< Luka 20 >

1 Siku moja, Yesu alipokuwa akifundisha watu Hekaluni na kuhubiri habari njema, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria, pamoja na wazee wa watu wakamjia.
I stało się z onych dni dnia jednego, gdy uczył lud w kościele i kazał Ewangeliję, że nadeszli przedniejsi kapłani i nauczeni w Piśmie z starszymi,
2 Wakamuuliza, “Tuambie, unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ni nani aliyekupa mamlaka haya?”
I rzekli do niego, mówiąc: Powiedz nam, którą mocą to czynisz, albo kto jest ten, coć dał tę moc?
3 Akawajibu, “Nami nitawauliza swali.
A on odpowiadając, rzekł do nich: Spytam i ja was o jednę rzecz, a powiedzcie mi:
4 Je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?”
Chrzest Jana byłli z nieba, czyli z ludzi?
5 Wakahojiana wao kwa wao wakisema, “Kama tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Mbona hamkumwamini?’
A oni myślili sami w sobie, mówiąc: Jeźli powiemy, z nieba, rzecze: Czemużeście mu tedy nie wierzyli?
6 Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ watu wote watatupiga mawe, kwa sababu wanaamini kwamba Yohana alikuwa nabii.”
Jeźliż zasię rzeczemy, z ludzi, wszystek lud ukamionuje nas, ponieważ za pewne mają, że Jan jest prorokiem.
7 Basi wakajibu, “Hatujui ulikotoka.”
I odpowiedzieli, że nie wiedzą, skąd by był.
8 Yesu akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”
A Jezus im rzekł: I ja wam nie powiem, którą mocą to czynię.
9 Akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima fulani, kisha akasafiri kwa muda mrefu.
I począł do ludu mówić to podobieństwo: Człowiek niektóry nasadził winnicę, i najął ją winiarzom, i odjechał precz na czas niemały.
10 Wakati wa mavuno ulipofika, akamtuma mtumishi wake kwa hao wapangaji ili wampe sehemu ya mavuno ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga, wakamfukuza mikono mitupu.
A czasu swego posłał sługę do onych winiarzy, aby mu dali z pożytku onej winnicy; ale oni winiarze ubiwszy go, odesłali próżnego.
11 Akamtuma mtumishi mwingine, huyo naye wakampiga, wakamfanyia mambo ya aibu na kumfukuza.
I posłał zasię drugiego sługę; ale oni i tego ubiwszy i zelżywszy, odesłali próżnego.
12 Bado akamtuma na mwingine wa tatu, huyu pia wakamjeruhi na kumtupa nje ya shamba.
I posłał zasię trzeciego; ale oni i tego zraniwszy, wyrzucili precz.
13 “Basi yule mwenye shamba la mizabibu akasema, ‘Nifanye nini? Nitamtuma mwanangu mpendwa, huenda yeye watamheshimu.’
A tak rzekł Pan onej winnicy: Cóż uczynię? poślę syna mego miłego, snać gdy tego ujrzą, zawstydzą się.
14 “Lakini wale wapangaji walipomwona, wakasemezana wao kwa wao. Wakasema, ‘Huyu ndiye mrithi. Basi na tumuue ili urithi uwe wetu.’
Ale winiarze ujrzawszy go, rzekli między sobą, mówiąc: Tenci jest dziedzic; pójdźcie zabijmy go, aby nasze było dziedzictwo.
15 Kwa hiyo wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamuua.” “Sasa basi yule mwenye shamba la mizabibu atawafanyia nini wapangaji hawa?
I wypchnąwszy go precz z winnicy, zabili. Cóż im tedy uczyni Pan onej winnicy?
16 Atakuja na kuwaua hao wapangaji, na kuwapa wapangaji wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia hayo wakasema, “Mungu apishie mbali jambo hili lisitokee!”
Przyjdzie, a potraci one winiarze, a winnicę odda innym. Co oni usłyszawszy, rzekli: Nie daj tego Boże!
