< Luka 21 >
1 Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
And he looked up and saw the rich men casting their gifts into the treasury.
2 Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
And he saw also a certain poor widow casting in thither two mites.
3 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
And he said, In truth I say to you, that this poor widow hath cast in more than they all.
4 Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
For all these out of their abundance cast in to the offerings; but she out of her penury cast in all the living that she had.
5 Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
And as some were saying of the temple, that it was adorned with goodly stones, and sacred gifts, he said,
6 “Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
As for these things which ye behold, the days will come, in which there will not be left here one stone upon another, that will not be throw down.
7 Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
And they asked him, saying, Teacher, when then will these things be? and what will be the sign when these things are about to come to pass?
8 Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
And he said, Take heed that ye be not deceived. For many will come in my name, saying, I am He, and the time is at hand. Go not after them.
9 Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
And when ye hear of wars and tumults, be not terrified; for these things must first come to pass; but not immediately is the end.
10 Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
Then he said to them, Nation will rise against nation, and kingdom against kingdom;
11 Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
and there will be great earthquakes, and in divers places famines and pestilences; and there will be fearful sights and great signs from heaven.
12 “Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
But before all these things they will lay their hands on you and persecute you, delivering you up to synagogues, and into prisons, and bringing you before kings and governors on account of my name.
13 Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
It will turn out to you an opportunity for bearing testimony.
14 Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
Settle it therefore in your hearts not to meditate l beforehand what ye shall answer.
15 Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
For I will give you a mouth and wisdom, which all your adversaries will not be able to withstand or gainsay.
16 Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
And ye will be delivered up both by parents and brothers and kinsmen and friends; and some of you will they put to death.
17 Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
And ye will be hated by all on account of my name.
18 Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
But not a hair of your head will be lost.
19 Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
By your constancy secure your lives.
20 “Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
But when ye see Jerusalem encompassed by armies, then know that her desolation is at hand.
21 Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
Then let those who are in Judaea flee to the mountains; and let those who are within the city go out of it, and let not those in the open country enter it.
22 Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
For these are days of vengeance, that all things which are written may be fulfilled.
23 Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
But woe to the women with child, and to those having children at the breast, in those days! For there will be great distress in the land, and wrath upon this people;
24 Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
and they will fall by the edge of the sword, and will be led away captive into all the nations; and Jerusalem will be trodden down by the gentiles, until the times of the gentiles are fulfilled.
25 “Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
And there will be signs in the sun and moon and stars; and on the earth distress of nations, in perplexity at the roaring of the sea and waves;
26 Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
men's hearts failing them from fear, and from looking for those things which are coming on the world; for the powers of the heavens will be shaken.
27 Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
And then will they see the Son of man coming in a cloud with power and great glory.
28 Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
And when these things begin to come to pass, look up, and lift up your heads; for your redemption draweth nigh.
29 Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
And he spoke to them a parable: Behold the fig-tree and all the trees;
30 Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
when they have already shot forth, ye see it, and know of yourselves that summer is now nigh at hand.
31 Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
So also, when ye see these things coming to pass, know ye that the kingdom of God is nigh at hand.
32 “Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
Truly do I say to you, that this generation will not pass away, till all shall have taken place.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
Heaven and earth will pass away, but my words will not pass away.
34 “Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
But take heed to yourselves, lest at any time your hearts be weighed down with surfeiting and drunkenness and worldly cares, and that day come upon you unawares.
35 Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
For as a snare will it come on all that dwell on the face of the whole earth.
36 Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
But watch at all times, and pray that ye may be able to escape all the things that are about to come to pass, and to stand before the Son of man.
37 Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
And during the daytime he was teaching in the temple; but at night he went out, and lodged in the mount called the Mount of Olives.
38 Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.
And all the people came early in the morning to him in the temple, to hear him.