< Luka 19 >
1 Yesu akaingia Yeriko, naye alikuwa anapita katikati ya huo mji.
İsa Eriha'ya girdi. Kentin içinden geçiyordu.
2 Tazama, palikuwa na mtu mmoja mkuu wa watoza ushuru naye alikuwa tajiri, jina lake Zakayo.
Orada vergi görevlilerinin başı olan, Zakkay adında zengin bir adam vardı.
3 Yeye alikuwa akijitahidi kumwona Yesu ni mtu wa namna gani. Lakini kutokana na umati mkubwa wa watu hakuweza kwa sababu alikuwa mfupi wa kimo.
İsa'nın kim olduğunu görmek istiyor, ama boyu kısa olduğu için kalabalıktan ötürü göremiyordu.
4 Kwa hiyo akatangulia mbio mbele ya umati wa watu akapanda juu ya mkuyu ili amwone Yesu, kwa sababu angeipitia njia ile.
İsa'yı görebilmek için önden koşup bir yabanıl incir ağacına tırmandı. Çünkü İsa oradan geçecekti.
5 Yesu alipofika pale chini ya huo mkuyu, akatazama juu, akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, kwa maana leo nitakuwa mgeni nyumbani kwako!”
İsa oraya varınca yukarı bakıp, “Zakkay, çabuk aşağı in!” dedi. “Bugün senin evinde kalmam gerekiyor.”
6 Hivyo Zakayo akashuka upesi, akamkaribisha Yesu nyumbani kwake kwa furaha kubwa.
Zakkay hızla aşağı indi ve sevinç içinde İsa'yı evine buyur etti.
7 Watu wote walipoona hivyo, wakaanza kunungʼunika wakisema, “Amekwenda kuwa mgeni wa ‘mtu mwenye dhambi.’”
Bunu görenlerin hepsi söylenmeye başladı: “Gidip günahkâr birine konuk oldu!” dediler.
8 Lakini Zakayo akasimama na kumwambia Bwana, “Tazama, Bwana! Sasa hivi nusu ya mali yangu ninawapa maskini, nami kama nimemdhulumu mtu yeyote kitu chochote, nitamrudishia mara nne ya hicho kiwango.”
Zakkay ayağa kalkıp Rab'be şöyle dedi: “Ya Rab, işte malımın yarısını yoksullara veriyorum. Bir kimseden haksızlıkla bir şey aldımsa, dört katını geri vereceğim.”
9 Ndipo Yesu akamwambia, “Leo, wokovu umeingia nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Abrahamu.
İsa dedi ki, “Bu ev bugün kurtuluşa kavuştu. Çünkü bu adam da İbrahim'in oğludur.
10 Kwa maana Mwana wa Adamu amekuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.”
Nitekim İnsanoğlu, kaybolanı arayıp kurtarmak için geldi.”
11 Walipokuwa wanasikiliza haya, Yesu akaendelea kuwaambia mfano, kwa sababu alikuwa anakaribia Yerusalemu na watu walikuwa wakidhani ya kuwa Ufalme wa Mungu ulikuwa unakuja saa iyo hiyo.
Oradakiler bu sözleri dinlerken İsa konuşmasını bir benzetmeyle sürdürdü. Çünkü Yeruşalim'e yaklaşmıştı ve onlar, Tanrı'nın Egemenliği'nin hemen ortaya çıkacağını sanıyorlardı.
12 Hivyo akawaambia: “Mtu mmoja mwenye cheo kikubwa alisafiri kwenda nchi ya mbali ili akapokee madaraka ya kuwa mfalme, kisha arudi.
Bu nedenle İsa şöyle dedi: “Soylu bir adam, kral atanıp dönmek üzere uzak bir ülkeye gitti.
13 Hivyo akawaita kumi miongoni mwa watumishi wake, na akawapa kila mmoja fungu la fedha. Akawaambia, ‘Fanyeni biashara na fedha hizi mpaka nitakaporudi.’
Gitmeden önce kölelerinden onunu çağırıp onlara birer mina verdi. ‘Ben dönünceye dek bu paraları işletin’ dedi.
14 “Lakini raiya wa nchi yake walimchukia wakapeleka ujumbe na kusema, ‘Hatutaki huyu mtu awe mfalme wetu.’
“Ne var ki, ülkesinin halkı adamdan nefret ediyordu. Arkasından temsilciler göndererek, ‘Bu adamın üzerimize kral olmasını istemiyoruz’ diye haber ilettiler.
15 “Hata hivyo alirudi akiwa amekwisha kupokea mamlaka ya ufalme, akawaita wale watumishi wake aliokuwa amewaachia fedha, ili afahamu ni faida kiasi gani kila mmoja wao aliyopata kwa kufanya biashara.
