazana kusema, “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika Uyahudi yote, tangu Galilaya alikoanzia, hadi sehemu hii!”
tatastE punaH sAhaminO bhUtvAvadan, ESa gAlIla EtatsthAnaparyyantE sarvvasmin yihUdAdEzE sarvvAllOkAnupadizya kupravRttiM grAhItavAn|
6 Pilato aliposikia hayo akauliza, “Huyu mtu ni Mgalilaya?”
tadA pIlAtO gAlIlapradEzasya nAma zrutvA papraccha, kimayaM gAlIlIyO lOkaH?
7 Alipofahamu kwamba Yesu alikuwa chini ya mamlaka ya Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa pia Yerusalemu.
tataH sa gAlIlpradEzIyahErOdrAjasya tadA sthitEstasya samIpE yIzuM prESayAmAsa|
8 Herode alipomwona Yesu alifurahi sana, kwa sababu kwa muda mrefu alikuwa amesikia mambo mengi kumhusu yeye. Pia alitarajia kumwona akifanya miujiza kadha wa kadha.
tadA hErOd yIzuM vilOkya santutOSa, yataH sa tasya bahuvRttAntazravaNAt tasya kinjicadAzcaryyakarmma pazyati ityAzAM kRtvA bahukAlamArabhya taM draSTuM prayAsaM kRtavAn|
9 Herode akamuuliza maswali mengi, lakini Yesu hakumjibu lolote.
tasmAt taM bahukathAH papraccha kintu sa tasya kasyApi vAkyasya pratyuttaraM nOvAca|
10 Wakati huo viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwepo wakitoa mashtaka yao kwa nguvu sana.
atha pradhAnayAjakA adhyApakAzca prOttiSThantaH sAhasEna tamapavadituM prArEbhirE|
11 Herode na askari wake wakamdhihaki Yesu na kumfanyia mzaha. Wakamvika vazi zuri sana, wakamrudisha kwa Pilato.
hErOd tasya sEnAgaNazca tamavajnjAya upahAsatvEna rAjavastraM paridhApya punaH pIlAtaM prati taM prAhiNOt|
12 Siku hiyo, Herode na Pilato wakawa marafiki; kabla ya jambo hili walikuwa na uadui kati yao.
pUrvvaM hErOdpIlAtayOH parasparaM vairabhAva AsIt kintu taddinE dvayO rmElanaM jAtam|
13 Basi Pilato akawaita pamoja viongozi wa makuhani, viongozi wengine na watu,
pazcAt pIlAtaH pradhAnayAjakAn zAsakAn lOkAMzca yugapadAhUya babhASE,
14 akawaambia, “Ninyi mlimleta huyu mtu kwangu kana kwamba ni mtu anayewachochea watu ili waasi. Nimemhoji mbele yenu nami nimeona hakuna msingi wowote wa mashtaka yenu dhidi yake.
rAjyaviparyyayakArakOyam ityuktvA manuSyamEnaM mama nikaTamAnaiSTa kintu pazyata yuSmAkaM samakSam asya vicAraM kRtvApi prOktApavAdAnurUpENAsya kOpyaparAdhaH sapramANO na jAtaH,
15 Wala Herode hakumwona na kosa lolote, ndiyo sababu amemrudisha kwetu. Kama mnavyoona, mtu huyu hakufanya jambo lolote linalostahili kifo.
yUyanjca hErOdaH sannidhau prESitA mayA tatrAsya kOpyaparAdhastEnApi na prAptaH|pazyatAnEna vadhahEtukaM kimapi nAparAddhaM|
16 Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi na kumwachia.” [
tasmAdEnaM tAPayitvA vihAsyAmi|
17 Kwa kuwa ilikuwa lazima kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa Sikukuu.]
tatrOtsavE tESAmEkO mOcayitavyaH|
18 Ndipo watu wote wakapiga kelele kwa pamoja, “Mwondoe mtu huyo! Tufungulie Baraba!”
iti hEtOstE prOccairEkadA prOcuH, EnaM dUrIkRtya barabbAnAmAnaM mOcaya|
19 (Baraba alikuwa amefungwa gerezani kwa sababu ya maasi yaliyokuwa yametokea mjini, na kwa ajili ya uuaji.)
sa barabbA nagara upaplavavadhAparAdhAbhyAM kArAyAM baddha AsIt|
20 Pilato, akitaka kumwachia Yesu, akasema nao tena.
kintu pIlAtO yIzuM mOcayituM vAnjchan punastAnuvAca|
21 Lakini wao wakaendelea kupiga kelele wakisema, “Msulubishe! Msulubishe!”
tathApyEnaM kruzE vyadha kruzE vyadhEti vadantastE ruruvuH|
22 Kwa mara ya tatu, Pilato akawauliza, “Kwani amefanya kosa gani huyu mtu? Sikuona kwake sababu yoyote inayostahili adhabu ya kifo. Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi, na kisha nitamwachia.”
