< Luka 2 >

1 Siku zile Kaisari Augusto alitoa amri kwamba watu wote waandikishwe katika ulimwengu wa Kirumi.
And it came to pass in those days, there went forth a decree from Caesar Augustus that all the world be registered—
2 (Orodha hii ndiyo ya kwanza iliyofanyika wakati Krenio alikuwa mtawala wa Shamu).
this census first came to pass when Quirinius was governor of Syria—
3 Kila mtu alikwenda kuandikishwa katika mji wake alikozaliwa.
and all were going to be registered, each to his proper city,
4 Hivyo Yosefu akapanda kutoka mji wa Nazareti ulioko Galilaya kwenda Uyahudi, mpaka Bethlehemu, mji wa Daudi, kwa sababu yeye alikuwa wa ukoo na wa nyumba ya Daudi.
and Joseph also went up from Galilee, out of the city of Nazareth, to Judea, to the city of David, that is called Beth-Lehem, because of his being of the house and family of David,
5 Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na Maria, ambaye alikuwa amemposa naye alikuwa mjamzito.
to register himself with Mary his betrothed wife, being with Child.
6 Wakiwa Bethlehemu, wakati wa Maria wa kujifungua ukawa umetimia,
And it came to pass, in their being there, the days were fulfilled for her bringing forth,
7 naye akamzaa mwanawe, kifungua mimba. Akamfunika nguo za kitoto na kumlaza katika hori ya kulia ngʼombe, kwa sababu hapakuwa na nafasi katika nyumba ya wageni.
and she brought forth her Son—the firstborn, and wrapped Him up, and laid Him down in the manger, because there was not a place for them in the guest-chamber.
8 Katika eneo lile walikuwako wachungaji waliokuwa wakikaa mashambani, wakilinda makundi yao ya kondoo usiku.
And there were shepherds in the same region, lodging in the field and keeping the night-watches over their flock,
9 Ghafula tazama, malaika wa Bwana akawatokea, nao utukufu wa Bwana ukawangʼaria kotekote, wakaingiwa na hofu.
and behold, a messenger of the LORD stood over them, and the glory of the LORD shone around them, and they feared [with] a great fear.
10 Lakini malaika akawaambia: “Msiogope. Kwa maana tazama nawaletea habari njema za furaha itakayokuwa kwa watu wote.
And the messenger said to them, “Do not fear, for behold, I bring you good news of great joy that will be to all the people,
11 Leo katika mji wa Daudi kwa ajili yenu amezaliwa Mwokozi, ndiye Kristo Bwana.
because today in the city of David a Savior was born to you, who is Christ the LORD!
12 Hii ndiyo itakayokuwa ishara kwenu: Mtamkuta mtoto mchanga amefunikwa nguo za kitoto na kulazwa katika hori ya kulia ngʼombe.”
And this [is] the sign to you: you will find a Baby wrapped up, lying in the manger.”
13 Ghafula pakawa na jeshi kubwa la mbinguni pamoja na huyo malaika wakimsifu Mungu wakisema,
And suddenly there came with the messenger a multitude of the heavenly host, praising God, and saying,
14 “Atukuzwe Mungu juu mbinguni, na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.”
“Glory in the highest to God, and on earth peace, among men—good will!”
15 Hao malaika walipokwisha kuondoka na kwenda zao mbinguni, wale wachungaji wakasemezana wao kwa wao, “Twendeni Bethlehemu tukaone mambo haya ya ajabu yaliyotukia, ambayo Bwana ametuambia habari zake.”
And it came to pass, when the messengers were gone away from them to the heavens, that the men, the shepherds, said to one another, “We may indeed go over to Beth-Lehem and see this thing that has come to pass, that the LORD made known to us!”
16 Hivyo wakaenda haraka Bethlehemu, wakawakuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga akiwa amelala katika hori la kulia ngʼombe.
And they came, having hurried, and found both Mary, and Joseph, and the Baby lying in the manger,
17 Walipomwona yule mtoto, wakawaeleza yale waliyokuwa wameambiwa kuhusu huyo mtoto.
and having seen, they made known abroad concerning the saying spoken to them concerning the Child.
