< Luka 20 >

1 Siku moja, Yesu alipokuwa akifundisha watu Hekaluni na kuhubiri habari njema, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria, pamoja na wazee wa watu wakamjia.
有一天,耶稣在殿里教导众人,告诉他们好消息。祭司长、宗教老师和长老走上前来,
2 Wakamuuliza, “Tuambie, unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ni nani aliyekupa mamlaka haya?”
他们对他说:“告诉我们,你凭着什么权力做这些事?谁给你的这权力?”
3 Akawajibu, “Nami nitawauliza swali.
耶稣回答:“我也要问你们一个问题,告诉我,
4 Je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?”
约翰的洗礼是从天上来,还是从人间来?”
5 Wakahojiana wao kwa wao wakisema, “Kama tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Mbona hamkumwamini?’
这些人开始议论:“如果我们说‘从天上来’,他就会说‘那你们为什么不信他?’
6 Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ watu wote watatupiga mawe, kwa sababu wanaamini kwamba Yohana alikuwa nabii.”
如果我们说:‘从人间来’,众人会用石头打我们,因为他们认定约翰是先知。”
7 Basi wakajibu, “Hatujui ulikotoka.”
于是他们回答耶稣:“我们不知道从哪里来。”
8 Yesu akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”
耶稣说:“那我也不告诉你们,是谁给我权力做这一切。”
9 Akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima fulani, kisha akasafiri kwa muda mrefu.
随后耶稣向众人讲了一个故事:“一个人有一个葡萄园,由于住在距离这里很远的另外一个乡村,他便将葡萄园租给了农户。
10 Wakati wa mavuno ulipofika, akamtuma mtumishi wake kwa hao wapangaji ili wampe sehemu ya mavuno ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga, wakamfukuza mikono mitupu.
到了收获的季节,园主派一个仆人到农户那里,收取葡萄园应该上交的水果。但农户却打了那个仆人,让他空手回去。
11 Akamtuma mtumishi mwingine, huyo naye wakampiga, wakamfanyia mambo ya aibu na kumfukuza.
园主又派另一个仆人去,同样受到殴打和侮辱,空手而归。
12 Bado akamtuma na mwingine wa tatu, huyu pia wakamjeruhi na kumtupa nje ya shamba.
园主又派了第三人去,农户依旧把他打伤,然后把他赶走。
13 “Basi yule mwenye shamba la mizabibu akasema, ‘Nifanye nini? Nitamtuma mwanangu mpendwa, huenda yeye watamheshimu.’
园主暗自想:‘该怎么办?我知道了,派我的爱子去,也许这一次他们会尊敬他。’
14 “Lakini wale wapangaji walipomwona, wakasemezana wao kwa wao. Wakasema, ‘Huyu ndiye mrithi. Basi na tumuue ili urithi uwe wetu.’
农户一看见园主的儿子,立刻交头接耳说:‘这人会继承产业,我们杀了他,这产业就成为我们的了。’
15 Kwa hiyo wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamuua.” “Sasa basi yule mwenye shamba la mizabibu atawafanyia nini wapangaji hawa?
于是他们把园主之子推出葡萄园外杀了。那么主人会怎样对付他们呢?
16 Atakuja na kuwaua hao wapangaji, na kuwapa wapangaji wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia hayo wakasema, “Mungu apishie mbali jambo hili lisitokee!”
他会过来杀掉这些农户,把葡萄园租给别人。” 众人听了这个故事,就说:“希望这样的事情不要发生!”
17 Lakini Yesu akawakazia macho, akasema, “Basi ni nini maana ya yale yaliyoandikwa: “‘Jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni’?
但耶稣看着他们说:“那么经文中说:‘建筑工人弃用的石头,现在成了主要基石。’这是什么意思呢?
18 Kila mtu aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika vipande vipande, lakini yule litakayemwangukia atasagwa kabisa.”
任何人在那石头上摔倒,都会粉身碎骨,那石头落在任何人身上,都会砸着他们。”
19 Walimu wa sheria na viongozi wa makuhani wakatafuta njia ya kumkamata mara moja, kwa sababu walifahamu kwamba amesema mfano huo kwa ajili yao. Lakini waliwaogopa watu.
宗教老师和祭司长知道这比喻针对他们,当时就想把耶稣抓起来,可是又害怕民众的反应。
20 Kwa hiyo wakawa wanamchunguza na kutuma wapelelezi waliojifanya kuwa wenye haki ili wapate kumtega kwa maneno asemayo, ili wamtie katika uwezo na mamlaka ya mtawala.
他们找了个机会,派几名奸细假装虔诚信徒去找耶稣,想找到耶稣说话的把柄,然后把他交给总督裁决。
21 Hivyo wale wapelelezi wakamuuliza, “Mwalimu, tunajua unasema na kufundisha yaliyo kweli wala humpendelei mtu, bali wafundisha njia ya Mungu katika kweli.
奸细问耶稣:“老师,我们知道,你所说所教都是正道,你绝不会因其他人的意见而动摇,你真的是在将上帝之道传授众人。
22 Je, ni halali sisi kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
那么,我们是否应该向凯撒纳税?”
