< Luka 2 >

1 Siku zile Kaisari Augusto alitoa amri kwamba watu wote waandikishwe katika ulimwengu wa Kirumi.
apara ncha tasmin kAle rAjyasya sarvveShAM lokAnAM nAmAni lekhayitum agastakaisara Aj nApayAmAsa|
2 (Orodha hii ndiyo ya kwanza iliyofanyika wakati Krenio alikuwa mtawala wa Shamu).
tadanusAreNa kurINiyanAmani suriyAdeshasya shAsake sati nAmalekhanaM prArebhe|
3 Kila mtu alikwenda kuandikishwa katika mji wake alikozaliwa.
ato heto rnAma lekhituM sarvve janAH svIyaM svIyaM nagaraM jagmuH|
4 Hivyo Yosefu akapanda kutoka mji wa Nazareti ulioko Galilaya kwenda Uyahudi, mpaka Bethlehemu, mji wa Daudi, kwa sababu yeye alikuwa wa ukoo na wa nyumba ya Daudi.
tadAnIM yUShaph nAma lekhituM vAgdattayA svabhAryyayA garbbhavatyA mariyamA saha svayaM dAyUdaH sajAtivaMsha iti kAraNAd gAlIlpradeshasya nAsaratnagarAd
5 Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na Maria, ambaye alikuwa amemposa naye alikuwa mjamzito.
yihUdApradeshasya baitlehamAkhyaM dAyUdnagaraM jagAma|
6 Wakiwa Bethlehemu, wakati wa Maria wa kujifungua ukawa umetimia,
anyachcha tatra sthAne tayostiShThatoH sato rmariyamaH prasUtikAla upasthite
7 naye akamzaa mwanawe, kifungua mimba. Akamfunika nguo za kitoto na kumlaza katika hori ya kulia ngʼombe, kwa sababu hapakuwa na nafasi katika nyumba ya wageni.
sA taM prathamasutaM prAsoShTa kintu tasmin vAsagR^ihe sthAnAbhAvAd bAlakaM vastreNa veShTayitvA goshAlAyAM sthApayAmAsa|
8 Katika eneo lile walikuwako wachungaji waliokuwa wakikaa mashambani, wakilinda makundi yao ya kondoo usiku.
anantaraM ye kiyanto meShapAlakAH svameShavrajarakShAyai tatpradeshe sthitvA rajanyAM prAntare prahariNaH karmma kurvvanti,
9 Ghafula tazama, malaika wa Bwana akawatokea, nao utukufu wa Bwana ukawangʼaria kotekote, wakaingiwa na hofu.
teShAM samIpaM parameshvarasya dUta Agatyopatasthau; tadA chatuShpArshve parameshvarasya tejasaH prakAshitatvAt te. atishasha Nkire|
10 Lakini malaika akawaambia: “Msiogope. Kwa maana tazama nawaletea habari njema za furaha itakayokuwa kwa watu wote.
tadA sa dUta uvAcha mA bhaiShTa pashyatAdya dAyUdaH pure yuShmannimittaM trAtA prabhuH khrIShTo. ajaniShTa,
11 Leo katika mji wa Daudi kwa ajili yenu amezaliwa Mwokozi, ndiye Kristo Bwana.
sarvveShAM lokAnAM mahAnandajanakam imaM ma NgalavR^ittAntaM yuShmAn j nApayAmi|
12 Hii ndiyo itakayokuwa ishara kwenu: Mtamkuta mtoto mchanga amefunikwa nguo za kitoto na kulazwa katika hori ya kulia ngʼombe.”
yUyaM (tatsthAnaM gatvA) vastraveShTitaM taM bAlakaM goshAlAyAM shayanaM drakShyatha yuShmAn pratIdaM chihnaM bhaviShyati|
13 Ghafula pakawa na jeshi kubwa la mbinguni pamoja na huyo malaika wakimsifu Mungu wakisema,
dUta imAM kathAM kathitavati tatrAkasmAt svargIyAH pR^itanA Agatya kathAm imAM kathayitveshvarasya guNAnanvavAdiShuH, yathA,
14 “Atukuzwe Mungu juu mbinguni, na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.”
