< Luka 16 >

1 Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Palikuwa na tajiri mmoja na msimamizi wake. Ilisemekana kwamba huyo msimamizi alikuwa anatumia vibaya mali ya tajiri yake.
Yeecu yi nobbwankecebo tak, “nii cuwekako kangeni ki ni toman'nye, Lacin kwa kiyan nye ki nii toman nyewo kang cineut cuwekacokob.
2 Hivyo huyo tajiri akamwita na kumuuliza, ‘Ni mambo gani haya ninayoyasikia kukuhusu? Toa taarifa ya usimamizi wako, kwa sababu huwezi kuendelea kuwa msimamizi.’
La nii cuweka wuco yico, “fulan yer minuwa dor mwere? bowki kiyeka tomange mweke, wori mari mwa yila nii tomange mititak.
3 “Yule msimamizi akawaza moyoni mwake, ‘Nitafanya nini sasa? Bwana wangu ananiondoa katika kazi yangu. Sina nguvu za kulima, nami ninaona aibu kuombaomba.
Lamitomange toki neren, ma mangi, nilomi anyam tomanyewo kangmik? Wo, mimanki bikwantonet lami cwa kwenduwe meka cekoti.
4 Najua nitakalofanya ili nikiachishwa kazi yangu hapa, watu wanikaribishe nyumbani kwao.’
Minnyumwom dike ma matiyeu noci cukumye mor tomanye nindi, nubo ayoye lonici.
5 “Kwa hiyo akawaita wadeni wote wa bwana wake, mmoja mmoja. Akamuuliza wa kwanza, ‘Deni lako kwa bwana wangu ni kiasi gani?’
Dila nitomannye cwuningangum nubo teluwece bwanteng centiyeu, yi nii kaba, Nyi nii lomi bwangmwenten tiye?
6 “Akajibu, ‘Galoni 800za mafuta ya mizeituni.’ “Msimamizi akamwambia, ‘Chukua hati ya deni lako, ibadilishe upesi, uandike galoni 400.’
yiki, 'nuwannye kwini kwob' Isryico, Bifumer mwerowo, canakowo yikenyiye, mulangum kwini nung.
7 “Kisha akamuuliza wa pili, ‘Wewe deni lako ni kiasi gani?’ “Akajibu, ‘Vipimo 1,000vya ngano.’ “Yule msimamizi akamwambia, ‘Chukua hati yako, andika vipimo 800!’
Yilan yikannye, ciki bwangmwentuniyi? Yiki, cwayi bikate kwini kwob, 'bifumerwo mulangum kwini narub'.
8 “Yule bwana akamsifu yule msimamizi dhalimu kwa jinsi alivyotumia ujanja. Kwa maana watu wa dunia hii wana ujanja zaidi wanapojishughulisha na mambo ya dunia kuliko watu wa nuru. (aiōn g165)
Dila niwo caklang nii bwini bilengewo ki yulancero. Bibeyo kaleweu nyimem maka nyinong nubo ko kaleweu la bibei filange yulang. (aiōn g165)
9 Nawaambia, tumieni mali ya kidunia kujipatia marafiki, ili itakapokwisha, mkaribishwe katika makao ya milele. (aiōnios g166)
Miyi komti komma bifarak kannge cuweraka kannge buni bilinke, cawo cin dimri, naci yokom lonici wuro manki diks. (aiōnios g166)
10 “Yeyote aliye mwaminifu katika mambo madogo, pia ni mwaminifu hata katika mambo makubwa, naye mtu ambaye si mwaminifu katika mambo madogo pia si mwaminifu katika mambo makubwa.
Wo madikerti dongdong dor dikero biduwareri, cin nii dongdonge dor dikero dur, wo kebo nii bilinke don dikero bidurure, kebo ni bilinke dor dikero dur.
11 Ikiwa hamkuwa waaminifu katika mali ya kidunia, ni nani atakayewaaminia mali ya kweli?
Tano kommabo dike dongdonge di cuwekako kebo wucakeri, we aciya kumenti kicuweka wabilinkece?
12 Nanyi kama hamkuwa waaminifu na mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe?
No komma dike dongdonge ki kemer niidir we anekom kemer kumer tiye?
13 “Hakuna mtumishi awezaye kuwatumikia mabwana wawili. Kwa kuwa atamchukia huyu na kumpenda yule mwingine, au atashikamana sana na huyu na kumdharau yule mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu pamoja na Mali.”
Kange mami wo a wob nii luweti yobe, catin kowini, ci cui win kakka ci ciya winening, ci cuwe kangum wineu. mani ka wab kwaamatiri kom wab cuwekati.
14 Mafarisayo, waliokuwa wapenda fedha, waliyasikia hayo yote na wakamcheka kwa dharau.
Kambo faricawabo wuro cui cuwekatiyeu nuwa dikero biombori, cin macinen cuwelangka.
15 Yesu akawaambia, “Ninyi mnajionyesha kuwa wenye haki mbele za wanadamu, lakini Mungu anaijua mioyo yenu. Kwa maana vile vitu ambavyo wanadamu wanavithamini sana, kwa Mungu ni machukizo.
Inyici, “Kom ko tiki dor kumero kabum nubem, dila kwaama nyumuom nerkumero. Dikero nubo nedurketiye nyeu diker yeika fiye kwaama wiye.
