< Luka 14 >

1 Ikawa siku moja Yesu alipokuwa amekwenda kula chakula kwa mmoja wa viongozi wa Mafarisayo siku ya Sabato, watu walikuwa wakimchunguza kwa bidii.
Ühel hingamispäeval läks Jeesus einestama ühe variseride ülema koju, kus nad teda hoolikalt jälgisid.
2 Papo hapo mbele yake palikuwa na mtu mmoja mwenye ugonjwa wa kuvimba mwili.
Seal oli üks mees, kelle käed ja jalad olid tursunud.
3 Yesu akawauliza wale Mafarisayo na walimu wa sheria, “Je, ni halali kuponya watu siku ya Sabato au la?”
Niisiis küsis Jeesus vaimuliku seaduse tundjatelt ja variseridelt: „Kas seadus lubab hingamispäeval terveks teha või mitte?“
4 Wakakaa kimya. Hivyo Yesu akamshika yule mgonjwa mkono na kumponya, akamruhusu aende zake.
Aga nad vaikisid. Jeesus puudutas meest, tegi ta terveks ja saatis oma teed.
5 Kisha akawauliza, “Kama mmoja wenu angekuwa na mtoto au ngʼombe wake aliyetumbukia katika kisima siku ya Sabato, je, hamtamvuta mara moja na kumtoa?”
Siis ütles Jeesus neile: „Kui teie poeg või härg kukuks juhtumisi hingamispäeval kaevu, kas te ei tõmbaks teda siis kohe välja?“
6 Nao hawakuwa na la kusema.
Nad ei suutnud vastust anda.
7 Alipoona jinsi wageni walivyokuwa wanachagua mahali pa heshima wakati wa kula, akawaambia mfano huu:
Nii rääkis ta loo külalistele, sest ta märkas, kuidas nad olid valinud istumiseks aukohti.
8 “Mtu akikualika arusini, usikae mahali pa mgeni wa heshima kwa kuwa inawezekana amealikwa mtu mheshimiwa kuliko wewe.
„Kui sind on kutsutud pulmapeole, siis ära istu aukohale, sest võib-olla on kutsutud keegi, kes on sinust tähtsam, “alustas ta.
9 Kama mkifanya hivyo yule aliyewaalika ninyi wawili atakuja na kukuambia, ‘Mpishe huyu mtu kiti chako.’ Ndipo kwa aibu utalazimika kukaa katika nafasi ya chini kabisa.
„Sinu võõrustaja, kes on teid mõlemat kutsunud, tuleb ja ütleb sulle: „Anna oma koht sellele inimesele.“Siis pead sa piinlikkust tundes minema kohale, mis on järele jäänud.
10 Badala yake, unapoalikwa, chagua nafasi ya chini, ili yule mwenyeji wako atakapokuona atakuja na kukuambia, ‘Rafiki yangu, nenda kwenye nafasi iliyo bora zaidi.’ Kwa jinsi hii utakuwa umepewa heshima mbele ya wageni wenzako wote.
Kui sind on kutsutud, siis vali hoopis kõige tagasihoidlikum koht, nii et kui su võõrustaja tuleb sisse, ütleb ta sulle: „Mu sõber, palun mine paremale kohale.“Siis oleksid sa austatud kõigi külaliste ees, kes koos sinuga istuvad.
11 Kwa maana kila mtu ajikwezaye atashushwa, naye ajishushaye atakwezwa.”
Sest neid, kes end ise ülendavad, alandatakse, ja neid, kes end ise alandavad, ülendatakse.“
12 Kisha Yesu akamwambia yule aliyewaalika, “Uandaapo karamu ya chakula cha mchana au cha jioni, usialike rafiki zako au ndugu zako au jamaa zako au majirani zako walio matajiri tu. Ukifanya hivyo, wao nao wanaweza kukualika kwao, nawe ukawa umelipwa kile ulichofanya na kupata thawabu yako.
Seejärel ütles ta mehele, kes oli teda kutsunud: „Kui sa korraldad lõuna- või õhtusöögi, siis ära kutsu oma sõpru, vendi, sugulasi või rikkaid naabreid, et nad võiksid omakorda sind kutsuda ja nii saaksid sa tasu.
13 Bali ufanyapo karamu, waalike maskini, vilema na vipofu,
Kui sa korraldad pidusöögi, kutsu hoopis vaeseid, vigaseid, sante ja pimedaid,
14 nawe utabarikiwa kwa sababu hawa hawana uwezo wa kukulipa. Mungu atakulipa wakati wa ufufuo wa wenye haki.”
ning sa saad õnnistatud, sest neil ei ole sulle millegagi tasuda, ja sa saad tasu heade ülestõusmisel.“
15 Mmoja wa wale waliokuwa pamoja naye mezani aliposikia hivi akamwambia Yesu, “Amebarikiwa mtu yule atakayekula katika karamu ya Ufalme wa Mungu!”
Kui üks neist, kes koos Jeesusega lauas sõi, kuulis seda, ütles ta Jeesusele: „Kui imetore on neil, kes söövad peolauas Jumala riigis!“
16 Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alikuwa anaandaa karamu kubwa, akaalika watu wengi.
„Elas kord üks mees, kes valmistas suure pidusöögi ja kutsus palju külalisi, “vastas Jeesus.
17 Wakati wa karamu ulipofika, akamtuma mtumishi wake akawaambie wale walioalikwa, ‘Karibuni, kila kitu ki tayari sasa.’
„Kui saabus söögiaeg, saatis ta oma sulased kõigile kutsutuile ütlema: „Tulge, sest pidusöök on valmis!“
18 “Lakini wote, kila mmoja, wakaanza kutoa udhuru: Wa kwanza akasema, ‘Nimenunua shamba, lazima niende kuliona. Tafadhali niwie radhi.’
