< Luka 2 >
1 Siku zile Kaisari Augusto alitoa amri kwamba watu wote waandikishwe katika ulimwengu wa Kirumi.
A w tych dniach wyszedł dekret cesarza Augusta, aby spisano cały świat.
2 (Orodha hii ndiyo ya kwanza iliyofanyika wakati Krenio alikuwa mtawala wa Shamu).
A ten pierwszy spis odbył się, gdy Kwiryniusz był namiestnikiem Syrii.
3 Kila mtu alikwenda kuandikishwa katika mji wake alikozaliwa.
Szli więc wszyscy, aby dać się spisać, każdy do swego miasta.
4 Hivyo Yosefu akapanda kutoka mji wa Nazareti ulioko Galilaya kwenda Uyahudi, mpaka Bethlehemu, mji wa Daudi, kwa sababu yeye alikuwa wa ukoo na wa nyumba ya Daudi.
Poszedł też Józef z Galilei, z miasta Nazaret, do Judei, do miasta Dawida, zwanego Betlejem, ponieważ pochodził z domu i z rodu Dawida;
5 Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na Maria, ambaye alikuwa amemposa naye alikuwa mjamzito.
Aby dać się spisać z Marią, poślubioną sobie małżonką, która była brzemienna.
6 Wakiwa Bethlehemu, wakati wa Maria wa kujifungua ukawa umetimia,
A gdy tam byli, nadszedł czas porodu.
7 naye akamzaa mwanawe, kifungua mimba. Akamfunika nguo za kitoto na kumlaza katika hori ya kulia ngʼombe, kwa sababu hapakuwa na nafasi katika nyumba ya wageni.
I urodziła swego pierworodnego syna, owinęła go w pieluszki i położyła w żłobie, gdyż nie było dla nich miejsca w gospodzie.
8 Katika eneo lile walikuwako wachungaji waliokuwa wakikaa mashambani, wakilinda makundi yao ya kondoo usiku.
A byli w tej okolicy pasterze przebywający w polu i trzymający straż nocną nad swoim stadem.
9 Ghafula tazama, malaika wa Bwana akawatokea, nao utukufu wa Bwana ukawangʼaria kotekote, wakaingiwa na hofu.
I oto stanął przy nich anioł Pana, a chwała Pana zewsząd ich oświeciła. I ogarnął ich wielki strach.
10 Lakini malaika akawaambia: “Msiogope. Kwa maana tazama nawaletea habari njema za furaha itakayokuwa kwa watu wote.
I powiedział do nich anioł: Nie bójcie się, bo oto zwiastuję wam wielką radość, która będzie [udziałem] całego ludu.
11 Leo katika mji wa Daudi kwa ajili yenu amezaliwa Mwokozi, ndiye Kristo Bwana.
Dziś bowiem w mieście Dawida narodził się wam Zbawiciel, którym jest Chrystus Pan.
12 Hii ndiyo itakayokuwa ishara kwenu: Mtamkuta mtoto mchanga amefunikwa nguo za kitoto na kulazwa katika hori ya kulia ngʼombe.”
A to [będzie] dla was znakiem: Znajdziecie niemowlę owinięte w pieluszki i leżące w żłobie.
13 Ghafula pakawa na jeshi kubwa la mbinguni pamoja na huyo malaika wakimsifu Mungu wakisema,
I zaraz z aniołem przybyło mnóstwo wojsk niebieskich chwalących Boga i mówiących:
14 “Atukuzwe Mungu juu mbinguni, na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.”
Chwała na wysokościach Bogu, a na ziemi pokój, wobec ludzi dobra wola.
15 Hao malaika walipokwisha kuondoka na kwenda zao mbinguni, wale wachungaji wakasemezana wao kwa wao, “Twendeni Bethlehemu tukaone mambo haya ya ajabu yaliyotukia, ambayo Bwana ametuambia habari zake.”
A gdy aniołowie odeszli od nich do nieba, pasterze mówili między sobą: Chodźmy aż do Betlejem i zobaczmy to, co się wydarzyło, a co Pan nam oznajmił.
16 Hivyo wakaenda haraka Bethlehemu, wakawakuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga akiwa amelala katika hori la kulia ngʼombe.
Spiesząc się więc, przyszli i znaleźli Marię, Józefa i niemowlę leżące w żłobie.
17 Walipomwona yule mtoto, wakawaeleza yale waliyokuwa wameambiwa kuhusu huyo mtoto.
A ujrzawszy, rozgłosili to, co zostało im powiedziane o tym dziecku.