16 “Sheria na Manabii vilihubiriwa mpaka kuja kwa Yohana Mbatizaji. Tangu wakati huo habari njema za Ufalme wa Mungu zinahubiriwa, na kila mmoja hujiingiza kwa nguvu.
Biwerer bifumer nob tomangebo inwi yakenciko Yahaya nin. Kwama wuro cin bwanten ker liyar kwaaranarotiye, kwarub kutannyi kwamacuo ci bwangten ker liyar kwaamarotiye, kwanrub ci ma bwi dokka dorekti morece.
17 Lakini ni rahisi zaidi mbingu na dunia kupita kuliko hata herufi moja kuondoka katika Sheria.
Gwamm kangero, atin yilam bwaibo diko kange bitineu nabecum, na diker win nabi weretro na dim.
18 “Mtu yeyote amwachaye mkewe na kumwoa mwanamke mwingine anazini, naye mwanaume amwoaye mwanamke aliyetalikiwa anazini.
Niwo nyankan wucenin naukangeri inma buroka, ken niwo nau nawiyewo cinyam kanngeri inma buroka.
19 “Palikuwa na mtu mmoja tajiri aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, ambaye aliishi kwa anasa kila siku.
Nii cuwakakko kanngenwi, wo dukulen kemero yoryoreu nuwa luma kalecokoti.
20 Hapo penye mlango wake aliishi maskini mmoja, jina lake Lazaro, mwenye vidonda mwili mzima.
Cin yoken nii kini kannge nyiloco, dencero Liazaru, wo bwiceu ka deti.
21 Huyo Lazaro alitamani kujishibisha kwa makombo yaliyoanguka kutoka mezani kwa yule tajiri. Hata mbwa walikuwa wakija na kuramba vidonda vyake.
Ceu ci cuiti naci bwam fwercero ki fiti cari yarangum ti fiye caka carik nii cuweka nyo kibi cuwetincer bom biyablam bwiceti.
22 “Wakati ukafika yule maskini akafa, nao malaika wakamchukua akae pamoja na Abrahamu. Yule tajiri naye akafa na akazikwa.
Laniwo bwiyamri, nobtomangeb kwaamabo tu co yakenciko Ibrayim nin. Ni cuweks buyam, cin fwerumco,
23 Kule kuzimu alipokuwa akiteseka, alitazama juu, akamwona Abrahamu kwa mbali, naye Lazaro alikuwa karibu yake. (Hadēs g86)
ci mor Adece ci nuwa dotange ti, la cin kun doro cinto Ibrayim kutan, kan'nge Liazaru cantangcek. (Hadēs g86)
24 Hivyo yule tajiri akamwita, ‘Baba Abrahamu, nihurumie na umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake ndani ya maji aupoze ulimi wangu, kwa sababu nina maumivu makuu kwenye moto huu.’
Lacin cobicoro ciki, Tee Ibrayim, ci bwinni mito, twomun Liazaru adokti biwurece mwem abelti menti biyenmin, wori indotange minuwati mor kirewe.
25 “Lakini Abrahamu akamjibu, ‘Mwanangu, kumbuka kwamba wakati wa uhai wako ulipata mambo mazuri, lakini Lazaro alipata mambo mabaya. Lakini sasa anafarijiwa hapa na wewe uko katika maumivu makuu.
Dila Ibrayim yico, Bwe, kwabi ki kwamawo mu kalemweu munuwa luma cuweka mwekobi, munyo kulentinimbo ken, La Liazaru nuwati ka dotange. Dila naweu luma cinecotide, mwe munuwa dotangeti.
26 Zaidi ya hayo, kati yetu na ninyi huko kumewekwa shimo kubwa, ili wale wanaotaka kutoka huku kuja huko wasiweze, wala mtu yeyote asiweze kuvuka kutoka huko kuja kwetu.’
Nobo nyori dila buwako cuwa cuwau inwi, wori birombi coi yabkati kumeneu nadolde, tak kannge na yabuurefo nyinnen.
27 “Akasema, ‘Basi, nakuomba, umtume Lazaro aende nyumbani kwa baba yangu,
Lamicuweks yiki, Lami kennenti Tee Ibrayim, twornco lo Tee ni-
28 maana ninao ndugu watano. Awaonye, ili wasije nao wakafika mahali hapa pa mateso.’
wori minweki keb mib bi beibayilobe nyo nung, amincinen biweret kayilo cibuo fiye dotangewo.
29 “Abrahamu akamjibu, ‘Ndugu zako wana Maandiko ya Mose na Manabii, wawasikilize hao.’
Dila Ibrayim yiki, cin wiki Musa kannge kannge nob toman'ngebi nyori ciya nuwaci,
30 “Yule tajiri akasema, ‘Hapana, baba Abrahamu, lakini mtu kutoka kwa wafu akiwaendea, watatubu.’
Dilla nii cuweka ciyaki, 'O, on, Tee Ibrayim, cano kan'nge mor birombo biyam biya yacinendi, ciyam yiloten.
31 “Abrahamu akamwambia, ‘Kama wasipowasikiliza Mose na Manabii, hawataweza kushawishika hata kama mtu akifufuka kutoka kwa wafu.’”
Dilla Ibrayim yico, cono ci Musa kan'ge nobtoman'gebo ri, cabunano kan'nge fulou duwendi maciya nuwacoti”

< Luka 16 >