< Luka 22 >
1 Wakati huu Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa imekaribia.
Now the feast of unleavened bread, which is called the passover, was drawing near;
2 Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwa wanatafuta njia ya kumuua Yesu, kwa sababu waliwaogopa watu.
and the chief priests and the scribes were seeking how they might kill him; for they feared the people.
3 Shetani akamwingia Yuda, aliyeitwa Iskariote, mmoja wa wale Kumi na Wawili.
And Satan entered into Judas called Iscariot, who was of the number of the twelve.
4 Yuda akaenda kwa viongozi wa makuhani na kwa maafisa wa walinzi wa Hekalu, akazungumza nao jinsi ambavyo angeweza kumsaliti Yesu.
And he went away, and consulted with the chief priests and captains, how he might deliver him up to them.
5 Wakafurahi na wakakubaliana kumpa fedha.
And they were glad, and covenanted to give him money.
6 Naye akakubali, akaanza kutafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Yesu kwao, wakati ambapo hakuna umati wa watu.
And he agreed with them, and sought a good opportunity to deliver him up to them in the absence of the multitude.
7 Basi ikawadia siku ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa.
Then came the day of unleavened bread, when the passover must be killed;
8 Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohana, akisema, “Nendeni mkatuandalie chakula cha Pasaka ili tuweze kuila.”
and he sent Peter and John, saying, Go and make ready for us the passover, that we may eat it.
9 Wakamuuliza, “Unataka tukuandalie wapi?”
And they said to him, Where wilt thou that we make it ready?
10 Yesu akawaambia, “Tazameni, mtakapokuwa mkiingia mjini, mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka kwenye nyumba atakayoingia.
And he said to them, Lo! when ye have entered the city, there will meet you a man bearing a pitcher of water; follow him into the house where he goeth in;
11 Nanyi mwambieni mwenye nyumba, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’
and ye shall say to the master of the house, The Teacher saith to thee, Where is the guest-chamber, where I may eat the passover with my disciples?
12 Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani, kikiwa kimepambwa vizuri. Andaeni humo.”
And he will show you a large upper room furnished; there make ready.
13 Wakaenda, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.
And they went and found as he had said to them; and they made ready the passover.
14 Wakati ulipowadia, Yesu akaketi mezani pamoja na wale mitume wake.
And when the hour had come, he placed himself at table, and the apostles with him.
15 Kisha akawaambia, “Nimetamani sana kuila Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
And he said to them, Earnestly have I desired to eat this passover with you, before I suffer.
16 Kwa maana, nawaambia, sitaila tena Pasaka mpaka itakapotimizwa katika Ufalme wa Mungu.”
For I say to you, that I shall eat it no more, until it be fulfilled in the kingdom of God.
17 Akiisha kukichukua kikombe, akashukuru, akasema, “Chukueni hiki mnywe wote.
And he took a cup, and gave thanks, and said, Take this, and divide it among yourselves.
18 Kwa maana nawaambia tangu sasa sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
For I say to you, that I shall not drink henceforth of the fruit of the vine, until the kingdom of God shall have come.
19 Kisha akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa, akisema, “Huu ni mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”
And he took a loaf, and gave thanks, and broke it, and gave it to them, saying, This is my body, which is given for you; this do in remembrance of me.
20 Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, imwagikayo kwa ajili yenu.
And in like manner he took the cup after supper, saying, This cup is the new covenant in my blood, which is about to be shed for you.
21 Lakini mkono wake huyo atakayenisaliti uko hapa mezani pamoja nami.
But lo! the hand of him that betrayeth me is with me on the table.
22 Mwana wa Adamu anaenda zake kama ilivyokusudiwa. Lakini ole wake mtu huyo amsalitiye.”
For the Son of man indeed goeth away, as it hath been determined; but woe to that man by whom he is betrayed.
23 Wakaanza kuulizana wenyewe ni nani miongoni mwao angeweza kufanya jambo hilo.
And they began to inquire among themselves, which of them it was that was about to do this.
24 Pia yakazuka mabishano katikati ya wanafunzi kwamba ni nani aliyeonekana kuwa mkuu kuliko wote miongoni mwao.
And there arose also a contention among them, which of them should be accounted the greatest.
25 Yesu akawaambia, “Wafalme na watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu. Nao wenye mamlaka juu yao hujiita ‘Wafadhili.’
And he said to them, The kings of the nations rule as lords over them, and they who exercise authority over them are called benefactors.
26 Lakini ninyi msifanane nao. Bali yeye aliye mkuu kuliko wote miongoni mwenu, inampasa kuwa kama yeye aliye mdogo wa wote, naye atawalaye na awe kama yeye ahudumuye.
But it is not to be so with you; but let the greatest among you be as the youngest; and he that is chief, as he that serveth.
27 Kwani ni nani aliye mkuu? Ni yule aketiye mezani au ni yule ahudumuye? Si ni yule aliyekaa mezani? Lakini mimi niko miongoni mwenu kama yule ahudumuye.
For which is greater? he who reclineth at the table, or he who serveth? Is not he that reclineth at the table? But I am in the midst of you as he who serveth.