18 Nao wote waliosikia habari hizi wakastaajabia yale waliyoambiwa na wale wachungaji wa kondoo.
A wszyscy, którzy słyszeli, dziwili się temu, co pasterze im mówili.
19 Lakini Maria akayaweka mambo haya yote moyoni mwake na kuyatafakari.
Lecz Maria zachowywała wszystkie te słowa, rozważając je w swoim sercu.
20 Wale wachungaji wakarudi, huku wakimtukuza Mungu na kumsifu kwa ajili ya mambo yote waliyokuwa wameambiwa na kuyaona.
I wrócili pasterze, wielbiąc i chwaląc Boga za wszystko, co słyszeli i widzieli, tak jak im zostało powiedziane.
21 Hata zilipotimia siku nane, ulikuwa ndio wakati wa kumtahiri mtoto, akaitwa Yesu, jina alilokuwa amepewa na malaika kabla hajatungwa mimba.
A gdy minęło osiem dni i [należało] obrzezać dziecko, nadano mu imię Jezus, którym nazwał je anioł, zanim się poczęło w łonie.
22 Ulipotimia wakati wa utakaso wake Maria kwa mujibu wa Sheria ya Mose, basi Yosefu na Maria walimpeleka mtoto Yerusalemu, ili kumweka wakfu kwa Bwana
Gdy też według Prawa Mojżesza minęły dni jej oczyszczenia, przynieśli go do Jerozolimy, aby stawić go przed Panem;
23 (kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana, kwamba, “Kila mtoto wa kiume kifungua mimba atawekwa wakfu kwa Bwana”),
(Tak jak jest napisane w Prawie Pana: Każdy mężczyzna otwierający łono będzie nazywany świętym Panu);
24 na pia kutoa dhabihu kulingana na yale yaliyonenwa katika Sheria ya Bwana: “Hua wawili au makinda mawili ya njiwa.”
I żeby złożyć ofiarę według [tego], co zostało powiedziane w Prawie Pana, parę synogarlic albo dwa gołąbki.
25 Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli, na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
A był w Jerozolimie człowiek imieniem Symeon. Ten człowiek był sprawiedliwy i bogobojny, oczekujący pociechy Izraela, a Duch Święty był nad nim.
26 Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana.
I objawił mu Bóg przez Ducha Świętego, że nie ujrzy śmierci, dopóki nie zobaczy Chrystusa Pańskiego.
27 Simeoni, akiwa ameongozwa na Roho Mtakatifu, alikwenda Hekaluni. Wazazi walipomleta mtoto Yesu ili kumfanyia kama ilivyokuwa desturi ya Sheria,
Przyszedł on [prowadzony] przez Ducha [Świętego] do świątyni. A gdy rodzice wnosili dziecko – Jezusa, aby postąpić z nim według zwyczaju prawa;
28 ndipo Simeoni akampokea mtoto mikononi mwake na kumsifu Mungu, akisema:
Wtedy on, wziąwszy go na ręce, chwalił Boga i mówił:
29 “Bwana Mwenyezi, kama ulivyoahidi, sasa wamruhusu mtumishi wako aende zake kwa amani.
Teraz pozwalasz odejść twemu słudze, Panie, w pokoju, według twego słowa;
30 Kwa maana macho yangu yameuona wokovu wako,
Gdyż moje oczy ujrzały twoje zbawienie;
31 ulioweka tayari machoni pa watu wote,
Które przygotowałeś wobec wszystkich ludzi;
32 nuru kwa ajili ya ufunuo kwa watu wa Mataifa na kwa ajili ya utukufu kwa watu wako Israeli.”
Światłość na oświecenie pogan i chwałę twego ludu, Izraela.
33 Naye Yosefu na mama yake mtoto wakastaajabu kwa yale yaliyokuwa yamesemwa kumhusu huyo mtoto.
A Józef i jego matka dziwili się temu, co o nim mówiono.
34 Kisha Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu amewekwa kwa makusudi ya kuanguka na kuinuka kwa wengi katika Israeli. Atakuwa ishara ambayo watu watanena dhidi yake,
I błogosławił im Symeon, i powiedział do Marii, jego matki: Oto ten położony jest na upadek i na powstanie wielu w Izraelu, i na znak, przeciwko któremu będą mówić;
35 ili mawazo ya mioyo mingi yadhihirike. Nao upanga utauchoma moyo wako.”
(I twoją duszę miecz przeniknie), aby myśli wielu serc zostały objawione.
