< Luka 19 >
1 Yesu akaingia Yeriko, naye alikuwa anapita katikati ya huo mji.
Isusu auntrat ăn Jerihon. Pănd jel atrikut p trgula,
2 Tazama, palikuwa na mtu mmoja mkuu wa watoza ushuru naye alikuwa tajiri, jina lake Zakayo.
afost ănklo unu om karje sa kimat Zakej. Jel irja glavni porezniku ăn aja regija d Rim š mult bogat om.
3 Yeye alikuwa akijitahidi kumwona Yesu ni mtu wa namna gani. Lakini kutokana na umati mkubwa wa watu hakuweza kwa sababu alikuwa mfupi wa kimo.
Apokušăt s vjadă p Isusu činje je jel, ali afost mik š nu putja s l vjadă pisti multă lumje.
4 Kwa hiyo akatangulia mbio mbele ya umati wa watu akapanda juu ya mkuyu ili amwone Yesu, kwa sababu angeipitia njia ile.
Jel daja adat fuga la intje s s urče p smokvă pănglă karje atribja Isusu s trjače s puată p ja s l vjadă.
5 Yesu alipofika pale chini ya huo mkuyu, akatazama juu, akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, kwa maana leo nitakuwa mgeni nyumbani kwako!”
Kănd Isusu ažuns pănla smokvă, sa ujtat ăn sus š ja zăs aluj: “Zakeju, majdată dătje ăn zos! Astăz mora s viuv la tinje ăn gostjamje.”
6 Hivyo Zakayo akashuka upesi, akamkaribisha Yesu nyumbani kwake kwa furaha kubwa.
Zakej majdată sa dat ăn zos š la primit p Isusu ăn gostjamje, tot bukurat.
7 Watu wote walipoona hivyo, wakaanza kunungʼunika wakisema, “Amekwenda kuwa mgeni wa ‘mtu mwenye dhambi.’”
Ali tuată lumja karje avizut aja ančiput s čakaljaskă: “Nu trjebje s pljače ăn gostjamje la omu rov!”
8 Lakini Zakayo akasimama na kumwambia Bwana, “Tazama, Bwana! Sasa hivi nusu ya mali yangu ninawapa maskini, nami kama nimemdhulumu mtu yeyote kitu chochote, nitamrudishia mara nne ya hicho kiwango.”
A maj ănklo Zakej saskulat š zăče alu Domnuluj Isusuluj: “Jakă pola d imanja amja dau alu lumjej karje je sărakă, a p tot ăla p karje la šălat s ji tork d patru vorj kăta amlat dăla jel.”
9 Ndipo Yesu akamwambia, “Leo, wokovu umeingia nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Abrahamu.
Isusu azăs p aja: “Astăz ăn kasasta avinjit spasjala k š omusta je prava sămănca alu Abraham!
10 Kwa maana Mwana wa Adamu amekuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.”
Jo, Bijatu alu Omuluj, amvinjit s kat š s spasăsk p lumja karje je purdută.”
11 Walipokuwa wanasikiliza haya, Yesu akaendelea kuwaambia mfano, kwa sababu alikuwa anakaribia Yerusalemu na watu walikuwa wakidhani ya kuwa Ufalme wa Mungu ulikuwa unakuja saa iyo hiyo.
Pănd lumje apus urjajke la Isusu, daja če irja la upruapje d Jeruzalem š jej agăndit k s cara alu Dimizov akuma s pojavjaštje, Isusu lja spus asta vorbă:
12 Hivyo akawaambia: “Mtu mmoja mwenye cheo kikubwa alisafiri kwenda nchi ya mbali ili akapokee madaraka ya kuwa mfalme, kisha arudi.
“Njeki om dăn familjije bună sa sprimit s putujaskă p dăpartje pămănt. Jel atribut s pljače ănklo s dobidjaskă vlastu dăla caru marje. Atunča s ăntuarče ăn pămăntu aluj s puată s vladjaskă ka caru.
13 Hivyo akawaita kumi miongoni mwa watumishi wake, na akawapa kila mmoja fungu la fedha. Akawaambia, ‘Fanyeni biashara na fedha hizi mpaka nitakaporudi.’
Majdată njego ča pljikat akimat p zjače argac aluj, adat alu tot usută kovanic d arđint š lja zăs: ‘Trgujic pănă god jo nu vinja.’
14 “Lakini raiya wa nchi yake walimchukia wakapeleka ujumbe na kusema, ‘Hatutaki huyu mtu awe mfalme wetu.’
Ali lumja d pămăntula aluj l mrza š atrimjes la caru alu marje p poslanikurlje s zăkă: ‘Nu vrjem jel s carujaskă p noj.’
15 “Hata hivyo alirudi akiwa amekwisha kupokea mamlaka ya ufalme, akawaita wale watumishi wake aliokuwa amewaachia fedha, ili afahamu ni faida kiasi gani kila mmoja wao aliyopata kwa kufanya biashara.
Ali jel adobidit vlastu s fije car. Š kănd sa tors akasă, azapovidit s kjamje p argacă alu karje jel adat banji. Avrut s štije kăt tot ăla zaradit d jel.
