< Luka 17 >
1 Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mambo yanayosababisha watu watende dhambi hayana budi kutukia. Lakini ole wake mtu yule anayeyasababisha.
耶稣又对门徒说:“诱惑不可避免,但那些传递诱惑之人有祸了!
2 Ingekuwa heri kama mtu huyo angefungiwa jiwe la kusagia shingoni na kutoswa baharini, kuliko kumsababisha mmojawapo wa hawa wadogo kutenda dhambi.
对这种人,最好把一块大磨石拴在他的脖子上,将他沉在海里,总比让这些儿童犯罪要好。
3 Kwa hiyo, jilindeni. “Kama ndugu yako akikukosea mwonye, naye akitubu, msamehe.
所以做每件事都要小心。如果你兄弟犯下罪行,要警告他。如果他幡然悔悟,要宽恕他。
4 Kama akikukosea mara saba kwa siku moja na mara saba kwa siku moja akaja kwako akisema, ‘Ninatubu,’ msamehe.”
就算他每天有七次用罪冒犯你,但又七次回来对你说:‘我真的很抱歉!’你也要宽恕他。”
5 Mitume wake wakamwambia Bwana, “Tuongezee imani.”
门徒对主说:“请帮助我们获得更多信心。”
6 Bwana akawajibu, “Kama mkiwa na imani ndogo kama punje ya haradali, mngeweza kuuambia mti huu wa mkuyu, ‘Ngʼoka ukaote baharini,’ nao ungewatii.
主回答:“即使你们的信心微小如一粒芥菜种,也能命令这棵桑树:‘把根拔起,自己栽到海里去!’它就会听你的命令。
7 “Ikiwa mmoja wenu ana mtumishi anayelima shambani au anayechunga kondoo, je, mtumishi huyo arudipo atamwambia, ‘Karibu hapa keti ule chakula?’
假设你有个仆人负责耕地或放羊,当他从田里回来,你是不是会对他说:‘快过来坐下吃饭’,
8 Je, badala yake, hatamwambia, ‘Niandalie chakula, nile, jifunge unitumikie ninapokula na kunywa; baadaye waweza kula na kunywa?’
不,你会这样说:‘给我准备饭菜,穿戴整齐来服侍我,你等我用晚餐后才能吃饭。’
9 Je, huyo mtu atamshukuru mtumishi huyo kwa kutimiza yale aliyoamriwa?
如果仆人做了主人吩咐的事,主人是否还要感谢他?不需要。
10 Vivyo hivyo nanyi mkiisha kufanya mliyoagizwa, semeni, ‘Sisi tu watumishi tusiostahili; tumefanya tu yale tuliyopaswa kufanya.’”
同样,你做了别人吩咐你做的事,只需说:‘我们不是最好的仆人,只是做了分内之事。’”
11 Yesu alipokuwa njiani akienda Yerusalemu, alipitia mpakani mwa Samaria na Galilaya.
耶稣继续向耶路撒冷走去,途径撒玛利亚和加利利的边境。
12 Alipokuwa akiingia kwenye kijiji kimoja, watu kumi waliokuwa na ukoma wakakutana naye. Wakasimama mbali,
他走进一个村庄,遇到了十个麻风病人站在远处。
13 wakapaza sauti, wakasema, “Yesu, Bwana, tuhurumie!”
他们大声喊:“耶稣,主啊,可怜可怜我们吧!”
14 Alipowaona akawaambia, “Nendeni mkajionyeshe kwa makuhani.” Nao walipokuwa njiani wakienda, wakatakasika.
耶稣看见他们就说:“去让祭司看看你们吧。”他们在见祭司的途中就痊愈了。
15 Mmoja wao alipoona kwamba amepona, akarudi kwa Yesu, akimsifu Mungu kwa sauti kuu.
其中一个人见自己痊愈,就回到耶稣面前大声颂赞上帝。
16 Akajitupa miguuni mwa Yesu akamshukuru. Yeye alikuwa Msamaria.
这个撒玛利亚人伏倒在耶稣脚前,感谢耶稣。
17 Yesu akauliza, “Je, hawakutakaswa wote kumi? Wako wapi wale wengine tisa?
耶稣说:“十个人都治愈了吗?其他九人在哪里?
