< Luka 16 >

1 Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Palikuwa na tajiri mmoja na msimamizi wake. Ilisemekana kwamba huyo msimamizi alikuwa anatumia vibaya mali ya tajiri yake.
And he went on to say, unto his disciples also, —There was, a certain rich man, who had a steward, and, the same, was accused to him as squandering his goods.
2 Hivyo huyo tajiri akamwita na kumuuliza, ‘Ni mambo gani haya ninayoyasikia kukuhusu? Toa taarifa ya usimamizi wako, kwa sababu huwezi kuendelea kuwa msimamizi.’
And, accosting him, he said unto him—What is this I hear of thee? Render the account of thy stewardship, for thou canst no longer be steward.
3 “Yule msimamizi akawaza moyoni mwake, ‘Nitafanya nini sasa? Bwana wangu ananiondoa katika kazi yangu. Sina nguvu za kulima, nami ninaona aibu kuombaomba.
And the steward said within himself—What shall I do, because my lord taketh away the stewardship from me? Dig, I cannot: to beg, I am ashamed.
4 Najua nitakalofanya ili nikiachishwa kazi yangu hapa, watu wanikaribishe nyumbani kwao.’
I know what I will do, that, when I am removed out of the stewardship, they may welcome me into their own houses.
5 “Kwa hiyo akawaita wadeni wote wa bwana wake, mmoja mmoja. Akamuuliza wa kwanza, ‘Deni lako kwa bwana wangu ni kiasi gani?’
And, calling unto him each one of the debtors of his own lord, he was saying unto the first, —How much owest thou my lord?
6 “Akajibu, ‘Galoni 800za mafuta ya mizeituni.’ “Msimamizi akamwambia, ‘Chukua hati ya deni lako, ibadilishe upesi, uandike galoni 400.’
And, he, said—A hundred baths of oil. And, he, said unto him—Kindly take thine accounts, and, sitting down, make haste and write—Fifty!
7 “Kisha akamuuliza wa pili, ‘Wewe deni lako ni kiasi gani?’ “Akajibu, ‘Vipimo 1,000vya ngano.’ “Yule msimamizi akamwambia, ‘Chukua hati yako, andika vipimo 800!’
After that, unto another, he said—And how much owest, thou? And, he, said—A hundred homers of wheat. He saith unto him—Kindly take thine accounts, and write—Eighty!
8 “Yule bwana akamsifu yule msimamizi dhalimu kwa jinsi alivyotumia ujanja. Kwa maana watu wa dunia hii wana ujanja zaidi wanapojishughulisha na mambo ya dunia kuliko watu wa nuru. (aiōn g165)
And the lord praised the unrighteous steward, in that with forethought he acted: —Because, the sons of this age, have more forethought than the sons of light, respecting their own generation. (aiōn g165)
9 Nawaambia, tumieni mali ya kidunia kujipatia marafiki, ili itakapokwisha, mkaribishwe katika makao ya milele. (aiōnios g166)
And, I, unto you, say—For yourselves, make ye friends, with the unjust Riches, in order that, as soon as it shall fail, they may welcome you into the age-abiding tents. (aiōnios g166)
10 “Yeyote aliye mwaminifu katika mambo madogo, pia ni mwaminifu hata katika mambo makubwa, naye mtu ambaye si mwaminifu katika mambo madogo pia si mwaminifu katika mambo makubwa.
The faithful in least, in much also, is, faithful, and, he that in least is unrighteous, in much also, is, unrighteous.
11 Ikiwa hamkuwa waaminifu katika mali ya kidunia, ni nani atakayewaaminia mali ya kweli?
If therefore, in the unjust Riches ye proved unfaithful, the true, who, unto you, will entrust?
12 Nanyi kama hamkuwa waaminifu na mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe?
And, if, in what was another’s, ye proved unfaithful, your own, who will give unto you?
13 “Hakuna mtumishi awezaye kuwatumikia mabwana wawili. Kwa kuwa atamchukia huyu na kumpenda yule mwingine, au atashikamana sana na huyu na kumdharau yule mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu pamoja na Mali.”
No domestic, can, unto two masters, be in service; for either, the one, he will hate, and, the other, love, or, unto the one, he will hold, and, the other, despise: Ye cannot, unto God, be in service, and unto Riches.
14 Mafarisayo, waliokuwa wapenda fedha, waliyasikia hayo yote na wakamcheka kwa dharau.
Now the Pharisees, who were, lovers of money, were hearing all these things, and were openly sneering at him.
15 Yesu akawaambia, “Ninyi mnajionyesha kuwa wenye haki mbele za wanadamu, lakini Mungu anaijua mioyo yenu. Kwa maana vile vitu ambavyo wanadamu wanavithamini sana, kwa Mungu ni machukizo.
And he said unto them—Ye, are they who justify themselves before men, but, God, knoweth your hearts; because, that which amongst men is lofty, is an abomination before God.
