< Luka 19 >
1 Yesu akaingia Yeriko, naye alikuwa anapita katikati ya huo mji.
And he entered and was passing through Jericho.
2 Tazama, palikuwa na mtu mmoja mkuu wa watoza ushuru naye alikuwa tajiri, jina lake Zakayo.
And lo! a man named Zacchaeus; and he was a chief publican, and he was rich.
3 Yeye alikuwa akijitahidi kumwona Yesu ni mtu wa namna gani. Lakini kutokana na umati mkubwa wa watu hakuweza kwa sababu alikuwa mfupi wa kimo.
And he sought to see Jesus, what sort of man he was; and he could not on account of the multitude; because he was small of stature.
4 Kwa hiyo akatangulia mbio mbele ya umati wa watu akapanda juu ya mkuyu ili amwone Yesu, kwa sababu angeipitia njia ile.
And he ran on before, and climbed up a sycamore-tree to see him; for he was to pass that way.
5 Yesu alipofika pale chini ya huo mkuyu, akatazama juu, akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, kwa maana leo nitakuwa mgeni nyumbani kwako!”
And when Jesus came to the place, he looked up, and said to him, Zacchaeas, make haste and come down; for today I must abide at thy house.
6 Hivyo Zakayo akashuka upesi, akamkaribisha Yesu nyumbani kwake kwa furaha kubwa.
And he made haste and came down, and received him joyfully.
7 Watu wote walipoona hivyo, wakaanza kunungʼunika wakisema, “Amekwenda kuwa mgeni wa ‘mtu mwenye dhambi.’”
And when they saw it, they all murmured, saying, He hath gone in to be the guest of a sinner.
8 Lakini Zakayo akasimama na kumwambia Bwana, “Tazama, Bwana! Sasa hivi nusu ya mali yangu ninawapa maskini, nami kama nimemdhulumu mtu yeyote kitu chochote, nitamrudishia mara nne ya hicho kiwango.”
And Zacchaeus stood up, and said to the Lord, Behold, Lord, the half of my goods I give to the poor; and if I have taken anything from any one by false representation, I restore him four-fold.
9 Ndipo Yesu akamwambia, “Leo, wokovu umeingia nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Abrahamu.
And Jesus said to him, This day hath salvation come to this house, inasmuch as he also is a son of Abraham;
10 Kwa maana Mwana wa Adamu amekuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.”
for the Son of man came to seek and to save that which was lost.
11 Walipokuwa wanasikiliza haya, Yesu akaendelea kuwaambia mfano, kwa sababu alikuwa anakaribia Yerusalemu na watu walikuwa wakidhani ya kuwa Ufalme wa Mungu ulikuwa unakuja saa iyo hiyo.
And while they were hearing these things, he proceeded and spoke a parable, because he was near to Jerusalem, and they thought that the kingdom of God would immediately appear.
12 Hivyo akawaambia: “Mtu mmoja mwenye cheo kikubwa alisafiri kwenda nchi ya mbali ili akapokee madaraka ya kuwa mfalme, kisha arudi.
He said therefore, A certain nobleman went into a far country to receive for himself a kingdom, and to return.
13 Hivyo akawaita kumi miongoni mwa watumishi wake, na akawapa kila mmoja fungu la fedha. Akawaambia, ‘Fanyeni biashara na fedha hizi mpaka nitakaporudi.’
And he called his ten servants, and gave them ten pounds, and said to them, Trade with these, till I come.
14 “Lakini raiya wa nchi yake walimchukia wakapeleka ujumbe na kusema, ‘Hatutaki huyu mtu awe mfalme wetu.’
But his citizens hated him, and sent an embassy after him, saying, We will not have this man to reign over us.
15 “Hata hivyo alirudi akiwa amekwisha kupokea mamlaka ya ufalme, akawaita wale watumishi wake aliokuwa amewaachia fedha, ili afahamu ni faida kiasi gani kila mmoja wao aliyopata kwa kufanya biashara.
