< Luka 2 >
1 Siku zile Kaisari Augusto alitoa amri kwamba watu wote waandikishwe katika ulimwengu wa Kirumi.
Erah tokdi Luungwanglong Agastas ih Roman noksong loongtang rookweh thuk ano neng men ah le ni raangthiin thuk rumta.
2 (Orodha hii ndiyo ya kwanza iliyofanyika wakati Krenio alikuwa mtawala wa Shamu).
Erah phang raang et thukta tok adi, Siria hate Kobono ah Kurinus angta.
3 Kila mtu alikwenda kuandikishwa katika mji wake alikozaliwa.
Eno, warep ih neng teewah men ah, maama hah ni raangwan rumta.
4 Hivyo Yosefu akapanda kutoka mji wa Nazareti ulioko Galilaya kwenda Uyahudi, mpaka Bethlehemu, mji wa Daudi, kwa sababu yeye alikuwa wa ukoo na wa nyumba ya Daudi.
Josep ah Galili hah Najeret nawa, Dewid luungwang tup hadaang Judia hah Betlehem ni kata. Tumeah Josep ah Dewid sutoom angta.
5 Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na Maria, ambaye alikuwa amemposa naye alikuwa mjamzito.
Josep ih Meeri heh suh nook raang ih kakhatta damdi, heh men ah wak raang wanta. Heh ah sakjih angta,
6 Wakiwa Bethlehemu, wakati wa Maria wa kujifungua ukawa umetimia,
eno neng Betlehem ni ang tokdi, nootup rangwuung ah thok taha.
7 naye akamzaa mwanawe, kifungua mimba. Akamfunika nguo za kitoto na kumlaza katika hori ya kulia ngʼombe, kwa sababu hapakuwa na nafasi katika nyumba ya wageni.
Heh sah phangkhoh rah miwasah eh tupta, eno nyuh rah ih khoon ano maan tokkhuung ni jupthiinta naangjam nok laje thoi eah.
8 Katika eneo lile walikuwako wachungaji waliokuwa wakikaa mashambani, wakilinda makundi yao ya kondoo usiku.
Erah deek adi mararah saapriimte loong rangphe pheetang ih phek ni, neng saapsah loong ban sok rumta.
9 Ghafula tazama, malaika wa Bwana akawatokea, nao utukufu wa Bwana ukawangʼaria kotekote, wakaingiwa na hofu.
Rangsah rah neng reeni dongchapta, eno Teesu chaan ah neng khothung ni phaakta. Eno neng ah rapne ih cho rumta,
10 Lakini malaika akawaambia: “Msiogope. Kwa maana tazama nawaletea habari njema za furaha itakayokuwa kwa watu wote.
enoothong Rangsah rah ih liirumta, “Nakcho an! Ngah aradi sen suh Ruurang Ese huijah halang, erah ih mina loongtang suh rapne tenroon thuk ah.
11 Leo katika mji wa Daudi kwa ajili yenu amezaliwa Mwokozi, ndiye Kristo Bwana.
Chiinyah Dewid hadaang ni sen pangte tupta—Teesu Kristo ah!
12 Hii ndiyo itakayokuwa ishara kwenu: Mtamkuta mtoto mchanga amefunikwa nguo za kitoto na kulazwa katika hori ya kulia ngʼombe.”
Eno sen suh erah jatthuk han: sen ih noodek esiit nyuh ih khoon ano maan tokkhuung nah jupthiin arah tup an.”
13 Ghafula pakawa na jeshi kubwa la mbinguni pamoja na huyo malaika wakimsifu Mungu wakisema,
Baphuk ih heh damdi rangsah loong hantek ih rang nawa dong taha, eno boongkaat lam ih Rangte rangphoong rumta:
14 “Atukuzwe Mungu juu mbinguni, na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.”
“Rangte chaan ah echoong thoon rangmong ni phaakjaaja, erah dam ih hah nah semroongroong ang thuk ah heh thunghaanla loong asuh ah!”
