< Luka 20 >
1 Siku moja, Yesu alipokuwa akifundisha watu Hekaluni na kuhubiri habari njema, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria, pamoja na wazee wa watu wakamjia.
It happened on one of those days, as he was teaching the people in the temple and preaching the Good News, that the chief priests and scribes came to him with the elders.
2 Wakamuuliza, “Tuambie, unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ni nani aliyekupa mamlaka haya?”
They asked him, "Tell us: by what authority do you do these things? Or who is giving you this authority?"
3 Akawajibu, “Nami nitawauliza swali.
He answered them, "I also will ask you one question. Tell me:
4 Je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?”
the baptism of Yukhanan, was it from heaven, or from man?"
5 Wakahojiana wao kwa wao wakisema, “Kama tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Mbona hamkumwamini?’
They reasoned with themselves, saying, "If we say, 'From heaven,' he will say, 'Why did you not believe him?'
6 Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ watu wote watatupiga mawe, kwa sababu wanaamini kwamba Yohana alikuwa nabii.”
But if we say, 'From man,' all the people will stone us, for they are persuaded that Yukhanan was a prophet."
7 Basi wakajibu, “Hatujui ulikotoka.”
They answered that they did not know where it was from.
8 Yesu akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”
Yeshua said to them, "Neither will I tell you by what authority I do these things."
9 Akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima fulani, kisha akasafiri kwa muda mrefu.
He began to tell the people this parable. "A man planted a vineyard, and rented it out to some farmers, and went on a journey for a long time.
10 Wakati wa mavuno ulipofika, akamtuma mtumishi wake kwa hao wapangaji ili wampe sehemu ya mavuno ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga, wakamfukuza mikono mitupu.
At the proper season, he sent a servant to the farmers to collect his share of the fruit of the vineyard. But the farmers beat him, and sent him away empty.
11 Akamtuma mtumishi mwingine, huyo naye wakampiga, wakamfanyia mambo ya aibu na kumfukuza.
He sent yet another servant, and they also beat him, and treated him shamefully, and sent him away empty.
12 Bado akamtuma na mwingine wa tatu, huyu pia wakamjeruhi na kumtupa nje ya shamba.
He sent yet a third, and they also wounded him, and threw him out.
13 “Basi yule mwenye shamba la mizabibu akasema, ‘Nifanye nini? Nitamtuma mwanangu mpendwa, huenda yeye watamheshimu.’
The lord of the vineyard said, 'What am I to do? I will send my beloved son. It may be that they will respect him.'
14 “Lakini wale wapangaji walipomwona, wakasemezana wao kwa wao. Wakasema, ‘Huyu ndiye mrithi. Basi na tumuue ili urithi uwe wetu.’
"But when the farmers saw him, they reasoned among themselves, saying, 'This is the heir. Let us kill him, that the inheritance may be ours.'
15 Kwa hiyo wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamuua.” “Sasa basi yule mwenye shamba la mizabibu atawafanyia nini wapangaji hawa?
They threw him out of the vineyard, and killed him. What therefore will the lord of the vineyard do to them?
16 Atakuja na kuwaua hao wapangaji, na kuwapa wapangaji wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia hayo wakasema, “Mungu apishie mbali jambo hili lisitokee!”
He will come and destroy these farmers, and will give the vineyard to others." When they heard it, they said, "May it never be."
17 Lakini Yesu akawakazia macho, akasema, “Basi ni nini maana ya yale yaliyoandikwa: “‘Jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni’?
But he looked at them, and said, "Then what is this that is written, 'The stone which the builders rejected, this one was made the cornerstone?'
18 Kila mtu aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika vipande vipande, lakini yule litakayemwangukia atasagwa kabisa.”
Everyone who falls on that stone will be broken to pieces; but on whomever it falls, it will crush him."
19 Walimu wa sheria na viongozi wa makuhani wakatafuta njia ya kumkamata mara moja, kwa sababu walifahamu kwamba amesema mfano huo kwa ajili yao. Lakini waliwaogopa watu.
The chief priests and the scribes sought to lay hands on him that very hour, but they feared the people—for they knew he had spoken this parable against them.
20 Kwa hiyo wakawa wanamchunguza na kutuma wapelelezi waliojifanya kuwa wenye haki ili wapate kumtega kwa maneno asemayo, ili wamtie katika uwezo na mamlaka ya mtawala.
They watched him, and sent out spies, who pretended to be righteous, that they might trap him in something he said, so as to deliver him up to the power and authority of the governor.
21 Hivyo wale wapelelezi wakamuuliza, “Mwalimu, tunajua unasema na kufundisha yaliyo kweli wala humpendelei mtu, bali wafundisha njia ya Mungu katika kweli.
They asked him, "Teacher, we know that you say and teach what is right, and are not partial to anyone, but truly teach the way of God.
22 Je, ni halali sisi kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
Is it lawful for us to pay taxes to Caesar, or not?"
