< Luka 2 >
1 Siku zile Kaisari Augusto alitoa amri kwamba watu wote waandikishwe katika ulimwengu wa Kirumi.
Tymczasem August, rzymski cezar, wydał dekret o powszechnym spisie ludności w swoim państwie.
2 (Orodha hii ndiyo ya kwanza iliyofanyika wakati Krenio alikuwa mtawala wa Shamu).
Był to pierwszy taki spis od chwili, gdy Kwiryniusz został gubernatorem Syrii.
3 Kila mtu alikwenda kuandikishwa katika mji wake alikozaliwa.
Wszyscy udawali się więc do swoich rodzinnych miejscowości, aby dać się tam zapisać.
4 Hivyo Yosefu akapanda kutoka mji wa Nazareti ulioko Galilaya kwenda Uyahudi, mpaka Bethlehemu, mji wa Daudi, kwa sababu yeye alikuwa wa ukoo na wa nyumba ya Daudi.
Józef musiał wyruszyć z Nazaretu w Galilei do Betlejem w Judei, rodzinnego miasta króla Dawida. Pochodził bowiem z jego rodu.
5 Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na Maria, ambaye alikuwa amemposa naye alikuwa mjamzito.
Wybrał się więc w drogę wraz z Marią, swoją narzeczoną, która była już w zaawansowanej ciąży.
6 Wakiwa Bethlehemu, wakati wa Maria wa kujifungua ukawa umetimia,
Gdy tam dotarli, nadszedł czas porodu
7 naye akamzaa mwanawe, kifungua mimba. Akamfunika nguo za kitoto na kumlaza katika hori ya kulia ngʼombe, kwa sababu hapakuwa na nafasi katika nyumba ya wageni.
i Maria urodziła swojego pierwszego Syna. Owinęła Go w pieluszki i położyła w stajennym żłobie, gdyż nie było już dla nich miejsca w tamtejszym zajeździe.
8 Katika eneo lile walikuwako wachungaji waliokuwa wakikaa mashambani, wakilinda makundi yao ya kondoo usiku.
Tej właśnie nocy, na pobliskich łąkach pasterze pilnowali owiec.
9 Ghafula tazama, malaika wa Bwana akawatokea, nao utukufu wa Bwana ukawangʼaria kotekote, wakaingiwa na hofu.
Nagle stanął pośród nich anioł, a wokół zajaśniała chwała Pana. Bardzo się przestraszyli,
10 Lakini malaika akawaambia: “Msiogope. Kwa maana tazama nawaletea habari njema za furaha itakayokuwa kwa watu wote.
lecz anioł rzekł: —Nie bójcie się! Przynoszę wam radosną nowinę, która dotyczy wszystkich ludzi.
11 Leo katika mji wa Daudi kwa ajili yenu amezaliwa Mwokozi, ndiye Kristo Bwana.
Dzisiaj w Betlejem narodził się Zbawiciel, długo oczekiwany Mesjasz i Pan!
12 Hii ndiyo itakayokuwa ishara kwenu: Mtamkuta mtoto mchanga amefunikwa nguo za kitoto na kulazwa katika hori ya kulia ngʼombe.”
Oto jak Go rozpoznacie: Ujrzycie Niemowlę owinięte w pieluszki, leżące w żłobie.
13 Ghafula pakawa na jeshi kubwa la mbinguni pamoja na huyo malaika wakimsifu Mungu wakisema,
W tym momencie pojawiło się całe mnóstwo aniołów, którzy wielbili Boga:
14 “Atukuzwe Mungu juu mbinguni, na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.”
—Chwała Bogu w niebie, a na ziemi pokój tym, których On kocha!
15 Hao malaika walipokwisha kuondoka na kwenda zao mbinguni, wale wachungaji wakasemezana wao kwa wao, “Twendeni Bethlehemu tukaone mambo haya ya ajabu yaliyotukia, ambayo Bwana ametuambia habari zake.”
Gdy aniołowie powrócili do nieba, pasterze powiedzieli: —Chodźmy do Betlejem i zobaczmy ten cud, o którym usłyszeliśmy.
16 Hivyo wakaenda haraka Bethlehemu, wakawakuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga akiwa amelala katika hori la kulia ngʼombe.
Pobiegli do miasteczka i odnaleźli Marię z Józefem. Zobaczyli też leżące w żłobie Niemowlę.
17 Walipomwona yule mtoto, wakawaeleza yale waliyokuwa wameambiwa kuhusu huyo mtoto.
A wszystkim napotkanym ludziom opowiadali o tym, co przeżyli i co anioł mówił o Dziecku.