sarvvordvvasthairIshvarasya mahimA samprakAshyatAM| shAntirbhUyAt pR^ithivyAstu santoShashcha narAn prati||
15 Hao malaika walipokwisha kuondoka na kwenda zao mbinguni, wale wachungaji wakasemezana wao kwa wao, “Twendeni Bethlehemu tukaone mambo haya ya ajabu yaliyotukia, ambayo Bwana ametuambia habari zake.”
tataH paraM teShAM sannidhe rdUtagaNe svargaM gate meShapAlakAH parasparam avechan AgachChata prabhuH parameshvaro yAM ghaTanAM j nApitavAn tasyA yAtharyaM j nAtuM vayamadhunA baitlehampuraM yAmaH|
16 Hivyo wakaenda haraka Bethlehemu, wakawakuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga akiwa amelala katika hori la kulia ngʼombe.
pashchAt te tUrNaM vrajitvA mariyamaM yUShaphaM goshAlAyAM shayanaM bAlaka ncha dadR^ishuH|
17 Walipomwona yule mtoto, wakawaeleza yale waliyokuwa wameambiwa kuhusu huyo mtoto.
itthaM dR^iShTvA bAlakasyArthe proktAM sarvvakathAM te prAchArayA nchakruH|
18 Nao wote waliosikia habari hizi wakastaajabia yale waliyoambiwa na wale wachungaji wa kondoo.
tato ye lokA meSharakShakANAM vadanebhyastAM vArttAM shushruvuste mahAshcharyyaM menire|
19 Lakini Maria akayaweka mambo haya yote moyoni mwake na kuyatafakari.
kintu mariyam etatsarvvaghaTanAnAM tAtparyyaM vivichya manasi sthApayAmAsa|
20 Wale wachungaji wakarudi, huku wakimtukuza Mungu na kumsifu kwa ajili ya mambo yote waliyokuwa wameambiwa na kuyaona.
tatpashchAd dUtavij naptAnurUpaM shrutvA dR^iShTvA cha meShapAlakA Ishvarasya guNAnuvAdaM dhanyavAda ncha kurvvANAH parAvR^itya yayuH|
21 Hata zilipotimia siku nane, ulikuwa ndio wakati wa kumtahiri mtoto, akaitwa Yesu, jina alilokuwa amepewa na malaika kabla hajatungwa mimba.
atha bAlakasya tvakChedanakAle. aShTamadivase samupasthite tasya garbbhasthiteH purvvaM svargIyadUto yathAj nApayat tadanurUpaM te tannAmadheyaM yIshuriti chakrire|
22 Ulipotimia wakati wa utakaso wake Maria kwa mujibu wa Sheria ya Mose, basi Yosefu na Maria walimpeleka mtoto Yerusalemu, ili kumweka wakfu kwa Bwana
tataH paraM mUsAlikhitavyavasthAyA anusAreNa mariyamaH shuchitvakAla upasthite,
23 (kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana, kwamba, “Kila mtoto wa kiume kifungua mimba atawekwa wakfu kwa Bwana”),
"prathamajaH sarvvaH puruShasantAnaH parameshvare samarpyatAM," iti parameshvarasya vyavasthayA
24 na pia kutoa dhabihu kulingana na yale yaliyonenwa katika Sheria ya Bwana: “Hua wawili au makinda mawili ya njiwa.”
yIshuM parameshvare samarpayitum shAstrIyavidhyuktaM kapotadvayaM pArAvatashAvakadvayaM vA baliM dAtuM te taM gR^ihItvA yirUshAlamam AyayuH|
25 Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli, na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
yirUshAlampuranivAsI shimiyonnAmA dhArmmika eka AsIt sa isrAyelaH sAntvanAmapekShya tasthau ki ncha pavitra AtmA tasminnAvirbhUtaH|
26 Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana.
