< Luka 21 >

1 Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
Pogledavši pa gor, videl je bogatine, da mečejo darove svoje v zakladnico.
2 Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
Videl je pa tudi eno vdovo ubogo, da je vrgla dva vinarja.
3 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
Ter reče: Resnično vam pravim, da je ta uboga vdova vrgla več od vseh:
4 Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
Kajti vsi ti so vrgli od obilnosti svoje v dar Bogu, a ta je od uboštva svojega vrgla ves živež svoj, kterega je imela.
5 Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
In ko so nekteri pravili za tempelj, da je olepšan z lepim kamenjem in dragocenostmi, reče:
6 “Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
Prišli bodo dnevi, ko od tega, kar vidite, ne bo ostal kamen na kamenu, kteri ne bi razpadel.
7 Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
In vprašajo ga, govoreč: Učenik, kedaj pa bo to? in kaj bo znamenje, kedar se ima to zgoditi?
8 Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
On pa reče: Varujte se, da vas ne premotijo! kajti veliko jih bo prišlo v ime moje, in porekó: Jaz sem! in: Čas se je približal! Ne hodite torej za njimi.
9 Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
Kedar boste pa slišali vojske in vstaje, ne uplašite se; kajti to se mora najprej zgoditi: ali konca ne bo precej.
10 Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
Tedaj jim je pravil: Vstal bo narod na narod, in kraljestvo na kraljestvo;
11 Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
In veliki potresi bodo po krajih in lakote in kuge, groza in znamenja velika bodo na nebu.
12 “Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
A pred vsem tem bodo položili roke svoje na vas, in preganjali vas bodo in izdajali v shajališča in ječe, in vodili pred kralje in poglavarje, za voljo imena mojega.
13 Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
A to vam se bo zgodilo na pričevanje.
14 Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
Položite torej v srce svoje, da ne skrbite naprej, kako se boste zagovarjali;
15 Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
Kajti jaz vam bom dal usta in modrost, kterej ne bodo mogli nasprotovati, ne upirati se vsi nasprotniki vaši.
16 Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
Izdajali vas bodo pa tudi roditelji in bratje in sorodniki in prijatelji, in nektere od vas bodo umorili.
17 Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
In sovražili vas bodo vsi za voljo imena mojega.
18 Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
Pa las z glave vam ne bo poginil.
19 Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
H potrpljenjem svojim pridobivajte duše svoje.
20 “Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
Kedar boste pa videli, da Jeruzalem oblega vojska, tedaj vedite, da se je približalo razdejanje njegovo.
21 Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
Tedaj naj, kteri so v Judeji, odbežé na gore: in kteri so sredi njega, izidejo naj na polje; in kteri so na polji, naj ne hodijo va-nj.
22 Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
Kajti ti dnevi bodo dnevi maščevanja, da se izpolnijo vsa pisma.
23 Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
Gorjé pa nosečim in doječim v tistih dnéh; kajti velika nadloga bo na zemlji, in jeza nad tem narodom.
24 Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
In padali bodo od ostrice meča, in gonili jih bodo v sužnost po vseh narodih, in Jeruzalem bodo gazili pogani, dokler se ne izpolnijo časi poganov.
25 “Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
In znamenja bodo v solncu, in mesecu in zvezdah, in narodom na zemlji žalost od obupa, šuma morskega in valovja;
26 Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
Ludjé bodo mrli od strahu in pričakovanja tega, kar ima na zemljo priti: kajti sile nebeške se bodo pregibale.
27 Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
In tedaj bodo ugledali sina človečjega, da gre na oblaku z veliko močjó in slavo.
28 Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
Ko se bo pa to jelo goditi, ozrite se gor in povzdignite glave svoje, ker se približuje odrešenje vaše.
29 Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
In pové jim priliko: Poglejte smokvo in vse drevje.
30 Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
Kedar vidite, da je uže pognalo, sami véste, da je pomlad uže blizu.
31 Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
Tako tudi vi, ko boste videli, da se to godí, védite, da je blizu kraljestvo Božje.
32 “Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
Resnično vam pravim, da ne bo prešel ta rod, dokler se vse ne zgodí.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
Nebo in zemlja bosta prešla, a besede moje ne bodo prešle.
34 “Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
Varujte se pa, da vam ne otežajo srca s požrešnostjo in pijanstvom in skrbmí tega sveta, in vam ne pride ta dan iznenada.
35 Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
Kajti prišel bo kakor zanka na vse, kteri prebivajo na lici vse zemlje.
36 Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
Čujte torej vsak čas, in molite, da bi bili vredni ubežati vsemu temu, kar se ima zgoditi, in pred sinom človečjim stati.
37 Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
In po dnevi je učil v tempeljnu; a po noči je izhajal prenočevat na goro, ktera se imenuje Oljska.
38 Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.
In dohajalo je vse ljudstvo zgodaj k njemu v tempelj poslušat ga.

< Luka 21 >