18 Nao wote waliosikia habari hizi wakastaajabia yale waliyoambiwa na wale wachungaji wa kondoo.
And all who heard [it] wondered concerning the things spoken to them by the shepherds;
19 Lakini Maria akayaweka mambo haya yote moyoni mwake na kuyatafakari.
and Mary was preserving all these things, pondering [them] in her heart;
20 Wale wachungaji wakarudi, huku wakimtukuza Mungu na kumsifu kwa ajili ya mambo yote waliyokuwa wameambiwa na kuyaona.
and the shepherds turned back, glorifying and praising God for all those things they heard and saw, as it was spoken to them.
21 Hata zilipotimia siku nane, ulikuwa ndio wakati wa kumtahiri mtoto, akaitwa Yesu, jina alilokuwa amepewa na malaika kabla hajatungwa mimba.
And when eight days were fulfilled to circumcise the Child, then was His Name called Jesus, having been so called by the messenger before His being conceived in the womb.
22 Ulipotimia wakati wa utakaso wake Maria kwa mujibu wa Sheria ya Mose, basi Yosefu na Maria walimpeleka mtoto Yerusalemu, ili kumweka wakfu kwa Bwana
And when the days of their purification were fulfilled, according to the Law of Moses, they brought Him up to Jerusalem, to present to the LORD,
23 (kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana, kwamba, “Kila mtoto wa kiume kifungua mimba atawekwa wakfu kwa Bwana”),
as it has been written in the Law of the LORD: “Every male opening a womb will be called holy to the LORD,”
24 na pia kutoa dhabihu kulingana na yale yaliyonenwa katika Sheria ya Bwana: “Hua wawili au makinda mawili ya njiwa.”
and to give a sacrifice, according to that said in the Law of the LORD: “A pair of turtle-doves, or two young pigeons.”
25 Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli, na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
And behold, there was a man in Jerusalem whose name [is] Simeon, and this man is righteous and devout, looking for the comforting of Israel, and the Holy Spirit was on him,
26 Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana.
and it has been divinely told him by the Holy Spirit—not to see death before he may see the Christ of the LORD.
27 Simeoni, akiwa ameongozwa na Roho Mtakatifu, alikwenda Hekaluni. Wazazi walipomleta mtoto Yesu ili kumfanyia kama ilivyokuwa desturi ya Sheria,
And he came in the Spirit into the temple, and in the parents bringing in the child Jesus, for their doing according to the custom of the Law regarding Him,
28 ndipo Simeoni akampokea mtoto mikononi mwake na kumsifu Mungu, akisema:
then he took Him in his arms, and blessed God, and he said,
29 “Bwana Mwenyezi, kama ulivyoahidi, sasa wamruhusu mtumishi wako aende zake kwa amani.
“Now You send Your servant away, O LORD, according to Your word, in peace,
30 Kwa maana macho yangu yameuona wokovu wako,
because my eyes saw Your salvation,
31 ulioweka tayari machoni pa watu wote,
which You prepared before the face of all the peoples,
32 nuru kwa ajili ya ufunuo kwa watu wa Mataifa na kwa ajili ya utukufu kwa watu wako Israeli.”
a light to the uncovering of nations, and the glory of Your people Israel.”
33 Naye Yosefu na mama yake mtoto wakastaajabu kwa yale yaliyokuwa yamesemwa kumhusu huyo mtoto.
And Joseph and His mother were wondering at the things spoken concerning Him,
34 Kisha Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu amewekwa kwa makusudi ya kuanguka na kuinuka kwa wengi katika Israeli. Atakuwa ishara ambayo watu watanena dhidi yake,
and Simeon blessed them and said to His mother Mary, “Behold, this [One] is set for the falling and rising again of many in Israel, and for a sign spoken against—
35 ili mawazo ya mioyo mingi yadhihirike. Nao upanga utauchoma moyo wako.”
(and also a sword will pass through your own soul)—that the reasonings of many hearts may be revealed.”