aparaM prabhuNA parameshvareNAbhiShikte trAtari tvayA na dR^iShTe tvaM na mariShyasIti vAkyaM pavitreNa AtmanA tasma prAkathyata|
27 Simeoni, akiwa ameongozwa na Roho Mtakatifu, alikwenda Hekaluni. Wazazi walipomleta mtoto Yesu ili kumfanyia kama ilivyokuwa desturi ya Sheria,
apara ncha yadA yIshoH pitA mAtA cha tadarthaM vyavasthAnurUpaM karmma karttuM taM mandiram AninyatustadA
28 ndipo Simeoni akampokea mtoto mikononi mwake na kumsifu Mungu, akisema:
shimiyon Atmana AkarShaNena mandiramAgatya taM kroDe nidhAya Ishvarasya dhanyavAdaM kR^itvA kathayAmAsa, yathA,
29 “Bwana Mwenyezi, kama ulivyoahidi, sasa wamruhusu mtumishi wako aende zake kwa amani.
he prabho tava dAsoyaM nijavAkyAnusArataH| idAnIntu sakalyANo bhavatA saMvisR^ijyatAm|
30 Kwa maana macho yangu yameuona wokovu wako,
yataH sakaladeshasya dIptaye dIptirUpakaM|
31 ulioweka tayari machoni pa watu wote,
isrAyelIyalokasya mahAgauravarUpakaM|
32 nuru kwa ajili ya ufunuo kwa watu wa Mataifa na kwa ajili ya utukufu kwa watu wako Israeli.”
yaM trAyakaM janAnAntu sammukhe tvamajIjanaH| saeva vidyate. asmAkaM dhravaM nayananagochare||
33 Naye Yosefu na mama yake mtoto wakastaajabu kwa yale yaliyokuwa yamesemwa kumhusu huyo mtoto.
tadAnIM tenoktA etAH sakalAH kathAH shrutvA tasya mAtA yUShaph cha vismayaM menAte|
34 Kisha Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu amewekwa kwa makusudi ya kuanguka na kuinuka kwa wengi katika Israeli. Atakuwa ishara ambayo watu watanena dhidi yake,
tataH paraM shimiyon tebhya AshiShaM dattvA tanmAtaraM mariyamam uvAcha, pashya isrAyelo vaMshamadhye bahUnAM pAtanAyotthApanAya cha tathA virodhapAtraM bhavituM, bahUnAM guptamanogatAnAM prakaTIkaraNAya bAlakoyaM niyuktosti|
35 ili mawazo ya mioyo mingi yadhihirike. Nao upanga utauchoma moyo wako.”
tasmAt tavApi prANAH shUlena vyatsyante|
36 Tena alikuwako Hekaluni nabii mmoja mwanamke, jina lake Ana binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa mzee sana; naye alikuwa ameolewa na kuishi na mume kwa miaka saba tu, kisha mumewe akafa.
apara ncha Asherasya vaMshIyaphinUyelo duhitA hannAkhyA atijaratI bhaviShyadvAdinyekA yA vivAhAt paraM sapta vatsarAn patyA saha nyavasat tato vidhavA bhUtvA chaturashItivarShavayaHparyyanataM
37 Hivyo alikuwa mjane na umri wake ulikuwa miaka themanini na minne. Yeye hakuondoka humo Hekaluni usiku wala mchana, bali alikuwa akimwabudu Mungu, akifunga na kuomba.
mandire sthitvA prArthanopavAsairdivAnisham Ishvaram asevata sApi strI tasmin samaye mandiramAgatya
38 Wakati huo huo, Ana alikuja akaanza kusifu, akimshukuru Mungu na kusema habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wakitarajia ukombozi wa Yerusalemu.
parameshvarasya dhanyavAdaM chakAra, yirUshAlampuravAsino yAvanto lokA muktimapekShya sthitAstAn yIshorvR^ittAntaM j nApayAmAsa|
39 Yosefu na Maria walipokuwa wamekamilisha mambo yote yaliyotakiwa na Sheria ya Bwana, walirudi mjini kwao Nazareti huko Galilaya.
