< Luka 22 >
1 Wakati huu Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa imekaribia.
Now the feast of unleavened bread drew nigh, which is called the Passover.
2 Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwa wanatafuta njia ya kumuua Yesu, kwa sababu waliwaogopa watu.
And the chief priests and the scribes sought how they might put him to death; for they feared the people.
3 Shetani akamwingia Yuda, aliyeitwa Iskariote, mmoja wa wale Kumi na Wawili.
And Satan entered into Judas who was called Iscariot, being of the number of the twelve.
4 Yuda akaenda kwa viongozi wa makuhani na kwa maafisa wa walinzi wa Hekalu, akazungumza nao jinsi ambavyo angeweza kumsaliti Yesu.
And he went away, and communed with the chief priests and captains, how he might deliver him unto them.
5 Wakafurahi na wakakubaliana kumpa fedha.
And they were glad, and covenanted to give him money.
6 Naye akakubali, akaanza kutafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Yesu kwao, wakati ambapo hakuna umati wa watu.
And he consented, and sought opportunity to deliver him unto them in the absence of the multitude.
7 Basi ikawadia siku ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa.
And the day of unleavened bread came, on which the passover must be sacrificed.
8 Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohana, akisema, “Nendeni mkatuandalie chakula cha Pasaka ili tuweze kuila.”
And he sent Peter and John, saying, Go and make ready for us the passover, that we may eat.
9 Wakamuuliza, “Unataka tukuandalie wapi?”
And they said unto him, Where wilt thou that we make ready?
10 Yesu akawaambia, “Tazameni, mtakapokuwa mkiingia mjini, mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka kwenye nyumba atakayoingia.
And he said unto them, Behold, when ye are entered into the city, there shall meet you a man bearing a pitcher of water; follow him into the house whereinto he goeth.
11 Nanyi mwambieni mwenye nyumba, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’
And ye shall say unto the goodman of the house, The Master saith unto thee, Where is the guest-chamber, where I shall eat the passover with my disciples?
12 Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani, kikiwa kimepambwa vizuri. Andaeni humo.”
And he will shew you a large upper room furnished: there make ready.
13 Wakaenda, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.
And they went, and found as he had said unto them: and they made ready the passover.
14 Wakati ulipowadia, Yesu akaketi mezani pamoja na wale mitume wake.
And when the hour was come, he sat down, and the apostles with him.
15 Kisha akawaambia, “Nimetamani sana kuila Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
And he said unto them, With desire I have desired to eat this passover with you before I suffer:
16 Kwa maana, nawaambia, sitaila tena Pasaka mpaka itakapotimizwa katika Ufalme wa Mungu.”
for I say unto you, I will not eat it, until it be fulfilled in the kingdom of God.
17 Akiisha kukichukua kikombe, akashukuru, akasema, “Chukueni hiki mnywe wote.
And he received a cup, and when he had given thanks, he said, Take this, and divide it among yourselves:
18 Kwa maana nawaambia tangu sasa sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
for I say unto you, I will not drink from henceforth of the fruit of the vine, until the kingdom of God shall come.
19 Kisha akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa, akisema, “Huu ni mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”
And he took bread, and when he had given thanks, he brake it, and gave to them, saying, This is my body which is given for you: this do in remembrance of me.
20 Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, imwagikayo kwa ajili yenu.
And the cup in like manner after supper, saying, This cup is the new covenant in my blood, [even] that which is poured out for you.
21 Lakini mkono wake huyo atakayenisaliti uko hapa mezani pamoja nami.
But behold, the hand of him that betrayeth me is with me on the table.
22 Mwana wa Adamu anaenda zake kama ilivyokusudiwa. Lakini ole wake mtu huyo amsalitiye.”
For the Son of man indeed goeth, as it hath been determined: but woe unto that man through whom he is betrayed!
23 Wakaanza kuulizana wenyewe ni nani miongoni mwao angeweza kufanya jambo hilo.
And they began to question among themselves, which of them it was that should do this thing.
24 Pia yakazuka mabishano katikati ya wanafunzi kwamba ni nani aliyeonekana kuwa mkuu kuliko wote miongoni mwao.
And there arose also a contention among them, which of them is accounted to be greatest.
25 Yesu akawaambia, “Wafalme na watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu. Nao wenye mamlaka juu yao hujiita ‘Wafadhili.’
And he said unto them, The kings of the Gentiles have lordship over them; and they that have authority over them are called Benefactors.
26 Lakini ninyi msifanane nao. Bali yeye aliye mkuu kuliko wote miongoni mwenu, inampasa kuwa kama yeye aliye mdogo wa wote, naye atawalaye na awe kama yeye ahudumuye.
But ye [shall] not [be] so: but he that is the greater among you, let him become as the younger; and he that is chief, as he that doth serve.
27 Kwani ni nani aliye mkuu? Ni yule aketiye mezani au ni yule ahudumuye? Si ni yule aliyekaa mezani? Lakini mimi niko miongoni mwenu kama yule ahudumuye.
For whether is greater, he that sitteth at meat, or he that serveth? is not he that sitteth at meat? but I am in the midst of you as he that serveth.
