< Luka 2 >

1 Siku zile Kaisari Augusto alitoa amri kwamba watu wote waandikishwe katika ulimwengu wa Kirumi.
Chuphat lai chun Rome gamvaipo, Augustus chun Rome gamsung pumpia minsut ding thupeh ahin neitan ahi.
2 (Orodha hii ndiyo ya kwanza iliyofanyika wakati Krenio alikuwa mtawala wa Shamu).
(Hiche hi minsut amasapen Quirinius Syria gamvaipo ahilai anahi).
3 Kila mtu alikwenda kuandikishwa katika mji wake alikozaliwa.
Mijouse ama ama hung kondoh na khopi ah minsut na a kijihlut dingin akile un ahi.
4 Hivyo Yosefu akapanda kutoka mji wa Nazareti ulioko Galilaya kwenda Uyahudi, mpaka Bethlehemu, mji wa Daudi, kwa sababu yeye alikuwa wa ukoo na wa nyumba ya Daudi.
Chule Joseph chu leng David chilhah ahijeh chun, Judea gam Bethlehem, David gollui laiya achenna in'a ache angaitai. Chua chun ama akholjin in Galilee gam Nazareth kho a pat in akipatdoh'e.
5 Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na Maria, ambaye alikuwa amemposa naye alikuwa mjamzito.
Aman agolngai Mary chu akipuiyin, amanu chu agaiyah ahi akichen in ahi.
6 Wakiwa Bethlehemu, wakati wa Maria wa kujifungua ukawa umetimia,
Chule chumun a aum laiyun, naoso phat chu ahung lhing tan ahi.
7 naye akamzaa mwanawe, kifungua mimba. Akamfunika nguo za kitoto na kumlaza katika hori ya kulia ngʼombe, kwa sababu hapakuwa na nafasi katika nyumba ya wageni.
Amanun acha masa, chapa khat ahingin, pon'in phatah in ajel in gan ankong ah alupsah'e, ajeh chu gemun amaho dia onglou anahi.
8 Katika eneo lile walikuwako wachungaji waliokuwa wakikaa mashambani, wakilinda makundi yao ya kondoo usiku.
Chuche jan chun kelngoi chingho loujao anai dungah aum'un, kelngoiho aventup u ahi.
9 Ghafula tazama, malaika wa Bwana akawatokea, nao utukufu wa Bwana ukawangʼaria kotekote, wakaingiwa na hofu.
Phulou helouvin Pakai vantil khat ahenguvah ahung kilah in, chule Pakai loupina in akimvel'u asalvah soh'e. Amaho akichauvin,
10 Lakini malaika akawaambia: “Msiogope. Kwa maana tazama nawaletea habari njema za furaha itakayokuwa kwa watu wote.
ahivangin vantil chun alhamon in, “Kicha hih'un” tin aseiyin “Keiman nangho kipana thupha, mijouse dinga kipana hinso ding kahin pohpeh uve.
11 Leo katika mji wa Daudi kwa ajili yenu amezaliwa Mwokozi, ndiye Kristo Bwana.
Huhhingpu, ahi, Messiah chu, Pakai chu tunin David khopi Bethlehem ah apengtai!
12 Hii ndiyo itakayokuwa ishara kwenu: Mtamkuta mtoto mchanga amefunikwa nguo za kitoto na kulazwa katika hori ya kulia ngʼombe.”
Chule nanghon hiche melchihna a hi nahetdoh thei diu ahi: Nanghon naosen pon ajol jol'a kitup sel'a kijel, gan ankonga kilupsah nagamu diu ahi,” ati.
13 Ghafula pakawa na jeshi kubwa la mbinguni pamoja na huyo malaika wakimsifu Mungu wakisema,
Phulou helouvin vantil chu vanmi janel honpi hon ahinjop'un–van sepai hotoh–Pathen avahchoiyun chule hitin aseiyuve,
14 “Atukuzwe Mungu juu mbinguni, na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.”