Aga nad kõik hakkasid vabandusi esitama. Esimene ütles: „Ostsin just põllu ja pean minema seda vaatama. Palun vabanda mind.“
19 “Mwingine akasema, ‘Ndipo tu nimenunua jozi tano za ngʼombe wa kulimia, nami ninakwenda kuwajaribu, tafadhali niwie radhi.’
Teine ütles: „Ostsin just viis paari härgi ja ma pean minema neid katsetama. Palun vabanda mind.“Kolmas ütles:
20 Naye mwingine akasema, ‘Nimeoa mke, kwa hiyo siwezi kuja.’
„Võtsin just naise, nii et ma ei saa tulla.“
21 “Yule mtumishi akarudi, akampa bwana wake taarifa. Ndipo yule mwenye nyumba akakasirika, akamwagiza yule mtumishi wake, akisema, ‘Nenda upesi kwenye mitaa na vichochoro vya mjini uwalete maskini, vilema, vipofu na viwete.’
Sulane läks tagasi ja rääkis oma isandale, mida nad olid öelnud. Majaisand sai pahaseks ja ütles oma sulasele: „Mine ruttu välja linna tänavatele ja kõrvaltänavatele ning too sisse vaesed, vigased, pimedad ja sandid.“
22 “Yule mtumishi akamwambia, ‘Bwana, yale uliyoniagiza nimefanya, lakini bado ipo nafasi.’
Siis ütles sulane: „Isand, ma tegin nii, nagu sa käskisid, aga ikka on veel tühje kohti.“
23 “Ndipo yule bwana akamwambia mtumishi wake, ‘Nenda kwenye barabara na vijia vilivyoko nje ya mji na uwalazimishe watu waingie ili nyumba yangu ipate kujaa.
Nii käskis isand sulast: „Mine välja maanteedele ja külatänavatele ning sunni inimesi tulema. Ma tahan, et koda saaks täis.
24 Kwa maana nawaambia, hakuna hata mmoja wa wale walioalikwa atakayeionja karamu yangu.’”
Ma ütlen sulle, ükski neist kutsututest ei saa mu pidusööki maitsta.““
25 Umati mkubwa wa watu ulikuwa ukisafiri pamoja na Yesu, naye akageuka, akawaambia,
Jeesusega käis kaasas suur rahvahulk. Ta pöördus ja ütles neile:
26 “Mtu yeyote anayekuja kwangu hawezi kuwa mwanafunzi wangu kama hatanipenda mimi zaidi ya baba yake na mama yake, mke wake na watoto wake, ndugu zake na dada zake, naam, hata maisha yake mwenyewe.
„Kui te tahate mind järgida, kuid ei vihka oma isa ja ema, naist ja lapsi, vendi ja õdesid − koguni oma elu −, ei saa te mu jüngrid olla.
27 Yeyote asiyeuchukua msalaba wake na kunifuata hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
Kui te ei võta oma risti ega järgne mulle, ei saa te mu jüngrid olla.
28 “Ni nani miongoni mwenu ambaye kama anataka kujenga nyumba, hakai kwanza chini na kufanya makisio ya gharama aone kama ana fedha za kutosha kukamilisha?
Kui kavatsete torni ehitada, kas ei arvuta te kõigepealt, kui palju see maksma läheb, ega vaata, kas teil on piisavalt raha selle lõpetamiseks?
29 La sivyo, akiisha kuweka msingi, naye akiwa hana uwezo wa kuikamilisha, wote waionao wataanza kumdhihaki,
Kui te pärast vundamendi rajamist ei suuda seda valmis teha, siis naeraksid kõik, kes teid näevad, ja ütleksid:
30 wakisema, ‘Mtu huyu alianza kujenga lakini hakuweza kukamilisha.’
„Vaadake teda: ta alustas ehitamist, kuid ei suutnud lõpetada.“
31 “Au ni mfalme gani atokaye kwenda kupigana vita na mfalme mwingine, ambaye hakai chini kwanza na kufikiri iwapo akiwa na jeshi la watu 10,000 ataweza kupigana na yule anayekuja na jeshi la watu 20,000?
Missugune kuningas läheb teise kuningaga sõtta, ilma et istuks enne koos nõuandjatega maha ega arvutaks, kas tema ja ta kümme tuhat meest suudavad võita tema vastu marssivad kakskümmend tuhat?
32 Kama hawezi, basi wakati yule mwingine akiwa bado yuko mbali, yeye hutuma ujumbe wa watu na kuomba masharti ya amani.
Kui ta ei suuda, saadab ta esindajad rahu paluma siis, kui teine kuningas on veel väga kaugel.
33 Vivyo hivyo, yeyote miongoni mwenu ambaye hawezi kuacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
Samamoodi on igaühega teist: kes ei loobu kõigest, ei saa minu jünger olla.
34 “Chumvi ni nzuri, lakini chumvi ikiwa imepoteza ladha yake, itafanywaje ili iweze kukolea tena?
Sool on hea, aga kui see kaotab oma maitse, kuidas saab selle taas soolaseks muuta?
35 Haifai ardhi wala kwa lundo la mbolea, bali hutupwa nje. “Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
Sellest pole kasu mulla ega väetisena – te viskate selle lihtsalt välja. Kellel kõrvad on, see kuulaku!“

< Luka 14 >