36 Tena alikuwako Hekaluni nabii mmoja mwanamke, jina lake Ana binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa mzee sana; naye alikuwa ameolewa na kuishi na mume kwa miaka saba tu, kisha mumewe akafa.
And there was Anna, a prophetess, daughter of Phanuel, of the tribe of Asher, she was much advanced in days, having lived with a husband seven years from her virginity,
37 Hivyo alikuwa mjane na umri wake ulikuwa miaka themanini na minne. Yeye hakuondoka humo Hekaluni usiku wala mchana, bali alikuwa akimwabudu Mungu, akifunga na kuomba.
and she [is] a widow of about eighty-four years, who did not depart from the temple, serving with fasts and supplications, night and day,
38 Wakati huo huo, Ana alikuja akaanza kusifu, akimshukuru Mungu na kusema habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wakitarajia ukombozi wa Yerusalemu.
and she, at that hour, having come in, was confessing, likewise, to the LORD, and was speaking concerning Him to all those looking for redemption in Jerusalem.
39 Yosefu na Maria walipokuwa wamekamilisha mambo yote yaliyotakiwa na Sheria ya Bwana, walirudi mjini kwao Nazareti huko Galilaya.
And when they completed all things according to the Law of the LORD, they turned back to Galilee, to their city of Nazareth;
40 Naye yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu, akiwa amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
and the Child grew and was strengthened in spirit, being filled with wisdom, and the grace of God was on Him.
41 Kila mwaka Yosefu na Maria mama yake Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kwa ajili ya Sikukuu ya Pasaka.
And His parents were going yearly to Jerusalem, at the Celebration of the Passover,
42 Yesu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walipanda kwenda kwenye Sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
and when He became twelve years old, they having gone up to Jerusalem according to the custom of the celebration,
43 Baada ya Sikukuu kumalizika, wakati Yosefu na Maria mama yake walipokuwa wakirudi nyumbani, Yesu alibaki Yerusalemu lakini hawakutambua.
and having finished the days, in their returning the child Jesus remained behind in Jerusalem, and Joseph and His mother did not know,
44 Wao wakidhani kuwa yuko miongoni mwa wasafiri, walienda mwendo wa kutwa nzima. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa zao na marafiki.
and having supposed Him to be in the company, they went a day’s journey, and were seeking Him among the relatives and among the acquaintances,
45 Walipomkosa walirudi Yerusalemu ili kumtafuta.
and having not found Him, they turned back to Jerusalem seeking Him.
46 Baada ya siku tatu wakamkuta ndani ya Hekalu, akiwa ameketi katikati ya walimu wa sheria, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
And it came to pass, after three days they found Him in the temple, sitting in the midst of the teachers, both hearing them and questioning them,
47 Wote waliomsikia walistaajabishwa na uwezo wake mkubwa wa kuelewa, na majibu aliyoyatoa.
and all those hearing Him were astonished at His understanding and answers.
48 Yosefu na Maria mama yake walipomwona walishangaa. Mama yake akamuuliza, “Mwanangu, mbona umetufanyia hivi? Tazama, mimi na baba yako tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa kila mahali.”
And having seen Him, they were amazed, and His mother said to Him, “Child, why did You do this to us? Behold, Your father and I, sorrowing, were seeking You.”
49 Yesu akawaambia, “Kwa nini kunitafuta? Hamkujua kwamba imenipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
And He said to them, “Why [is it] that you were seeking Me? Did you not know that it is necessary for Me to be in the things of My Father?”
50 Lakini wao hawakuelewa maana ya lile alilowaambia.
And they did not understand the saying that He spoke to them,
51 Ndipo akashuka pamoja nao hadi Nazareti, naye alikuwa mtiifu kwao. Lakini mama yake akayaweka moyoni mwake mambo haya yote.
and He went down with them, and came to Nazareth, and He was subject to them, and His mother was keeping all these sayings in her heart,
52 Naye Yesu akakua katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.
and Jesus was advancing in wisdom, and in stature, and in favor with God and men.

< Luka 2 >