“Van chungnung pen'a Pathen loupi hen, chule leiset chunga Pathen lunglhaina mi ho lah'a cham leng hen,” atiuve.
15 Hao malaika walipokwisha kuondoka na kwenda zao mbinguni, wale wachungaji wakasemezana wao kwa wao, “Twendeni Bethlehemu tukaone mambo haya ya ajabu yaliyotukia, ambayo Bwana ametuambia habari zake.”
Vantilte van lam'a akilephat un kelngoi chingho khat le khat akihouvun, “Bethlehem a cheu hite! Hiche thilsoh ho Pakaiyin eiseipeh uhi gaveuhite,” akitiuve.
16 Hivyo wakaenda haraka Bethlehemu, wakawakuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga akiwa amelala katika hori la kulia ngʼombe.
Amaho khosung a chun kinloi tah'in acheuvin Mary le Joseph agamu uvin, chule naosen chu gan ankong a chun analum'e.
17 Walipomwona yule mtoto, wakawaeleza yale waliyokuwa wameambiwa kuhusu huyo mtoto.
Ama amuphat uvin kelngoi chinghon thilsoh ho le vantil in naosen chungchanga amaho jah'a aseiho mijouse aseipeh tauvin ahi.
18 Nao wote waliosikia habari hizi wakastaajabia yale waliyoambiwa na wale wachungaji wa kondoo.
Kelngoi chingho thusei jajouse chu alungdong lheh jeng tauvin,
19 Lakini Maria akayaweka mambo haya yote moyoni mwake na kuyatafakari.
ahivangin Mary'n hitiho jouse hi alungsungah akoiyin khatvei vei kom le ahin geldoh ji'e.
20 Wale wachungaji wakarudi, huku wakimtukuza Mungu na kumsifu kwa ajili ya mambo yote waliyokuwa wameambiwa na kuyaona.
Kelngoi chingho akelngoi hon teu hengah akile kit un, athilmu hou le ajah hou jal'in Pathen aloupisah un chule avahchoi tauve. Vantil in aseipeh'u bang chet in thil asoh'e.
21 Hata zilipotimia siku nane, ulikuwa ndio wakati wa kumtahiri mtoto, akaitwa Yesu, jina alilokuwa amepewa na malaika kabla hajatungwa mimba.
Niget jouvin naosen chu chep atanpeh un amin Yeshua asah tauve, hichu vantil in akijil masanga pat'a anaminsah sa ahitai.
22 Ulipotimia wakati wa utakaso wake Maria kwa mujibu wa Sheria ya Mose, basi Yosefu na Maria walimpeleka mtoto Yerusalemu, ili kumweka wakfu kwa Bwana
Chuin kisuhthengna thilto phat alhing tan, Mose dan'in chapang khat apen jouva boldinga angeh dungjuiyin; chuti chun anu le apan Pakai henga pehdoh dingin Jerusalem'a ahin pui lhon'e.
23 (kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana, kwamba, “Kila mtoto wa kiume kifungua mimba atawekwa wakfu kwa Bwana”),
Pakai danthu chun hitia hi asei ahi, “Numei cha masa chu pasal ahia leh, amapa chu Pakai henga kikatdoh ding ahi.”
24 na pia kutoa dhabihu kulingana na yale yaliyonenwa katika Sheria ya Bwana: “Hua wawili au makinda mawili ya njiwa.”
Chuin Pakai danthua kingeh bangtah in kilhaina chu atoh lhon in ahi–vakhu kop khat ahiloule vapal ni hiji ahi.
25 Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli, na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
Chuphat lai chun Jerusalem ah Simeon kiti mikhat anaum'e. Amachu michonpha le Pathen hou guttah chule Messiah ahunga Israel ahung lhatdoh ding kinem'a ngahjing khat anahi. Lhagao Theng achungah achun,
26 Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana.
chule Pakai Messiah amutokah'a thilou dinga anaseipeh anahi.
