< Luka 21 >

1 Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
Na nakhlo but palo adava, o Isus vazdinđa plo šero hem dikhlja sar o barvale manuša čhivena pumare pare ani e hramesiri kutija zako čediba.
2 Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
Ađahar dikhlja hem jekha čorora udovica sar čhivela samo duj najtikore kovanice.
3 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
Tegani phenđa: “Čače vaćerava tumenđe, akaja čorori udovica čhivđa više sarijendar.
4 Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
Adalese so sare akala dinde oto buderi so isi len, a oj, kojai čorori, dinđa sa so inola zako živiba.”
5 Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
I sar nesave učenici vaćerena ine adalestar sari o Hram šukar ukrasime šuže bare barencar hem e daronencar savei posvetime e Devlese, o Isus phenđa:
6 “Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
“Ka avel o dive kad oto sa akava so dikhena naka ačhol ni bar upro bar. Svako ka ovel peravdo.”
7 Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
I on pučle e Isuse: “Učitelju, kad adava ka ovel? Savo znako ka mothoj amenđe da ka ovel adava?”
8 Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
A o Isus phenđa: “Dikhen te na oven hovavde. Adalese so but džene ka aven ano mlo anav vaćerindoj: ‘Me injum o Hrist’ hem: ‘Alo paše o kraj akale vremesoro.’ Ma džan palo lende!
9 Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
A kad šunena zako mariba hem zako pobune, ma te daran. Adalese so prvo adava valjani te ovel, ali nane odmah o kraj.”
10 Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
Tegani phenđa lenđe: “Jekh nacija ka uštel upri aver nacija hem jekh carstvo upro aver carstvo.
11 Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
Ko but thana ka oven bare zemljotresija, bokhalipe hem zaraze. Ka mothoven pe čudesna znakija ko nebo savendar o manuša ka daran.
12 “Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
Ali angleder so sa adava te ovel, ka dolen tumen hem ka progoninen tumen, ka legaren tumen ko sudo ano sinagoge hem ko phandlipe, ka legaren tumen anglo carija hem anglo vladarija, hem sa adava zbog mande.
13 Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
Adava ka ovel tumenđe te šaj svedočinen lenđe mandar.
14 Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
Adalese zapamtinen: ma pripreminen tumen angleder save lafencar ka braninen tumen.
15 Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
Adalese so me ka dav tumen mudrost hem lafija ko save nijekh tumaro protivniko naka šaj te irini lafi.
16 Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
A ka izdajinen tumen čak hem tumare dada hem o daja, tumare phralja, tumari familija hem tumare amala; hem nesaven tumendar ka mudaren.
17 Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
I sare ka mrzinen tumen zbog mande,
18 Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
ali ni jekh bal tumare šerestar naka perel.
19 Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
Adaleja so ka ačhoven verna, ka dobinen o večno dživdipe.”
20 “Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
O Isus phenđa hem akava: “I kad ka dikhen sar o Jerusalim opkolime e vojskendar, te džanen da alo lesoro vreme te ovel uništime.
21 Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
Tegani okola kola živinena ani e judejakiri regija nek našen ko gore. Okola kola živinena ano Jerusalim nek ikljon avri, a kolai ko polje, te na đerdinen ani diz.
22 Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
Adalese so adala ka oven o dive oti e Devlesiri kazna, te pherđol sa soi pisime ano Sveto lil.
23 Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
Jao e khamnjenđe hem okolenđe kola dena čuči ko adala dive! Adalese so bari nevolja ka ovel upri phuv hem e Devlesiri holi ka perel upro akava narodo.
24 Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
Nesave olendar ka oven mudarde mačeja, a avera ka oven legarde ko ropstvo maškaro sa o nacije. O Jerusalim ka ovel gazime e manušendar oto avera nacije sa đikote na nakhela lengoro vreme.”
25 “Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
O Isus phenđa hem akava: “I ka oven čudna znakija ko kham, ko masek hem ko čerenja, a ki phuv o nacije naka džanen so te ćeren oti dar zbog adava so o more ka ćerel glasna zvukija hem bare talasija.
26 Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
O manuša ka meren oti dar hem oto adžićeriba o bišukaripe savo avela ki phuv, adalese so o zoralipa e nebosere ka oven potresime.
27 Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
Tegani sare ka dikhen man, e Čhave e manušesere, sar avava upro oblako ano zoralipe hem ani bari slava.
28 Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
A kad sa adava ka počini te ovel, terđoven ko pre bizi dar hem vazden tumare šere adalese soi paše tumaro spasenje.”
29 Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
Tegani o Isus phenđa lenđe akaja priča: “Dikhen i smokva ili bilo savo aver kaš.
30 Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
Kad dikhena da ikljona listija upro leste, korkore džanen dai paše o linaj.
31 Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
Ađahar hem tumen kad dikhena da ovela sa adava, te džanen dai o carstvo e Devlesoro paše.
32 “Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
Čače vaćerava tumenđe, akaja generacija naka nakhel đikote sa adava na ovela.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
O nebo hem i phuv ka nakhen, ali mle lafija nikad naka nakhen.”
34 “Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
I o Isus phenđa lenđe: “Arakhen tumen te na oven zaokupirime pibnaja, mačojbnaja hem akale dživdipnasere brigencar i te resel tumen otojekhvar adava dive.
35 Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
Adalese so adava dive ka avel sar zamka upro sa o manuša ki phuv.
36 Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
Adalese oven džangale hem stalno molinen te šaj nakhaven sa adava so valjani te ovel hem te terđoven anglo Čhavo e manušesoro.”
37 Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
Diveja o Isus sikaj ine ano Hram, a raćaja ikljola ine tari diz hem džala te nakhaj i rat ki gora vičimi e Maslinakiri.
38 Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.
I sa o manuša rano sabaleja džana ine ko Hram te šunen le.

< Luka 21 >