And it came to pass, when he had returned, having received the kingdom, that he commanded these servants to whom he had given the money to be called to him, that he might know what each had gained by trading.
16 “Wa kwanza akaja na kusema, ‘Bwana, kutokana na fedha uliyoniachia, nimepata faida mara kumi zaidi.’
And the first came, saying, Lord, thy pound hath gained ten pounds.
17 “Yule bwana akamjibu, ‘Umefanya vizuri mtumishi mwema! Kwa sababu umekuwa mwaminifu katika wajibu mdogo sana, nakupa mamlaka juu ya miji kumi.’
And he said to him, Well done, good servant! because thou hast been faithful in a very little, have authority over ten cities.
18 “Wa pili naye akaja. Akasema, ‘Bwana, fedha yako imeleta faida mara tano zaidi.’
And the second came, saying, Lord, thy pound hath gained five pounds.
19 “Bwana wake akajibu, ‘Nakupa mamlaka juu ya miji mitano.’
And he said also to this servant, And be thou over five cities.
20 “Kisha akaja yule mtumishi mwingine, akasema, ‘Bwana, hii hapa fedha yako. Niliitunza vizuri kwenye kitambaa.
And another came, saying, Lord, behold thy pound, which I have kept laid up in a napkin.
21 Nilikuogopa, kwa sababu wewe ni mtu mgumu. Unachukua ambapo hukuweka kitu, na unavuna mahali ambapo hukupanda kitu.’
For I feared thee, because thou art a harsh man; thou takest up what thou didst not lay down, and reapest what thou didst not sow.
22 “Bwana wake akamjibu, ‘Nitakuhukumu kwa maneno yako mwenyewe, wewe mtumishi mwovu! Kama ulifahamu kwamba mimi ni mtu mgumu, nichukuaye mahali ambapo sikuweka kitu na kuvuna mahali ambapo sikupanda,
He saith to him, Out of thy mouth will I judge thee, wicked servant! thou knewest that I was a harsh man, taking up what I laid not down, and reaping what I did not sow;
23 kwa nini basi hukuweka fedha zangu kwa watoa riba, ili nitakaporudi nichukue iliyo yangu na riba yake?’
why then didst thou not put my money into a bank? Then I at my coming might have received it back with interest.
24 “Ndipo akawaambia wale waliokuwa wamesimama karibu, ‘Mnyangʼanyeni fungu lake la fedha, mkampe yule mwenye kumi.’
And he said to them that stood by, Take from him the pound, and give it to him that hath the ten pounds.
25 “Wakamwambia, ‘Bwana, mbona; tayari anayo mafungu kumi!’
(And they said to him, He hath ten pounds, Lord.)
26 “Akawajibu, ‘Nawaambia kwamba kila aliye na kitu, ataongezewa. Lakini yule asiye na kitu, hata alicho nacho atanyangʼanywa.
I say to you, that to every one who hath, will be given; but from him that hath not, even what he hath will be taken away.
27 Lakini wale adui zangu ambao hawakutaka mimi niwe mfalme juu yao. Waleteni hapa mkawaue mbele yangu.’”
But as for those enemies of mine, who would not that I should reign over them, bring them here, and slay them before me.
28 Baada ya Yesu kusema haya, alitangulia kupanda kwenda Yerusalemu.
And when he had thus spoken, he went forward, going up to Jerusalem.
29 Naye alipokaribia Bethfage na Bethania kwenye mlima uitwao Mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili, akawaambia,
And it came to pass, as he drew near to Bethphage and Bethany, at the mount called the Mount of Olives, he sent two of his disciples,
30 “Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu. Na mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana-punda amefungwa hapo, ambaye hajapandwa na mtu bado. Mfungueni, mkamlete hapa.
saying, Go to the village over against us; on entering which ye will find a colt tied, whereon no man ever sat; and loose, and bring it.