27 Simeoni, akiwa ameongozwa na Roho Mtakatifu, alikwenda Hekaluni. Wazazi walipomleta mtoto Yesu ili kumfanyia kama ilivyokuwa desturi ya Sheria,
Hiche ni chun Lhagao chun Houin sungah apuilut in ahi. Chuin Mary le Joseph chun naosen chu Pakai koma danthua kingeh dungjuiya ahung pehdoh lhon chun,
28 ndipo Simeoni akampokea mtoto mikononi mwake na kumsifu Mungu, akisema:
Simeon chu anaum in ahi. Aman naosen chu alan Pathen athangvah in, hitin ati,
29 “Bwana Mwenyezi, kama ulivyoahidi, sasa wamruhusu mtumishi wako aende zake kwa amani.
“Chungnungpen Pakai, tun nasohpa lungmongin thisah tan nakitepna bangin,
30 Kwa maana macho yangu yameuona wokovu wako,
Keiman namihuhhingna kamutai,
31 ulioweka tayari machoni pa watu wote,
Mijouse dinga nagon chu,
32 nuru kwa ajili ya ufunuo kwa watu wa Mataifa na kwa ajili ya utukufu kwa watu wako Israeli.”
Ama hi namtin vaipi henga Pathen phongdoh ding vah chu ahi, chule ama hi nami Israelte loupina chu ahi.”
33 Naye Yosefu na mama yake mtoto wakastaajabu kwa yale yaliyokuwa yamesemwa kumhusu huyo mtoto.
Yeshua nu le pachu ama chungchang thu kisei ho jeh chun alungdong lheh jeng lhon'e.
34 Kisha Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu amewekwa kwa makusudi ya kuanguka na kuinuka kwa wengi katika Israeli. Atakuwa ishara ambayo watu watanena dhidi yake,
Chuin Simeon in amaho chu phatthei aboh in chule Mary, naosen nu koma chun aseitai, “Hiche chapang hi Israel sunga mi tamtah lhuhna dinga got'a um ahi, ahivanga midang tampi a dinga kipana hiding ahi. Ama hi Pathen'a kona melchih na a hung kisol ahin, hinlah mi tamtah'in adoudal ding ahi.
35 ili mawazo ya mioyo mingi yadhihirike. Nao upanga utauchoma moyo wako.”
Chuho jeh'a mi tamtah lunggel thuhpen ho kiphongdoh ding ahi. Chule chemjam in nalhagao asutkhah ding ahi.”
36 Tena alikuwako Hekaluni nabii mmoja mwanamke, jina lake Ana binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa mzee sana; naye alikuwa ameolewa na kuishi na mume kwa miaka saba tu, kisha mumewe akafa.
Themgao khat amin Anna kiti khat jong Houin a chu umah ahi. Amanu chu Phanuel chanu Asher phung'a mi ahin, chule hateh'a teh ahitai. A-inneipu chu akichen lhon kum sagi bep sunga thi ahitai.
37 Hivyo alikuwa mjane na umri wake ulikuwa miaka themanini na minne. Yeye hakuondoka humo Hekaluni usiku wala mchana, bali alikuwa akimwabudu Mungu, akifunga na kuomba.
Chutia chu amanu hin kum somget le li jen meithai hinkho ahin man ahi. Amanun Houin adalha ngai pon, asun ajan in aum jingin, an-ngol le taona pumin Pathen ahoujinge.
38 Wakati huo huo, Ana alikuja akaanza kusifu, akimshukuru Mungu na kusema habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wakitarajia ukombozi wa Yerusalemu.
Simeon chun Mary le Joseph koma thu aseilai chun amanu jong ahungin Pathen avahchoi pantai. Chapang chungchang thudol Pathen in Jerusalem ahuhdoh nadinga gingcha tah'a ngah jing ho jouse komah aseiyin ahi.