28 Ninyi mmekuwa pamoja nami katika majaribu yangu.
But ye are they which have continued with me in my temptations;
29 Nami kama Baba yangu alivyonipa ufalme, kadhalika mimi nami ninawapa ninyi,
and I appoint unto you a kingdom, even as my Father appointed unto me,
30 ili mpate kula na kunywa mezani pangu katika karamu ya ufalme wangu, na kukaa katika viti vya enzi, mkihukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.”
that ye may eat and drink at my table in my kingdom; and ye shall sit on thrones judging the twelve tribes of Israel.
31 Yesu akasema, “Simoni, Simoni, sikiliza, Shetani ameomba kuwapepeta ninyi wote kama ngano.
Simon, Simon, behold, Satan asked to have you, that he might sift you as wheat:
32 Lakini nimekuombea wewe Simoni ili imani yako isishindwe, nawe ukiisha kunirudia, uwaimarishe ndugu zako.”
but I made supplication for thee, that thy faith fail not: and do thou, when once thou hast turned again, stablish thy brethren.
33 Petro akajibu, “Bwana, niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani na hata kifoni.”
And he said unto him, Lord, with thee I am ready to go both to prison and to death.
34 Yesu akamjibu, “Ninakuambia Petro, kabla jogoo hajawika usiku wa leo, utakana mara tatu kwamba hunijui mimi.”
And he said, I tell thee, Peter, the cock shall not crow this day, until thou shalt thrice deny that thou knowest me.
35 Kisha Yesu akawauliza, “Nilipowatuma bila mfuko, wala mkoba, wala viatu, mlipungukiwa na kitu chochote?” Wakajibu, “La, hatukupungukiwa na kitu chochote.”
And he said unto them, When I sent you forth without purse, and wallet, and shoes, lacked ye any thing? And they said, Nothing.
36 Akawaambia, “Lakini sasa, aliye na mfuko na auchukue, na aliye na mkoba vivyo hivyo. Naye asiye na upanga, auze joho lake anunue mmoja.
And he said unto them, But now, he that hath a purse, let him take it, and likewise a wallet: and he that hath none, let him sell his cloke, and buy a sword.
37 Kwa sababu, nawaambia, andiko hili lazima litimizwe juu yangu, kwamba, ‘Alihesabiwa pamoja na wakosaji’; kwa kweli yaliyoandikwa kunihusu mimi hayana budi kutimizwa.”
For I say unto you, that this which is written must be fulfilled in me, And he was reckoned with transgressors: for that which concerneth me hath fulfillment.
38 Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, tazama hapa kuna panga mbili.” Akawajibu, “Inatosha.”
And they said, Lord, behold, here are two swords. And he said unto them, It is enough.
39 Yesu akatoka, akaenda kwenye Mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa kawaida yake, nao wanafunzi wake wakamfuata.
And he came out, and went, as his custom was, unto the mount of Olives; and the disciples also followed him.
40 Walipofika huko, akawaambia wanafunzi wake, “Ombeni, msije mkaingia majaribuni.”
And when he was at the place, he said unto them, Pray that ye enter not into temptation.
41 Akajitenga nao kama umbali wa kutupa jiwe, akapiga magoti, akaomba
And he was parted from them about a stone’s cast; and he kneeled down and prayed,
42 akisema, “Baba, kama ni mapenzi yako, niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo, bali mapenzi yako yatendeke.”
saying, Father, if thou be willing, remove this cup from me: nevertheless not my will, but thine, be done.
43 Malaika kutoka mbinguni akamtokea, akamtia nguvu.
And there appeared unto him an angel from heaven, strengthening him.
44 Naye akiwa katika maumivu makuu, akaomba kwa bidii, nalo jasho lake likawa kama matone ya damu yakidondoka ardhini.
And being in an agony he prayed more earnestly: and his sweat became as it were great drops of blood falling down upon the ground.
45 Baada ya kuomba, akawarudia wanafunzi wake akawakuta wamelala, wakiwa wamechoka kutokana na huzuni.
And when he rose up from his prayer, he came unto the disciples, and found them sleeping for sorrow,
46 Naye akawauliza, “Mbona mmelala? Amkeni, mwombe ili msije mkaingia majaribuni.”
and said unto them, Why sleep ye? rise and pray, that ye enter not into temptation.
47 Yesu alipokuwa bado anazungumza, umati mkubwa wa watu ukaja. Uliongozwa na Yuda, ambaye alikuwa mmoja wa wale wanafunzi Kumi na Wawili. Akamkaribia Yesu ili ambusu.
While he yet spake, behold, a multitude, and he that was called Judas, one of the twelve, went before them; and he drew near unto Jesus to kiss him.
48 Lakini Yesu akamwambia, “Yuda, je, unamsaliti Mwana wa Adamu kwa busu?”
But Jesus said unto him, Judas, betrayest thou the Son of man with a kiss?
49 Wafuasi wa Yesu walipoona yale yaliyokuwa yanakaribia kutokea, wakasema, “Bwana, tuwakatekate kwa panga zetu?”
And when they that were about him saw what would follow, they said, Lord, shall we smite with the sword?