18 Hakuna hata mmoja aliyeonekana kurudi ili kumshukuru Mungu isipokuwa huyu mgeni?”
除了这个异教徒,难道没有别人回来颂赞上帝吗?”
19 Yesu akamwambia, “Inuka na uende zako, imani yako imekuponya.”
耶稣就对他说:“起来走吧,你的信任治愈了你。”
20 Yesu alipoulizwa na Mafarisayo Ufalme wa Mungu utakuja lini, yeye akawajibu, “Ufalme wa Mungu hauji kwa kuchunguza kwa bidii,
有一次,法利赛人过来问耶稣上帝之国何时降临。他回答:“上帝之国降临之时,不会有任何让你看到的迹象。
21 wala watu hawatasema, ‘Huu hapa,’ au ‘Ule kule,’ kwa maana Ufalme wa Mungu umo ndani yenu.”
人们不会说:‘看,在这里’,或说:‘看,在那里’,因为上帝之国就在你们之中。”
22 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Wakati utafika ambapo mtatamani kuiona moja ya siku ya Mwana wa Adamu, lakini hamtaiona.
然后耶稣又对门徒说:“那个时刻快到了,就是你们渴望看到人子的日子,但你们其实看不到。
23 Watu watawaambia, ‘Yule kule!’ Au, ‘Huyu hapa!’ Msiwakimbilie.
有人会对你们说:‘看呐,他在那里。看呐,他在这里。’不要跑去追随他们。
24 Kwa maana kama vile umeme wa radi umulikavyo katika anga kuanzia mwisho mmoja hadi mwingine, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu katika siku yake.
当人子到来之际,会如闪电发出光亮,从天空的一侧到另一侧闪过,将天空点亮。
25 Lakini kwanza itampasa kuteseka katika mambo mengi na kukataliwa na kizazi hiki.
但首先他必须经受许多苦,被这个世界所抛弃。
26 “Kama ilivyokuwa siku za Noa, ndivyo itakavyokuwa katika siku za Mwana wa Adamu.
人子到来的时代,会像诺亚所面临的那一刻。
27 Watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka siku ile Noa alipoingia katika safina. Ndipo gharika ikaja na kuwaangamiza wote.
当时人们都在吃吃喝喝,忙着嫁娶,直到诺亚进入方舟的那一天,洪水到来,摧毁了一切。
28 “Ndivyo ilivyokuwa katika siku za Loti: Watu walikuwa wakila na kunywa, wakinunua na kuuza, wakilima na kujenga.
那一刻就像罗得所面临的时代。当时众人忙着吃吃喝喝,做买卖、种地或者盖房子。
29 Lakini siku ile Loti alipoondoka Sodoma, ikanyesha mvua ya moto na kiberiti kutoka mbinguni ukawaangamiza wote.
在罗得离开索多玛的那一天,天空落下火与硫磺,摧毁了一切。
30 “Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile Mwana wa Adamu atakapofunuliwa.
人子出现的那一天就是这样。
31 Siku hiyo, mtu yeyote aliye juu ya dari ya nyumba yake, hata vitu vyake vikiwa ndani ya hiyo nyumba, asishuke kuvichukua. Vivyo hivyo mtu aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua chochote.
到了那一天,如果你站在房顶,家当都在屋里,不要跑下去拿。如果你在田里,不要回家。
32 Mkumbukeni mke wa Loti!
记着罗得妻子的教训。
33 Mtu yeyote anayejaribu kuyaokoa maisha yake atayapoteza, na yeyote atakayeyapoteza maisha yake atayaokoa.
如果你想抓住生命,就会失去生命,如果你失去生命,就会拯救生命。
34 Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa wamelala kitanda kimoja; naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa.
告诉你们吧,在那个时刻,如果一张床上躺着两个人,一人会被接走,一个会被留下。
35 Wanawake wawili watakuwa wanasaga nafaka pamoja; naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa. [
如果有两个女人一起磨谷子,一个人会被接走,一个会被留下。”
36 Wanaume wawili watakuwa wanafanya kazi pamoja shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.]”
37 Kisha wakamuuliza, “Haya yatatukia wapi Bwana?” Akawaambia, “Pale ulipo mzoga, huko ndiko tai watakapokusanyika.”
门徒问耶稣:“主啊,它会在哪里发生?”耶稣回答:“哪里有尸首,哪里就会围着秃鹫。”