< Luka 19 >
1 Yesu akaingia Yeriko, naye alikuwa anapita katikati ya huo mji.
And he entered and was passing through Jericho.
2 Tazama, palikuwa na mtu mmoja mkuu wa watoza ushuru naye alikuwa tajiri, jina lake Zakayo.
And behold, a man called by name Zacchaeus; and he was a chief publican, and he was rich.
3 Yeye alikuwa akijitahidi kumwona Yesu ni mtu wa namna gani. Lakini kutokana na umati mkubwa wa watu hakuweza kwa sababu alikuwa mfupi wa kimo.
And he sought to see Jesus who he was; and could not for the crowd, because he was little of stature.
4 Kwa hiyo akatangulia mbio mbele ya umati wa watu akapanda juu ya mkuyu ili amwone Yesu, kwa sababu angeipitia njia ile.
And he ran on before, and climbed up into a sycomore tree to see him: for he was to pass that way.
5 Yesu alipofika pale chini ya huo mkuyu, akatazama juu, akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, kwa maana leo nitakuwa mgeni nyumbani kwako!”
And when Jesus came to the place, he looked up, and said unto him, Zacchaeus, make haste, and come down; for today I must abide at thy house.
6 Hivyo Zakayo akashuka upesi, akamkaribisha Yesu nyumbani kwake kwa furaha kubwa.
And he made haste, and came down, and received him joyfully.
7 Watu wote walipoona hivyo, wakaanza kunungʼunika wakisema, “Amekwenda kuwa mgeni wa ‘mtu mwenye dhambi.’”
And when they saw it, they all murmured, saying, He is gone in to lodge with a man that is a sinner.
8 Lakini Zakayo akasimama na kumwambia Bwana, “Tazama, Bwana! Sasa hivi nusu ya mali yangu ninawapa maskini, nami kama nimemdhulumu mtu yeyote kitu chochote, nitamrudishia mara nne ya hicho kiwango.”
And Zacchaeus stood, and said unto the Lord, Behold, Lord, the half of my goods I give to the poor; and if I have wrongfully exacted aught of any man, I restore fourfold.
9 Ndipo Yesu akamwambia, “Leo, wokovu umeingia nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Abrahamu.
And Jesus said unto him, Today is salvation come to this house, forasmuch as he also is a son of Abraham.
10 Kwa maana Mwana wa Adamu amekuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.”
For the Son of man came to seek and to save that which was lost.
11 Walipokuwa wanasikiliza haya, Yesu akaendelea kuwaambia mfano, kwa sababu alikuwa anakaribia Yerusalemu na watu walikuwa wakidhani ya kuwa Ufalme wa Mungu ulikuwa unakuja saa iyo hiyo.
And as they heard these things, he added and spake a parable, because he was nigh to Jerusalem, and [because] they supposed that the kingdom of God was immediately to appear.
12 Hivyo akawaambia: “Mtu mmoja mwenye cheo kikubwa alisafiri kwenda nchi ya mbali ili akapokee madaraka ya kuwa mfalme, kisha arudi.
He said therefore, A certain nobleman went into a far country, to receive for himself a kingdom, and to return.
13 Hivyo akawaita kumi miongoni mwa watumishi wake, na akawapa kila mmoja fungu la fedha. Akawaambia, ‘Fanyeni biashara na fedha hizi mpaka nitakaporudi.’
And he called ten servants of his, and gave them ten pounds, and said unto them, Trade ye [herewith] till I come.
14 “Lakini raiya wa nchi yake walimchukia wakapeleka ujumbe na kusema, ‘Hatutaki huyu mtu awe mfalme wetu.’
But his citizens hated him, and sent an ambassage after him, saying, We will not that this man reign over us.
15 “Hata hivyo alirudi akiwa amekwisha kupokea mamlaka ya ufalme, akawaita wale watumishi wake aliokuwa amewaachia fedha, ili afahamu ni faida kiasi gani kila mmoja wao aliyopata kwa kufanya biashara.