“Adam kral atanmış olarak geri döndüğünde, parayı vermiş olduğu köleleri çağırtıp ne kazandıklarını öğrenmek istedi.
16 “Wa kwanza akaja na kusema, ‘Bwana, kutokana na fedha uliyoniachia, nimepata faida mara kumi zaidi.’
Birincisi geldi, ‘Efendimiz’ dedi, ‘Senin bir minan on mina daha kazandı.’
17 “Yule bwana akamjibu, ‘Umefanya vizuri mtumishi mwema! Kwa sababu umekuwa mwaminifu katika wajibu mdogo sana, nakupa mamlaka juu ya miji kumi.’
“Efendisi ona, ‘Aferin, iyi köle!’ dedi. ‘En küçük işte güvenilir olduğunu gösterdiğin için on kent üzerinde yetkili olacaksın.’
18 “Wa pili naye akaja. Akasema, ‘Bwana, fedha yako imeleta faida mara tano zaidi.’
“İkincisi gelip, ‘Efendimiz, senin bir minan beş mina daha kazandı’ dedi.
19 “Bwana wake akajibu, ‘Nakupa mamlaka juu ya miji mitano.’
“Efendisi ona da, ‘Sen beş kent üzerinde yetkili olacaksın’ dedi.
20 “Kisha akaja yule mtumishi mwingine, akasema, ‘Bwana, hii hapa fedha yako. Niliitunza vizuri kwenye kitambaa.
“Başka biri geldi, ‘Efendimiz’ dedi, ‘İşte senin minan! Onu bir mendile sarıp sakladım.
21 Nilikuogopa, kwa sababu wewe ni mtu mgumu. Unachukua ambapo hukuweka kitu, na unavuna mahali ambapo hukupanda kitu.’
Çünkü senden korktum, sert adamsın; kendinden koymadığını alır, ekmediğini biçersin.’
22 “Bwana wake akamjibu, ‘Nitakuhukumu kwa maneno yako mwenyewe, wewe mtumishi mwovu! Kama ulifahamu kwamba mimi ni mtu mgumu, nichukuaye mahali ambapo sikuweka kitu na kuvuna mahali ambapo sikupanda,
“Efendisi ona, ‘Ey kötü köle, seni kendi ağzından çıkan sözle yargılayacağım’ dedi. ‘Kendinden koymadığını alan, ekmediğini biçen sert bir adam olduğumu bildiğine göre,
23 kwa nini basi hukuweka fedha zangu kwa watoa riba, ili nitakaporudi nichukue iliyo yangu na riba yake?’
neden paramı faize vermedin? Ben de geldiğimde onu faiziyle geri alırdım.’
24 “Ndipo akawaambia wale waliokuwa wamesimama karibu, ‘Mnyangʼanyeni fungu lake la fedha, mkampe yule mwenye kumi.’
“Sonra çevrede duranlara, ‘Elindeki minayı alın, on minası olana verin’ dedi.
25 “Wakamwambia, ‘Bwana, mbona; tayari anayo mafungu kumi!’
“Ona, ‘Efendimiz’ dediler, ‘Onun zaten on minası var!’
26 “Akawajibu, ‘Nawaambia kwamba kila aliye na kitu, ataongezewa. Lakini yule asiye na kitu, hata alicho nacho atanyangʼanywa.
“O da, ‘Size şunu söyleyeyim, kimde varsa ona daha çok verilecek. Ama kimde yoksa, kendisinde olan da elinden alınacak’ dedi.
27 Lakini wale adui zangu ambao hawakutaka mimi niwe mfalme juu yao. Waleteni hapa mkawaue mbele yangu.’”
‘Beni kral olarak istemeyen o düşmanlarıma gelince, onları buraya getirin ve gözümün önünde kılıçtan geçirin!’”
28 Baada ya Yesu kusema haya, alitangulia kupanda kwenda Yerusalemu.
İsa, bu sözleri söyledikten sonra önden yürüyerek Yeruşalim'e doğru ilerledi.
29 Naye alipokaribia Bethfage na Bethania kwenye mlima uitwao Mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili, akawaambia,
Zeytin Dağı'nın yamacındaki Beytfaci ile Beytanya'ya yaklaştığında iki öğrencisini önden gönderdi. Onlara, “Karşıdaki köye gidin” dedi, “Köye girince, üzerine daha hiç kimsenin binmediği, bağlı duran bir sıpa bulacaksınız. Onu çözüp bana getirin.
30 “Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu. Na mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana-punda amefungwa hapo, ambaye hajapandwa na mtu bado. Mfungueni, mkamlete hapa.