50 Mmoja wao akampiga mtumishi wa kuhani mkuu kwa upanga, akamkata sikio la kuume.
And a certain one of them smote the servant of the high priest, and struck off his right ear.
51 Lakini Yesu akasema, “Acheni!” Akaligusa lile sikio la yule mtu na kumponya.
But Jesus answered and said, Suffer ye thus far. And he touched his ear, and healed him.
52 Kisha Yesu akawaambia wale viongozi wa makuhani, maafisa wa walinzi wa Hekalu, pamoja na wazee waliokuwa wamekuja kumkamata, “Mmekuja na panga na marungu, kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi?
And Jesus said unto the chief priests, and captains of the temple, and elders, which were come against him, Are ye come out, as against a robber, with swords and staves?
53 Siku kwa siku nilikuwa pamoja nanyi Hekaluni lakini hamkunikamata. Lakini hii ni saa yenu, wakati giza linatawala!”
When I was daily with you in the temple, ye stretched not forth your hands against me: but this is your hour, and the power of darkness.
54 Kisha wakamkamata Yesu, wakamchukua, wakaenda naye mpaka nyumbani kwa kuhani mkuu. Lakini Petro akafuata kwa mbali.
And they seized him, and led him [away], and brought him into the high priest’s house. But Peter followed afar off.
55 Walipokwisha kuwasha moto katikati ya ua na kuketi pamoja, Petro naye akaketi pamoja nao.
And when they had kindled a fire in the midst of the court, and had sat down together, Peter sat in the midst of them.
56 Mtumishi mmoja wa kike akamwona kwa mwanga wa moto akiwa ameketi pale. Akamtazama sana, akasema, “Huyu mtu pia alikuwa pamoja na Yesu!”
And a certain maid seeing him as he sat in the light [of the fire], and looking stedfastly upon him, said, This man also was with him.
57 Lakini Petro akakana, akasema, “Ewe mwanamke, hata simjui!”
But he denied, saying, Woman, I know him not.
58 Baadaye kidogo, mtu mwingine alimwona Petro akasema, “Wewe pia ni mmoja wao!” Petro akajibu, “Wewe mtu, mimi sio mmoja wao!”
And after a little while another saw him, and said, Thou also art [one] of them. But Peter said, Man, I am not.
59 Baada ya muda wa kama saa moja hivi, mtu mwingine akazidi kusisitiza, “Kwa hakika huyu mtu naye alikuwa pamoja na Yesu, kwa maana yeye pia ni Mgalilaya.”
And after the space of about one hour another confidently affirmed, saying, Of a truth this man also was with him: for he is a Galilaean.
60 Petro akajibu, “Wewe mtu, mimi sijui unalosema!” Wakati huo huo, akiwa bado anazungumza, jogoo akawika.
But Peter said, Man, I know not what thou sayest. And immediately, while he yet spake, the cock crew.
61 Naye Bwana akageuka, akamtazama Petro. Ndipo Petro akakumbuka lile neno ambalo Bwana alimwambia: “Kabla jogoo hajawika leo, utanikana mara tatu.”
And the Lord turned, and looked upon Peter. And Peter remembered the word of the Lord, how that he said unto him, Before the cock crow this day, thou shalt deny me thrice.
62 Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.
And he went out, and wept bitterly.
63 Watu waliokuwa wanamlinda Yesu wakaanza kumdhihaki na kumpiga.
And the men that held [Jesus] mocked him, and beat him.
64 Wakamfunga kitambaa machoni na kumuuliza, “Tabiri! Tuambie ni nani aliyekupiga?”
And they blindfolded him, and asked him, saying, Prophesy: who is he that struck thee?
65 Wakaendelea kumtukana kwa matusi mengi.
And many other things spake they against him, reviling him.
66 Kulipopambazuka, baraza la wazee wa watu, yaani viongozi wa makuhani na walimu wa sheria, wakakutana pamoja, naye Yesu akaletwa mbele yao.
And as soon as it was day, the assembly of the elders of the people was gathered together, both chief priests and scribes; and they led him away into their council, saying,
67 Wakamwambia, “Kama wewe ndiye Kristo, tuambie.” Yesu akawajibu, “Hata nikiwaambia hamtaamini.
If thou art the Christ, tell us. But he said unto them, If I tell you, ye will not believe:
68 Nami nikiwauliza swali, hamtanijibu.
and if I ask [you], ye will not answer.
69 Lakini kuanzia sasa, Mwana wa Adamu ataketi mkono wa kuume wa Mungu Mwenye Nguvu.”
But from henceforth shall the Son of man be seated at the right hand of the power of God.
70 Wote wakauliza, “Wewe basi ndiwe Mwana wa Mungu?” Yeye akawajibu, “Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye.”
And they all said, Art thou then the Son of God? And he said unto them, Ye say that I am.
71 Kisha wakasema, “Tuna haja gani tena ya ushahidi zaidi? Tumesikia wenyewe kutoka kinywani mwake.”
And they said, What further need have we of witness? for we ourselves have heard from his own mouth.