28 Ninyi mmekuwa pamoja nami katika majaribu yangu.
Ye however are they who have continued steadfastly with me in my trials.
29 Nami kama Baba yangu alivyonipa ufalme, kadhalika mimi nami ninawapa ninyi,
And I appoint to you a kingdom, as my Father appointed to me;
30 ili mpate kula na kunywa mezani pangu katika karamu ya ufalme wangu, na kukaa katika viti vya enzi, mkihukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.”
that ye may eat and drink at my table in my kingdom; and ye shall sit on thrones, judging the twelve tribes of Israel.
31 Yesu akasema, “Simoni, Simoni, sikiliza, Shetani ameomba kuwapepeta ninyi wote kama ngano.
Simon, Simon, lo! Satan hath asked for you, that he may sift you as wheat.
32 Lakini nimekuombea wewe Simoni ili imani yako isishindwe, nawe ukiisha kunirudia, uwaimarishe ndugu zako.”
But I have prayed for thee, that thy faith fail not. And do thou, when thou hast returned to me, strengthen thy brethren.
33 Petro akajibu, “Bwana, niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani na hata kifoni.”
And he said to him, Lord, I am ready to go with thee both to prison and to death.
34 Yesu akamjibu, “Ninakuambia Petro, kabla jogoo hajawika usiku wa leo, utakana mara tatu kwamba hunijui mimi.”
And he said, I tell thee, Peter, a cock will not crow this day, till thou hast thrice denied that thou knowest me.
35 Kisha Yesu akawauliza, “Nilipowatuma bila mfuko, wala mkoba, wala viatu, mlipungukiwa na kitu chochote?” Wakajibu, “La, hatukupungukiwa na kitu chochote.”
And he said to them, When I sent you without purse, or bag, or sandals, were ye in need of anything? And they said, Of nothing. Then he said to them,
36 Akawaambia, “Lakini sasa, aliye na mfuko na auchukue, na aliye na mkoba vivyo hivyo. Naye asiye na upanga, auze joho lake anunue mmoja.
But now, he that hath a purse, let him take it, and likewise a bag; and he that hath not, let him sell his garment, and buy a sword.
37 Kwa sababu, nawaambia, andiko hili lazima litimizwe juu yangu, kwamba, ‘Alihesabiwa pamoja na wakosaji’; kwa kweli yaliyoandikwa kunihusu mimi hayana budi kutimizwa.”
For I say to you, that this which is written must be accomplished in me: “And he was reckoned among transgressors.” For that which concerneth me also hath an end.
38 Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, tazama hapa kuna panga mbili.” Akawajibu, “Inatosha.”
And they said, Lord, behold, here are two swords. And he said to him, It is enough!
39 Yesu akatoka, akaenda kwenye Mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa kawaida yake, nao wanafunzi wake wakamfuata.
And going out, he went, as he was wont, to the Mount of Olives; and the disciples followed him.
40 Walipofika huko, akawaambia wanafunzi wake, “Ombeni, msije mkaingia majaribuni.”
And when he was at the place, he said to them, Pray that ye may not enter into temptation.
41 Akajitenga nao kama umbali wa kutupa jiwe, akapiga magoti, akaomba
And he withdrew from them about a stone's throw; and kneeling down he prayed,
42 akisema, “Baba, kama ni mapenzi yako, niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo, bali mapenzi yako yatendeke.”
saying, Father, if thou art willing to remove this cup from me—yet not my will, but thine be done!
43 Malaika kutoka mbinguni akamtokea, akamtia nguvu.
And there appeared to him an angel from heaven, strengthening him.
44 Naye akiwa katika maumivu makuu, akaomba kwa bidii, nalo jasho lake likawa kama matone ya damu yakidondoka ardhini.
And being in an agony, he prayed more earnestly. And his sweat was as it were great drops of blood falling to the ground.
45 Baada ya kuomba, akawarudia wanafunzi wake akawakuta wamelala, wakiwa wamechoka kutokana na huzuni.
And rising up from prayer, he came to the disciples, and found them sleeping for sorrow,
46 Naye akawauliza, “Mbona mmelala? Amkeni, mwombe ili msije mkaingia majaribuni.”
and said to them, Why sleep ye? Rise, and pray that ye may not enter into temptation.
47 Yesu alipokuwa bado anazungumza, umati mkubwa wa watu ukaja. Uliongozwa na Yuda, ambaye alikuwa mmoja wa wale wanafunzi Kumi na Wawili. Akamkaribia Yesu ili ambusu.
While he was yet speaking, lo! a multitude, and he that was called Judas, one of the twelve, was at the head of them; and he drew near to Jesus to kiss him.
48 Lakini Yesu akamwambia, “Yuda, je, unamsaliti Mwana wa Adamu kwa busu?”
But Jesus said to him, Judas, dost thou betray the Son of man with a kiss?
49 Wafuasi wa Yesu walipoona yale yaliyokuwa yanakaribia kutokea, wakasema, “Bwana, tuwakatekate kwa panga zetu?”
And they who were about him, seeing what would follow, said, Lord, shall we smite with the sword?