And it came to pass, when he was come back again, having received the kingdom, that he commanded these servants, unto whom he had given the money, to be called to him, that he might know what they had gained by trading.
16 “Wa kwanza akaja na kusema, ‘Bwana, kutokana na fedha uliyoniachia, nimepata faida mara kumi zaidi.’
And the first came before him, saying, Lord, thy pound hath made ten pounds more.
17 “Yule bwana akamjibu, ‘Umefanya vizuri mtumishi mwema! Kwa sababu umekuwa mwaminifu katika wajibu mdogo sana, nakupa mamlaka juu ya miji kumi.’
And he said unto him, Well done, thou good servant: because thou wast found faithful in a very little, have thou authority over ten cities.
18 “Wa pili naye akaja. Akasema, ‘Bwana, fedha yako imeleta faida mara tano zaidi.’
And the second came, saying, Thy pound, Lord, hath made five pounds.
19 “Bwana wake akajibu, ‘Nakupa mamlaka juu ya miji mitano.’
And he said unto him also, Be thou also over five cities.
20 “Kisha akaja yule mtumishi mwingine, akasema, ‘Bwana, hii hapa fedha yako. Niliitunza vizuri kwenye kitambaa.
And another came, saying, Lord, behold, [here is] thy pound, which I kept laid up in a napkin:
21 Nilikuogopa, kwa sababu wewe ni mtu mgumu. Unachukua ambapo hukuweka kitu, na unavuna mahali ambapo hukupanda kitu.’
for I feared thee, because thou art an austere man: thou takest up that thou layedst not down, and reapest that thou didst not sow.
22 “Bwana wake akamjibu, ‘Nitakuhukumu kwa maneno yako mwenyewe, wewe mtumishi mwovu! Kama ulifahamu kwamba mimi ni mtu mgumu, nichukuaye mahali ambapo sikuweka kitu na kuvuna mahali ambapo sikupanda,
He saith unto him, Out of thine own mouth will I judge thee, thou wicked servant. Thou knewest that I am an austere man, taking up that I laid not down, and reaping that I did not sow;
23 kwa nini basi hukuweka fedha zangu kwa watoa riba, ili nitakaporudi nichukue iliyo yangu na riba yake?’
then wherefore gavest thou not my money into the bank, and I at my coming should have required it with interest?
24 “Ndipo akawaambia wale waliokuwa wamesimama karibu, ‘Mnyangʼanyeni fungu lake la fedha, mkampe yule mwenye kumi.’
And he said unto them that stood by, Take away from him the pound, and give it unto him that hath the ten pounds.
25 “Wakamwambia, ‘Bwana, mbona; tayari anayo mafungu kumi!’
And they said unto him, Lord, he hath ten pounds.
26 “Akawajibu, ‘Nawaambia kwamba kila aliye na kitu, ataongezewa. Lakini yule asiye na kitu, hata alicho nacho atanyangʼanywa.
I say unto you, that unto every one that hath shall be given; but from him that hath not, even that which he hath shall be taken away from him.
27 Lakini wale adui zangu ambao hawakutaka mimi niwe mfalme juu yao. Waleteni hapa mkawaue mbele yangu.’”
Howbeit these mine enemies, which would not that I should reign over them, bring hither, and slay them before me.
28 Baada ya Yesu kusema haya, alitangulia kupanda kwenda Yerusalemu.
And when he had thus spoken, he went on before, going up to Jerusalem.
29 Naye alipokaribia Bethfage na Bethania kwenye mlima uitwao Mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili, akawaambia,
And it came to pass, when he drew nigh unto Bethphage and Bethany, at the mount that is called [the mount] of Olives, he sent two of the disciples,
30 “Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu. Na mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana-punda amefungwa hapo, ambaye hajapandwa na mtu bado. Mfungueni, mkamlete hapa.
saying, Go your way into the village over against [you]; in the which as ye enter ye shall find a colt tied, whereon no man ever yet sat: loose him, and bring him.