16 “Wa kwanza akaja na kusema, ‘Bwana, kutokana na fedha uliyoniachia, nimepata faida mara kumi zaidi.’
Prvi argat avinjit š zăče: ‘Gospodarulje amkoristit banjišta karje maj dat š afukut zaradă d zjače vorj maj mult.’
17 “Yule bwana akamjibu, ‘Umefanya vizuri mtumishi mwema! Kwa sababu umekuwa mwaminifu katika wajibu mdogo sana, nakupa mamlaka juu ya miji kumi.’
Zăče caru: ‘Bun lukru! Bun ješt argat. Daja ča fost vjeran ăn maj mikă, c dau s vladješt p zjače trgurj.’
18 “Wa pili naye akaja. Akasema, ‘Bwana, fedha yako imeleta faida mara tano zaidi.’
Altu argat avinjit š zăče: ‘Gospodarulje, amkoristit banjišta karje maj dat š afukut zaradă d još činč vorj maj mult.’
19 “Bwana wake akajibu, ‘Nakupa mamlaka juu ya miji mitano.’
Š p aja caru zăče: ‘Tu osă vladjaštje p činč trgurj.’
20 “Kisha akaja yule mtumishi mwingine, akasema, ‘Bwana, hii hapa fedha yako. Niliitunza vizuri kwenye kitambaa.
Ali aldă trje argat avinjit frzdă zaradă š ji zăče: ‘Gospodarulje, jakăc arđintu. Lam cănut skuns ăn maramică.
21 Nilikuogopa, kwa sababu wewe ni mtu mgumu. Unachukua ambapo hukuweka kitu, na unavuna mahali ambapo hukupanda kitu.’
Ma fost frikă d tinje daja če ješt strog om. Jaj tuată zaradă dăla ăla če alcă uložăt d tinje š căj tuată bugacija dăla jej karje lukrizat d tinje.’
22 “Bwana wake akamjibu, ‘Nitakuhukumu kwa maneno yako mwenyewe, wewe mtumishi mwovu! Kama ulifahamu kwamba mimi ni mtu mgumu, nichukuaye mahali ambapo sikuweka kitu na kuvuna mahali ambapo sikupanda,
Caru ja zăs: ‘Argatulje alu rov! C sudjesk p aja ča zăs tu. Tu zăč k sănt strog. Tu zăč jo jav tuată zarada dăla ăla če alcă auložăt d minje š jo căv tuată bugacija dăla jej karje lukrizat d minje!
23 kwa nini basi hukuweka fedha zangu kwa watoa riba, ili nitakaporudi nichukue iliyo yangu na riba yake?’
Dăče atunča na pus banji alji mje p bankă? Aša barem adobidja kamatje.’
24 “Ndipo akawaambia wale waliokuwa wamesimama karibu, ‘Mnyangʼanyeni fungu lake la fedha, mkampe yule mwenye kumi.’
Atunča caru zăče alu lumje karje afost aiča upruapje: ‘Lăcăj dăla jel usută kovanic d arđint š dăcăj alu ăla karje zaradit zjače vorj maj mult!’
25 “Wakamwambia, ‘Bwana, mbona; tayari anayo mafungu kumi!’
Jej azăs: ‘Ali, gospodarulje, jel arje mij kovanic d arđint!’
26 “Akawajibu, ‘Nawaambia kwamba kila aliye na kitu, ataongezewa. Lakini yule asiye na kitu, hata alicho nacho atanyangʼanywa.
Caru azăs, ‘Istina je tot ăla karje koristjaštje binilje aja ča dobidit, osă dobidjaskă još maj mult, a toc karje nu koristjaštje binilje aja ča dobidit, osă s s ja š aja če arje.
27 Lakini wale adui zangu ambao hawakutaka mimi niwe mfalme juu yao. Waleteni hapa mkawaue mbele yangu.’”
Ali ălja dušmani alji mjej, karje na vurut s lji fiuv caru, dučecălje aiča š lji umurăc la intja amja.’”
28 Baada ya Yesu kusema haya, alitangulia kupanda kwenda Yerusalemu.
Dăpă aja če Isusu azăs, nastavit s pljače la intja alor kătri Jeruzalem.
29 Naye alipokaribia Bethfage na Bethania kwenye mlima uitwao Mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili, akawaambia,
Kănd avinjit la upruapje d saturj Betfaga š Betanija maj upruapje p djal Maslina, atrimjes la intje p doj učenikurj.
30 “Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu. Na mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana-punda amefungwa hapo, ambaye hajapandwa na mtu bado. Mfungueni, mkamlete hapa.
Lja zăs: “Fuđic ăn satula la intja avuastră. Š čim untrăc, osă vidjec p magaracu alu tănăr karje je ljigat karje nimilja nu la jahit. Dizljigăcălăj š dučecălăj aiča.
31 Kama mtu akiwauliza, ‘Mbona mnamfungua?’ Mwambieni, ‘Bwana anamhitaji.’”
Akă ăntrijabă njeko p voj: ‘Dăče dizljigăc p magaracu alu tănăr?’ Zăčec samo: ‘Trjebje alu Domnuluj.’”
