< Luka 22 >

1 Wakati huu Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa imekaribia.
Bushiku bwakukondwa bwa kulya shinkwa wabula cishikufufumusha, ubo bwalikukwiweti Pasika mpobwalashika pepi.
2 Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwa wanatafuta njia ya kumuua Yesu, kwa sababu waliwaogopa watu.
Bamakulene beshimilumbo, ne beshikwiyisha Milawo balikabayandaula nshila yakushininamo Yesu. Nomba bali kutina bantu.
3 Shetani akamwingia Yuda, aliyeitwa Iskariote, mmoja wa wale Kumi na Wawili.
Lino Satana walengila muli Yudasi, walikukwiweti Isikalyoti, uyo walikuba umo wa beshikwiya bali likumi ne babili ba Yesu.
4 Yuda akaenda kwa viongozi wa makuhani na kwa maafisa wa walinzi wa Hekalu, akazungumza nao jinsi ambavyo angeweza kumsaliti Yesu.
Neco Yudasi walaya kupangana ne bamakulene beshimilumbo ne beshikwendelesha Ng'anda ya Lesa ncobela kwinsa kwambeti amuyabe Yesu kulyendibo.
5 Wakafurahi na wakakubaliana kumpa fedha.
Lino balakondwa, kayi balasuminishana kumulipila mali.
6 Naye akakubali, akaanza kutafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Yesu kwao, wakati ambapo hakuna umati wa watu.
Yudasi walasumina ne kutatika kuyandaula cindi caina cakumuyabilapo, bantu bonse kabatacinshi.
7 Basi ikawadia siku ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa.
Bwalashika busuba bwakukondwa bwakulya shinkwa wakutafufumusha, busuba bwakushina twana twambelele twakulya pabusuba bwa Pasika.
8 Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohana, akisema, “Nendeni mkatuandalie chakula cha Pasaka ili tuweze kuila.”
Lino Yesu walatuma Petulo ne Yohane ne kubambileti, “Kamuyani mutubambile byakulya bya pabusuba bwa Pasika kwambeti tulye.”
9 Wakamuuliza, “Unataka tukuandalie wapi?”
Balo balamwipusheti, “Nikupeyo nkomulayandanga kwambeti twenga tubambile?”
10 Yesu akawaambia, “Tazameni, mtakapokuwa mkiingia mjini, mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka kwenye nyumba atakayoingia.
Yesu walabambileti, “Kamunyumfwani! mwengila mu Yelusalemu nimucane mutuloba wanyamuna nongo ya menshi, mu mukonkele mpaka mung'anda moshi engile.
11 Nanyi mwambieni mwenye nyumba, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’
Lino mu mwambile mwine ng'andeti, Bashikwiyisha balepushungeti, ‘Nomba cili kupeyo cipinda moshi balyele byakulya bya Pasika ne beshikwiya babo’
12 Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani, kikiwa kimepambwa vizuri. Andaeni humo.”
Lino na amuboneshe cipinda cinene ca pelu cabambiwa cena, mopelomo emoti mutubambile byakulya.”
13 Wakaenda, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.
Lino balaya kucana bintu byonse mbuli mwalabambilila Yesu. Lino balatatika kubamba byakulya bya Pasika.
14 Wakati ulipowadia, Yesu akaketi mezani pamoja na wale mitume wake.
Lino mpocalashika cindi cakulya Yesu walekala pa tebulu pamo ne batumwa bakendi kwambeti balye.
15 Kisha akawaambia, “Nimetamani sana kuila Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
Lino Yesu walabambileti, “Ndayandishishanga kulya Pasika pamo nenjamwe nkantana kutatika kupenshewa.
16 Kwa maana, nawaambia, sitaila tena Pasaka mpaka itakapotimizwa katika Ufalme wa Mungu.”
Ndamwambilinga cakubinga nteshi nkalyepo Pasika, kushikila cikakwanilishiwe mu Bwami bwa Lesa.”
17 Akiisha kukichukua kikombe, akashukuru, akasema, “Chukueni hiki mnywe wote.
Lino Yesu mpwalamanta nkomeshi nekulumba Lesa, walabambileti, “Kamutambulani munwe mwense.
