< Luka 20 >
1 Siku moja, Yesu alipokuwa akifundisha watu Hekaluni na kuhubiri habari njema, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria, pamoja na wazee wa watu wakamjia.
AND it was on one of the days, while he taught the people in the temple and evangelized, the chief priests and scribes with the elders rose up against him,
2 Wakamuuliza, “Tuambie, unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ni nani aliyekupa mamlaka haya?”
and said to him, Tell us by what authority thou doest these, and who is he who gave thee this authority?
3 Akawajibu, “Nami nitawauliza swali.
Jeshu answered and said to them, I will also ask of you a word, and tell you me:
4 Je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?”
the baptism of Juchanon, from heaven was it, or from the sons of men?
5 Wakahojiana wao kwa wao wakisema, “Kama tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Mbona hamkumwamini?’
But they reasoned within themselves, saying, If we shall say, From heaven, he saith to us, Why did you not believe him?
6 Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ watu wote watatupiga mawe, kwa sababu wanaamini kwamba Yohana alikuwa nabii.”
But if we shall say, From men, all the people will stone us; for they are persuaded that Juchanon was a prophet.
7 Basi wakajibu, “Hatujui ulikotoka.”
And they said to him, We know not from whence it is.
8 Yesu akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”
Jeshu saith to them, Nor tell I you by what authority I do these.
9 Akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima fulani, kisha akasafiri kwa muda mrefu.
And he began to speak to the people this parable: A certain man planted a vinery, and let it to husbandmen, and removed for a great time.
10 Wakati wa mavuno ulipofika, akamtuma mtumishi wake kwa hao wapangaji ili wampe sehemu ya mavuno ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga, wakamfukuza mikono mitupu.
And at the season he sent his servant to the husbandmen that they should give him of the fruit of the vinery. But the husbandmen beat him, and sent him away empty.
11 Akamtuma mtumishi mwingine, huyo naye wakampiga, wakamfanyia mambo ya aibu na kumfukuza.
And he added and sent another servant; but they beat him also, and maltreated him, and sent him away empty.
12 Bado akamtuma na mwingine wa tatu, huyu pia wakamjeruhi na kumtupa nje ya shamba.
And he added and sent a third; but they also wounded him, and cast him out.
13 “Basi yule mwenye shamba la mizabibu akasema, ‘Nifanye nini? Nitamtuma mwanangu mpendwa, huenda yeye watamheshimu.’
The lord of the vinery saith, What shall I do? I will send my son, the beloved; now will they see him and reverence him.
14 “Lakini wale wapangaji walipomwona, wakasemezana wao kwa wao. Wakasema, ‘Huyu ndiye mrithi. Basi na tumuue ili urithi uwe wetu.’
But when the husbandmen saw him, they reasoned among themselves, saying, This is the heir: come, let us kill him, and the inheritance will be ours.
15 Kwa hiyo wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamuua.” “Sasa basi yule mwenye shamba la mizabibu atawafanyia nini wapangaji hawa?
And they cast him out of the vinery, and killed him. What therefore shall the lord of the vinery do to them?
16 Atakuja na kuwaua hao wapangaji, na kuwapa wapangaji wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia hayo wakasema, “Mungu apishie mbali jambo hili lisitokee!”
He will come and destroy those husbandmen, and will give the vinery to others. But when they heard, they said, May this not be!
17 Lakini Yesu akawakazia macho, akasema, “Basi ni nini maana ya yale yaliyoandikwa: “‘Jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni’?
But he beheld them, and said, And what is that which is written, The stone which the builders rejected is become the head of the corner?
18 Kila mtu aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika vipande vipande, lakini yule litakayemwangukia atasagwa kabisa.”
And every one who shall fall upon this stone shall be broken; and every one on whom it shall fall it will scatter him.
19 Walimu wa sheria na viongozi wa makuhani wakatafuta njia ya kumkamata mara moja, kwa sababu walifahamu kwamba amesema mfano huo kwa ajili yao. Lakini waliwaogopa watu.
But the chief priests and Sophree sought to lay hands on him in that very hour; but they feared the people, for they knew that concerning them(selves) he had spoken this parable.
20 Kwa hiyo wakawa wanamchunguza na kutuma wapelelezi waliojifanya kuwa wenye haki ili wapate kumtega kwa maneno asemayo, ili wamtie katika uwezo na mamlaka ya mtawala.
And they sent to him spies, who should resemble just men, that they might take him in discourse, and deliver him to the judgment and to the authority of the governor.
21 Hivyo wale wapelelezi wakamuuliza, “Mwalimu, tunajua unasema na kufundisha yaliyo kweli wala humpendelei mtu, bali wafundisha njia ya Mungu katika kweli.
And they asked him, and said to him, Doctor, we know that thou speakest and teachest rightly, neither dost thou deceive, but with integrity thou teachest the way of Aloha.
22 Je, ni halali sisi kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
Is it lawful for us to give head-silver to Cesar or not?
