< Luka 21 >

1 Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
Un Savas acis pacēlis, Viņš redzēja bagātos savas dāvanas metam Dieva šķirstā.
2 Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
Un Viņš arī redzēja, ka viena nabaga atraitne divas artavas iemeta tur iekšā,
3 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
Un sacīja: “Es jums tiešām saku, ka šī nabaga atraitne vairāk ir iemetusi, nekā visi.
4 Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
Jo šie visi no savas bagātības ir iemetuši pie tām Dieva dāvanām, bet šī no savas nabadzības ir iemetusi visu savu padomu, cik viņai bija.”
5 Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
Un kādiem par Dieva namu runājot, ka tas esot izgreznots ar dārgiem akmeņiem un jaukām uzkārtām dāvanām, Viņš sacīja:
6 “Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
“Laiks nāks, kad no tā, ko jūs redzat, ne akmens uz akmens netaps pamests, ko nenolauzīs.”
7 Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
Un tie Viņam vaicāja sacīdami: “Mācītāj, kad tad tas būs? Un kāda tā zīme, kad šīs lietas notiks?”
8 Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
Bet Viņš sacīja: “Pielūkojiet, ka jūs netopat pievilti. Jo daudzi nāks Manā Vārdā sacīdami: es tas esmu, un tas laiks ir tuvu klāt nācis. Tad nu neejat viņiem pakaļ,
9 Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
Bet kad jūs dzirdēsiet karus un dumpjus, tad neiztrūcinājaties, jo šim visam būs papriekš notikt, bet tūdaļ vēl nav tas gals.”
10 Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
Tad Viņš uz tiem sacīja: “Tauta celsies pret tautu un valsts pret valsti.
11 Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
Un lielas zemes trīcēšanas būs dažās vietās un bada laiki un mēri arī bailīgas lietas un lielas zīmes no debesīm notiks.
12 “Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
Bet pirms viss tas notiks, tie savas rokas jums pieliks un jūs vajās un nodos baznīcās un cietumos, un jūs vedīs priekš ķēniņiem un valdniekiem Mana Vārda dēļ.
13 Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
Bet tas notiks jums par liecību.
14 Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
Tad nu apņematies savās sirdīs, nerūpēties iepriekš, kā jūs aizbildināsities.
15 Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
Jo Es jums došu muti un gudrību, kam nevarēs pretī runāt nedz pretī stāvēt neviens no tiem, kas pret jums ceļas.
16 Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
Bet jūs tapsiet nodoti arī no vecākiem un brāļiem un radiem un draugiem. Un tie citus no jums nonāvēs.
17 Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
Un jūs būsiet ienīdēti no visiem Mana Vārda dēļ
18 Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
Un tomēr ne matam no jūsu galvas nebūs zust.
19 Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
Caur savu pacietību izglābsiet savas dvēseles.
20 “Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
Bet kad jūs redzēsiet Jeruzālemi visapkārt apstātu no karaspēka, tad zināt, ka viņas izpostīšana ir tuvu klāt.
21 Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
Tad lai bēg kalnos, kas ir Jūdu zemē, un lai steidzās projām, kas ir viņas vidū; un tie, kas uz laukiem, lai neiet tur iekšā.
22 Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
Jo šīs ir tās atriebšanas dienas, lai viss top piepildīts, kas ir rakstīts.
23 Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
Bet, ak vai, tām grūtām un zīdītājām tanīs dienās, jo tur būs lielas bēdas virs zemes un dusmas par šo tautu.
24 Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
Un tie kritīs caur zobena asmeni un gūstīti taps novesti pie visām tautām, un Jeruzāleme taps samīdīta no pagāniem, tiekams pagānu laiki būs piepildīti.
25 “Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
Un zīmes notiks pie saules, pie mēneša un pie zvaigznēm, un virs zemes tiem ļaudīm būs bail, un tie būs pārbijušies, un jūra un ūdens viļņi kauks.
26 Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
Un cilvēki nīcin iznīks no bailības, gaidīdami tās lietas, kas nāks virs zemes, jo debess stiprumi kustināsies.
27 Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
Un tad tie redzēs To Cilvēka Dēlu padebesī nākam ar lielu spēku un godu.
28 Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
Bet kad tas iesāks notikt, tad savas galvas paceldami skatāties uz augšu, tāpēc ka jūsu pestīšana jo tuvu nāk.”
29 Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
Un Viņš tiem sacīja vienu līdzību: “Uzlūkojiet vīģes koku un visus kokus!
30 Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
Tūdaļ kad tie izplaukst, tad jūs to redzēdami paši nomaniet, ka vasara jau tuvu.
31 Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
Tā tad arī, redzēdami šo visu notiekam, ziniet, ka Dieva valstība tuvu.
32 “Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
Patiesi, Es jums saku: šī cilts nezudīs, tiekams viss tas būs noticis.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
Debess un zeme zudīs, bet Mani vārdi nezudīs.
34 “Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
Bet sargājaties, ka jūsu sirdis nekļūst apgrūtinātas ar lieku ēšanu un ar zūdīšanos pēc uztura, un ka šī diena piepeši jums neuzbrūk.
35 Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
Jo viņa nāks, kā kāds slazda valgs pār visiem, kas dzīvo pa visu zemes virsu.
36 Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
Tāpēc esiet modrīgi allažiņ un lūdziet, lai varat šim visam izbēgt, kas notiks, un pastāvēt Tā Cilvēka Dēla priekšā.”
37 Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
Un Viņš pa tām dienām bija Dieva namā mācīdams; un pa tām naktīm Viņš izgāja un palika tai kalnā, kas top saukts Eļļas kalns.
38 Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.
Un visi ļaudis nāca agri no rīta pie Viņa Dieva namā, Viņu klausīties.

< Luka 21 >