15 Hao malaika walipokwisha kuondoka na kwenda zao mbinguni, wale wachungaji wakasemezana wao kwa wao, “Twendeni Bethlehemu tukaone mambo haya ya ajabu yaliyotukia, ambayo Bwana ametuambia habari zake.”
Rangsah loong ah neng re nawa rang ni ngaakwangta adi, saapriimte loong ah neng chamchi ni waan rumta, “Betlehem nah kah ih no, erah ni tumjih angla Teesu ih baat tahe loong ah sokkah ih.”
16 Hivyo wakaenda haraka Bethlehemu, wakawakuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga akiwa amelala katika hori la kulia ngʼombe.
Eno neng ah echaan ih Meeri nyia Josep reeni karum ano noodek ah maan tokkhuung ni jupthiin arah japtup karumta.
17 Walipomwona yule mtoto, wakawaeleza yale waliyokuwa wameambiwa kuhusu huyo mtoto.
Saapriimte loong ah ih heh ah sok rum ano, Rangsah ih noodek tiit tumjih baatta loong ah neng suh we toombaat rumta.
18 Nao wote waliosikia habari hizi wakastaajabia yale waliyoambiwa na wale wachungaji wa kondoo.
Saapriimte loong ih baatta rah japchaatte loong ah paatja ih rumta.
19 Lakini Maria akayaweka mambo haya yote moyoni mwake na kuyatafakari.
Meeri ih erah loong tiit ah dokthun ano rapne ih samthunta.
20 Wale wachungaji wakarudi, huku wakimtukuza Mungu na kumsifu kwa ajili ya mambo yote waliyokuwa wameambiwa na kuyaona.
Saapriimte loong ah ngaakwang rum ano, neng ih tup rumta nyia chaat rumta loong asuh boongkaat damdi neng Rangte ah phoongpha rumta; erah ah rangsah ih mamet baat rumta jun ih angta.
21 Hata zilipotimia siku nane, ulikuwa ndio wakati wa kumtahiri mtoto, akaitwa Yesu, jina alilokuwa amepewa na malaika kabla hajatungwa mimba.
Saasinet lini noodek ah heh khoopkhan banlam hoontok thok kohaano, heh ah Jisu et men rumta, marah rangsah ih heh nuh mong ni maangje tokdi dook ban menta men rah ah.
22 Ulipotimia wakati wa utakaso wake Maria kwa mujibu wa Sheria ya Mose, basi Yosefu na Maria walimpeleka mtoto Yerusalemu, ili kumweka wakfu kwa Bwana
Moses Hootthe ih baatta jun ih Meeri nyia Josep, sak saasiit hoon banlam saapoot ah thok ih taha. Eno nyi noodek ah Jerusalem hadaang ni Teesu suh baat kokaat suh huikaat nyuuta,
23 (kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana, kwamba, “Kila mtoto wa kiume kifungua mimba atawekwa wakfu kwa Bwana”),
erah langla Teesu Hootthe ni raangthiin cho angta: “Warep ih ephangtup ela phokhothoon noodek ah Teesu suh kottheng.”
24 na pia kutoa dhabihu kulingana na yale yaliyonenwa katika Sheria ya Bwana: “Hua wawili au makinda mawili ya njiwa.”
Erah damdi nyi ih tokparusah enyi adoleh wotuupi enyi, Teesu Hootthe jun ih nyi siik hoon et koh nyuuta.
25 Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli, na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
Erah tokdi Jerusalem hadaang ni mih wasiit heh men ah Simoon songtongta. Heh ah wase nyia Rangte ra choote mina angta, eno Ijirel mina loong khopui suh heh ih Rangte ah ban sok ruh eta. Esa Chiiala ah heh damdi angta
26 Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana.
erah dam ih heh suh Teesu ih thoomhoon cho Kristo ah maang tuptup an tatiiko ih kakhamta.