39 Yosefu na Maria walipokuwa wamekamilisha mambo yote yaliyotakiwa na Sheria ya Bwana, walirudi mjini kwao Nazareti huko Galilaya.
Yeshua nu le pan Pakai danthu dungjuiya boldinga lom cheng abulhit soh lhon phat in, a-in'u Galilee gam Nazereth kho ah akile tauve.
40 Naye yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu, akiwa amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
Chumun a chun chapangpa chu tahsa damthei tah le hattah in ahung khanglen in ahi. Amachu chihna adimset in chule Pathen khotona achungah aume. Jerusalem Hou'in a Yeshua
41 Kila mwaka Yosefu na Maria mama yake Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kwa ajili ya Sikukuu ya Pasaka.
Kumseh le Yeshua nu le pa Kalchuh Kut mang'in acheji lhonin ahi.
42 Yesu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walipanda kwenda kwenye Sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
Yeshua kum somleni alhin chun angaima bangin hiche kut mang ding chun acheuve.
43 Baada ya Sikukuu kumalizika, wakati Yosefu na Maria mama yake walipokuwa wakirudi nyumbani, Yesu alibaki Yerusalemu lakini hawakutambua.
Kut kichaiyin inlang Nazereth a kile din akipan tauvin, ahin Yeshua chu Jerusalem ah aumden tan ahi. Anu le apan atil'in hichu ahedoh lhon pon,
44 Wao wakidhani kuwa yuko miongoni mwa wasafiri, walienda mwendo wa kutwa nzima. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa zao na marafiki.
ajeh chu kholjin dang hotoh kilhon khom dan a angaito lhon ahi. Ahivangin ama chuche nilhah'a ahung kilulah loubeh phat in asopi aheng akom le aloi agol ho komah aga vele lhontai.
45 Walipomkosa walirudi Yerusalemu ili kumtafuta.
Amulhon loubeh phat in Jerusalem lamah ama holdin akile kit lhon tai.
46 Baada ya siku tatu wakamkuta ndani ya Hekalu, akiwa ameketi katikati ya walimu wa sheria, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
Nithum jouvin achainakeiyin Houin sungah agamudoh lhonin, houhil ho lah a atouva, athuseiyu angaiya, chule thudoh anei chu amudoh lhon tai.
47 Wote waliomsikia walistaajabishwa na uwezo wake mkubwa wa kuelewa, na majibu aliyoyatoa.
Ama thusei jajouse chun athuhet le athudoh donbut ho chu adatmah lheh jeng tauve.
48 Yosefu na Maria mama yake walipomwona walishangaa. Mama yake akamuuliza, “Mwanangu, mbona umetufanyia hivi? Tazama, mimi na baba yako tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa kila mahali.”
Anu le apan ima lunggel je jong ahelhon tapoi. Chuin anun ahinseiyin, “Chapa,” ipijeh'a hiche hi keini koma nabol ham? Napa le keiman munjouse kahol lhon'a lunggim a kahilhon tai, ati.
49 Yesu akawaambia, “Kwa nini kunitafuta? Hamkujua kwamba imenipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
“Ahivanga ipijeh'a neihol khoh u ngai ham?” tin adongin, “Nahet lou u ham kapa in'a kaum ding mong ahi hi?” tin adonge.
50 Lakini wao hawakuelewa maana ya lile alilowaambia.
Ahivangin ipi aseina ahi ahedoh lhon pon ahi.
51 Ndipo akashuka pamoja nao hadi Nazareti, naye alikuwa mtiifu kwao. Lakini mama yake akayaweka moyoni mwake mambo haya yote.
Chuin amaho chutoh Nazareth lam'a a-kile un chuva chun anu apa thunoiya aumtai. Chule anun hitiho jouse hi alungthimah aguh'in avop jing in ahi.
52 Naye Yesu akakua katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.
Yeshua chu chihna le atahsa in akhangin chule Pathen le mihem deisah na in aumtan ahi.

< Luka 2 >