itthaM parameshvarasya vyavasthAnusAreNa sarvveShu karmmasu kR^iteShu tau punashcha gAlIlo nAsaratnAmakaM nijanagaraM pratasthAte|
40 Naye yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu, akiwa amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
tatpashchAd bAlakaH sharIreNa vR^iddhimetya j nAnena paripUrNa AtmanA shaktimAMshcha bhavitumArebhe tathA tasmin IshvarAnugraho babhUva|
41 Kila mwaka Yosefu na Maria mama yake Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kwa ajili ya Sikukuu ya Pasaka.
tasya pitA mAtA cha prativarShaM nistArotsavasamaye yirUshAlamam agachChatAm|
42 Yesu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walipanda kwenda kwenye Sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
apara ncha yIshau dvAdashavarShavayaske sati tau parvvasamayasya rItyanusAreNa yirUshAlamaM gatvA
43 Baada ya Sikukuu kumalizika, wakati Yosefu na Maria mama yake walipokuwa wakirudi nyumbani, Yesu alibaki Yerusalemu lakini hawakutambua.
pArvvaNaM sampAdya punarapi vyAghuyya yAtaH kintu yIshurbAlako yirUshAlami tiShThati| yUShaph tanmAtA cha tad aviditvA
44 Wao wakidhani kuwa yuko miongoni mwa wasafiri, walienda mwendo wa kutwa nzima. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa zao na marafiki.
sa sa NgibhiH saha vidyata etachcha budvvA dinaikagamyamArgaM jagmatuH| kintu sheShe j nAtibandhUnAM samIpe mR^igayitvA taduddeshamaprApya
45 Walipomkosa walirudi Yerusalemu ili kumtafuta.
tau punarapi yirUshAlamam parAvR^ityAgatya taM mR^igayA nchakratuH|
46 Baada ya siku tatu wakamkuta ndani ya Hekalu, akiwa ameketi katikati ya walimu wa sheria, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
atha dinatrayAt paraM paNDitAnAM madhye teShAM kathAH shR^iNvan tattvaM pR^ichChaMshcha mandire samupaviShTaH sa tAbhyAM dR^iShTaH|
47 Wote waliomsikia walistaajabishwa na uwezo wake mkubwa wa kuelewa, na majibu aliyoyatoa.
tadA tasya buddhyA pratyuttaraishcha sarvve shrotAro vismayamApadyante|
48 Yosefu na Maria mama yake walipomwona walishangaa. Mama yake akamuuliza, “Mwanangu, mbona umetufanyia hivi? Tazama, mimi na baba yako tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa kila mahali.”
tAdR^ishaM dR^iShTvA tasya janako jananI cha chamachchakratuH ki ncha tasya mAtA tamavadat, he putra, kathamAvAM pratItthaM samAcharastvam? pashya tava pitAha ncha shokAkulau santau tvAmanvichChAvaH sma|
49 Yesu akawaambia, “Kwa nini kunitafuta? Hamkujua kwamba imenipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
tataH sovadat kuto mAm anvaichChataM? piturgR^ihe mayA sthAtavyam etat kiM yuvAbhyAM na j nAyate?
50 Lakini wao hawakuelewa maana ya lile alilowaambia.
kintu tau tasyaitadvAkyasya tAtparyyaM boddhuM nAshaknutAM|
51 Ndipo akashuka pamoja nao hadi Nazareti, naye alikuwa mtiifu kwao. Lakini mama yake akayaweka moyoni mwake mambo haya yote.
tataH paraM sa tAbhyAM saha nAsarataM gatvA tayorvashIbhUtastasthau kintu sarvvA etAH kathAstasya mAtA manasi sthApayAmAsa|
52 Naye Yesu akakua katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.
atha yIsho rbuddhiH sharIra ncha tathA tasmin Ishvarasya mAnavAnA nchAnugraho varddhitum Arebhe|

< Luka 2 >