31 Kama mtu akiwauliza, ‘Mbona mnamfungua?’ Mwambieni, ‘Bwana anamhitaji.’”
And if any one ask you, Why are ye loosing it? ye shall say thus, The Lord hath need of it.
32 Wale waliotumwa wakaenda, wakakuta kila kitu kama vile Yesu alivyokuwa amewaambia.
And they who were sent went and found just as he told them.
33 Walipokuwa wanamfungua yule mwana-punda, wenyewe wakawauliza, “Mbona mnamfungua huyo mwana-punda?”
And as they were loosing the colt, its owners said to them, Why are ye loosing the colt?
34 Wale wanafunzi wakajibu, “Bwana anamhitaji.”
And they said, The Lord hath need of it.
35 Wakamleta kwa Yesu, nao baada ya kutandika mavazi yao juu ya huyo mwana-punda, wakampandisha Yesu juu yake.
And they brought it to Jesus; and having thrown their garments on the colt, they set Jesus thereon.
36 Alipokuwa akienda akiwa amempanda, watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
And as he went on, they spread their garments in the road.
37 Alipokaribia mahali yanapoanzia materemko ya Mlima wa Mizeituni, umati wote wa wafuasi wake wakaanza kumsifu Mungu kwa furaha kwa sauti kuu kwa ajili ya matendo yote ya miujiza waliyoyaona. Wakasema:
And as he was drawing near, just at the descent of the Mount of Olives, the whole multitude of the disciples began to rejoice and praise God with a loud voice for all the miracles which they had seen;
38 “Amebarikiwa Mfalme ajaye kwa Jina la Bwana!” “Amani mbinguni na utukufu huko juu sana.”
saying, Blessed be the King in the name of the Lord! Peace in heaven, and glory in the highest heavens!
39 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwamo miongoni mwa ule umati wa watu wakamwambia, “Mwalimu, waamuru wanafunzi wako wanyamaze.”
And some of the Pharisees from among the multitude said to him, Teacher, rebuke thy disciples.
40 Yesu akawajibu, “Nawaambia ninyi, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapiga kelele.”
And he answering said, I tell you, that if these are silent, the stones will cry out.
41 Alipokaribia Yerusalemu na kuuona mji, aliulilia,
And when he came near, as he beheld the city, he wept over it,
42 akisema, “Laiti ungalijua hata wewe leo yale ambayo yangeleta amani, lakini sasa yamefichika machoni pako.
saying, If thou hadst known, even thou, and that in this thy day, the things that concern thy peace! but now they are hidden from thine eyes.
43 Hakika siku zinakujia, ambazo adui zako watakuzingira, nao watakuzunguka pande zote na kukuzuilia ndani.
For the days will come upon thee, when thine enemies will cast up a mound about thee, and compass thee round, and shut thee in on every side,
44 Watakuponda chini, wewe na watoto walioko ndani ya kuta zako. Nao hawataacha hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu hukutambua wakati wa kujiliwa kwako.”
and will level thee with the ground, and thy children within thee; and they will not leave in thee one stone upon another; because thou knewest not the time of thy visitation.
45 Ndipo akaingia eneo la Hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza vitu humo.
And entering the temple, he began to cast out those who sold,
46 Naye akawaambia, “Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,’ lakini ninyi mmeifanya kuwa ‘pango la wanyangʼanyi.’”
saying to them, It is written, “And my house shall be a house of prayer; but ye have made it a den of robbers.”
47 Kila siku alikuwa akifundisha Hekaluni. Lakini viongozi wa makuhani, walimu wa sheria na viongozi wa watu walikuwa wakitafuta njia ili kumuua.
And he was teaching daily in the temple; but the chief priests, and the scribes, and the leading men of the people sought to destroy him.
48 Lakini hawakupata nafasi kwa sababu watu wote walimfuata wakiyasikiliza maneno yake kwa usikivu mwingi.
And they could not find an opportunity of doing any thing; for all the people hung upon him, listening.