< Luka 21 >
1 Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
And he looked up, and saw the rich men casting their gifts into the treasury.
2 Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
And he saw also a certain poor widow casting in thither two mites.
3 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
And he said, Of a truth I say unto you, that this poor widow hath cast in more than they all:
4 Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
For all these have of their abundance cast in unto the offerings to Elohim: but she of her penury hath cast in all the living that she had.
5 Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
And as some spake of the temple, how it was adorned with goodly stones and gifts, he said,
6 “Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
As for these things which ye behold, the days will come, in the which there shall not be left one stone upon another, that shall not be thrown down.
7 Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
And they asked him, saying, Master, but when shall these things be? and what sign will there be when these things shall come to pass?
8 Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
And he said, Take heed that ye be not deceived: for many shall come in my name, saying, I am the Messiah; and the time draweth near: go ye not therefore after them.
9 Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
But when ye shall hear of wars and commotions, be not terrified: for these things must first come to pass; but the end is not by and by.
10 Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
Then said he unto them, Nation shall rise against nation, and kingdom against kingdom:
11 Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
And great earthquakes shall be in divers places, and famines, and pestilences; and fearful sights and great signs shall there be from heaven.
12 “Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
But before all these, they shall lay their hands on you, and persecute you, delivering you up to the synagogues, and into prisons, being brought before kings and rulers for my name's sake.
13 Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
And it shall turn to you for a testimony.
14 Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
Settle it therefore in your hearts, not to meditate before what ye shall answer:
15 Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
For I will give you a mouth and wisdom, which all your adversaries shall not be able to gainsay nor resist.
16 Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
And ye shall be betrayed both by parents, and brethren, and kinsfolks, and friends; and some of you shall they cause to be put to death.
17 Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
And ye shall be hated of all men for my name's sake.
18 Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
But there shall not an hair of your head perish.
19 Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
In your patience possess ye your souls.
20 “Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
And when ye shall see Jerusalem compassed with armies, then know that the desolation thereof is nigh.
21 Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
Then let them which are in Judaea flee to the mountains; and let them which are in the midst of it depart out; and let not them that are in the countries enter thereinto.
22 Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
For these be the days of vengeance, that all things which are written may be fulfilled.
23 Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
But woe unto them that are with child, and to them that give suck, in those days! for there shall be great distress in the land, and wrath upon this people.
24 Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
And they shall fall by the edge of the sword, and shall be led away captive into all nations: and Jerusalem shall be trodden down of the Gentiles, until the times of the Gentiles be fulfilled.
25 “Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
And there shall be signs in the sun, and in the moon, and in the stars; and upon the earth distress of nations, with perplexity; the sea and the waves roaring;
26 Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
Men's hearts failing them for fear, and for looking after those things which are coming on the earth: for the powers of heaven shall be shaken.
27 Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
And then shall they see the Son of man coming in a cloud with power and great glory.
28 Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
And when these things begin to come to pass, then look up, and lift up your heads; for your redemption draweth nigh.
29 Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
And he spake to them a parable; Behold the fig tree, and all the trees;
30 Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
When they now shoot forth, ye see and know of your own selves that summer is now nigh at hand.
31 Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
So likewise ye, when ye see these things come to pass, know ye that the kingdom of YHWH is nigh at hand.
32 “Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
Verily I say unto you, This generation shall not pass away, till all be fulfilled.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
Heaven and earth shall pass away: but my words shall not pass away.
34 “Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
And take heed to yourselves, lest at any time your hearts be overcharged with surfeiting, and drunkenness, and cares of this life, and so that day come upon you unawares.
35 Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
For as a snare shall it come on all them that dwell on the face of the whole earth.
36 Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
Watch ye therefore, and pray always, that ye may be accounted worthy to escape all these things that shall come to pass, and to stand before the Son of man.
37 Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
And in the day time he was teaching in the temple; and at night he went out, and abode in the mount that is called the mount of Olives.
38 Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.
And all the people came early in the morning to him in the temple, for to hear him.