< Luka 15 >
1 Basi watoza ushuru na wenye dhambi wote walikuwa wanakusanyika ili wapate kumsikiliza Yesu.
Kõik maksukogujad ja patused kogunesid teda kuulama.
2 Lakini Mafarisayo na walimu wa sheria wakanungʼunika wakisema, “Huyu mtu anawakaribisha wenye dhambi na kula nao.”
Aga variserid ja kirjatundjad nurisesid: „See mees võtab vastu patuseid ja sööb koos nendega!“
3 Ndipo Yesu akawaambia mfano huu:
Siis Jeesus rääkis neile tähendamissõna:
4 “Ikiwa mmoja wenu ana kondoo mia moja, naye akapoteza mmoja wao, je, hawaachi wale tisini na tisa nyikani na kwenda kumtafuta huyo aliyepotea mpaka ampate?
„Kui kellelgi teie hulgast oleks sada lammast ja ta ühe neist kaotaks, kas ta ei jätaks üheksakümmend üheksat tühermaale ega läheks kadunut otsima, kuni ta tema leiab?
5 Naye akishampata, humbeba mabegani mwake kwa furaha
Ja kui ta on tema leidnud, võtab ta tema rõõmuga oma õlgadele
6 na kwenda nyumbani. Kisha huwaita rafiki zake na majirani, na kuwaambia, ‘Furahini pamoja nami; nimempata kondoo wangu aliyepotea.’
ja läheb koju. Ta kutsub kokku sõbrad ja naabrid ning ütleb: „Rõõmustage koos minuga, sest ma olen leidnud oma kadunud lamba!“
7 Nawaambieni, vivyo hivyo kutakuwa na furaha zaidi mbinguni kwa sababu ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa wenye haki tisini na tisa ambao hawana haja ya kutubu.”
Ma ütlen teile, samamoodi on taevas ühe meelt parandanud patuse pärast rohkem rõõmu kui üheksakümne üheksa õige pärast, kellele ei ole vaja meeleparandust.
8 “Au ikiwa mwanamke ana sarafu za fedha kumi, naye akapoteza moja, je, hawashi taa na kufagia nyumba na kuitafuta kwa bidii mpaka aipate?
Või naine, kellel on kümme hõbemünti ja ta kaotab neist ühe. Kas ta ei süüta lampi ega pühi kogu maja ega otsi tähelepanelikult, kuni ta selle leiab?
9 Naye akiisha kuipata, huwaita rafiki zake na majirani na kuwaambia, ‘Furahini pamoja nami; nimeipata ile sarafu yangu ya fedha iliyopotea.’
Ja kui ta selle on leidnud, kutsub ta kokku sõbrad ja naabrid ning ütleb: „Rõõmustage koos minuga, sest ma olen leidnud oma kadunud mündi!“
10 Vivyo hivyo, nawaambia, kuna furaha mbele ya malaika wa Mungu juu ya mwenye dhambi mmoja atubuye.”
Samamoodi, ma ütlen teile, rõõmustatakse Jumala inglite ees ühe patuse pärast, kes meelt parandab.“
11 Yesu akaendelea kusema: “Kulikuwa na mtu mmoja aliyekuwa na wana wawili.
Jeesus jätkas: „Ühel mehel oli kaks poega.
12 Yule mdogo akamwambia baba yake, ‘Baba, nipe urithi wangu.’ Hivyo akawagawia wanawe mali yake.
Noorem ütles isale: „Isa, anna mulle kätte minu osa pärandist!“Ja ta jagas vara nende vahel.
13 “Baada ya muda mfupi, yule mdogo akakusanya vitu vyote alivyokuwa navyo, akaenda nchi ya mbali, na huko akaitapanya mali yake kwa maisha ya anasa.
Mõne päeva pärast kogus noorem poeg kõik kokku ning läks kaugele maale ja raiskas prassides oma vara.
14 Baada ya kutumia kila kitu alichokuwa nacho, kukawa na njaa kali katika nchi ile yote, naye akawa hana chochote.
Kui ta oli kõik ära kulutanud, tuli suur näljahäda sellele maale, ja talle tuli puudus kätte.
15 Kwa hiyo akaenda akaajiriwa na mwenyeji mmoja wa nchi ile ambaye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe.
Nii ta läks ühe kohaliku inimese juurde, kes saatis ta oma väljadele sigu karjatama.
16 Akatamani kujishibisha kwa maganda waliyokula wale nguruwe, wala hakuna mtu aliyempa chochote.
Ta igatses kõhtu täita kaunadega, mida sead sõid; aga ükski ei andnud talle.
17 “Lakini alipozingatia moyoni mwake, akasema, ‘Ni watumishi wangapi walioajiriwa na baba yangu ambao wana chakula cha kuwatosha na kusaza, bali mimi hapa nakufa kwa njaa!
