< Luka 21 >

1 Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
And looking on, he saw the rich men cast their gifts into the treasury.
2 Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
And he saw also a certain poor widow casting in two brass mites.
3 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
And he said: Verily I say to you, that this poor widow hath cast in more than they all:
4 Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
For all these have of their abundance cast into the offerings of God: but she of her want, hath cast in all the living that she had.
5 Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
And some saying of the temple, that it was adorned with goodly stones and gifts, he said:
6 “Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
These things which you see, the days will come in which there shall not be left a stone upon a stone that shall not be thrown down.
7 Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
And they asked him, saying: Master, when shall these things be? and what shall be the sign when they shall begin to come to pass?
8 Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
Who said: Take heed you be not seduced; for many will come in my name, saying, I am he; and the time is at hand: go ye not therefore after them.
9 Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
And when you shall hear of wars and seditions, be not terrified: these things must first come to pass; but the end is not yet presently.
10 Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
Then he said to them: Nation shall rise against nation, and kingdom against kingdom.
11 Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
And there shall be great earthquakes in divers places, and pestilences, and famines, and terrors from heaven; and there shall be great signs.
12 “Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
But before all these things, they will lay their hands upon you, and persecute you, delivering you up to the synagogues and into prisons, dragging you before kings and governors, for my name’s sake.
13 Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
And it shall happen unto you for a testimony.
14 Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
Lay it up therefore into your hearts, not to meditate before how you shall answer:
15 Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
For I will give you a mouth and wisdom, which all your adversaries shall not be able to resist and gainsay.
16 Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
And you shall be betrayed by your parents and brethren, and kinsmen and friends; and some of you they will put to death.
17 Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
And you shall be hated by all men for my name’s sake.
18 Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
But a hair of your head shall not perish.
19 Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
In your patience you shall possess your souls.
20 “Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
And when you shall see Jerusalem compassed about with an army; then know that the desolation thereof is at hand.
21 Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
Then let those who are in Judea, flee to the mountains; and those who are in the midst thereof, depart out: and those who are in the countries, not enter into it.
22 Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
For these are the days of vengeance, that all things may be fulfilled, that are written.
23 Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
But woe to them that are with child, and give suck in those days; for there shall be great distress in the land, and wrath upon this people.
24 Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
And they shall fall by the edge of the sword; and shall be led away captives into all nations; and Jerusalem shall be trodden down by the Gentiles; till the times of the nations be fulfilled.
25 “Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
And there shall be signs in the sun, and in the moon, and in the stars; and upon the earth distress of nations, by reason of the confusion of the roaring of the sea and of the waves;
26 Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
Men withering away for fear, and expectation of what shall come upon the whole world. For the powers of heaven shall be moved;
27 Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
And then they shall see the Son of man coming in a cloud, with great power and majesty.
28 Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
But when these things begin to come to pass, look up, and lift up your heads, because your redemption is at hand.
29 Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
And he spoke to them in a similitude. See the fig tree, and all the trees:
30 Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
When they now shoot forth their fruit, you know that summer is nigh;
31 Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
So you also, when you shall see these things come to pass, know that the kingdom of God is at hand.
32 “Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
Amen, I say to you, this generation shall not pass away, till all things be fulfilled.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
Heaven and earth shall pass away, but my words shall not pass away.
34 “Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
And take heed to yourselves, lest perhaps your hearts be overcharged with surfeiting and drunkenness, and the cares of this life, and that day come upon you suddenly.
35 Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
For as a snare shall it come upon all that sit upon the face of the whole earth.
36 Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
Watch ye, therefore, praying at all times, that you may be accounted worthy to escape all these things that are to come, and to stand before the Son of man.
37 Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
And in the daytime, he was teaching in the temple; but at night, going out, he abode in the mount that is called Olivet.
38 Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.
And all the people came early in the morning to him in the temple, to hear him.

< Luka 21 >