50 Mmoja wao akampiga mtumishi wa kuhani mkuu kwa upanga, akamkata sikio la kuume.
And one of them smote the servant of the high-priest, and cut off his right ear.
51 Lakini Yesu akasema, “Acheni!” Akaligusa lile sikio la yule mtu na kumponya.
But Jesus answering said, Permit thus far; and touched his ear, and healed him.
52 Kisha Yesu akawaambia wale viongozi wa makuhani, maafisa wa walinzi wa Hekalu, pamoja na wazee waliokuwa wamekuja kumkamata, “Mmekuja na panga na marungu, kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi?
Then Jesus said to the chief priests and captains of the temple and elders who had come to him, Ye have come out as against a robber, with swords and clubs;
53 Siku kwa siku nilikuwa pamoja nanyi Hekaluni lakini hamkunikamata. Lakini hii ni saa yenu, wakati giza linatawala!”
when I was daily with you in the temple, ye did not put forth your hands against me; but this is your hour, and the power of darkness.
54 Kisha wakamkamata Yesu, wakamchukua, wakaenda naye mpaka nyumbani kwa kuhani mkuu. Lakini Petro akafuata kwa mbali.
And they seized him, and led him away, and brought him into the house of the high-priest. And Peter followed afar off.
55 Walipokwisha kuwasha moto katikati ya ua na kuketi pamoja, Petro naye akaketi pamoja nao.
And when they had kindled a fire in the midst of the court, and had sat down together, Peter sat down among them.
56 Mtumishi mmoja wa kike akamwona kwa mwanga wa moto akiwa ameketi pale. Akamtazama sana, akasema, “Huyu mtu pia alikuwa pamoja na Yesu!”
But a certain maid-servant saw him sitting at the fire, and steadily looking at him said, This man also was with him.
57 Lakini Petro akakana, akasema, “Ewe mwanamke, hata simjui!”
And he denied him, saying, Woman, I do not know him.
58 Baadaye kidogo, mtu mwingine alimwona Petro akasema, “Wewe pia ni mmoja wao!” Petro akajibu, “Wewe mtu, mimi sio mmoja wao!”
And after a little while another saw him, and said, Thou also art one of them. And Peter said, Man, I am not.
59 Baada ya muda wa kama saa moja hivi, mtu mwingine akazidi kusisitiza, “Kwa hakika huyu mtu naye alikuwa pamoja na Yesu, kwa maana yeye pia ni Mgalilaya.”
And in about one hour's time, another confidently affirmed, saying, In truth this man also was with him; for he is a Galilaean.
60 Petro akajibu, “Wewe mtu, mimi sijui unalosema!” Wakati huo huo, akiwa bado anazungumza, jogoo akawika.
And Peter said, Man, I know not what thou sayest. And immediately, while he was yet speaking, a cock crew.
61 Naye Bwana akageuka, akamtazama Petro. Ndipo Petro akakumbuka lile neno ambalo Bwana alimwambia: “Kabla jogoo hajawika leo, utanikana mara tatu.”
And the Lord turned and looked upon Peter; and Peter remembered the word of the Lord, that he had said to him, Before a cock crows this day, thou wilt thrice deny me.
62 Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.
And he went out, and wept bitterly.
63 Watu waliokuwa wanamlinda Yesu wakaanza kumdhihaki na kumpiga.
And the men that held Jesus mocked him, and beat him;
64 Wakamfunga kitambaa machoni na kumuuliza, “Tabiri! Tuambie ni nani aliyekupiga?”
and having blindfolded him, they asked him, saying, Prophesy, who is it that struck thee?
65 Wakaendelea kumtukana kwa matusi mengi.
And many other things did they scoffingly say against him.
66 Kulipopambazuka, baraza la wazee wa watu, yaani viongozi wa makuhani na walimu wa sheria, wakakutana pamoja, naye Yesu akaletwa mbele yao.
And when it was day, the elders of the people, both chief priests and scribes, came together, and brought him before their council, saying,
67 Wakamwambia, “Kama wewe ndiye Kristo, tuambie.” Yesu akawajibu, “Hata nikiwaambia hamtaamini.
If thou art the Christ, tell us. And he said to them, If I tell you, ye will not believe;
68 Nami nikiwauliza swali, hamtanijibu.
and if I ask, ye will not answer.
69 Lakini kuanzia sasa, Mwana wa Adamu ataketi mkono wa kuume wa Mungu Mwenye Nguvu.”
But from this time the Son of man will sit on the right hand of the power of God.
70 Wote wakauliza, “Wewe basi ndiwe Mwana wa Mungu?” Yeye akawajibu, “Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye.”
Then they all said, Art thou then the Son of God? And he said to them, Ye say what is true; for I am.
71 Kisha wakasema, “Tuna haja gani tena ya ushahidi zaidi? Tumesikia wenyewe kutoka kinywani mwake.”
And they said, What further need have we of testimony? For we have ourselves heard from his own mouth.