< Luka 21 >

1 Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
耶稣抬头观看,见财主把捐项投在库里,
2 Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
又见一个穷寡妇投了两个小钱,
3 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
就说:“我实在告诉你们,这穷寡妇所投的比众人还多;
4 Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
因为众人都是自己有余,拿出来投在捐项里,但这寡妇是自己不足,把她一切养生的都投上了。”
5 Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
有人谈论圣殿是用美石和供物妆饰的;
6 “Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
耶稣就说:“论到你们所看见的这一切,将来日子到了,在这里没有一块石头留在石头上,不被拆毁了。”
7 Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
他们问他说:“夫子!什么时候有这事呢?这事将到的时候有什么预兆呢?”
8 Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
耶稣说:“你们要谨慎,不要受迷惑;因为将来有好些人冒我的名来,说:‘我是基督’,又说:‘时候近了’,你们不要跟从他们!
9 Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
你们听见打仗和扰乱的事,不要惊惶;因为这些事必须先有,只是末期不能立时就到。”
10 Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
当时,耶稣对他们说:“民要攻打民,国要攻打国;
11 Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
地要大大震动,多处必有饥荒、瘟疫,又有可怕的异象和大神迹从天上显现。
12 “Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
但这一切的事以先,人要下手拿住你们,逼迫你们,把你们交给会堂,并且收在监里,又为我的名拉你们到君王诸侯面前。
13 Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
但这些事终必为你们的见证。
14 Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
所以,你们当立定心意,不要预先思想怎样分诉;
15 Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
因为我必赐你们口才、智慧,是你们一切敌人所敌不住、驳不倒的。
16 Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
连你们的父母、弟兄、亲族、朋友也要把你们交官;你们也有被他们害死的。
17 Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
你们要为我的名被众人恨恶,
18 Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
然而,你们连一根头发也必不损坏。
19 Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
你们常存忍耐,就必保全灵魂。”
20 “Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
“你们看见耶路撒冷被兵围困,就可知道它成荒场的日子近了。
21 Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
那时,在犹太的应当逃到山上;在城里的应当出来;在乡下的不要进城;
22 Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
因为这是报应的日子,使经上所写的都得应验。
23 Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
当那些日子,怀孕的和奶孩子的有祸了!因为将有大灾难降在这地方,也有震怒临到这百姓。
24 Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
他们要倒在刀下,又被掳到各国去。耶路撒冷要被外邦人践踏,直到外邦人的日期满了。”
25 “Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
“日、月、星辰要显出异兆,地上的邦国也有困苦;因海中波浪的响声,就慌慌不定。
26 Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
天势都要震动,人想起那将要临到世界的事,就都吓得魂不附体。
27 Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
那时,他们要看见人子有能力,有大荣耀驾云降临。
28 Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
一有这些事,你们就当挺身昂首,因为你们得赎的日子近了。”
29 Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
耶稣又设比喻对他们说:“你们看无花果树和各样的树;它发芽的时候,你们一看见,自然晓得夏天近了。
30 Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
31 Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
这样,你们看见这些事渐渐地成就,也该晓得 神的国近了。
32 “Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
我实在告诉你们,这世代还没有过去,这些事都要成就。
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
天地要废去,我的话却不能废去。”
34 “Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
“你们要谨慎,恐怕因贪食、醉酒,并今生的思虑累住你们的心,那日子就如同网罗忽然临到你们;
35 Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
因为那日子要这样临到全地上一切居住的人。
36 Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
你们要时时警醒,常常祈求,使你们能逃避这一切要来的事,得以站立在人子面前。”
37 Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
耶稣每日在殿里教训人,每夜出城在一座山,名叫橄榄山住宿。
38 Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.
众百姓清早上圣殿,到耶稣那里,要听他讲道。

< Luka 21 >