18 Kwa maana nawaambia tangu sasa sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
Lino ndamwambilinga kufuma lelo nteshi nkanwepo waini, kushikila Bwami bwa Lesa bukese.”
19 Kisha akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa, akisema, “Huu ni mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”
Kufumapo Yesu walamanta shinkwa, walalumba Lesa, nekukomona nekupa beshikwiya bakendi nekwambeti, “Uyu emubili wakame ulayabwa cebo canjamwe. Kamwinsanga ici lyonse pakunganukila.”
20 Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, imwagikayo kwa ajili yenu.
Copeleco mpobalapwisha kulya mulalilo, Yesu walapa beshikwiya bakendi nkomeshi nekubambileti, “Nkomeshi iyi nicipangano calino lino ca Lesa, nemilopa yakame yeshi iketike pacebo cenu.
21 Lakini mkono wake huyo atakayenisaliti uko hapa mezani pamoja nami.
“Nsombi kamubona! Uyo lanjabanga kubalwani lalinga pamo nenjame patebulu pano.
22 Mwana wa Adamu anaenda zake kama ilivyokusudiwa. Lakini ole wake mtu huyo amsalitiye.”
Pakwinga Mwana Muntu nakafwe kwelana ne kuyanda kwa Lesa. Nsombi muntu lamuyabanga Mwana Muntu nakapenge. Caina muntuyo nalabula kusemwa.”
23 Wakaanza kuulizana wenyewe ni nani miongoni mwao angeweza kufanya jambo hilo.
Lino beshikwiya balatatika kulipusheti, nomba welakwinseco niyani pakati petu.
24 Pia yakazuka mabishano katikati ya wanafunzi kwamba ni nani aliyeonekana kuwa mkuu kuliko wote miongoni mwao.
Lino beshikwiya balatatika kupikishaneti, “Inga niyani mukulene pakati petu?”
25 Yesu akawaambia, “Wafalme na watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu. Nao wenye mamlaka juu yao hujiita ‘Wafadhili.’
Lino Yesu walabambileti, “Bami ba bantu bakunsa bakute ngofu pabantu babo kayi bakute kulyela masuku pamutwi bantu, bakute kukwiweti, ‘Beshikwinsa byaina kubantu.’
26 Lakini ninyi msifanane nao. Bali yeye aliye mkuu kuliko wote miongoni mwenu, inampasa kuwa kama yeye aliye mdogo wa wote, naye atawalaye na awe kama yeye ahudumuye.
Nsombi pakati penu citabanga mushoboyu. Cakubinga mukulene pali amwe abe weshikulicepesha kupita bonse, neye weshi kwendelesha abe musha wenu.
27 Kwani ni nani aliye mkuu? Ni yule aketiye mezani au ni yule ahudumuye? Si ni yule aliyekaa mezani? Lakini mimi niko miongoni mwenu kama yule ahudumuye.
Nomba mukulene niyani? Sena ni usa lalinga pa tebulu na ni musha? Sena nte usa lalyelenga pa tebulu? Nomba ame ndilyeti musha pakati penu.
28 Ninyi mmekuwa pamoja nami katika majaribu yangu.
“Amwe mulekala nenjame mumasunko akame onse.
29 Nami kama Baba yangu alivyonipa ufalme, kadhalika mimi nami ninawapa ninyi,
Lino copeleco, mbuli ba Ta ncobalampa ngofu shakwendelesha, nenjame nindimupeni ngofu.
30 ili mpate kula na kunywa mezani pangu katika karamu ya ufalme wangu, na kukaa katika viti vya enzi, mkihukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.”
Nimukalye ne kunwa pamo nenjame, kayi nimukekale pabipuna bya Bwami ne kubeteka mishobo likumi ne ibili ya ba Isilaeli.”
31 Yesu akasema, “Simoni, Simoni, sikiliza, Shetani ameomba kuwapepeta ninyi wote kama ngano.
“Shimoni, Shimoni, nyumfwa! Satana layandanga kumupupulusha mumasunko mbuli mulimi ncakute kupupulusha maila.
