< Luka 19 >
1 Yesu akaingia Yeriko, naye alikuwa anapita katikati ya huo mji.
穌進了耶里哥,正進過的時候,
2 Tazama, palikuwa na mtu mmoja mkuu wa watoza ushuru naye alikuwa tajiri, jina lake Zakayo.
有一個人,名叫匝凱,他原是稅吏長,是個富有的人。
3 Yeye alikuwa akijitahidi kumwona Yesu ni mtu wa namna gani. Lakini kutokana na umati mkubwa wa watu hakuweza kwa sababu alikuwa mfupi wa kimo.
他想要看看耶穌是什麼人;但由於人多,不能看見,因為他身材短小。
4 Kwa hiyo akatangulia mbio mbele ya umati wa watu akapanda juu ya mkuyu ili amwone Yesu, kwa sababu angeipitia njia ile.
於是他往前奔跑,攀上了一棵野桑樹,要看看耶穌,因為耶穌就要從那裏經過。
5 Yesu alipofika pale chini ya huo mkuyu, akatazama juu, akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, kwa maana leo nitakuwa mgeni nyumbani kwako!”
耶穌來到那地方,抬頭一看,對他說:「匝凱,你快下來!因為我今天必須往在你家中。」
6 Hivyo Zakayo akashuka upesi, akamkaribisha Yesu nyumbani kwake kwa furaha kubwa.
他便趕快下來,喜悅地款留耶穌。
7 Watu wote walipoona hivyo, wakaanza kunungʼunika wakisema, “Amekwenda kuwa mgeni wa ‘mtu mwenye dhambi.’”
眾人見了,都竊竊私議說:「他竟到有罪的人那裏投宿。」
8 Lakini Zakayo akasimama na kumwambia Bwana, “Tazama, Bwana! Sasa hivi nusu ya mali yangu ninawapa maskini, nami kama nimemdhulumu mtu yeyote kitu chochote, nitamrudishia mara nne ya hicho kiwango.”
匝凱站起來對主說:「主,你看,我把我一半的財物施捨給窮人;我如果欺騙過誰,我就以四倍賠償。」
9 Ndipo Yesu akamwambia, “Leo, wokovu umeingia nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Abrahamu.
耶穌對他說:「今天救恩來到了這一家,因為他也是亞巴郎之子。
10 Kwa maana Mwana wa Adamu amekuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.”
因為人子來,是為尋找及拯救迷失了的人。」
11 Walipokuwa wanasikiliza haya, Yesu akaendelea kuwaambia mfano, kwa sababu alikuwa anakaribia Yerusalemu na watu walikuwa wakidhani ya kuwa Ufalme wa Mungu ulikuwa unakuja saa iyo hiyo.
眾人聽這話的時候,耶穌因為已臨近耶路撒冷,而且他們都以為天主的國快要出現,遂設了一個比喻說:
12 Hivyo akawaambia: “Mtu mmoja mwenye cheo kikubwa alisafiri kwenda nchi ya mbali ili akapokee madaraka ya kuwa mfalme, kisha arudi.
「有一個貴人起身到遠方去,為取得了王位再回來。
13 Hivyo akawaita kumi miongoni mwa watumishi wake, na akawapa kila mmoja fungu la fedha. Akawaambia, ‘Fanyeni biashara na fedha hizi mpaka nitakaporudi.’
他將自己的十個僕人叫來,交給他們十個「米納」,並囑咐說:你們拿去做生意,直到我回來。
14 “Lakini raiya wa nchi yake walimchukia wakapeleka ujumbe na kusema, ‘Hatutaki huyu mtu awe mfalme wetu.’
他本國的人,一向懷恨他,遂在他在後面派代表說:我們不願意這人為王統治我們。
15 “Hata hivyo alirudi akiwa amekwisha kupokea mamlaka ya ufalme, akawaita wale watumishi wake aliokuwa amewaachia fedha, ili afahamu ni faida kiasi gani kila mmoja wao aliyopata kwa kufanya biashara.