27 Simeoni, akiwa ameongozwa na Roho Mtakatifu, alikwenda Hekaluni. Wazazi walipomleta mtoto Yesu ili kumfanyia kama ilivyokuwa desturi ya Sheria,
Chiiala ah ih siit ano Simoon ah rangsoomnok ni wangta. Heh jaatang ih khobaang Jisu ah rangsoomnok ni Hootthe ih jamha jun ih piijah nyuuha di,
28 ndipo Simeoni akampokea mtoto mikononi mwake na kumsifu Mungu, akisema:
Simoon ih noodek ah heh lakkhoni toonpi ano Rangte suh lakookmi liita:
29 “Bwana Mwenyezi, kama ulivyoahidi, sasa wamruhusu mtumishi wako aende zake kwa amani.
“Teesu, an ih thoomhoon jengdang ah thiincho, eno an laksuh ah semroongroong et kaat thuk uh.
30 Kwa maana macho yangu yameuona wokovu wako,
Nga mikmik ih an jiin dowa khopiiroidong ah tup ih hang,
31 ulioweka tayari machoni pa watu wote,
marah an ih loongtang pandi hoon thiin tu rah ah:
32 nuru kwa ajili ya ufunuo kwa watu wa Mataifa na kwa ajili ya utukufu kwa watu wako Israeli.”
Jehudi lah angte loong suh an tenthun ah jathuk suh weephaak ah phaak ah no an mina Ijirel loong tenroon ih phaakjaaja ang rum ah.”
33 Naye Yosefu na mama yake mtoto wakastaajabu kwa yale yaliyokuwa yamesemwa kumhusu huyo mtoto.
Simoon ih Jisu tiit baatta ah chaat nyu ano heh nuh nyi wah ah paatja ih nyuuta.
34 Kisha Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu amewekwa kwa makusudi ya kuanguka na kuinuka kwa wengi katika Israeli. Atakuwa ishara ambayo watu watanena dhidi yake,
Simoon ih nyi suh romseetam koh nyuuta no heh nuh Meeri, suh baatta, “Arah noodek ah Rangte ih danje cho Ijirel loong thet haat nyia khopiipang raangtaan ih ah. Heh ah Rangte mikthe ang ano warep mina ih heh thetbaatte totoh ang ah
35 ili mawazo ya mioyo mingi yadhihirike. Nao upanga utauchoma moyo wako.”
erah thoi ih neng husah tenthun loong ah dongjat ah. Eno an ten ah langtheh ih dook arah likhiik, sattiiti ih sat uh.”
36 Tena alikuwako Hekaluni nabii mmoja mwanamke, jina lake Ana binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa mzee sana; naye alikuwa ameolewa na kuishi na mume kwa miaka saba tu, kisha mumewe akafa.
Teewadi khonuh wikuh, thaknuh heh men ah Anna, Ashir nok hate Phanual sah angta. Heh sawah suh nookta dowa ih paang sinet ba angta eno heh miwah ah tiita. Heh paang rook asat paang baji angta. Heh ih Rangteenok ah babah uh tathiin haatta; rangwuung rangphe heh Rangte rangsoom, nyi samurangsoom ih tongta.
37 Hivyo alikuwa mjane na umri wake ulikuwa miaka themanini na minne. Yeye hakuondoka humo Hekaluni usiku wala mchana, bali alikuwa akimwabudu Mungu, akifunga na kuomba.
38 Wakati huo huo, Ana alikuja akaanza kusifu, akimshukuru Mungu na kusema habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wakitarajia ukombozi wa Yerusalemu.
Erah pootdi Anna thok haano Rangte suh jengseeraata. Eno Jerusalem ah Rangte ih piipang et ah ih bansokte loong asuh noodek tiit ah baatta.
39 Yosefu na Maria walipokuwa wamekamilisha mambo yote yaliyotakiwa na Sheria ya Bwana, walirudi mjini kwao Nazareti huko Galilaya.