32 Lakini nimekuombea wewe Simoni ili imani yako isishindwe, nawe ukiisha kunirudia, uwaimarishe ndugu zako.”
Nsombi ndakupailili kwambeti lushomo lwakobe lutapwa. Lino obe wakatembenuka mumuyo ukayuminishe banobe.”
33 Petro akajibu, “Bwana, niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani na hata kifoni.”
Nsombi Petulo walakumbuleti, “Mwami, ame ndalibambila kuya nenjamwe mujele nambi kufwa.”
34 Yesu akamjibu, “Ninakuambia Petro, kabla jogoo hajawika usiku wa leo, utakana mara tatu kwamba hunijui mimi.”
Yesu walakumbuleti, “Ndakwambilinga Petulo, lelo kombwe nkatana alila, nunkane mankanda atatu eti nkonjinshipo.”
35 Kisha Yesu akawauliza, “Nilipowatuma bila mfuko, wala mkoba, wala viatu, mlipungukiwa na kitu chochote?” Wakajibu, “La, hatukupungukiwa na kitu chochote.”
Yesu walepusha beshikwiya bakendi eti, “Pasa mpondalamutuma nkamubulile mpotomona, cola nambi nkwabilo nomba nicani ncomwapengapo?” Balo balakumbuleti, “Kuliyawa.”
36 Akawaambia, “Lakini sasa, aliye na mfuko na auchukue, na aliye na mkoba vivyo hivyo. Naye asiye na upanga, auze joho lake anunue mmoja.
Lino walabambileti, “Muntu uliyense ukute mpotomona nambi cola, anyamune. Neye uyo wabula mupeni, aulishe byakufwala byakendi kwambeti aule mupeni.
37 Kwa sababu, nawaambia, andiko hili lazima litimizwe juu yangu, kwamba, ‘Alihesabiwa pamoja na wakosaji’; kwa kweli yaliyoandikwa kunihusu mimi hayana budi kutimizwa.”
Cakubinga celela kwinshika calalembwa Mumabala eti, ‘Neye balamubelengela pamo ne babwipishi.’ Ndamwambilingeti Mabala aya alenshikinga cancinencine.”
38 Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, tazama hapa kuna panga mbili.” Akawajibu, “Inatosha.”
Beshikwiya balambeti, “Kamubona Mwami tukute bibeshi bibili,” Yesu walabakumbuleti, “Ni ningi byopelebyo.”
39 Yesu akatoka, akaenda kwenye Mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa kawaida yake, nao wanafunzi wake wakamfuata.
Yesu walafumamo mu Yelusalemu nekuya ku mulundu wa maolifi mbuli ncalikwinsa lyonse. Naboyo beshikwiya bakendi balamukonkela.
40 Walipofika huko, akawaambia wanafunzi wake, “Ombeni, msije mkaingia majaribuni.”
Mpwalashika pamusena uyo Yesu walabambileti, “Kamupailani kwambeti mutengila mumasunko.”
41 Akajitenga nao kama umbali wa kutupa jiwe, akapiga magoti, akaomba
Lino Yesu walabashiya, walendako pang'ana walafukama nekupaila.
42 akisema, “Baba, kama ni mapenzi yako, niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo, bali mapenzi yako yatendeke.”
Walambeti, “Bata, na musuni kamufunyani nkomeshi ya mapensho iyi. Necikabeco mutensa kuyanda kwakame, nsombi mwinse kuyanda kwenu.”
43 Malaika kutoka mbinguni akamtokea, akamtia nguvu.
Lino mungelo wakwilu walesa kumuyuminisha.
44 Naye akiwa katika maumivu makuu, akaomba kwa bidii, nalo jasho lake likawa kama matone ya damu yakidondoka ardhini.
Pacebo cakupenshewa mumoyo, walapaila cangofu kupita pakutanguna. Lino inkasalo yakendi yalikubeti mandondo a milopa alakanga panshi.