Kui ta arusaamisele tuli, ütles ta: „Kui paljudel minu isa palgalistel on toitu küllaga, aga mina suren siin nälga!
18 Nitaondoka na kurudi kwa baba yangu na kumwambia: Baba, nimetenda dhambi mbele za Mungu na mbele yako.
Ma asun teele ja lähen tagasi oma isa juurde ja ütlen talle: „Isa, ma olen pattu teinud taeva vastu ja sinu vastu.
19 Sistahili tena kuitwa mwanao; nifanye kama mmoja wa watumishi wako.’
Ma ei ole enam väärt, et mind su pojaks hüütaks! Tee mind üheks oma palgalistest!““
20 Basi akaondoka, akaenda kwa baba yake. “Lakini alipokuwa bado yuko mbali, baba yake akamwona, moyo wake ukajawa na huruma. Akamkimbilia mwanawe, akamkumbatia na kumbusu.
Nii ta tõusis ja läks oma isa juurde. Aga kui ta veel kaugel oli, nägi isa teda ja tal oli temast kahju. Ta jooksis pojale vastu, langes talle kaela ja suudles teda.
21 “Yule mwana akamwambia baba yake, ‘Baba, nimekosa mbele za Mungu na mbele yako. Sistahili kuitwa mwanao tena.’
Poeg ütles talle: „Isa, ma olen teinud pattu taeva vastu ja sinu vastu. Ma ei ole enam väärt, et mind su pojaks hüütaks!“
22 “Lakini baba yake akawaambia watumishi, ‘Leteni upesi joho lililo bora sana, tieni pete kidoleni mwake na viatu miguuni mwake.
Aga isa ütles oma sulastele: „Ruttu! Tooge parim rüü ja pange talle selga! Pange sõrmus ta sõrme ja sandaalid talle jalga!
23 Leteni ndama aliyenona, mkamchinje ili tuwe na karamu, tule na kufurahi.
Tooge nuumvasikas ja tapke see! Tehkem pidusöök ja rõõmustagem!
24 Kwa maana huyu mwanangu alikuwa amekufa na sasa yu hai tena; alikuwa amepotea na sasa amepatikana!’ Nao wakaanza kufanya tafrija.
Sest mu poeg oli surnud, aga ta elab jälle; ta oli kadunud, ja on leitud!“Ja nii nad hakkasid pidutsema.
25 “Wakati huo, yule mwana mkubwa alikuwa shambani. Alipokaribia nyumbani, akasikia sauti ya nyimbo na watu wakicheza.
Samal ajal oli vanem poeg põllul. Kui ta kodule lähenes, kuulis ta muusikat ja tantsu.
26 Akamwita mmoja wa watumishi na kumuuliza, ‘Kuna nini?’
Ta kutsus ühe sulastest ja küsis, mis lahti on.
27 Akamwambia, ‘Ndugu yako amekuja, naye baba yako amemchinjia ndama aliyenona kwa sababu mwanawe amerudi nyumbani akiwa salama na mzima.’
„Su vend on tulnud koju, “vastas ta, „ja su isa on tapnud nuumvasika, sest ta on tervena tagasi.“
28 “Yule mwana mkubwa akakasirika, akakataa kuingia ndani. Basi baba yake akatoka nje na kumsihi.
Ent vanem vend vihastas ja keeldus sisse minemast. Siis tuli isa välja ja veenis teda.
29 Lakini yeye akamjibu baba yake, ‘Tazama! Miaka yote hii nimekutumikia na hata siku moja sijaacha kutii amri zako, lakini hujanipa hata mwana-mbuzi ili nifurahi na rafiki zangu.
Tema aga vastas isale: „Vaata! Kõik need aastad olen ma orjanud ega ole kunagi astunud üle su käsust. Aga mulle pole sa andnud isegi noort sikku, et ma võiksin oma sõpradega pidutseda!
30 Lakini huyu mwanao ambaye ametapanya mali yako kwa makahaba aliporudi nyumbani, wewe umemchinjia ndama aliyenona!’
Aga kui see sinu poeg tuleb koju, kes su varanduse on hooradega ära raisanud, tapad sa talle nuumvasika!“
31 “Baba yake akamjibu, ‘Mwanangu, umekuwa nami siku zote na vyote nilivyo navyo ni vyako.
„Mu poeg, “vastas isa, „sina oled alati minu juures, ja kõik, mis on mul, kuulub ka sulle.
32 Lakini ilitubidi tufurahi na kushangilia kwa sababu huyu ndugu yako alikuwa amekufa na sasa yu hai; alikuwa amepotea naye amepatikana.’”
Nüüd aga oli meil tarvis pidutseda ja olla rõõmsad, sest see su vend oli surnud ja ta elab jälle, ta oli kadunud ja on leitud.““