18 Nao wote waliosikia habari hizi wakastaajabia yale waliyoambiwa na wale wachungaji wa kondoo.
Słuchający ich nie mogli wyjść z podziwu,
19 Lakini Maria akayaweka mambo haya yote moyoni mwake na kuyatafakari.
a Maria zachowywała to wszystko w swoim sercu i wiele o tym rozmyślała.
20 Wale wachungaji wakarudi, huku wakimtukuza Mungu na kumsifu kwa ajili ya mambo yote waliyokuwa wameambiwa na kuyaona.
Pasterze zaś powrócili do swoich stad, wielbiąc Boga za to, że usłyszeli i zobaczyli dokładnie to, co im zapowiedział anioł.
21 Hata zilipotimia siku nane, ulikuwa ndio wakati wa kumtahiri mtoto, akaitwa Yesu, jina alilokuwa amepewa na malaika kabla hajatungwa mimba.
Po ośmiu dniach, podczas ceremonii obrzezania, nadano Dziecku imię Jezus, zgodnie z tym, co nakazał anioł, zanim jeszcze się poczęło.
22 Ulipotimia wakati wa utakaso wake Maria kwa mujibu wa Sheria ya Mose, basi Yosefu na Maria walimpeleka mtoto Yerusalemu, ili kumweka wakfu kwa Bwana
Gdy zakończył się okres poporodowego oczyszczenia, ustalony w Prawie Mojżesza, rodzice zanieśli Jezusa do Jerozolimy, aby Go poświęcić Panu.
23 (kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana, kwamba, “Kila mtoto wa kiume kifungua mimba atawekwa wakfu kwa Bwana”),
W Prawie napisano bowiem: „Każdego pierwszego syna poświęcicie Panu”.
24 na pia kutoa dhabihu kulingana na yale yaliyonenwa katika Sheria ya Bwana: “Hua wawili au makinda mawili ya njiwa.”
Złożyli też ofiarę oczyszczenia, którą według Prawa mogła być para synogarlic lub dwa młode gołębie.
25 Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli, na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
A mieszkał wtedy w Jerozolimie niejaki Symeon. Był to człowiek prawy, bardzo pobożny i posłuszny Duchowi Świętemu. Nieustannie oczekiwał nadejścia upragnionego przez Żydów Mesjasza.
26 Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana.
Duch Święty objawił mu, że nie umrze, dopóki Go nie ujrzy.
27 Simeoni, akiwa ameongozwa na Roho Mtakatifu, alikwenda Hekaluni. Wazazi walipomleta mtoto Yesu ili kumfanyia kama ilivyokuwa desturi ya Sheria,
Tego właśnie dnia Symeon, kierowany przez Ducha, przyszedł do świątyni. Gdy więc rodzice przynieśli Jezusa, by zgodnie z Prawem poświęcić Go Panu,
28 ndipo Simeoni akampokea mtoto mikononi mwake na kumsifu Mungu, akisema:
spotkali Symeona. On zaś wziął Dziecko na ręce i uwielbił Boga, mówiąc:
29 “Bwana Mwenyezi, kama ulivyoahidi, sasa wamruhusu mtumishi wako aende zake kwa amani.
—Teraz, Wszechmocny Panie, mogę spokojnie umrzeć.
30 Kwa maana macho yangu yameuona wokovu wako,
Zobaczyłem bowiem Zbawiciela,
31 ulioweka tayari machoni pa watu wote,
którego dałeś wszystkim ludom.
32 nuru kwa ajili ya ufunuo kwa watu wa Mataifa na kwa ajili ya utukufu kwa watu wako Israeli.”
On jest światłem dla narodów i chwałą Twojego ludu, Izraela!
33 Naye Yosefu na mama yake mtoto wakastaajabu kwa yale yaliyokuwa yamesemwa kumhusu huyo mtoto.
Słysząc te słowa o Jezusie, Józef i Maria zdumieli się.
34 Kisha Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu amewekwa kwa makusudi ya kuanguka na kuinuka kwa wengi katika Israeli. Atakuwa ishara ambayo watu watanena dhidi yake,
Symeon zaś pobłogosławił ich i rzekł do Marii: —Ten Chłopiec stanie się przyczyną kontrowersji w Izraelu: jedni Go odrzucą, ściągając na siebie zgubę, a inni z radością Go przyjmą.
35 ili mawazo ya mioyo mingi yadhihirike. Nao upanga utauchoma moyo wako.”
W ten sposób wyjdą na jaw najskrytsze ludzkie myśli. Twoją zaś duszę przeniknie miecz cierpienia.