45 Baada ya kuomba, akawarudia wanafunzi wake akawakuta wamelala, wakiwa wamechoka kutokana na huzuni.
Mpwalafuma akupaila walabwelela kuli beshikwiya bakendi. Walacana nkabalibona pacebo ca miyeyo,
46 Naye akawauliza, “Mbona mmelala? Amkeni, mwombe ili msije mkaingia majaribuni.”
Yesu walabepusheti, “Nipacebo cini mona tulo? Kamupundukani mupaile kwambeti mutengila mumasunko.”
47 Yesu alipokuwa bado anazungumza, umati mkubwa wa watu ukaja. Uliongozwa na Yuda, ambaye alikuwa mmoja wa wale wanafunzi Kumi na Wawili. Akamkaribia Yesu ili ambusu.
Yesu nkacamba, likoto lya bantu, lyalesa kalili lyatanguninwa ne Yudasi, umo wabeshikwiya likumi nebabili. Walesa pepi walamupa mutende ne kumushonshota.
48 Lakini Yesu akamwambia, “Yuda, je, unamsaliti Mwana wa Adamu kwa busu?”
Nsombi Yesu walamwambileti, “Yudasi, sena ulayabanga Mwana Muntu kupitila mukumushonshota?”
49 Wafuasi wa Yesu walipoona yale yaliyokuwa yanakaribia kutokea, wakasema, “Bwana, tuwakatekate kwa panga zetu?”
Lino beshikwiya balikuba ne Yesu mpobalabona calikwinshika balepusha Yesu eti, “Mwami, Se tubayase ne bibeshi?”
50 Mmoja wao akampiga mtumishi wa kuhani mkuu kwa upanga, akamkata sikio la kuume.
Lino umo wa beshikwiya walatimbula litwi lya kululyo lya musebenshi wa mukulene wa beshimilumbo bonse.
51 Lakini Yesu akasema, “Acheni!” Akaligusa lile sikio la yule mtu na kumponya.
Nsombi Yesu walambeti, “Cilekeni kwinseco.” Popelapo Yesu walekata litwi lya muntu uyo nekumushilika.
52 Kisha Yesu akawaambia wale viongozi wa makuhani, maafisa wa walinzi wa Hekalu, pamoja na wazee waliokuwa wamekuja kumkamata, “Mmekuja na panga na marungu, kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi?
Yesu walambila bonse abo balesa kumwikata, bamakulene ba beshimilumbo nebamukulene baba kamulonda ba Ng'anda ya Lesa, kayi nebamakulene ba Bayuda. Walabepusheti, “Sena mulenshi kwisa ne mipeni nemingwala eti nde kapondo?
53 Siku kwa siku nilikuwa pamoja nanyi Hekaluni lakini hamkunikamata. Lakini hii ni saa yenu, wakati giza linatawala!”
Ndalikuba nenjamwe mu Ng'anda ya Lesa lyonse, nomba muliya kunjikatapo. Lino cino cindi nicenu ca ngofu sha mwami wa mushinshe.”
54 Kisha wakamkamata Yesu, wakamchukua, wakaenda naye mpaka nyumbani kwa kuhani mkuu. Lakini Petro akafuata kwa mbali.
Lino balekata Yesu nekumutwala kung'anda ya mukulene wa beshimilumbo bonse. Neye Petulo walikakonkela Yesu capatali.
55 Walipokwisha kuwasha moto katikati ya ua na kuketi pamoja, Petro naye akaketi pamoja nao.
Lino balakunka mulilo pakati palubansa lwang'anda, bonse balekala panshi pamo. Neye Petulo walekala pakati pabo.
56 Mtumishi mmoja wa kike akamwona kwa mwanga wa moto akiwa ameketi pale. Akamtazama sana, akasema, “Huyu mtu pia alikuwa pamoja na Yesu!”
Lino mutukashi umo wa basebenshi mpwalabona Petulo kayota mulilo wamulangishisha, ne kwambeti, “Uyu neye walikuba ne Yesu.”
57 Lakini Petro akakana, akasema, “Ewe mwanamke, hata simjui!”
Nsombi Petulo nendi walakana nekwambeti, “Sobwe obe mutukashi nkandimwinshipo uyu ame.”