17 Lakini Yesu akawakazia macho, akasema, “Basi ni nini maana ya yale yaliyoandikwa: “‘Jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni’?
Lecz on spojrzawszy na nie, rzekł: Cóż tedy jest ono, co napisano: Kamień, który odrzucili budujący, ten się stał głową węgielną?
18 Kila mtu aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika vipande vipande, lakini yule litakayemwangukia atasagwa kabisa.”
Wszelki, który upadnie na ten kamień, roztrąci się, a na kogo by upadł, zetrze go.
19 Walimu wa sheria na viongozi wa makuhani wakatafuta njia ya kumkamata mara moja, kwa sababu walifahamu kwamba amesema mfano huo kwa ajili yao. Lakini waliwaogopa watu.
I starali się przedniejsi kapłani i nauczeni w Piśmie, jakoby nań ręce wrzucili onejże godziny, ale się ludu bali; albowiem poznali, iż przeciwko nim wyrzekł to podobieństwo.
20 Kwa hiyo wakawa wanamchunguza na kutuma wapelelezi waliojifanya kuwa wenye haki ili wapate kumtega kwa maneno asemayo, ili wamtie katika uwezo na mamlaka ya mtawala.
A tak podstrzegając go, posłali szpiegi, którzy zmyślali, jakoby byli sprawiedliwymi, aby go podchwycili w mowie jego, a potem aby go podali zwierzchności i w moc starościną.
21 Hivyo wale wapelelezi wakamuuliza, “Mwalimu, tunajua unasema na kufundisha yaliyo kweli wala humpendelei mtu, bali wafundisha njia ya Mungu katika kweli.
I pytali go, mówiąc: Nauczycielu! wiemy, że dobrze mówisz i uczysz, ani przyjmujesz osób; ale drogi Bożej w prawdzie uczysz.
22 Je, ni halali sisi kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
Godzili się nam dać czynsz cesarzowi, czyli nie?
23 Lakini Yesu akatambua hila yao, kwa hiyo akawaambia,
Ale on obaczywszy chytrość ich, rzekł do nich: Czemuż mię kusicie?
24 “Nionyesheni dinari. Je, sura hii na maandishi haya yaliyoko juu yake ni vya nani?”
Ukażcie mi grosz; czyj ma obraz i napis? A odpowiadając rzekli: Cesarza.
25 Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Akawaambia, “Basi mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.”
Zatem on im rzekł: Oddawajcież tedy, co jest cesarskiego, cesarzowi, a co jest Bożego, Bogu.
26 Wakashindwa kumkamata kwa yale aliyokuwa amesema hadharani. Nao wakashangazwa mno na majibu yake, wakanyamaza kimya.
I nie mogli go podchwycić w mowie jego przed ludem, a zadziwiwszy się odpowiedzi jego, umilknęli.
27 Baadhi ya Masadukayo, wale wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu na kumuuliza,
A przyszedłszy niektórzy z Saduceuszów, (którzy przeczą i mówią, iż nie masz zmartwychwstania), pytali go,
28 “Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu wa mtu akifa na kumwacha mkewe bila mtoto, basi huyo mtu inampasa amwoe huyo mjane ili amzalie ndugu yake watoto.
Mówiąc: Nauczycielu! Mojżesz nam napisał: Jeźliby komu brat umarł, mając żonę, a umarłby bez dziatek, aby brat jego pojął jego żonę, a wzbudził nasienie bratu swemu.
29 Basi palikuwepo ndugu saba. Yule wa kwanza akaoa, akafa bila kuzaa mtoto.
Było tedy siedm braci, z których pierwszy pojąwszy żonę, umarł bez dziatek.
30 Kisha yule wa pili akamwoa huyo mjane, naye akafa bila mtoto,
I pojął wtóry onę żonę, a umarł i ten bez dziatek.
31 naye wa tatu pia akamwoa. Vivyo hivyo ndugu wote saba wakawa wamemwoa huyo mwanamke, na wote wakafa pasipo yeyote kupata mtoto.