36 Tena alikuwako Hekaluni nabii mmoja mwanamke, jina lake Ana binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa mzee sana; naye alikuwa ameolewa na kuishi na mume kwa miaka saba tu, kisha mumewe akafa.
Tego dnia była również w świątyni prorokini Anna, córka Fanuela, z rodu Asera. Została ona wdową po siedmiu latach małżeństwa,
37 Hivyo alikuwa mjane na umri wake ulikuwa miaka themanini na minne. Yeye hakuondoka humo Hekaluni usiku wala mchana, bali alikuwa akimwabudu Mungu, akifunga na kuomba.
a obecnie miała już osiemdziesiąt cztery lata—była więc w podeszłym wieku. Przez cały czas nie opuszczała jednak świątyni—dniem i nocą służyła bowiem Bogu, modląc się i powstrzymując się od posiłków.
38 Wakati huo huo, Ana alikuja akaanza kusifu, akimshukuru Mungu na kusema habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wakitarajia ukombozi wa Yerusalemu.
Gdy spotkała Marię z małym Jezusem, zaczęła wychwalać Boga. Potem zaś wszystkim mieszkańcom Jerozolimy, którzy oczekiwali przyjścia Zbawiciela, mówiła, że Mesjasz już się narodził.
39 Yosefu na Maria walipokuwa wamekamilisha mambo yote yaliyotakiwa na Sheria ya Bwana, walirudi mjini kwao Nazareti huko Galilaya.
Po spełnieniu wszystkich wymogów Bożego Prawa, rodzice Jezusa powrócili do rodzinnego Nazaretu w Galilei.
40 Naye yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu, akiwa amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
Z upływem czasu Chłopiec dorastał, nabierał sił i stawał się coraz mądrzejszy, a Bóg nieustannie mu błogosławił.
41 Kila mwaka Yosefu na Maria mama yake Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kwa ajili ya Sikukuu ya Pasaka.
Jego rodzice każdego roku udawali się do Jerozolimy na święto Paschy.
42 Yesu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walipanda kwenda kwenye Sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
Gdy Jezus ukończył dwanaście lat, zabrali Go ze sobą.
43 Baada ya Sikukuu kumalizika, wakati Yosefu na Maria mama yake walipokuwa wakirudi nyumbani, Yesu alibaki Yerusalemu lakini hawakutambua.
Po skończonych uroczystościach wszyscy udali się w drogę powrotną, ale Jezus został w Jerozolimie. Początkowo rodzice tego nie zauważyli.
44 Wao wakidhani kuwa yuko miongoni mwa wasafiri, walienda mwendo wa kutwa nzima. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa zao na marafiki.
Szukali Go wśród krewnych i przyjaciół, bo sądzili, że idzie gdzieś w tłumie.
45 Walipomkosa walirudi Yerusalemu ili kumtafuta.
Gdy Go nie znaleźli, wrócili do Jerozolimy, by tam kontynuować poszukiwania.
46 Baada ya siku tatu wakamkuta ndani ya Hekalu, akiwa ameketi katikati ya walimu wa sheria, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
Dopiero po trzech dniach odnaleźli Jezusa. Siedział w świątyni, w gronie nauczycieli Prawa Mojżesza. Słuchał ich i zadawał im pytania,
47 Wote waliomsikia walistaajabishwa na uwezo wake mkubwa wa kuelewa, na majibu aliyoyatoa.
a wszystkich obecnych zadziwiał swoimi wypowiedziami i mądrością.
48 Yosefu na Maria mama yake walipomwona walishangaa. Mama yake akamuuliza, “Mwanangu, mbona umetufanyia hivi? Tazama, mimi na baba yako tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa kila mahali.”
Rodzice byli zaskoczeni tym widokiem. —Synu—powiedziała matka—dlaczego tak postąpiłeś? Szukaliśmy Cię z ojcem i bardzo się niepokoiliśmy.
49 Yesu akawaambia, “Kwa nini kunitafuta? Hamkujua kwamba imenipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
—Dlaczego Mnie szukaliście?—zapytał. —Nie wiedzieliście, że powinienem zajmować się sprawami mojego Ojca?
50 Lakini wao hawakuelewa maana ya lile alilowaambia.
Ale oni nie zrozumieli, co chciał przez to powiedzieć.
51 Ndipo akashuka pamoja nao hadi Nazareti, naye alikuwa mtiifu kwao. Lakini mama yake akayaweka moyoni mwake mambo haya yote.
Wrócił razem z nimi do Nazaretu i był im posłuszny, a Jego matka wszystko to zachowywała w swoim sercu.
52 Naye Yesu akakua katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.
Jezus zaś rósł i nabierał mądrości, ciesząc się przychylnością Boga i ludzi.