31 Kama mtu akiwauliza, ‘Mbona mnamfungua?’ Mwambieni, ‘Bwana anamhitaji.’”
And if any one ask you, Why do ye loose him? thus shall ye say, The Lord hath need of him.
32 Wale waliotumwa wakaenda, wakakuta kila kitu kama vile Yesu alivyokuwa amewaambia.
And they that were sent went away, and found even as he had said unto them.
33 Walipokuwa wanamfungua yule mwana-punda, wenyewe wakawauliza, “Mbona mnamfungua huyo mwana-punda?”
And as they were loosing the colt, the owners thereof said unto them, Why loose ye the colt?
34 Wale wanafunzi wakajibu, “Bwana anamhitaji.”
And they said, The Lord hath need of him.
35 Wakamleta kwa Yesu, nao baada ya kutandika mavazi yao juu ya huyo mwana-punda, wakampandisha Yesu juu yake.
And they brought him to Jesus: and they threw their garments upon the colt, and set Jesus thereon.
36 Alipokuwa akienda akiwa amempanda, watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
And as he went, they spread their garments in the way.
37 Alipokaribia mahali yanapoanzia materemko ya Mlima wa Mizeituni, umati wote wa wafuasi wake wakaanza kumsifu Mungu kwa furaha kwa sauti kuu kwa ajili ya matendo yote ya miujiza waliyoyaona. Wakasema:
And as he was now drawing nigh, [even] at the descent of the mount of Olives, the whole multitude of the disciples began to rejoice and praise God with a loud voice for all the mighty works which they had seen;
38 “Amebarikiwa Mfalme ajaye kwa Jina la Bwana!” “Amani mbinguni na utukufu huko juu sana.”
saying, Blessed [is] the King that cometh in the name of the Lord: peace in heaven, and glory in the highest.
39 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwamo miongoni mwa ule umati wa watu wakamwambia, “Mwalimu, waamuru wanafunzi wako wanyamaze.”
And some of the Pharisees from the multitude said unto him, Master, rebuke thy disciples.
40 Yesu akawajibu, “Nawaambia ninyi, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapiga kelele.”
And he answered and said, I tell you that, if these shall hold their peace, the stones will cry out.
41 Alipokaribia Yerusalemu na kuuona mji, aliulilia,
And when he drew nigh, he saw the city and wept over it,
42 akisema, “Laiti ungalijua hata wewe leo yale ambayo yangeleta amani, lakini sasa yamefichika machoni pako.
saying, If thou hadst known in this day, even thou, the things which belong unto peace! but now they are hid from thine eyes.
43 Hakika siku zinakujia, ambazo adui zako watakuzingira, nao watakuzunguka pande zote na kukuzuilia ndani.
For the days shall come upon thee, when thine enemies shall cast up a bank about thee, and compass thee round, and keep thee in on every side,
44 Watakuponda chini, wewe na watoto walioko ndani ya kuta zako. Nao hawataacha hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu hukutambua wakati wa kujiliwa kwako.”
and shall dash thee to the ground, and thy children within thee; and they shall not leave in thee one stone upon another; because thou knewest not the time of thy visitation.
45 Ndipo akaingia eneo la Hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza vitu humo.
And he entered into the temple, and began to cast out them that sold,
46 Naye akawaambia, “Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,’ lakini ninyi mmeifanya kuwa ‘pango la wanyangʼanyi.’”
saying unto them, It is written, And my house shall be a house of prayer: but ye have made it a den of robbers.
47 Kila siku alikuwa akifundisha Hekaluni. Lakini viongozi wa makuhani, walimu wa sheria na viongozi wa watu walikuwa wakitafuta njia ili kumuua.
And he was teaching daily in the temple. But the chief priests and the scribes and the principal men of the people sought to destroy him:
48 Lakini hawakupata nafasi kwa sababu watu wote walimfuata wakiyasikiliza maneno yake kwa usikivu mwingi.
and they could not find what they might do; for the people all hung upon him, listening.