16 “Sheria na Manabii vilihubiriwa mpaka kuja kwa Yohana Mbatizaji. Tangu wakati huo habari njema za Ufalme wa Mungu zinahubiriwa, na kila mmoja hujiingiza kwa nguvu.
The law and the prophets, were until John, —from that time, the good news of the kingdom of God, is being proclaimed, and, everyone, thereinto, is forcing his way.
17 Lakini ni rahisi zaidi mbingu na dunia kupita kuliko hata herufi moja kuondoka katika Sheria.
But it is, easier, for heaven and earth to pass away, than that, of the law, one little point, should fail.
18 “Mtu yeyote amwachaye mkewe na kumwoa mwanamke mwingine anazini, naye mwanaume amwoaye mwanamke aliyetalikiwa anazini.
Every one divorcing his wife and marrying another, committeth adultery; and, he that marrieth a woman divorced from a husband, committeth adultery.
19 “Palikuwa na mtu mmoja tajiri aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, ambaye aliishi kwa anasa kila siku.
Now, a certain man, was rich, and he used to clothe himself with purple and fine linen, making merry day by day, brilliantly.
20 Hapo penye mlango wake aliishi maskini mmoja, jina lake Lazaro, mwenye vidonda mwili mzima.
And, a certain beggar, by name Lazarus, used to be cast near his gate, full of sores,
21 Huyo Lazaro alitamani kujishibisha kwa makombo yaliyoanguka kutoka mezani kwa yule tajiri. Hata mbwa walikuwa wakija na kuramba vidonda vyake.
and to long to be fed from the crumbs that fell from the table of the rich man: nay! even, the dogs, used to come and lick his sores.
22 “Wakati ukafika yule maskini akafa, nao malaika wakamchukua akae pamoja na Abrahamu. Yule tajiri naye akafa na akazikwa.
And it came to pass that the beggar died, and was carried away by the messengers, into the bosom of Abraham. And, the rich man also, died, and was buried.
23 Kule kuzimu alipokuwa akiteseka, alitazama juu, akamwona Abrahamu kwa mbali, naye Lazaro alikuwa karibu yake. (Hadēs g86)
And, in hades, lifting up his eyes, being in torments, he seeth Abraham afar off, and Lazarus in his bosom. (Hadēs g86)
24 Hivyo yule tajiri akamwita, ‘Baba Abrahamu, nihurumie na umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake ndani ya maji aupoze ulimi wangu, kwa sababu nina maumivu makuu kwenye moto huu.’
And, he, calling out, said—Father Abraham! have mercy upon me, and send Lazarus, that he may dip the tip of his finger in water, and cool my tongue, —because I am in anguish in this flame.
25 “Lakini Abrahamu akamjibu, ‘Mwanangu, kumbuka kwamba wakati wa uhai wako ulipata mambo mazuri, lakini Lazaro alipata mambo mabaya. Lakini sasa anafarijiwa hapa na wewe uko katika maumivu makuu.
But Abraham said—Child! remember—That thou didst duly received thy good things in thy life, and, Lazarus, in like manner, the evil things; but, now, here, he is comforted, and, thou, art in anguish.
26 Zaidi ya hayo, kati yetu na ninyi huko kumewekwa shimo kubwa, ili wale wanaotaka kutoka huku kuja huko wasiweze, wala mtu yeyote asiweze kuvuka kutoka huko kuja kwetu.’
And, besides all these things, betwixt us and you, a great chasm, hath been fixed, —so that, they who might wish to cross over from hence unto you, should not be able, nor any, from thence unto us, be crossing over.
27 “Akasema, ‘Basi, nakuomba, umtume Lazaro aende nyumbani kwa baba yangu,
But he said—I request thee then, father, that thou wouldst send him unto my father’s house, —
28 maana ninao ndugu watano. Awaonye, ili wasije nao wakafika mahali hapa pa mateso.’
for I have five brethren; —that he may solemnly testify unto them, lest, they also, come into this place of torment.
29 “Abrahamu akamjibu, ‘Ndugu zako wana Maandiko ya Mose na Manabii, wawasikilize hao.’
But Abraham saith—They have Moses and the Prophets: Let them hearken unto them.
30 “Yule tajiri akasema, ‘Hapana, baba Abrahamu, lakini mtu kutoka kwa wafu akiwaendea, watatubu.’
But, he, said—Nay! father Abraham, but, if one, from the dead, should go unto them, they would repent.
31 “Abrahamu akamwambia, ‘Kama wasipowasikiliza Mose na Manabii, hawataweza kushawishika hata kama mtu akifufuka kutoka kwa wafu.’”
But he said unto him—If, unto Moses and the Prophets, they do not hearken, neither, if one, from among the dead, should arise, would they be persuaded.

< Luka 16 >