23 Lakini Yesu akatambua hila yao, kwa hiyo akawaambia,
耶稣看透了他们的诡计,于是说:
24 “Nionyesheni dinari. Je, sura hii na maandishi haya yaliyoko juu yake ni vya nani?”
“给我一个银币,上面是谁的形象?”他们回答:“凯撒。”
25 Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Akawaambia, “Basi mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.”
耶稣说:“那么,是凯撒的就应属于凯撒,是上帝的就应当属于上帝。”
26 Wakashindwa kumkamata kwa yale aliyokuwa amesema hadharani. Nao wakashangazwa mno na majibu yake, wakanyamaza kimya.
耶稣向众人所说的话,让他们无法抓住把柄,这番话也让他们很震惊,于是就沉默了。
27 Baadhi ya Masadukayo, wale wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu na kumuuliza,
几个撒都该人来到耶稣这里,他们从来都不相信人死会复活。他们问到,
28 “Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu wa mtu akifa na kumwacha mkewe bila mtoto, basi huyo mtu inampasa amwoe huyo mjane ili amzalie ndugu yake watoto.
“老师,摩西在律法中写道:‘如果一个男人娶了妻子,但未留下一儿半女就死了,他弟弟就应当娶嫂子,为哥哥留后。’
29 Basi palikuwepo ndugu saba. Yule wa kwanza akaoa, akafa bila kuzaa mtoto.
从前有兄弟七人,老大娶了妻子后死了,没有留下后代,
30 Kisha yule wa pili akamwoa huyo mjane, naye akafa bila mtoto,
随后老二,
31 naye wa tatu pia akamwoa. Vivyo hivyo ndugu wote saba wakawa wamemwoa huyo mwanamke, na wote wakafa pasipo yeyote kupata mtoto.
老三一直到老七都娶了她,但都没有留下孩子就死了。
32 Mwishowe, yule mwanamke naye akafa.
最终那女人也死了。
33 Sasa basi, siku ya ufufuo huyo mwanamke atakuwa mke wa nani, maana aliolewa na ndugu wote saba?”
那么,这女人复活的时候,要做哪个兄弟的妻子呢?因为七个人都娶过她。”
34 Yesu akawajibu, “Katika maisha haya watu huoa na kuolewa. (aiōn g165)
耶稣说:“只有在这里的人才嫁娶。 (aiōn g165)
35 Lakini wale ambao wamehesabiwa kwamba wanastahili kupata nafasi katika ulimwengu ule na katika ufufuo wa wafu, hawaoi wala hawaolewi. (aiōn g165)
但对于那些有资格进入新世界的人,那些死而复生之人,不娶也不嫁。 (aiōn g165)
36 Hawa hawawezi kufa tena, kwa maana wao ni kama malaika. Wao ni watoto wa Mungu, kwa sababu ni watoto wa ufufuo.
他们和天使一样不会死亡,因为他们是复活之子,也就是上帝的之子。
37 Hata Mose alidhihirisha kuwa wafu wanafufuka, kwa habari ya kile kichaka kilichokuwa kikiwaka moto bila kuteketea, alipomwita Bwana, ‘Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo.’
至于死人复活的问题,摩西在关于荆棘的经文中写过,他口中的主是:亚伯拉罕的上帝、以撒的上帝、雅各的上帝。
38 Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai, kwa kuwa kwake wote ni hai.”
他不是死人的上帝,而是活人的上帝,因为在他那里的人都活着。”
39 Baadhi ya walimu wa sheria wakasema, “Mwalimu, umesema sawasawa kabisa!”
几个宗教老师说:“老师,你说得好。”
40 Baada ya hayo hakuna mtu aliyethubutu kumuuliza maswali tena.
然后他们就不敢再提出任何问题了。
41 Kisha Yesu akawaambia, “Imekuwaje basi wao husema Kristoni Mwana wa Daudi?
耶稣问他们:“为什么说基督是大卫的子孙?
42 Daudi mwenyewe anasema katika Kitabu cha Zaburi: “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume,
因为大卫自己在《诗篇》中说:主对我的主说‘坐在我的右边,
43 hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
我会让你的敌人变成你的脚凳。’
44 Ikiwa Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ basi atakuwaje mwanawe?”
大卫称他为‘主’,所以他怎会是大卫的子孙呢?”
45 Wakati watu wote walikuwa wanamsikiliza, Yesu akawaambia wanafunzi wake,
众人聚精会神地听着,耶稣对门徒说:
46 “Jihadharini na walimu wa sheria. Wao hupenda kutembea wakiwa wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa kwa heshima masokoni. Hupenda kukaa kwenye viti vya mbele katika masinagogi, na kukaa kwenye nafasi za heshima katika karamu.
“你们要小心宗教老师,他们喜欢穿长袍走来走去,喜欢人们在集市中向他们恭敬问安,喜欢坐会堂里的高位、宴席上的首座。
47 Wao hula nyumba za wajane, na ili waonekane kuwa wema, wanasali sala ndefu. Watu kama hawa watapata hukumu iliyo kuu sana.”
他们骗光寡妇的财产,通过冗长的祈祷伪装自己。这些人在审判中必受到严重的责罚。”

< Luka 20 >