tataH sa tRtIyavAraM jagAda kutaH? sa kiM karmma kRtavAn? nAhamasya kamapi vadhAparAdhaM prAptaH kEvalaM tAPayitvAmuM tyajAmi|
23 Lakini watu wakazidi kupiga kelele kwa nguvu zaidi, wakidai kwamba Yesu asulubiwe. Hivyo, kelele zao zikashinda.
tathApi tE punarEnaM kruzE vyadha ityuktvA prOccairdRPhaM prArthayAnjcakrirE;
24 Kwa hiyo Pilato akatoa hukumu kwamba madai yao yatimizwe.
tataH pradhAnayAjakAdInAM kalaravE prabalE sati tESAM prArthanArUpaM karttuM pIlAta AdidEza|
25 Akamfungua yule mtu aliyekuwa amefungwa gerezani kwa kuhusika katika uasi dhidi ya serikali na mauaji. Akamkabidhi Yesu mikononi mwao, wamfanyie watakavyo.
rAjadrOhavadhayOraparAdhEna kArAsthaM yaM janaM tE yayAcirE taM mOcayitvA yIzuM tESAmicchAyAM samArpayat|
26 Walipokuwa wakienda naye, wakamkamata mtu mmoja aitwaye Simoni mwenyeji wa Kirene, aliyekuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shambani. Wakambebesha msalaba, wakamlazimisha auchukue nyuma ya Yesu.
atha tE yIzuM gRhItvA yAnti, Etarhi grAmAdAgataM zimOnanAmAnaM kurINIyaM janaM dhRtvA yIzOH pazcAnnEtuM tasya skandhE kruzamarpayAmAsuH|
27 Idadi kubwa ya watu wakamfuata Yesu, wakiwamo wanawake waliokuwa wakimlilia na kumwombolezea.
tatO lOkAraNyamadhyE bahustriyO rudatyO vilapantyazca yIzOH pazcAd yayuH|
28 Yesu akawageukia, akawaambia, “Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi bali jililieni ninyi wenyewe na watoto wenu.
kintu sa vyAghuTya tA uvAca, hE yirUzAlamO nAryyO yuyaM madarthaM na ruditvA svArthaM svApatyArthanjca ruditi;
29 Kwa maana wakati utafika mtakaposema, ‘Wamebarikiwa wanawake tasa, ambao matumbo yao hayakuzaa, wala matiti yao hayakunyonyesha!’
pazyata yaH kadApi garbhavatyO nAbhavan stanyanjca nApAyayan tAdRzI rvandhyA yadA dhanyA vakSyanti sa kAla AyAti|
30 Ndipo “‘wataiambia milima, “Tuangukieni!” na vilima, “Tufunikeni!”’
tadA hE zailA asmAkamupari patata, hE upazailA asmAnAcchAdayata kathAmIdRzIM lOkA vakSyanti|
31 Kwa maana kama wamefanya hivi kwa mti mbichi, kwa mti mkavu itakuwaje?”
yataH satEjasi zAkhini cEdEtad ghaTatE tarhi zuSkazAkhini kiM na ghaTiSyatE?
32 Watu wengine wawili wahalifu, walipelekwa pamoja na Yesu ili wakasulubiwe.
tadA tE hantuM dvAvaparAdhinau tEna sArddhaM ninyuH|
33 Walipofika mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, hapo ndipo walipomsulubisha Yesu pamoja na hao wahalifu, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wake wa kushoto.
aparaM ziraHkapAlanAmakasthAnaM prApya taM kruzE vividhuH; taddvayOraparAdhinOrEkaM tasya dakSiNO tadanyaM vAmE kruzE vividhuH|
34 Yesu akasema, “Baba, wasamehe, kwa maana hawajui walitendalo!” Wakagawana nguo zake kwa kupiga kura.
tadA yIzurakathayat, hE pitarEtAn kSamasva yata EtE yat karmma kurvvanti tan na viduH; pazcAttE guTikApAtaM kRtvA tasya vastrANi vibhajya jagRhuH|
35 Watu wakasimama hapo wakimwangalia, nao viongozi wa Wayahudi wakamdhihaki wakisema, “Aliokoa wengine! Ajiokoe mwenyewe basi, kama yeye ndiye Kristo wa Mungu, Mteule wake.”
tatra lOkasaMghastiSThan dadarza; tE tESAM zAsakAzca tamupahasya jagaduH, ESa itarAn rakSitavAn yadIzvarENAbhirucitO 'bhiSiktastrAtA bhavati tarhi svamadhunA rakSatu|
36 Askari nao wakaja, wakamdhihaki. Wakamletea siki ili anywe,
tadanyaH sEnAgaNA Etya tasmai amlarasaM datvA parihasya prOvAca,
37 na wakamwambia, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.”
cEttvaM yihUdIyAnAM rAjAsi tarhi svaM rakSa|
38 Kwenye msalaba juu ya kichwa chake, kulikuwa na maandishi haya: Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi. Maandishi haya yalikuwa yameandikwa kwa lugha za Kiyunani, Kilatini na Kiebrania.
yihUdIyAnAM rAjEti vAkyaM yUnAnIyarOmIyEbrIyAkSarai rlikhitaM tacchirasa UrddhvE'sthApyata|
39 Mmoja wa wale wahalifu waliosulubiwa pamoja naye akamtukana, akasema: “Wewe si ndiye Kristo? Jiokoe mwenyewe na utuokoe na sisi.”
