< Luka 16 >
1 Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Palikuwa na tajiri mmoja na msimamizi wake. Ilisemekana kwamba huyo msimamizi alikuwa anatumia vibaya mali ya tajiri yake.
And He said also to his disciples, There was a certain rich man, who had a steward; and he was accused to him of wasting his goods.
2 Hivyo huyo tajiri akamwita na kumuuliza, ‘Ni mambo gani haya ninayoyasikia kukuhusu? Toa taarifa ya usimamizi wako, kwa sababu huwezi kuendelea kuwa msimamizi.’
And he called him, and said unto him, What is this I hear of thee? give up the accounts of thy stewardship, for thou canst be no longer steward.
3 “Yule msimamizi akawaza moyoni mwake, ‘Nitafanya nini sasa? Bwana wangu ananiondoa katika kazi yangu. Sina nguvu za kulima, nami ninaona aibu kuombaomba.
And the steward said in himself, What shall I do? now my master takes away the stewardship from me; I am not able to work, and I am ashamed to beg.
4 Najua nitakalofanya ili nikiachishwa kazi yangu hapa, watu wanikaribishe nyumbani kwao.’
I know what I will do, that when I am turned out of my place, they may receive me into their houses.
5 “Kwa hiyo akawaita wadeni wote wa bwana wake, mmoja mmoja. Akamuuliza wa kwanza, ‘Deni lako kwa bwana wangu ni kiasi gani?’
So he called his master's debtors to him, and said to the first, How much owest thou to my master? and he said, an hundred baths of oil.
6 “Akajibu, ‘Galoni 800za mafuta ya mizeituni.’ “Msimamizi akamwambia, ‘Chukua hati ya deni lako, ibadilishe upesi, uandike galoni 400.’
And he said to him, Take thy bill, and sit down and write but fifty.
7 “Kisha akamuuliza wa pili, ‘Wewe deni lako ni kiasi gani?’ “Akajibu, ‘Vipimo 1,000vya ngano.’ “Yule msimamizi akamwambia, ‘Chukua hati yako, andika vipimo 800!’
Then he said to another, And how much owest thou? and he said, an hundred measures of wheat: and he said to him, Take thy bill, and write fourscore.
8 “Yule bwana akamsifu yule msimamizi dhalimu kwa jinsi alivyotumia ujanja. Kwa maana watu wa dunia hii wana ujanja zaidi wanapojishughulisha na mambo ya dunia kuliko watu wa nuru. (aiōn )
And his master commended the dishonest steward as having acted prudently: for the men of this world are as to their affairs wiser than the children of light. (aiōn )
9 Nawaambia, tumieni mali ya kidunia kujipatia marafiki, ili itakapokwisha, mkaribishwe katika makao ya milele. (aiōnios )
And I say unto you, Make to yourselves friends with these unrighteous treasures, that when they fail, ye may be received into everlasting habitations. (aiōnios )
10 “Yeyote aliye mwaminifu katika mambo madogo, pia ni mwaminifu hata katika mambo makubwa, naye mtu ambaye si mwaminifu katika mambo madogo pia si mwaminifu katika mambo makubwa.
He, that is faithful in the lest, is faithful also in much: and he, that is unjust in the lest, is unjust also in much.
11 Ikiwa hamkuwa waaminifu katika mali ya kidunia, ni nani atakayewaaminia mali ya kweli?
If therefore ye have not been faithful in the false riches, who will intrust you with the true?
12 Nanyi kama hamkuwa waaminifu na mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe?
and if ye have not been faithful in that which was another's, who will give you that which is your own?
13 “Hakuna mtumishi awezaye kuwatumikia mabwana wawili. Kwa kuwa atamchukia huyu na kumpenda yule mwingine, au atashikamana sana na huyu na kumdharau yule mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu pamoja na Mali.”
No servant can serve two masters; for either he will hate the one, and love the other; or at lest he will be attached to the one, and neglect the other. Ye cannot serve God and Mammon.
14 Mafarisayo, waliokuwa wapenda fedha, waliyasikia hayo yote na wakamcheka kwa dharau.
And the pharisees also, who were covetous, heard all these things; and derided Him.
15 Yesu akawaambia, “Ninyi mnajionyesha kuwa wenye haki mbele za wanadamu, lakini Mungu anaijua mioyo yenu. Kwa maana vile vitu ambavyo wanadamu wanavithamini sana, kwa Mungu ni machukizo.
And He said unto them, Ye justify yourselves before men, but God knoweth your hearts: for that which is highly esteemed among men is abomination in the sight of God.