Potem ją pojął i trzeci, także i oni wszyscy siedmiu, a nie zostawiwszy dziatek, pomarli.
32 Mwishowe, yule mwanamke naye akafa.
Po wszystkich też umarła i ona niewiasta.
33 Sasa basi, siku ya ufufuo huyo mwanamke atakuwa mke wa nani, maana aliolewa na ndugu wote saba?”
Przetoż przy zmartwychwstaniu, któregoż z nich ona będzie żoną, ponieważ siedmiu ich miało ją za żonę?
34 Yesu akawajibu, “Katika maisha haya watu huoa na kuolewa. (aiōn g165)
Tedy odpowiadając, rzekł im Jezus: Synowie tego wieku żenią się i za mąż wydają. (aiōn g165)
35 Lakini wale ambao wamehesabiwa kwamba wanastahili kupata nafasi katika ulimwengu ule na katika ufufuo wa wafu, hawaoi wala hawaolewi. (aiōn g165)
Ale ci, którzy godni są, aby dostąpili onego wieku, i powstaną od umarłych, ani się żenić, ani za mąż dawać będą. (aiōn g165)
36 Hawa hawawezi kufa tena, kwa maana wao ni kama malaika. Wao ni watoto wa Mungu, kwa sababu ni watoto wa ufufuo.
Albowiem umierać więcej nie będą mogli; bo będą równi Aniołom, będąc synami Bożymi, gdyż są synami zmartwychwstania.
37 Hata Mose alidhihirisha kuwa wafu wanafufuka, kwa habari ya kile kichaka kilichokuwa kikiwaka moto bila kuteketea, alipomwita Bwana, ‘Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo.’
A iż umarli zmartwychwstaną, i Mojżesz pokazał przy onym krzaku, gdy zowie Pana Boga Bogiem Abrahamowym i Bogiem Izaakowym i Bogiem Jakóbowym.
38 Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai, kwa kuwa kwake wote ni hai.”
A Bógci nie jest Bogiem umarłych, ale żywych; bo jemu wszyscy żyją.
39 Baadhi ya walimu wa sheria wakasema, “Mwalimu, umesema sawasawa kabisa!”
Tedy odpowiadając niektórzy z nauczonych w Piśmie, rzekli: Nauczycielu! dobrześ powiedział.
40 Baada ya hayo hakuna mtu aliyethubutu kumuuliza maswali tena.
I nie śmieli go więcej o nic pytać.
41 Kisha Yesu akawaambia, “Imekuwaje basi wao husema Kristoni Mwana wa Daudi?
I rzekł do nich: Jakoż powiadają, że Chrystus jest synem Dawidowym?
42 Daudi mwenyewe anasema katika Kitabu cha Zaburi: “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume,
A sam Dawid mówi w księgach Psalmów: Rzekł Pan Panu memu: Siądź po prawicy mojej
43 hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
Aż położę nieprzyjacioły twoje podnóżkiem nóg twoich.
44 Ikiwa Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ basi atakuwaje mwanawe?”
Ponieważ go tedy Dawid nazywa Panem, i jakoż jest synem jego?
45 Wakati watu wote walikuwa wanamsikiliza, Yesu akawaambia wanafunzi wake,
A gdy słuchał wszystek lud, rzekł uczniom swoim:
46 “Jihadharini na walimu wa sheria. Wao hupenda kutembea wakiwa wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa kwa heshima masokoni. Hupenda kukaa kwenye viti vya mbele katika masinagogi, na kukaa kwenye nafasi za heshima katika karamu.
Strzeżcie się nauczonych w Piśmie, którzy chcą chodzić w szatach długich, i miłują pozdrawiania na rynkach i pierwsze stołki w bóżnicach, i pierwsze miejsca na wieczerzach;
47 Wao hula nyumba za wajane, na ili waonekane kuwa wema, wanasali sala ndefu. Watu kama hawa watapata hukumu iliyo kuu sana.”
Którzy pożerają domy wdów, a to pod pokrywką długich modlitw: cić odniosą cięższy sąd.

< Luka 20 >