他得了王位來以後,便傳令將那些領了他錢的僕人給他召來,想知道每個人做生意賺了多少。
16 “Wa kwanza akaja na kusema, ‘Bwana, kutokana na fedha uliyoniachia, nimepata faida mara kumi zaidi.’
第一前來對他說:主,你的那個「米納」賺了十個「米納」。
17 “Yule bwana akamjibu, ‘Umefanya vizuri mtumishi mwema! Kwa sababu umekuwa mwaminifu katika wajibu mdogo sana, nakupa mamlaka juu ya miji kumi.’
主人給他說:好,善僕!你既然在小事上忠信,你要有權掌管十座城。
18 “Wa pili naye akaja. Akasema, ‘Bwana, fedha yako imeleta faida mara tano zaidi.’
第二個前來說:主,你的那個「米納」賺了五個「米納」。
19 “Bwana wake akajibu, ‘Nakupa mamlaka juu ya miji mitano.’
主人也給給這人說:你也要掌管五座城。
20 “Kisha akaja yule mtumishi mwingine, akasema, ‘Bwana, hii hapa fedha yako. Niliitunza vizuri kwenye kitambaa.
另一個前來說:主,看,你那個「米納」,我收存在手巾裏。
21 Nilikuogopa, kwa sababu wewe ni mtu mgumu. Unachukua ambapo hukuweka kitu, na unavuna mahali ambapo hukupanda kitu.’
我一向害怕你,因為你是一個嚴厲的人:你沒有存放的,也要提取;沒有下種的,也要收割。
22 “Bwana wake akamjibu, ‘Nitakuhukumu kwa maneno yako mwenyewe, wewe mtumishi mwovu! Kama ulifahamu kwamba mimi ni mtu mgumu, nichukuaye mahali ambapo sikuweka kitu na kuvuna mahali ambapo sikupanda,
主人向說:惡僕,我就憑你的口供定你的罪。你不是知道失是嚴厲的人,沒有存放的,也要提取;沒有下種的,也要收割的嗎﹖
23 kwa nini basi hukuweka fedha zangu kwa watoa riba, ili nitakaporudi nichukue iliyo yangu na riba yake?’
為什麼你不把失的錢存於錢莊﹖待我回來時,我可以連本帶利取出來。
24 “Ndipo akawaambia wale waliokuwa wamesimama karibu, ‘Mnyangʼanyeni fungu lake la fedha, mkampe yule mwenye kumi.’
主人便向侍立左右人說:你們他那個「米納」奪過來,給那有十個的。
25 “Wakamwambia, ‘Bwana, mbona; tayari anayo mafungu kumi!’
他們向說:主,他已有十個「米納」了。
26 “Akawajibu, ‘Nawaambia kwamba kila aliye na kitu, ataongezewa. Lakini yule asiye na kitu, hata alicho nacho atanyangʼanywa.
我告訴你們:凡是有的,還要給他,那沒有的,連他所有的,也要從他奪去。
27 Lakini wale adui zangu ambao hawakutaka mimi niwe mfalme juu yao. Waleteni hapa mkawaue mbele yangu.’”
至於那些敵對我,不願意我作他們君王的人,你們把他押到這裏,在我在面前殺掉。」
28 Baada ya Yesu kusema haya, alitangulia kupanda kwenda Yerusalemu.
耶穌說了這些話,就領頭前行,上耶路撒冷去了。
29 Naye alipokaribia Bethfage na Bethania kwenye mlima uitwao Mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili, akawaambia,
及至臨近貝特法和伯達尼,在一座名叫橄欖那裏,耶穌派遺二個門徒說:
30 “Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu. Na mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana-punda amefungwa hapo, ambaye hajapandwa na mtu bado. Mfungueni, mkamlete hapa.