31 Kama mtu akiwauliza, ‘Mbona mnamfungua?’ Mwambieni, ‘Bwana anamhitaji.’”
Biri size, ‘Onu niçin çözüyorsunuz?’ diye sorarsa, ‘Rab'bin ona ihtiyacı var’ dersiniz.”
32 Wale waliotumwa wakaenda, wakakuta kila kitu kama vile Yesu alivyokuwa amewaambia.
Gönderilen öğrenciler gittiler, her şeyi İsa'nın kendilerine anlattığı gibi buldular.
33 Walipokuwa wanamfungua yule mwana-punda, wenyewe wakawauliza, “Mbona mnamfungua huyo mwana-punda?”
Sıpayı çözerlerken hayvanın sahipleri onlara, “Sıpayı niye çözüyorsunuz?” dediler.
34 Wale wanafunzi wakajibu, “Bwana anamhitaji.”
Onlar da, “Rab'bin ona ihtiyacı var” karşılığını verdiler.
35 Wakamleta kwa Yesu, nao baada ya kutandika mavazi yao juu ya huyo mwana-punda, wakampandisha Yesu juu yake.
Sıpayı İsa'ya getirdiler, üzerine kendi giysilerini atarak İsa'yı üstüne bindirdiler.
36 Alipokuwa akienda akiwa amempanda, watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
İsa ilerlerken halk, giysilerini yola seriyordu.
37 Alipokaribia mahali yanapoanzia materemko ya Mlima wa Mizeituni, umati wote wa wafuasi wake wakaanza kumsifu Mungu kwa furaha kwa sauti kuu kwa ajili ya matendo yote ya miujiza waliyoyaona. Wakasema:
İsa Zeytin Dağı'ndan aşağı inen yola yaklaştığı sırada, öğrencilerinden oluşan kalabalığın tümü, görmüş oldukları bütün mucizelerden ötürü, sevinç içinde yüksek sesle Tanrı'yı övmeye başladılar.
38 “Amebarikiwa Mfalme ajaye kwa Jina la Bwana!” “Amani mbinguni na utukufu huko juu sana.”
“Rab'bin adıyla gelen Kral'a övgüler olsun! Gökte esenlik, en yücelerde yücelik olsun!” diyorlardı.
39 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwamo miongoni mwa ule umati wa watu wakamwambia, “Mwalimu, waamuru wanafunzi wako wanyamaze.”
Kalabalığın içinden bazı Ferisiler O'na, “Öğretmen, öğrencilerini sustur!” dediler.
40 Yesu akawajibu, “Nawaambia ninyi, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapiga kelele.”
İsa, “Size şunu söyleyeyim, bunlar susacak olsa, taşlar bağıracaktır!” diye karşılık verdi.
41 Alipokaribia Yerusalemu na kuuona mji, aliulilia,
İsa Yeruşalim'e yaklaşıp kenti görünce ağladı.
42 akisema, “Laiti ungalijua hata wewe leo yale ambayo yangeleta amani, lakini sasa yamefichika machoni pako.
“Keşke bugün sen de esenliğe giden yolu bilseydin” dedi. “Ama şimdilik bu senin gözlerinden gizlendi.
43 Hakika siku zinakujia, ambazo adui zako watakuzingira, nao watakuzunguka pande zote na kukuzuilia ndani.
Senin için öyle günler gelecek ki, düşmanların seni setlerle çevirecek, kuşatıp her yandan sıkıştıracaklar.
44 Watakuponda chini, wewe na watoto walioko ndani ya kuta zako. Nao hawataacha hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu hukutambua wakati wa kujiliwa kwako.”
Seni de, bağrındaki çocukları da yere çalacaklar. Sende taş üstünde taş bırakmayacaklar. Çünkü Tanrı'nın senin yardımına geldiği zamanı farketmedin.”
45 Ndipo akaingia eneo la Hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza vitu humo.
Sonra İsa tapınağın avlusuna girerek satıcıları dışarı kovmaya başladı.
46 Naye akawaambia, “Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,’ lakini ninyi mmeifanya kuwa ‘pango la wanyangʼanyi.’”
Onlara, “‘Evim dua evi olacak’ diye yazılmıştır. Ama siz onu haydut inine çevirdiniz” dedi.
47 Kila siku alikuwa akifundisha Hekaluni. Lakini viongozi wa makuhani, walimu wa sheria na viongozi wa watu walikuwa wakitafuta njia ili kumuua.
İsa her gün tapınakta öğretiyordu. Başkâhinler, din bilginleri ve halkın ileri gelenleri ise O'nu yok etmek istiyor, ama bunu nasıl yapacaklarını bilemiyorlardı. Çünkü bütün halk O'nu can kulağıyla dinliyordu.
48 Lakini hawakupata nafasi kwa sababu watu wote walimfuata wakiyasikiliza maneno yake kwa usikivu mwingi.