tadObhayapArzvayO rviddhau yAvaparAdhinau tayOrEkastaM vinindya babhASE, cEttvam abhiSiktOsi tarhi svamAvAnjca rakSa|
40 Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake, akasema, “Je, wewe humwogopi Mungu, wakati uko kwenye adhabu iyo hiyo?
kintvanyastaM tarjayitvAvadat, IzvarAttava kinjcidapi bhayaM nAsti kiM? tvamapi samAnadaNPOsi,
41 Sisi tumehukumiwa kwa haki kwa kuwa tunapata tunayostahili kwa ajili ya matendo yetu. Lakini huyu mtu hajafanya kosa lolote.”
yOgyapAtrE AvAM svasvakarmmaNAM samucitaphalaM prApnuvaH kintvanEna kimapi nAparAddhaM|
42 Kisha akasema, “Yesu, unikumbuke utakapokuja katika Ufalme wako.”
atha sa yIzuM jagAda hE prabhE bhavAn svarAjyapravEzakAlE mAM smaratu|
43 Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
tadA yIzuH kathitavAn tvAM yathArthaM vadAmi tvamadyaiva mayA sArddhaM paralOkasya sukhasthAnaM prApsyasi|
44 Ilikuwa kama saa sita mchana, nalo giza likafunika nchi yote hadi saa tisa,
aparanjca dvitIyayAmAt tRtIyayAmaparyyantaM ravEstEjasOntarhitatvAt sarvvadEzO'ndhakArENAvRtO
45 kwa sababu jua liliacha kutoa nuru. Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili.
mandirasya yavanikA ca chidyamAnA dvidhA babhUva|
46 Yesu akapaza sauti yake akasema, “Baba, mikononi mwako naikabidhi roho yangu.” Baada ya kusema haya, akakata roho.
tatO yIzuruccairuvAca, hE pita rmamAtmAnaM tava karE samarpayE, ityuktvA sa prANAn jahau|
47 Yule jemadari alipoona yaliyotukia, akamsifu Mungu, akasema, “Hakika, mtu huyu alikuwa mwenye haki.”
tadaitA ghaTanA dRSTvA zatasEnApatirIzvaraM dhanyamuktvA kathitavAn ayaM nitAntaM sAdhumanuSya AsIt|
48 Watu wote waliokuwa wamekusanyika hapo kushuhudia tukio hili walipoyaona hayo, wakapigapiga vifua vyao kwa huzuni na kwenda zao.
atha yAvantO lOkA draSTum AgatAstE tA ghaTanA dRSTvA vakSaHsu karAghAtaM kRtvA vyAcuTya gatAH|
49 Lakini wale wote waliomfahamu, pamoja na wale wanawake waliokuwa wamemfuata kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiyatazama mambo haya.
yIzO rjnjAtayO yA yA yOSitazca gAlIlastEna sArddhamAyAtAstA api dUrE sthitvA tat sarvvaM dadRzuH|
50 Basi kulikuwa na mtu mmoja mwema na mwenye haki, jina lake Yosefu. Yeye alikuwa mjumbe wa Baraza la Wayahudi,
tadA yihUdIyAnAM mantraNAM kriyAnjcAsammanyamAna Izvarasya rAjatvam apEkSamANO
51 lakini yeye hakuwa amekubaliana na maamuzi na vitendo vya viongozi wenzake. Huyu alikuwa mwenyeji wa Arimathaya huko Uyahudi, naye alikuwa anaungojea Ufalme wa Mungu kwa matarajio makubwa.
yihUdidEzIyO 'rimathIyanagarIyO yUSaphnAmA mantrI bhadrO dhArmmikazca pumAn
52 Yosefu alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
pIlAtAntikaM gatvA yIzO rdEhaM yayAcE|
53 Akaushusha kutoka msalabani, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi, na kuuweka katika kaburi lililochongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limezikiwa mtu mwingine bado.
pazcAd vapuravarOhya vAsasA saMvESTya yatra kOpi mAnuSO nAsthApyata tasmin zailE svAtE zmazAnE tadasthApayat|
54 Ilikuwa Siku ya Maandalizi, nayo Sabato ilikuwa karibu kuanza.
taddinamAyOjanIyaM dinaM vizrAmavArazca samIpaH|
55 Wale wanawake waliokuwa wamekuja pamoja na Yesu wakimfuata kutoka Galilaya wakamfuata Yosefu, wakaliona kaburi na jinsi mwili wa Yesu ulivyolazwa.
aparaM yIzunA sArddhaM gAlIla AgatA yOSitaH pazcAditvA zmazAnE tatra yathA vapuH sthApitaM tacca dRSTvA
56 Kisha wakarudi nyumbani, wakaandaa manukato na marhamu ya kuupaka huo mwili. Lakini wakapumzika siku ya Sabato kama ilivyoamriwa.
vyAghuTya sugandhidravyatailAni kRtvA vidhivad vizrAmavArE vizrAmaM cakruH|

< Luka 23 >