36 Tena alikuwako Hekaluni nabii mmoja mwanamke, jina lake Ana binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa mzee sana; naye alikuwa ameolewa na kuishi na mume kwa miaka saba tu, kisha mumewe akafa.
A była [tam] prorokini Anna, córka Fanuela, z pokolenia Asera, która była w bardzo podeszłym wieku, a żyła siedem lat z mężem od swego dziewictwa.
37 Hivyo alikuwa mjane na umri wake ulikuwa miaka themanini na minne. Yeye hakuondoka humo Hekaluni usiku wala mchana, bali alikuwa akimwabudu Mungu, akifunga na kuomba.
A [była] wdową [mającą] około osiemdziesięciu czterech lat, która nie opuszczała świątyni, służąc [Bogu] w postach i modlitwach dniem i nocą.
38 Wakati huo huo, Ana alikuja akaanza kusifu, akimshukuru Mungu na kusema habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wakitarajia ukombozi wa Yerusalemu.
Ona też, przyszedłszy w tej właśnie chwili, dziękowała Panu i mówiła o nim wszystkim, którzy oczekiwali odkupienia w Jerozolimie.
39 Yosefu na Maria walipokuwa wamekamilisha mambo yote yaliyotakiwa na Sheria ya Bwana, walirudi mjini kwao Nazareti huko Galilaya.
A gdy wykonali wszystko według prawa Pana, wrócili do Galilei, do swego miasta, Nazaretu.
40 Naye yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu, akiwa amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
Dziecko zaś rosło i umacniało się w duchu, będąc pełne mądrości, a łaska Boga była nad nim.
41 Kila mwaka Yosefu na Maria mama yake Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kwa ajili ya Sikukuu ya Pasaka.
A jego rodzice chodzili co roku do Jerozolimy na święto Paschy.
42 Yesu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walipanda kwenda kwenye Sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
I gdy miał dwanaście lat, poszli do Jerozolimy, zgodnie ze zwyczajem tego święta.
43 Baada ya Sikukuu kumalizika, wakati Yosefu na Maria mama yake walipokuwa wakirudi nyumbani, Yesu alibaki Yerusalemu lakini hawakutambua.
A gdy minęły te dni i już wracali, dziecię Jezus zostało w Jerozolimie, ale Józef i jego matka [o tym] nie wiedzieli.
44 Wao wakidhani kuwa yuko miongoni mwa wasafiri, walienda mwendo wa kutwa nzima. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa zao na marafiki.
Lecz sądząc, że jest w towarzystwie podróżnych, przeszli dzień drogi i szukali go wśród krewnych i znajomych.
45 Walipomkosa walirudi Yerusalemu ili kumtafuta.
A gdy go nie znaleźli, wrócili do Jerozolimy, szukając go.
46 Baada ya siku tatu wakamkuta ndani ya Hekalu, akiwa ameketi katikati ya walimu wa sheria, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
A po trzech dniach znaleźli go siedzącego w świątyni wśród nauczycieli, słuchającego i pytającego ich.
47 Wote waliomsikia walistaajabishwa na uwezo wake mkubwa wa kuelewa, na majibu aliyoyatoa.
I wszyscy, którzy go słuchali, zdumiewali się jego rozumem i odpowiedziami.
48 Yosefu na Maria mama yake walipomwona walishangaa. Mama yake akamuuliza, “Mwanangu, mbona umetufanyia hivi? Tazama, mimi na baba yako tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa kila mahali.”
A [rodzice], ujrzawszy go, zdziwili się. I powiedziała do niego jego matka: Synu, dlaczego nam to zrobiłeś? Oto twój ojciec i ja z bólem [serca] szukaliśmy ciebie.
49 Yesu akawaambia, “Kwa nini kunitafuta? Hamkujua kwamba imenipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
I powiedział do nich: Czemu mnie szukaliście? Czy nie wiedzieliście, że muszę być w tym, co należy do mego Ojca?
50 Lakini wao hawakuelewa maana ya lile alilowaambia.
Lecz oni nie zrozumieli tych słów, które im mówił.
51 Ndipo akashuka pamoja nao hadi Nazareti, naye alikuwa mtiifu kwao. Lakini mama yake akayaweka moyoni mwake mambo haya yote.
Wtedy poszedł z nimi i wrócił do Nazaretu, i był im posłuszny. A jego matka zachowywała wszystkie te słowa w swoim sercu.
52 Naye Yesu akakua katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.
A Jezusowi przybywało mądrości i wzrostu oraz łaski u Boga i u ludzi.