58 Baadaye kidogo, mtu mwingine alimwona Petro akasema, “Wewe pia ni mmoja wao!” Petro akajibu, “Wewe mtu, mimi sio mmoja wao!”
Mpopalapita kacindi kang'ana mutuloba naumbi neye walamubona Petulo nekumwambileti, “Obe njobe umo wabasa.” Nomba Petulo walakumbuleti, “Ntamepo sobwe.”
59 Baada ya muda wa kama saa moja hivi, mtu mwingine akazidi kusisitiza, “Kwa hakika huyu mtu naye alikuwa pamoja na Yesu, kwa maana yeye pia ni Mgalilaya.”
Mpopalapita kacindi kanda kukwana ola umo naumbi muntu walamba cangofu eti, “Nicakubinga muntu uyu walikuba ne Yesu pakwinga nimwine Galileya.”
60 Petro akajibu, “Wewe mtu, mimi sijui unalosema!” Wakati huo huo, akiwa bado anazungumza, jogoo akawika.
Petulo walakumbuleti, “Ayo makani ngolambanga nkandainshi ame nambi pang'ana.” Lino petulo kacamba, kombwe walalila.
61 Naye Bwana akageuka, akamtazama Petro. Ndipo Petro akakumbuka lile neno ambalo Bwana alimwambia: “Kabla jogoo hajawika leo, utanikana mara tatu.”
Mwami Yesu walafutatuka nekulangilisha Petulo. Lino nendi Petulo walanuka maswi a Mwami Yesu ngalamwambileti, “Kombwe nkatana alila lelo, obe Petulo nunkane mankanda atatu.”
62 Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.
Lino Petulo walafuma pansa, walalila cebo ca cikonko ncali kukute mumoyo.
63 Watu waliokuwa wanamlinda Yesu wakaanza kumdhihaki na kumpiga.
Lino bantu balikulonda Yesu, balatatika kumuseka nekumuma.
64 Wakamfunga kitambaa machoni na kumuuliza, “Tabiri! Tuambie ni nani aliyekupiga?”
Balamufweka pamenso, balamuma nekumwipusheti, “Lotela, nomba niyani lakumu?”
65 Wakaendelea kumtukana kwa matusi mengi.
Kayi balamba maswi angi akumucobola.
66 Kulipopambazuka, baraza la wazee wa watu, yaani viongozi wa makuhani na walimu wa sheria, wakakutana pamoja, naye Yesu akaletwa mbele yao.
Mpobwalaca bamakulene ba Bayuda, ne beshimilumbo, kayi ne beshikwiyisha Milawo balabungana. Balamumanta Yesu nekuya nendi kunkuta yabo.
67 Wakamwambia, “Kama wewe ndiye Kristo, tuambie.” Yesu akawajibu, “Hata nikiwaambia hamtaamini.
Balamwipusheti, “Twambile na njobe Mupulushi Walaiwa usa.” Nsombi nendi walabakumbuleti, “Nambi ndimwambile, nteshi mushome sobwe,
68 Nami nikiwauliza swali, hamtanijibu.
na ndimwipushe mwipusho, nteshi munkumbulepo.
69 Lakini kuanzia sasa, Mwana wa Adamu ataketi mkono wa kuume wa Mungu Mwenye Nguvu.”
Kufuma lelo ame nde Mwana Muntu nimbenga ndekala kulikasa lyakululyo kwa Lesa wangofu shonse.”
70 Wote wakauliza, “Wewe basi ndiwe Mwana wa Mungu?” Yeye akawajibu, “Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye.”
Lino bonse balepusheti, “Sena ulambangeti njobe Mwanendi Lesa?” Neye walakumbuleti, “Ee njame mbuli ncomulamba mobene.”
71 Kisha wakasema, “Tuna haja gani tena ya ushahidi zaidi? Tumesikia wenyewe kutoka kinywani mwake.”
Balo balambeti, “Sena lino inga katuciyandola nabambi bakamboni? Tulalinyufwili kendi ncalamba mwine.”

< Luka 22 >