23 Lakini Yesu akatambua hila yao, kwa hiyo akawaambia,
But he understood their subtilty, and said, Why tempt you me?
24 “Nionyesheni dinari. Je, sura hii na maandishi haya yaliyoko juu yake ni vya nani?”
Show me a dinara. Of whom upon it is the image and the inscription? But they said, Of Cesar.
25 Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Akawaambia, “Basi mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.”
Jeshu saith to them, Give then of Cesar's to Cesar, and of Aloha's unto Aloha.
26 Wakashindwa kumkamata kwa yale aliyokuwa amesema hadharani. Nao wakashangazwa mno na majibu yake, wakanyamaza kimya.
And they could not take hold of his words before the people; and they wondered at his answer, and were silent.
27 Baadhi ya Masadukayo, wale wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu na kumuuliza,
BUT some of the Zadukoyee approached, they who say that there is no resurrection;
28 “Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu wa mtu akifa na kumwacha mkewe bila mtoto, basi huyo mtu inampasa amwoe huyo mjane ili amzalie ndugu yake watoto.
and they questioned him, and said to him, Doctor, Musha wrote to us that if a man's brother die having a wife who hath not children, his brother shall take his wife, and raise up seed unto his brother.
29 Basi palikuwepo ndugu saba. Yule wa kwanza akaoa, akafa bila kuzaa mtoto.
But there were seven brethren; and the first took; a wife, and died without children.
30 Kisha yule wa pili akamwoa huyo mjane, naye akafa bila mtoto,
And the second took his wife, and he died without children.
31 naye wa tatu pia akamwoa. Vivyo hivyo ndugu wote saba wakawa wamemwoa huyo mwanamke, na wote wakafa pasipo yeyote kupata mtoto.
And the third also took her; and so also the seven of them: and they died and left no children.
32 Mwishowe, yule mwanamke naye akafa.
Died in the end also the woman.
33 Sasa basi, siku ya ufufuo huyo mwanamke atakuwa mke wa nani, maana aliolewa na ndugu wote saba?”
In the resurrection therefore, whose of them shall she be the wife? for the seven of them had taken her.
34 Yesu akawajibu, “Katika maisha haya watu huoa na kuolewa. (aiōn )
Jeshu saith to them, The sons of this world take wives, and women become (the wives) of men: (aiōn )
35 Lakini wale ambao wamehesabiwa kwamba wanastahili kupata nafasi katika ulimwengu ule na katika ufufuo wa wafu, hawaoi wala hawaolewi. (aiōn )
but they who of that world are worthy, and of the resurrection which is from among the dead, take not wives, neither do women become (the wives) of men. (aiōn )
36 Hawa hawawezi kufa tena, kwa maana wao ni kama malaika. Wao ni watoto wa Mungu, kwa sababu ni watoto wa ufufuo.
Neither again can they die, for they are as the angels; and the children are they of Aloha, because they have become the children of the resurrection.
37 Hata Mose alidhihirisha kuwa wafu wanafufuka, kwa habari ya kile kichaka kilichokuwa kikiwaka moto bila kuteketea, alipomwita Bwana, ‘Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo.’
But that the dead arise, Musha also showeth; for he commemorateth at the bush, while he saith, The Lord the God of Abraham, and the God of Ishok, and the God of Jakub.
38 Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai, kwa kuwa kwake wote ni hai.”
But he was not the God of the dead, but of the living: for they all live unto him.
39 Baadhi ya walimu wa sheria wakasema, “Mwalimu, umesema sawasawa kabisa!”
And some of the Sophree answered and said to him, Doctor, thou hast well said.
40 Baada ya hayo hakuna mtu aliyethubutu kumuuliza maswali tena.
And they dared not question him again of any thing.
41 Kisha Yesu akawaambia, “Imekuwaje basi wao husema Kristoni Mwana wa Daudi?
AND he said to them, How say the Sophree concerning the Meshicha, that he is the Son of David?
42 Daudi mwenyewe anasema katika Kitabu cha Zaburi: “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume,
And David himself saith in the book of Psalms, The Lord said unto my Lord, Sit thou at my right hand,
43 hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
until I put thine adversaries beneath thy feet.
44 Ikiwa Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ basi atakuwaje mwanawe?”
If David therefore calleth him Lord, how is he his son?
45 Wakati watu wote walikuwa wanamsikiliza, Yesu akawaambia wanafunzi wake,
And while all the people heard, he said to his disciples,
46 “Jihadharini na walimu wa sheria. Wao hupenda kutembea wakiwa wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa kwa heshima masokoni. Hupenda kukaa kwenye viti vya mbele katika masinagogi, na kukaa kwenye nafasi za heshima katika karamu.
Beware of the Sophree, who will to walk in stoles, and love the shaloma in public places, and the chief seats in the synagogues, and the chief reclining-places at evening feasts;
47 Wao hula nyumba za wajane, na ili waonekane kuwa wema, wanasali sala ndefu. Watu kama hawa watapata hukumu iliyo kuu sana.”
who devour the houses of widows, and for the occasion prolong their prayers: these shall receive the greater judgment.