23 Lakini Yesu akatambua hila yao, kwa hiyo akawaambia,
But he perceived their craftiness, and said to them,
24 “Nionyesheni dinari. Je, sura hii na maandishi haya yaliyoko juu yake ni vya nani?”
"Show me a denura. Whose image and inscription are on it?" They answered, "Caesar's."
25 Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Akawaambia, “Basi mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.”
He said to them, "Then give to Caesar the things that are Caesar's, and to God the things that are God's."
26 Wakashindwa kumkamata kwa yale aliyokuwa amesema hadharani. Nao wakashangazwa mno na majibu yake, wakanyamaza kimya.
They weren't able to trap him in his words before the people. And amazed at his answer, they fell silent.
27 Baadhi ya Masadukayo, wale wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu na kumuuliza,
Some of the Sadducees came to him, those who deny that there is a resurrection.
28 “Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu wa mtu akifa na kumwacha mkewe bila mtoto, basi huyo mtu inampasa amwoe huyo mjane ili amzalie ndugu yake watoto.
They asked him, "Teacher, Mushe wrote to us that if a man's brother dies having a wife, and he is childless, his brother should take the wife, and raise up children for his brother.
29 Basi palikuwepo ndugu saba. Yule wa kwanza akaoa, akafa bila kuzaa mtoto.
There were therefore seven brothers. The first took a wife, and died childless.
30 Kisha yule wa pili akamwoa huyo mjane, naye akafa bila mtoto,
The second and
31 naye wa tatu pia akamwoa. Vivyo hivyo ndugu wote saba wakawa wamemwoa huyo mwanamke, na wote wakafa pasipo yeyote kupata mtoto.
the third took her, and likewise the seven all left no children, and died.
32 Mwishowe, yule mwanamke naye akafa.
Afterward the woman also died.
33 Sasa basi, siku ya ufufuo huyo mwanamke atakuwa mke wa nani, maana aliolewa na ndugu wote saba?”
Therefore in the resurrection whose wife of them will she be? For the seven had her as a wife."
34 Yesu akawajibu, “Katika maisha haya watu huoa na kuolewa. (aiōn )
Yeshua said to them, "The people of this age marry and are given to someone to marry. (aiōn )
35 Lakini wale ambao wamehesabiwa kwamba wanastahili kupata nafasi katika ulimwengu ule na katika ufufuo wa wafu, hawaoi wala hawaolewi. (aiōn )
But those who are regarded as worthy of a place in that age and the resurrection from the dead neither marry nor are given to someone to marry. (aiōn )
36 Hawa hawawezi kufa tena, kwa maana wao ni kama malaika. Wao ni watoto wa Mungu, kwa sababu ni watoto wa ufufuo.
For they cannot die any more, for they are like the angels, and are children of God, being children of the resurrection.
37 Hata Mose alidhihirisha kuwa wafu wanafufuka, kwa habari ya kile kichaka kilichokuwa kikiwaka moto bila kuteketea, alipomwita Bwana, ‘Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo.’
But that the dead are raised, even Mushe showed at the bush, when he called the Lord 'The God of Avraham, the God of Iskhaq, and the God of Yaquv.'
38 Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai, kwa kuwa kwake wote ni hai.”
Now he is not the God of the dead, but of the living, for all are alive to him."
39 Baadhi ya walimu wa sheria wakasema, “Mwalimu, umesema sawasawa kabisa!”
Some of the scribes answered, "Teacher, you speak well."
40 Baada ya hayo hakuna mtu aliyethubutu kumuuliza maswali tena.
They did not dare to ask him any more questions.
41 Kisha Yesu akawaambia, “Imekuwaje basi wao husema Kristoni Mwana wa Daudi?
He said to them, "Why do they say that the Meshikha is Dawid's son?
42 Daudi mwenyewe anasema katika Kitabu cha Zaburi: “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume,
Dawid himself says in the scroll of Psalms, 'The Lord said to my Lord, "Sit at my right hand,
43 hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
until I make your enemies the footstool of your feet."'
44 Ikiwa Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ basi atakuwaje mwanawe?”
"Dawid therefore calls him Lord, so how is he his son?"
45 Wakati watu wote walikuwa wanamsikiliza, Yesu akawaambia wanafunzi wake,
In the hearing of all the people, he said to his disciples,
46 “Jihadharini na walimu wa sheria. Wao hupenda kutembea wakiwa wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa kwa heshima masokoni. Hupenda kukaa kwenye viti vya mbele katika masinagogi, na kukaa kwenye nafasi za heshima katika karamu.
"Beware of the scribes, who like to walk in long robes, and love greetings in the marketplaces, the best seats in the synagogues, and the best places at feasts;
47 Wao hula nyumba za wajane, na ili waonekane kuwa wema, wanasali sala ndefu. Watu kama hawa watapata hukumu iliyo kuu sana.”
who devour widows' houses, and for a pretense make long prayers: these will receive greater condemnation."