「你們往對面的村莊裏去,一進村,就會看見一匹拴著的驢駒,從來沒有人騎過,把牠解開,牽來。
31 Kama mtu akiwauliza, ‘Mbona mnamfungua?’ Mwambieni, ‘Bwana anamhitaji.’”
如果有人問你們說:你們為什麼解牠﹖你們要這樣說:主要用牠。」
32 Wale waliotumwa wakaenda, wakakuta kila kitu kama vile Yesu alivyokuwa amewaambia.
被派的人去了,所遇見的,正如對他們說過的一樣。
33 Walipokuwa wanamfungua yule mwana-punda, wenyewe wakawauliza, “Mbona mnamfungua huyo mwana-punda?”
他們正要解驢駒的時候,驢駒的主人對他們說:「你們為什麼解這驢駒﹖」
34 Wale wanafunzi wakajibu, “Bwana anamhitaji.”
他們說:「主要用牠。」
35 Wakamleta kwa Yesu, nao baada ya kutandika mavazi yao juu ya huyo mwana-punda, wakampandisha Yesu juu yake.
他們遂把驢駒牽到耶穌在跟前,把他們的外衣搭在驢駒上,扶耶穌騎上。
36 Alipokuwa akienda akiwa amempanda, watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
前行的時候,人們把自己的外衣舖在路上。
37 Alipokaribia mahali yanapoanzia materemko ya Mlima wa Mizeituni, umati wote wa wafuasi wake wakaanza kumsifu Mungu kwa furaha kwa sauti kuu kwa ajili ya matendo yote ya miujiza waliyoyaona. Wakasema:
當他們臨近橄欖山的下坡時,眾們徒為了所見過的一切奇能,都歡欣的大聲頌揚天主說:
38 “Amebarikiwa Mfalme ajaye kwa Jina la Bwana!” “Amani mbinguni na utukufu huko juu sana.”
「因上主之名而來的君王,應受讚頌!和平在天主,光榮於高天。」
39 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwamo miongoni mwa ule umati wa watu wakamwambia, “Mwalimu, waamuru wanafunzi wako wanyamaze.”
人群人有幾個法利賽人對耶穌說:「師傅,責斥你的門徒罷!」
40 Yesu akawajibu, “Nawaambia ninyi, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapiga kelele.”
耶穌回答說:「我告訴你們:這些人若不作聲,石頭就要喊叫了!」
41 Alipokaribia Yerusalemu na kuuona mji, aliulilia,
耶穌臨近的時候,望見京城,便哀哭她說:
42 akisema, “Laiti ungalijua hata wewe leo yale ambayo yangeleta amani, lakini sasa yamefichika machoni pako.
「恨不能在這一天,妳也知道有關妳平安的事;但這如今在妳眼中是隱藏的。
43 Hakika siku zinakujia, ambazo adui zako watakuzingira, nao watakuzunguka pande zote na kukuzuilia ndani.
的確,日子將臨於妳,妳的仇敵在妳四周築起壁壘,包圍妳,四面宭困妳;
44 Watakuponda chini, wewe na watoto walioko ndani ya kuta zako. Nao hawataacha hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu hukutambua wakati wa kujiliwa kwako.”
又要蕩平妳,及在妳內的子民,在妳內決不留一塊石頭在另一塊石頭上,因為妳沒有認識眷顧妳的時期。」
45 Ndipo akaingia eneo la Hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza vitu humo.
耶穌進了殿院,開始把買賣人趕出去。
46 Naye akawaambia, “Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,’ lakini ninyi mmeifanya kuwa ‘pango la wanyangʼanyi.’”
對他們說:「經上記載:我的殿宇應是祈禱之所,而你們意把它做了賊窩。」
47 Kila siku alikuwa akifundisha Hekaluni. Lakini viongozi wa makuhani, walimu wa sheria na viongozi wa watu walikuwa wakitafuta njia ili kumuua.
耶穌每天在聖殿內施教。司祭長及經師並人民的首領,設法要除掉祂,
48 Lakini hawakupata nafasi kwa sababu watu wote walimfuata wakiyasikiliza maneno yake kwa usikivu mwingi.
但是尋不出什麼辨法,因為眾百姓傾心聽祂。