32 Wale waliotumwa wakaenda, wakakuta kila kitu kama vile Yesu alivyokuwa amewaambia.
Jej apljikat š angăsăt toto kum lja zăs Isusu.
33 Walipokuwa wanamfungua yule mwana-punda, wenyewe wakawauliza, “Mbona mnamfungua huyo mwana-punda?”
Pănd jej adizljigat, lumja alu činje magaracu lja tribat: “Dăče dizljigăc p magaracu alu tănăr?”
34 Wale wanafunzi wakajibu, “Bwana anamhitaji.”
Jej lja zăs: “Alu Domnuluj ăntrjabje.”
35 Wakamleta kwa Yesu, nao baada ya kutandika mavazi yao juu ya huyo mwana-punda, wakampandisha Yesu juu yake.
Jej adus p magaracu alu tănăr la Isusu š prebacăt pisti jel ogrtači alor š apus p Isusu p magarac s šagă.
36 Alipokuwa akienda akiwa amempanda, watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
Pănd Isusu pljika mulc lumje raširit alor ogrtačurlje p drum la intja alu Isusuluj s ji pokazaskă častu.
37 Alipokaribia mahali yanapoanzia materemko ya Mlima wa Mizeituni, umati wote wa wafuasi wake wakaanza kumsifu Mungu kwa furaha kwa sauti kuu kwa ajili ya matendo yote ya miujiza waliyoyaona. Wakasema:
Kănd Isusu sa približăt undje drumu s slubadje dăpă djal Maslina, učenikurj š mulcă lumje karje kridja ăn Isusu ančiput p tot glasu s s radujaskă š s slavjaskă p Dimizov d tuată čuda karje avizut če Isusu majdată afukut.
38 “Amebarikiwa Mfalme ajaye kwa Jina la Bwana!” “Amani mbinguni na utukufu huko juu sana.”
Jej rubja: “Blagoslovit p caru p karje Domnu atrimjes! Hvaljic p Dimizov karje dă miru! Slava alu Dimizov karje vladjaštje p čerj!”
39 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwamo miongoni mwa ule umati wa watu wakamwambia, “Mwalimu, waamuru wanafunzi wako wanyamaze.”
Ali njeki farizeji karje irja ănklo azăs: “Učiteljulje, zapovidjaštje alu učenikurlje alji tej s takă!”
40 Yesu akawajibu, “Nawaambia ninyi, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapiga kelele.”
Isusu zăče: “Akă jej osă takă, istina je, š buluvanji p tot glasu osă s radujaskă!”
41 Alipokaribia Yerusalemu na kuuona mji, aliulilia,
Kănd Isusu avinjit la upruapje la Jeruzalem š avizut trgu, plănđja dăpă lumjaja ăn trgula
42 akisema, “Laiti ungalijua hata wewe leo yale ambayo yangeleta amani, lakini sasa yamefichika machoni pako.
š azăs: “Kănd barem samo s štijec če vuavă osă adukă miru! Ali akuma je vuavă skuns.
43 Hakika siku zinakujia, ambazo adui zako watakuzingira, nao watakuzunguka pande zote na kukuzuilia ndani.
K vinje vrijamja kănd dušmani alji voštri s gradjaskă kulje pănglă zidu alu trguluj s vu napadjaskă d tuatje părcă, vuastja alor osă vu okuljaskă š nu putjec s fuđic.
44 Watakuponda chini, wewe na watoto walioko ndani ya kuta zako. Nao hawataacha hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu hukutambua wakati wa kujiliwa kwako.”
Nusă s lasă ăn trgu alu vostru nič unu buluvan p buluvan. Jej osă uništjaskă tot trgu alu vostru š tot čije ăn jel voj daja če na prepoznajit asta vrijamje kănd Dimizov p voj avinjit s vu spasaskă.”
45 Ndipo akaingia eneo la Hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza vitu humo.
Kănd auntrat ăn dvorištja alu Hramuluj, Isusu ančiput dăn jel s putirjaskă p tuată lumja karje ănklo vindje.
46 Naye akawaambia, “Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,’ lakini ninyi mmeifanya kuwa ‘pango la wanyangʼanyi.’”
Isusu lja zăs: “Skris je ăn Svăntă pismă: ‘Alu mjov Hramu s fije loku d rugală’, a voj pretvorit ăn lok undje s strănđe lopovi!”
47 Kila siku alikuwa akifundisha Hekaluni. Lakini viongozi wa makuhani, walimu wa sheria na viongozi wa watu walikuwa wakitafuta njia ili kumuua.
Dăpă aja Isusu tuată zuva ănvăca ăn dvorištja alu Hramuluj. Glavni popurlje š učitelji d zakonu alu Mojsije š alcă vođe alu židovilor s ujta kum s l apuče p Isusu š s l osudjaskă p muartje.
48 Lakini hawakupata nafasi kwa sababu watu wote walimfuata wakiyasikiliza maneno yake kwa usikivu mwingi.
Ali jej nu ja putut nimika s ji fakă daja če tot narodu upija tuată vorba karje Isusu rubja.