16 “Sheria na Manabii vilihubiriwa mpaka kuja kwa Yohana Mbatizaji. Tangu wakati huo habari njema za Ufalme wa Mungu zinahubiriwa, na kila mmoja hujiingiza kwa nguvu.
The law and the prophets continued until John: from that time the kingdom of God is preached, and every one presseth into it.
17 Lakini ni rahisi zaidi mbingu na dunia kupita kuliko hata herufi moja kuondoka katika Sheria.
Though it is easier for heaven and earth to pass away, than one tittle of the law to fail.
18 “Mtu yeyote amwachaye mkewe na kumwoa mwanamke mwingine anazini, naye mwanaume amwoaye mwanamke aliyetalikiwa anazini.
Whosoever putteth away his wife, and marrieth another, committeth adultery; and whosoever marrieth her that is put away from her husband committeth adultery.
19 “Palikuwa na mtu mmoja tajiri aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, ambaye aliishi kwa anasa kila siku.
Now there was a certain rich man, who was clothed in purple and fine linen, living voluptuously and splendidly every day.
20 Hapo penye mlango wake aliishi maskini mmoja, jina lake Lazaro, mwenye vidonda mwili mzima.
And there was a poor man named Lazarus,
21 Huyo Lazaro alitamani kujishibisha kwa makombo yaliyoanguka kutoka mezani kwa yule tajiri. Hata mbwa walikuwa wakija na kuramba vidonda vyake.
who was laid at his gate full of sores, and desiring to be fed with the crumbs that fell from the rich man's table: and the dogs came and licked his sores. And it came to pass that the poor man died,
22 “Wakati ukafika yule maskini akafa, nao malaika wakamchukua akae pamoja na Abrahamu. Yule tajiri naye akafa na akazikwa.
and was carried by angels to Abraham's bosom: the rich man also died, and was buried.
23 Kule kuzimu alipokuwa akiteseka, alitazama juu, akamwona Abrahamu kwa mbali, naye Lazaro alikuwa karibu yake. (Hadēs )
And in hell he lifted up his eyes, being in torments, and seeth Abraham from afar, and Lazarus in his bosom. (Hadēs )
24 Hivyo yule tajiri akamwita, ‘Baba Abrahamu, nihurumie na umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake ndani ya maji aupoze ulimi wangu, kwa sababu nina maumivu makuu kwenye moto huu.’
And he cried out and said, Father Abraham, have pity on me, and send Lazarus, that he may dip the tip of his finger in water, and cool my tongue; for I am tormented in this flame.
25 “Lakini Abrahamu akamjibu, ‘Mwanangu, kumbuka kwamba wakati wa uhai wako ulipata mambo mazuri, lakini Lazaro alipata mambo mabaya. Lakini sasa anafarijiwa hapa na wewe uko katika maumivu makuu.
And Abraham said, Son, remember that thou receivedst thy good things in thy life-time, and likewise Lazarus his evils: but now he is comforted, and thou art tormented.
26 Zaidi ya hayo, kati yetu na ninyi huko kumewekwa shimo kubwa, ili wale wanaotaka kutoka huku kuja huko wasiweze, wala mtu yeyote asiweze kuvuka kutoka huko kuja kwetu.’
And besides, there is a great gulf fixed between us and you; so that they, who would pass from hence to you, cannot; nor can they pass to us, who would come from thence.
27 “Akasema, ‘Basi, nakuomba, umtume Lazaro aende nyumbani kwa baba yangu,
Then he said, Therefore I intreat thee, Father, that thou wouldst send him to my father's house:
28 maana ninao ndugu watano. Awaonye, ili wasije nao wakafika mahali hapa pa mateso.’
for I have five brethren; that he may testify to them my misery, least they also come into this place of torment.
29 “Abrahamu akamjibu, ‘Ndugu zako wana Maandiko ya Mose na Manabii, wawasikilize hao.’
Abraham answered him, They have Moses and the prophets, let them hear them:
30 “Yule tajiri akasema, ‘Hapana, baba Abrahamu, lakini mtu kutoka kwa wafu akiwaendea, watatubu.’
and he said, Nay, father Abraham, but if one went to them from the dead, they will repent.
31 “Abrahamu akamwambia, ‘Kama wasipowasikiliza Mose na Manabii, hawataweza kushawishika hata kama mtu akifufuka kutoka kwa wafu.’”
And he replied, If they hearken not to Moses and the prophets, neither will they be persuaded though one should rise from the dead.