Josep nyia Meeri ih Teesu Hootthe ih jamta loong ah jen khom hoon thiin nyu ano, nyi hah Galili ni Najaret hadaang adi ngaak wang nyuuta.
40 Naye yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu, akiwa amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
Noodek ah rongkopkop ih hakta; mongtham ese ah heh jiinni hantek angta, eno Rangte ih heh suh romseetam kota.
41 Kila mwaka Yosefu na Maria mama yake Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kwa ajili ya Sikukuu ya Pasaka.
Paang rookwih Jisu jaatang ah Khopui Kuwaang di Jerusalem ni bankah ruh kah ih rumta.
42 Yesu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walipanda kwenda kwenye Sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
Jisu asih paang nyi ih hak adi, neng erah kuh adi paang hoh dowa likhiik ih karumta.
43 Baada ya Sikukuu kumalizika, wakati Yosefu na Maria mama yake walipokuwa wakirudi nyumbani, Yesu alibaki Yerusalemu lakini hawakutambua.
Kuh ah thoon kano neng ah ngaak wang ih rumta, enoothong noodek Jisu ah Jerusalem ni tangtongta. Erah ah heh jaatang ih tajat rumta;
44 Wao wakidhani kuwa yuko miongoni mwa wasafiri, walienda mwendo wa kutwa nzima. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa zao na marafiki.
neng ih thunta heh ah sengdung ni eje heh angla eah, rah thoi neng henih nitang mokkhoom rumta eno Rekamdi neng joonte sano dung ni phang jam sok rumta.
45 Walipomkosa walirudi Yerusalemu ili kumtafuta.
Neng ih Heh ah tajap jam rumta, erah thoih ih neng Jerusalem ni ngaakwang rum ano eni jam sokwang rumta.
46 Baada ya siku tatu wakamkuta ndani ya Hekalu, akiwa ameketi katikati ya walimu wa sheria, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
Saajom di neng ih heh ah Rangteenok ni japtup rumta, Jehudi nok hate nyootte loong damdi, neng jeng boichaat nyia neng suh chengphi damdi tong arah ah.
47 Wote waliomsikia walistaajabishwa na uwezo wake mkubwa wa kuelewa, na majibu aliyoyatoa.
Warep ih heh tiit chaatte loong ah epaatja ih rumta heh ih jatwah jenglam ih ngaakbaat rum kano ah.
48 Yosefu na Maria mama yake walipomwona walishangaa. Mama yake akamuuliza, “Mwanangu, mbona umetufanyia hivi? Tazama, mimi na baba yako tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa kila mahali.”
Heh nuh nyi wah ah doonmoot ih rumta heh ah tup rum ano ah, eno heh nuh ih liita, “Nga sah, an ih tumjih hoon wan halu? “Sek ah anwah ah rapne ih sootsaam thuk haliitih, an ah noongrep ni taat tum jam sok hiitih.”
49 Yesu akawaambia, “Kwa nini kunitafuta? Hamkujua kwamba imenipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
Jisu ih ngaakbaatta, “Ngah set ih tumet suh jam sok hali tih? Set ih tanih jattansih ngah seng wah nok ni eah?”
50 Lakini wao hawakuelewa maana ya lile alilowaambia.
Jisu ih ngaakbaat rumta ah neng ih tajen samjat rumta.
51 Ndipo akashuka pamoja nao hadi Nazareti, naye alikuwa mtiifu kwao. Lakini mama yake akayaweka moyoni mwake mambo haya yote.
Eno Jisu ah neng damdi Najaret ni roong ngaakwangta, heh nuh nyi heh wah jeng chaatchaat ah. Erah di mamah angta erah loong ah heh nuh ih heh tenni lomthun ruh eta.
52 Naye Yesu akakua katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.
Jisu ah hansi nyia ese mongtham ni choocho ih hakta, mina nyi Rangte uh heko ih roopta.